< Amosi 1 >

1 Haya ni mambo yanayoihusu Israeli ambayo Amosi, mmoja wa wachungaji katika Tekoa, aliyapokea katika ufunuo. Alipokea haya mambo katika siku za Uzia mfalme wa Yuda, na pia katika siku za Yeroboamu mwana wa Yoashi mfalme wa Israeli, miaka miwili kabla ya tetemeko la aridhi.
The words of Amos, who was among the herdsmen of Tekoa, which he saw concerning Israel in the days of Uzziah king of Judah, and in the days of Jeroboam the son of Joash king of Israel, two years before the earthquake.
2 Alisema, “Yahwe atanguruma kutoka Sayuni; atainua sauti yake kutoka Yerusalemu. Malisho ya wachungaji yatanyamaza kimya; kilele cha Karmeli kitanyauka.”
And he said, Jehovah will roar from Zion, and utter his voice from Jerusalem, and the pastures of the shepherds shall mourn, and the top of Carmel shall wither.
3 Hivi ndivyo Yahwe asemavyo: “Kwa dhambi tatu za Damaskasi, hata kwa nne, sintobadilisha adhabu, kwa sababu wameipura Gileadi kwa vyombo vya chuma.
Thus says Jehovah: For three transgressions of Damascus, yea, for four, I will not turn away the punishment of it, because they have threshed Gilead with threshing instruments of iron.
4 Nitapeleka moto kwenye nyumba ya Hazaeli, na utaiteketeza ngome za Ben Hadadi.
But I will send a fire into the house of Hazael, and it shall devour the palaces of Ben-hadad.
5 Nitazivunja komeo za Damaskasi na kumkatilia mbali mtu ambaye aishiye katika Biqati Aveni, na pia yule mtu ashikaye fimbo ya kifalme katika Beth Edeni. Na watu wa shamu watakwenda utumwani hata Kiri,” asema Yahwe.
And I will break the bar of Damascus, and cut off the inhabitant from the valley of Aven, and he who holds the scepter from the house of Eden, and the people of Syria shall go into captivity to Kir, says Jehovah.
6 Hivi ndivyo Yahwe asemavyo: “Kwa dhambi tatu za Gaza, hata nne, sintobadilisha adhabu, kwa sababu waliwachukua mateka watu wote, kuwaweka juu ya mkono wa Edomu.
Thus says Jehovah: For three transgressions of Gaza, yea, for four, I will not turn away the punishment of it, because they carried away captive the whole people, to deliver them up to Edom.
7 Nitatuma moto kwenye kuta za Gaza, na kuziteketeza ngome zake.
But I will send a fire on the wall of Gaza, and it shall devour the palaces of it.
8 Nitamkatilia mbali yule mtu aishiye katika Ashdodi na mtu ashikaye fimbo ya kifalme kutoka Ashkeloni. Nitaugeuza mkono wangu dhidi ya Ekroni, na mabaki ya Wafilisti wataangamia,” asema Bwana Yahwe.
And I will cut off the inhabitant from Ashdod, and him who holds the scepter from Ashkelon. And I will turn my hand against Ekron, and the remnant of the Philistines shall perish, says the lord Jehovah.
9 Hivi ndivyo Yhawe asemavyo: “Kwa dhambi tatu za Tiro, hata kwa nne, sintobadili adhabu, kwa sababu waliwapelekea watu wote wa Edomu, na wamevunja agano lao la undugu.
Thus says Jehovah: For three transgressions of Tyre, yea, for four, I will not turn away the punishment of it, because they delivered up the whole people to Edom, and did not remember the brotherly covenant.
10 Nitapeleka moto kwenye kuta za Tiro, nao utaziteketeza ngome zake.”
But I will send a fire on the wall of Tyre, and it shall devour the palaces of it.
11 Hivi ndivyo Yahwe asemavyo, “Kwa dhambi tatu za Edomu, hata kwa nne, sintobadilisha adhabu, kwa sababu alimfuatilia ndugu yake kwa upanga na kutupilia mbali huruma zote. Hasira yake ikaendelea kuwa kali, na ghadhabu yake ikabaki milele.
Thus says Jehovah: For three transgressions of Edom, yea, for four, I will not turn away the punishment of it, because he pursued his brother with the sword, and cast off all pity. And his anger tore perpetually, and he kept his wrath forever.
12 Nitapeleka moto juu ya Temani, na utaziteketeza nyumb a za kifalme za Bozra.”
But I will send a fire upon Teman, and it shall devour the palaces of Bozrah.
13 Hivi ndivyo Yahwe asemavyo, “Kwa dhambi tatu za watu wa Amoni, hata kwa nne, sintobadilisha adhabu, kwa sababu wamewapasua wanawake wa Gileadi wenye mimba, ili waweze kupanua mipaka yao.
Thus says Jehovah: For three transgressions of the sons of Ammon, yea, for four, I will not turn away the punishment of it, because they have ripped up the women with child of Gilead, that they may enlarge their border.
14 Nitawasha moto katika kuta za Raba, nao utaziteketeza nyumba za kifalme, pamoja na kupiga kelele katika siku ya vita, pamoja na dhoruba katika siku ya kimbunga.
But I will kindle a fire in the wall of Rabbah, and it shall devour the palaces of it, with shouting in the day of battle, with a tempest in the day of the whirlwind.
15 Mfalme wao ataenda utumwani, yeye na maafisa wake pamoja,” asema Yahwe.
And their king shall go into captivity, he and his rulers together, says Jehovah.

< Amosi 1 >