< Matendo 21 >

1 Wakati tulipokua tumeachana nao, na tunasafiri baharini, tukafika moja kwa moja kwenye mji wa Kosi, na kesho yake tukafika mji wa Rodo, na kutoka huko tukafika mji wa Patara.
Et quand, nous étant arrachés d’auprès d’eux, nous avons mis à la voile, voguant en droite ligne, nous sommes arrivés à Cos, et le jour suivant à Rhodes, et de là à Patara.
2 Tulipopata meli inayovuka kwenda Foinike, tulipanda tukasafiri.
Et ayant trouvé un navire qui passait en Phénicie, nous y sommes montés et avons mis à la voile.
3 Tulipofika mbele ya kisiwa cha Kipro, tukaiacha upande wa kushoto, tukasafiri hadi Siria, tukaweka nanga katika mji wa Tiro, kwa sababu huko ndiko meli ilikuwa ipakuliwe shehena yake.
Et ayant découvert Chypre, et l’ayant laissée à gauche, nous avons vogué vers la Syrie et nous avons abordé à Tyr; car c’était là que le navire devait décharger sa cargaison.
4 Baada ya kuwaona wanafunzi, tukakaa huko siku saba. Wanafunzi hawa wakamwambia Paulo kupitia kwa Roho kwamba yeye asikanyage Yerusalemu.
Et ayant trouvé les disciples, nous y sommes demeurés sept jours. Et ils dirent à Paul, par l’Esprit, de ne pas monter à Jérusalem.
5 Hata tulipotimiza siku zile, sisi tukaondoka tukaenda zetu. Wote pamoja, na wanawake zao na watoto wao, walitusindikiza katika njia zetu hadi tulipotoka nje ya mji. Kisha tukapiga magoti pwani, tukaomba, tukaagana kila mmoja.
Mais ayant accompli ces jours, nous sommes partis et nous nous sommes mis en chemin; et tous nous accompagnèrent avec femmes et enfants jusque hors de la ville; et nous étant mis à genoux sur le rivage, nous avons prié.
6 Tukapanda meli, huku nao wakarudi nyumbani kwao tena.
Et après nous être embrassés les uns les autres, nous sommes montés sur le navire; et ils s’en retournèrent chez eux.
7 Hata tulipomaliza safari yetu kutoka Tiro, tukafika Tolemai. Pale tulisalimia ndugu, na kukakaa nao kwa siku moja.
Et quant à nous, achevant notre navigation, nous sommes arrivés de Tyr à Ptolémaïs; et ayant salué les frères, nous sommes demeurés un jour auprès d’eux.
8 Kesho yake tuliondoka tukaenda Kaisaria. Sisi tukaingia nyumbani mwa Filipo, mhubiri wa injili, aliyekuwa mmoja wa wale saba, nasi tukakaa pamoja naye.
Et le lendemain, étant partis, nous sommes venus à Césarée; et étant entrés dans la maison de Philippe l’évangéliste qui était [l’un] des sept, nous sommes demeurés chez lui.
9 Mtu huyu alikuwa na mabinti wanne mabikira ambao walitabiri.
Or il avait quatre filles vierges qui prophétisaient.
10 Baada ya kukaa huko kwa siku kadhaa, akashuka kutoka Uyahudi nabii mmoja aitwaye Agabo.
Et comme nous nous sommes arrêtés là plusieurs jours, un prophète nommé Agabus descendit de la Judée;
11 Yeye alikuja kwetu na akautwaa mkanda wa Paulo. kwa huo alijifunga miguu na mikono yake mwenyewe na kusema, “Roho Mtakatifu asema hivi,” “Wayahudi wa Yerusalemu watamfunga mtu anayemiliki mkanda huu, nao watamkabidhi mikononi mwa watu wa mataifa.”
et étant venu auprès de nous et ayant pris la ceinture de Paul, et s’étant lié les pieds et les mains, il dit: L’Esprit Saint dit ces choses: L’homme à qui est cette ceinture, les Juifs à Jérusalem le lieront ainsi et le livreront entre les mains des nations.
12 Tuliposikia mambo hayo, sisi na watu waliokuwa wakiishi mahali pale tulimsihi Paulo asipande kwende Yerusalemu.
Et quand nous avons entendu ces choses, nous et ceux qui étaient du lieu, nous l’avons supplié de ne pas monter à Jérusalem.
13 Ndipo Paulo alijibu, “Mnafanya nini, mnalia na kunivunja moyo wangu? Kwa maana niko tayari, siyo tu kufungwa, lakini pia kufia huko Yerusalemu kwa ajili ya jina la Bwana Yesu.”
