< Wakolosai 2 >

1 Kwa kuwa nataka mfahamu jinsi ambavyo nimekuwa na taabu nyingi kwa ajili yenu, kwa wote walioko Laodikia na kwa wote ambao hawajaona uso wangu katika mwili.
Denn ich will, daß ihr wisset, welch großen Kampf ich habe um euch und die in Laodicäa und so viele mein Angesicht im Fleische nicht gesehen haben,
2 Nafanya kazi ili kwamba mioyo yao iweze kufarijiwa kwa kuletwa pamoja katika upendo na katika utajiri wote wa wingi wa uhakika kamili wa maarifa, katika kuijua siri ya kweli ya Mungu, ambaye ni Kristo.
auf daß ihre Herzen getröstet sein mögen, vereinigt in Liebe und zu allem Reichtum der vollen Gewißheit des Verständnisses, zur Erkenntnis des Geheimnisses Gottes,
3 Katika Yeye hazina zote za hekima na maarifa zimefichwa.
in welchem verborgen sind alle Schätze der Weisheit und der Erkenntnis.
4 Nasema hivi ili kwamba mtu yeyote asije akawafanyia hila kwa hotuba yenye ushawishi.
Dies sage ich aber, auf daß niemand euch verführe durch überredende Worte.
5 Na ingawa sipo pamoja nanyi katika mwili, lakini nipo nanyi katika roho. Ninafurahi kuona utaratibu wenu mzuri na nguvu ya imani yenu katika Kristo.
Denn wenn ich auch dem Fleische nach abwesend bin, so bin ich doch im Geiste bei euch, mich freuend und sehend eure Ordnung und die Festigkeit eures Glaubens an Christum.
6 Kama mlivyompokea Kristo Bwana, tembeeni katika yeye.
Wie ihr nun den Christus Jesus, den Herrn, empfangen habt, so wandelt in ihm,
7 Mwimarishwe katika yeye, mjengwe katika yeye, mwimarishwe katika imani kama tu mlivyofundishwa, na kufungwa katika shukrani nyingi.
gewurzelt und auferbaut in ihm und befestigt [W. auferbaut werdend befestigt werdend] in dem Glauben, so wie ihr gelehrt worden seid, überströmend in demselben mit Danksagung.
8 Angalieni ya kwamba mtu yeyote asiwanase kwa falsafa na maneno matupu ya udanganyifu kulingana na mapokeo ya wanadamu, kulingana na kanuni za kidunia, na sio kulingana na Kristo.
Sehet zu, daß nicht jemand sei, der euch als Beute wegführe durch die Philosophie und durch eitlen Betrug, nach der Überlieferung der Menschen, nach den Elementen der Welt, und nicht nach Christo.
9 Kwa kuwa katika yeye ukamilifu wote wa Mungu unaishi katika mwili.
Denn in ihm wohnt die ganze Fülle der Gottheit leibhaftig;
10 Nanyi mmejazwa katika yeye. Yeye ni kichwa cha kila uweza na mamlaka.
und ihr seid vollendet [O. erfüllt, zur Fülle gebracht [vergl. v 9]] in ihm, welcher das Haupt jedes Fürstentums und jeder Gewalt ist;
11 Katika yeye pia mlitahiriwa kwa tohara isiyofanywa na wanadamu katika kuondolewa mwili wa nyama, lakini ni katika tohara ya Kristo.
in welchem ihr auch beschnitten worden seid mit einer nicht mit Händen geschehenen Beschneidung, in dem Ausziehen des Leibes des Fleisches, in der Beschneidung des Christus,
12 Mlizikwa pamoja naye katika ubatizo. Na kwa njia ya imani katika yeye mlifufuliwa kwa uweza wa Mungu, aliyemfufua kutoka kwa wafu.
mit ihm begraben in der Taufe, in welcher [O. welchem] ihr auch mitauferweckt worden seid durch den Glauben an die wirksame Kraft Gottes, der ihn aus den Toten auferweckt hat.
13 Na mlipokuwa mmekufa katika makosa yenu na kutokutahiriwa kwa miili yenu, aliwafanya hai pamoja naye na kutusamehe makosa yetu yote.
