< Wakolosai 1 >

1 Paulo, mtume wa Kristo Yesu kwa mapenzi ya Mungu, na Timotheo ndugu yetu,
Paul, apôtre de Jésus-Christ par la volonté de Dieu, et Timothée, notre frère,
2 kwa waumini na ndugu waaminifu katika Kristo walioko Kolosai. Neema iwe kwenu, na amani kutoka kwa Mungu Baba yetu.
aux saints et fidèles frères en Christ qui sont à Colosses: Grâce et paix à vous de la part de Dieu notre Père et du Seigneur Jésus-Christ.
3 Tunatoa shukrani kwa Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo, na tunawaombea mara kwa mara.
Nous rendons grâces à Dieu, le Père de notre Seigneur Jésus-Christ, en priant toujours pour vous,
4 Tumesikia imani yenu katika Yesu Kristo na upendo mlionao kwa wale wote waliotengwa kwa ajili ya Mungu.
ayant entendu parler de votre foi en Jésus-Christ et de l'amour que vous avez pour tous les saints,
5 Mna upendo huu kwa sababu ya taraja la uhakika lililohifadhiwa mbinguni kwa ajili yenu. Mlisikia kuhusu taraja hiyo ya uhakika kabla katika neno la kweli, injili,
à cause de l'espérance qui vous est réservée dans les cieux, et dont vous avez entendu parler auparavant dans la parole de vérité de la Bonne Nouvelle
6 ambayo imekuja kwenu. Injili hii inazaa tunda na inaenea ulimwenguni kote. Imekuwa ikifanya hivi ndani yenu pia tangu siku mlipoisikia na kujifunza kuhusu neema ya Mungu katika kweli.
qui vous est parvenue, comme elle est dans le monde entier, et qu'elle porte du fruit et croît, comme elle croît aussi en vous, depuis le jour où vous avez entendu et connu la grâce de Dieu dans la vérité,
7 Hii ndiyo injili mliyojifunza kutoka kwa Epafra, mpendwa wetu mtumishi mwenzetu, ambaye ni mtumishi mwaminifu wa Kristo kwa niaba yetu.
ainsi que vous l'avez appris d'Épaphras, notre bien-aimé compagnon de service, fidèle serviteur de Christ en votre faveur,
8 Epafra ameufanya ujulikane kwetu upendo wenu katika Roho.
qui nous a aussi déclaré votre amour dans l'Esprit.
9 Kwa sababu ya upendo huu, tangu siku tuliposikia hivi, hatujaacha kuwaombea. Tumekuwa tukiomba kwamba mtajazwa na maarifa ya mapenzi yake katika hekima yote na ufahamu wa kiroho.
C'est pourquoi, nous aussi, depuis le jour où nous l'avons appris, nous ne cessons de prier et de demander pour vous, afin que vous soyez remplis de la connaissance de sa volonté en toute sagesse et intelligence spirituelles,
10 Tumekuwa tukiomba kwamba mtatembea kwa ustahimilivu wa Bwana katika njia zipendezazo. Tumekuwa tukiomba kwamba mtazaa tunda katika kila tendo jema na kwamba mtakua katika maarifa ya Mungu.
afin que vous marchiez d'une manière digne du Seigneur, pour lui plaire à tous égards, portant du fruit en toute bonne œuvre et croissant dans la connaissance de Dieu,
11 Tunaomba mweze kutiwa nguvu katika kila uwezo kulingana na nguvu za utukufu wake katika uvumilivu na ustahimilivu wote.
fortifiés de toute puissance, selon la puissance de sa gloire, pour toute endurance et persévérance dans la joie,
12 Tunaomba kwamba, kwa furaha, mtatoa shukrani kwa Baba, aliyewafanya ninyi mweze kuwa na sehemu katika urithi wa waumini katika nuru.
en rendant grâces au Père, qui nous a rendus aptes à participer à l'héritage des saints dans la lumière,
13 Ametuokoa kutoka katika utawala wa giza na kutuhamishia katika ufalme wa Mwana wake mpendwa.
qui nous a délivrés de la puissance des ténèbres et nous a transportés dans le royaume du Fils de son amour,
14 Katika Mwanae tuna ukombozi, msamaha wa dhambi.
en qui nous avons notre rédemption, le pardon de nos péchés.
15 Mwana ni mfano wa Mungu asiyeonekana. Ni mzaliwa wa kwanza wa uumbaji wote.
Il est l'image du Dieu invisible, le premier-né de toute la création.
16 Kwakuwa kwa yeye vitu vyote viliumbwa, vile vilivyoko mbinguni na vilivyoko duniani, vitu vinavyoonekana na visivyoonekana. ikiwa ni vya enzi au mamlaka au utawala au wenye nguvu, vitu vyote viliumbwa na yeye na kwa ajili yake.
