< Amosi 1 >

1 Haya ni mambo yanayoihusu Israeli ambayo Amosi, mmoja wa wachungaji katika Tekoa, aliyapokea katika ufunuo. Alipokea haya mambo katika siku za Uzia mfalme wa Yuda, na pia katika siku za Yeroboamu mwana wa Yoashi mfalme wa Israeli, miaka miwili kabla ya tetemeko la aridhi.
The words of Amos, who was among the herdsmen of Tekoa, which he saw concerning Israel in the days of Uzziah king of Judah, and in the days of Jeroboam the son of Joash king of Israel, two years before the earthquake.
2 Alisema, “Yahwe atanguruma kutoka Sayuni; atainua sauti yake kutoka Yerusalemu. Malisho ya wachungaji yatanyamaza kimya; kilele cha Karmeli kitanyauka.”
He said: "The LORD will roar from Zion, and utter his voice from Jerusalem; and the pastures of the shepherds will mourn, and the top of Carmel will wither."
3 Hivi ndivyo Yahwe asemavyo: “Kwa dhambi tatu za Damaskasi, hata kwa nne, sintobadilisha adhabu, kwa sababu wameipura Gileadi kwa vyombo vya chuma.
Thus says the LORD: "For three transgressions of Damascus, yes, for four, I will not turn away its punishment; because they have threshed the pregnant women of Gilead with threshing instruments of iron;
4 Nitapeleka moto kwenye nyumba ya Hazaeli, na utaiteketeza ngome za Ben Hadadi.
but I will send a fire into the house of Hazael, and it will devour the palaces of Ben Hadad.
5 Nitazivunja komeo za Damaskasi na kumkatilia mbali mtu ambaye aishiye katika Biqati Aveni, na pia yule mtu ashikaye fimbo ya kifalme katika Beth Edeni. Na watu wa shamu watakwenda utumwani hata Kiri,” asema Yahwe.
I will break the bar of Damascus, and cut off the inhabitant from the Valley of Wickedness, and him who holds the scepter from Beth Eden; and the people of Aram shall go into captivity to Kir," says the LORD.
6 Hivi ndivyo Yahwe asemavyo: “Kwa dhambi tatu za Gaza, hata nne, sintobadilisha adhabu, kwa sababu waliwachukua mateka watu wote, kuwaweka juu ya mkono wa Edomu.
Thus says the LORD: "For three transgressions of Gaza, yes, for four, I will not turn away its punishment; because they carried away captive the whole community, to deliver them up to Edom;
7 Nitatuma moto kwenye kuta za Gaza, na kuziteketeza ngome zake.
but I will send a fire on the wall of Gaza, and it will devour its palaces.
8 Nitamkatilia mbali yule mtu aishiye katika Ashdodi na mtu ashikaye fimbo ya kifalme kutoka Ashkeloni. Nitaugeuza mkono wangu dhidi ya Ekroni, na mabaki ya Wafilisti wataangamia,” asema Bwana Yahwe.
I will cut off the inhabitant from Ashdod, and him who holds the scepter from Ashkelon; and I will turn my hand against Ekron; and the remnant of the Philistines will perish," says the LORD.
9 Hivi ndivyo Yhawe asemavyo: “Kwa dhambi tatu za Tiro, hata kwa nne, sintobadili adhabu, kwa sababu waliwapelekea watu wote wa Edomu, na wamevunja agano lao la undugu.
Thus says the LORD: "For three transgressions of Tyre, yes, for four, I will not turn away its punishment; because they delivered up the whole community to Edom, and did not remember the brotherly covenant;
10 Nitapeleka moto kwenye kuta za Tiro, nao utaziteketeza ngome zake.”
but I will send a fire on the wall of Tyre, and it will devour its palaces."
11 Hivi ndivyo Yahwe asemavyo, “Kwa dhambi tatu za Edomu, hata kwa nne, sintobadilisha adhabu, kwa sababu alimfuatilia ndugu yake kwa upanga na kutupilia mbali huruma zote. Hasira yake ikaendelea kuwa kali, na ghadhabu yake ikabaki milele.
Thus says the LORD: "For three transgressions of Edom, yes, for four, I will not turn away its punishment; because he pursued his brother with the sword, and cast off all pity, and his anger raged continually, and he kept his wrath forever;
12 Nitapeleka moto juu ya Temani, na utaziteketeza nyumb a za kifalme za Bozra.”
but I will send a fire on Teman, and it will devour the palaces of Bozrah."
13 Hivi ndivyo Yahwe asemavyo, “Kwa dhambi tatu za watu wa Amoni, hata kwa nne, sintobadilisha adhabu, kwa sababu wamewapasua wanawake wa Gileadi wenye mimba, ili waweze kupanua mipaka yao.
Thus says the LORD: "For three transgressions of the people of Ammon, yes, for four, I will not turn away its punishment; because they have ripped open the pregnant women of Gilead, that they may enlarge their border.
14 Nitawasha moto katika kuta za Raba, nao utaziteketeza nyumba za kifalme, pamoja na kupiga kelele katika siku ya vita, pamoja na dhoruba katika siku ya kimbunga.
But I will kindle a fire in the wall of Rabbah, and it will devour its palaces, with shouting in the day of battle, with a storm in the day of the whirlwind;
15 Mfalme wao ataenda utumwani, yeye na maafisa wake pamoja,” asema Yahwe.
and their king will go into captivity, he and his officials together," says the LORD.

< Amosi 1 >