< Amosi 8 >

1 Hiki ndicho ambacho bwana Yahwe amenionyesha. Tazama, kikapu cha matunda ya hari!
This is what Jehovah showed me: And look, a basket of summer fruit.
2 Akasema, “Unaona nini, Amosi?” Nikasema, “Kikapu cha matunda ya hari.” Kisha Yahwe akanambia, “Mwisho umefika kwa watu wangu Israeli; sintowaumiza tena.
He said, "Amos, what do you see?" I said, "A basket of summer fruit." Then Jehovah said to me, "The end has come on my people Israel. I will not again pass by them any more.
3 Nyimbo za kwenye hekalu zitakuwa vilio. Katika siku hiyo-hivi ndivyo asemavyo Bwana Yahwe. Mizoga itakuwa mingi, katika kila sehemu wataitupa katika ukimya!”
The songs of the temple will be wailings in that day," says Jehovah. "The dead bodies will be many. In every place they will throw them out with silence.
4 Lisikilizeni hili, ninyi mkanyagao maskini na kumuondoa fukara wa nchi.
Hear this, you who trample the needy, and destroy the poor of the land,
5 wakisema, “Wakati mwezi mpya utakapoisha, hivyo tunaweza kuuza mazao tena? Wakati siku ya Sabato itakapoisha, ili kwamba tuuze ngano? Tutafanya kipimo kidogo na kuongeza bei, tukidanganya kwa mizani za udanganyifu.
saying, 'When will the new moon be gone, that we may sell grain? And the Sabbath, that we may market wheat, making the ephah small, and the shekel large, and dealing falsely with balances of deceit;
6 Hivi ndivyo ambavyo tunaweza kuuza ngano mbaya, kununua fukara kwa fedha, na masikini kwa jozi moja ya kubadhi.”
that we may buy the poor for silver, and the needy for a pair of shoes, and sell the sweepings with the wheat?'"
7 Yahwe ameapa kwa fahari ya Yakobo, “Hakika sintoweza kusahau kazi zao hata moja.”
Jehovah has sworn by the pride of Jacob, "Surely I will never forget any of their works.
8 Je nchi haitatetemeka kwa hili, na kila mmoja aishiye kuombolezea? Yote hayo yatainuka kama Mto Naili, nayo itataabika juu na kupwa tena, kama mto wa Misri.
Won't the land tremble for this, and everyone mourn who dwells in it? Yes, it will rise up wholly like the River; and it will be stirred up and sink again, like the River of Egypt.
9 “Itakuja siku ambayo -huu ndio usemi wa Bwana Yahwe- kwamba nitafanya jua litue wakati wa mchana, na nitaiweka giza dunia wakati wa mchana.
It will happen in that day," says Jehovah, "that I will cause the sun to go down at noon, and I will darken the earth in the clear day.
10 Nitazigeuza sikukuu zenu kuwa maombolezo na nyimbo zenu zote kuwa masikitiko. Nitawafanya wote kuvaa nguo za magunia na kipara juu ya kila kichwa. Nitayafanya haya kama maombolezo kwa mwana pekee, na siku ya uchungu mwisho wake.
I will turn your feasts into mourning, and all your songs into lamentation; and I will make you wear sackcloth on all your bodies, and baldness on every head. I will make it like the mourning for an only son, and its end like a bitter day.
11 Tazama, siku zinakuja -asema Bwana Yahwe- wakati nitakapoleta njaa katika nchi, sio njaa ya mkate, wala kiu ya maji, ila kusikia maneno ya Yahwe.
Look, the days come," says Jehovah, "that I will send a famine in the land, not a famine of bread, nor a thirst for water, but of hearing the word of Jehovah.
12 watatangatanga kutoka bahari hata bahari; watakimbia kutoka kaskazini kwenda magharibi kutafuta neno la Yahwe, lakini hawatalipata.
They will wander from sea to sea, and from the north even to the east; they will run back and forth to seek the word of Jehovah, and will not find it.
13 Katika siku hiyo wanawali wazuri na wavulana watazimia kutokana na njaa.
In that day the beautiful virgins and the young men will faint for thirst.
14 Wale waapao kwa dhambi ya Samaria wataanguka na hawatainuka tena.”
Those who swear by the sin of Samaria, and say, 'As your god, Dan, lives;' and, 'As the way of Beersheba lives;' they will fall, and never rise up again."

< Amosi 8 >