Car par lui tout a été créé dans les cieux et sur la terre, les choses visibles et les choses invisibles, qu'il s'agisse de trônes, de dominations, de principautés ou de pouvoirs. Toutes choses ont été créées par lui et pour lui.
17 Yeye amekuwepo kabla ya vitu vyote, na katika yeye vitu vyote vinashikamana pamoja.
Il est avant toutes choses, et toutes choses subsistent en lui.
18 Na yeye ndiye kichwa cha mwili yaani kanisa, yeye ni mwanzo na mzaliwa wa kwanza kutoka miongoni mwa wafu, hivyo, ana nafasi ya kwanza miongoni mwa vitu vyote.
Il est la tête du corps, de l'assemblée, lui qui est le commencement, le premier-né d'entre les morts, afin d'avoir en toutes choses la prééminence.
19 Kwa kuwa Mungu alipendezwa kwamba utimilifu wake wote uishi ndani yake,
Car il a plu à toute la plénitude d'habiter en lui,
20 na kupatanisha vitu vyote kwake kwa njia ya Mwanawe. Mungu alifanya amani kupitia damu ya msalaba wake. Mungu alipatanisha vitu vyote kwake mwenyewe, ikiwa ni vitu vya duniani au vitu vya mbinguni.
et de réconcilier par lui toutes choses avec lui-même, tant celles qui sont sur la terre que celles qui sont dans les cieux, ayant établi la paix par le sang de sa croix.
21 Nanyi pia, kwa wakati mmoja mlikuwa wageni kwa Mungu na mlikuwa maadui wake katika akili na matendo maovu.
Vous qui, autrefois, étiez aliénés et ennemis dans votre esprit par vos mauvaises actions,
22 Lakini sasa amewapatanisha ninyi kwa mwili wake kupitia kifo. Alifanya hivi ili kuwaleta ninyi watakatifu, wasio na lawama na bila dosari mbele yake,
il vous a maintenant réconciliés par la mort dans le corps de sa chair, afin de vous présenter saints, irréprochables et sans défaut devant lui,
23 kama mkiendelea katika imani, mliyoimarishwa na kuwa thabiti, pasipo kuondoshwa mbali kutoka kwenye taraja la ujasiri la injili mliyoisikia. Hi ndiyo injili iliyotangazwa kwa kila mtu aliyeumbwa chini ya mbingu. Hii ndiyo injili ambayo kwayo mimi, Paulo, nimekuwa mtumishi.
si du moins vous persévérez dans la foi, fondés et inébranlables, sans vous détourner de l'espérance de la Bonne Nouvelle que vous avez entendue et qui est proclamée dans toute la création sous le ciel, dont moi, Paul, j'ai été fait serviteur.
24 Sasa nafurahia mateso yangu kwa ajili yenu. Nami natimiliza katika mwili wangu kinachopungua kwa mateso ya Kristo kwa ajili ya mwili wake, ambao ni kanisa.
Or, je me réjouis de mes souffrances à cause de vous, et je comble de mon côté ce qui manque aux souffrances de Christ dans ma chair, pour l'amour de son corps, qui est l'assemblée,
25 Mimi ni mtumishi wa kanisa hili, sawasawa na wajibu niliopewa kutoka kwa Mungu kwa ajili yenu, kulijaza neno la Mungu.
dont j'ai été fait serviteur selon l'office de Dieu qui m'a été confié envers vous pour l'accomplissement de la parole de Dieu,
26 Huu ni ukweli wa siri iliyokuwa imefichwa kwa miaka mingi na kwa vizazi. Lakini sasa imefunuliwa kwa wote waaminio katika Yeye. (aiōn g165)
mystère caché depuis des siècles et des générations. Mais maintenant il a été révélé à ses saints, (aiōn g165)
27 Ni kwa wale ambao Mungu alitaka kufunua kulivyo utajiri wa utukufu wa siri ya ukweli huu miongoni mwa Mataifa. Ni kwamba Kristo yumo ndani yenu, ujasiri wa utukufu ujao.
à qui Dieu a voulu faire connaître quelle est la richesse de la gloire de ce mystère parmi les païens, qui est le Christ en vous, l'espérance de la gloire.
28 Huyu ndiye tunayemtangaza. Tunamwonya kila mtu, na kumfundisha kila mtu kwa hekima yote, ili kwamba tumlete kila mtu mkamilifu katika Kristo.
Nous l'annonçons, en exhortant tout homme et en l'instruisant en toute sagesse, afin de rendre tout homme parfait en Jésus-Christ.
29 Kwa jili hii, mimi najibidisha na kujitahidi kulingana na nguvu yake ifanyayo kazi ndani yangu katika uweza.
C'est à quoi je m'efforce, moi aussi, selon son opération qui agit puissamment en moi.

< Wakolosai 1 >