Und euch, als ihr tot waret in den Vergehungen und in der Vorhaut eures Fleisches, hat er mitlebendig gemacht mit ihm, indem er uns alle Vergehungen vergeben hat;
14 Alifuta kumbukumbu ya madeni iliyoandikwa, na taratibu zilizokuwa kinyume nasi. Aliiondoa yote na kuigongomea msalabani.
als er ausgetilgt die uns entgegenstehende Handschrift [O. den Schuldbrief] in Satzungen, die wider uns war, hat er sie auch aus der Mitte weggenommen, indem er sie an das Kreuz nagelte;
15 Aliziondoa nguvu na mamlaka. Aliyaweka wazi na kuyafanya kuwa sherehe ya ushidi kwa njia ya msalaba wake.
als er die Fürstentümer und die Gewalten ausgezogen [d. h. völlig entwaffnet] hatte, stellte er sie öffentlich zur Schau, indem er durch dasselbe [O. an demselben, od. in sich] über sie einen Triumph hielt.
16 Kwa hiyo, mtu yeyote asiwahukumu ninyi katika kula au katika kunywa, au kuhusu siku ya sikukuu au mwezi mpya, au siku za Sabato.
So richte euch nun niemand über Speise oder Trank, oder in Ansehung eines Festes oder Neumondes oder von Sabbathen,
17 Hivi ni vivuli vya mambo yajayo, lakini kiini ni Kristo.
die ein Schatten der zukünftigen Dinge sind, der Körper aber ist Christi.
18 Mtu awaye yote asinyang'anywe tuzo yake kwa kutamani unyenyekevu na kwa kuabudu malaika. Mtu wa jinsi hiyo huingia katika mambo aliyoyaona na kushawishiwa na mawazo yake ya kimwili.
Laßt niemand euch um den Kampfpreis bringen, der seinen eigenen Willen tut [And. üb.: der dies tun will] in Demut und Anbetung der Engel, [O. Engelverehrung] indem er auf Dinge eingeht, die er nicht gesehen hat, [Da "nicht" in vielen Handschriften fehlt, so übers. and.: das was er geschaut hat [d. h. das Gebiet von Gesichten] betretend] eitler Weise aufgeblasen von dem Sinne seines Fleisches,
19 Yeye hakishikilii kichwa. Ni kutoka katika kichwa kwamba mwili wote kupitia viungo vyake na mifupa huungwa na kushikamanishwa kwa pamoja; na hukua kwa ukuaji utolewao na Mungu.
und nicht festhaltend das Haupt, aus welchem der ganze Leib, durch die Gelenke und Bande Darreichung empfangend und zusammengefügt, das Wachstum Gottes wächst.
20 Ikiwa mlikufa pamoja na Kristo kwa tabia za dunia, mbona mnaishi kama mnawajibika kwa dunia:
Wenn ihr mit Christo den Elementen der Welt [Eig. von den Elementen der Welt weg] gestorben seid, was unterwerfet ihr euch Satzungen, [O. was laßt ihr euch Satzungen auflegen] als lebtet ihr noch in der Welt?
21 “Msishike, wala kuonja, wala kugusa”?
Berühre nicht, koste nicht, betaste nicht!
22 Haya yote yameamuriwa kwa ajili ya uharibifu ujao na matumizi, kutokana na maelekezo na mafundisho ya wanadamu.
[Dinge, welche alle zur Zerstörung durch den Gebrauch bestimmt sind] nach den Geboten und Lehren der Menschen
23 Sheria hizi zina hekima ya dini zilizotengenezwa kwa ubinafsi na unyenyekevu na mateso ya mwili. Lakini hazina thamani dhidi ya tamaa za mwili.
[welche zwar einen Schein von Weisheit haben, in eigenwilligem Gottesdienst [O. eigenwilliger Verehrung] und in Demut und im Nichtverschonen des Leibes, und nicht in einer gewissen Ehre], [d. h. in dem, was dem Leibe zukommt] zur Befriedigung [And. üb: [ohne Klammer]: und nicht in irgendwelcher Ehre zur Befriedigung] des Fleisches.

< Wakolosai 2 >