Mais Paul répondit: Que faites-vous en pleurant et en brisant mon cœur? Car pour moi, je suis prêt, non seulement à être lié, mais encore à mourir à Jérusalem pour le nom du seigneur Jésus.
14 Kwa vile Paulo hakutaka kushawishiwa, tuliacha na kusema, “Basi mapenzi ya Bwana yafanyike.”
Et comme il ne se laissait pas persuader, nous nous sommes tus, disant: La volonté du Seigneur soit faite!
15 Baada ya siku hizi, tulichukua mifuko yetu na tukapanda Yerusalemu.
Et après ces jours, ayant rassemblé nos effets, nous sommes montés à Jérusalem.
16 Baadhi ya wanafunzi kutoka Kaisaria pia walifuatana nasi. Wakamleta mtu mmoja aitwaye Mnasoni, mtu wa Kipro, mwanafunzi wa zamani, ambaye tulikaa naye.
Et quelques-uns aussi des disciples de Césarée vinrent avec nous, amenant un certain Mnason, Cypriote, un ancien disciple, chez qui nous devions loger.
17 Tulipofika Yerusalemu, ndugu walitukaribisha kwa furaha.
Et quand nous sommes arrivés à Jérusalem, les frères nous reçurent avec joie.
18 Kesho yake Paulo alienda pamoja nasi kwa Yakobo, na wazee wote walikuwepo.
Et, le jour suivant, Paul entra avec nous chez Jacques, et tous les anciens y vinrent.
19 Baada ya kuwasalimu, aliwapa taarifa moja baada ya nyingine ya mambo ambayo Mungu aliyotenda miongoni mwa mataifa kwa kupitia huduma yake.
Et après qu’il les eut embrassés, il raconta une à une les choses que Dieu avait faites parmi les nations par son service.
20 Wakati waliposikia hayo, wakamsifu Mungu, na wakamwambia, “Unaona, ndugu, kuna maelfu wangapi wameamini miongoni mwa Wayahudi. Wao wote wana nia ya kushika sheria.
Et eux, l’ayant entendu, glorifièrent Dieu et dirent à Paul: Tu vois, frère, combien il y a de milliers de Juifs qui ont cru; et ils sont tous zélés pour la loi.
21 Wameambiwa kuhusu wewe, kwamba unafundisha Wayahudi wanaoishi kati ya mataifa kuachana na Musa, na kwamba unawaambia wasiwatahiri watoto wao, na wasifuate desturi za zamani.
Or ils ont entendu dire de toi, que tu enseignes à tous les Juifs qui sont parmi les nations de renoncer à Moïse, disant qu’ils ne doivent pas circoncire leurs enfants, ni vivre selon les coutumes.
22 Tunapaswa tufanye nini? Bila shaka watasikia kwamba wewe umekuja.
Qu’est-ce donc? Il faut absolument que la multitude s’assemble, car ils entendront dire que tu es arrivé.
23 Hivyo fanya kile sisi tunachokuambia sasa: tunao watu wanne ambao wameweka nadhiri.
Fais donc ce que nous te disons: Nous avons quatre hommes qui ont fait un vœu;
24 Wachukue watu hawa na ujitakase mwenyewe pamoja nao, na uwalipie gharama zao, ili waweze kunyoa vichwa vyao. Hivyo kila mmoja apate kujua kwamba mambo waliyoambiwa kuhusu wewe ni ya uongo. Watajifunza kwamba wewe pia unafuata sheria.
prends-les et purifie-toi avec eux, et paie leur dépense, afin qu’ils se rasent la tête, et tous sauront que rien n’est [vrai] des choses qu’ils ont entendu dire de toi, mais que toi aussi, tu marches gardant la loi.
25 Lakini kwa habari za mataifa ambao wamekuwa waumini, tuliandika na kutoa maagizo kwamba wanapaswa kujiepusha na vitu vilivyotolewa dhabihu kwa sanamu, na damu, kutokana na kile kilichonyongwa, na wajiepushe na uasherati.”
Mais à l’égard de ceux des nations qui ont cru, nous [en] avons écrit, ayant décidé qu’ils n’ont rien de semblable à observer, si ce n’est qu’ils se gardent et de ce qui est sacrifié aux idoles, et du sang, et de ce qui est étouffé, et de la fornication.
26 Ndipo, Paulo aliwatwaa wanaume, na siku ya pili, akajitakasa mwenyewe pamoja nao, akaingia Hekaluni, kutangaza kipindi cha siku za kujitakasa, hadi sadaka itolewa kwa ajili ya kila mmoja wao.
Alors Paul, ayant pris les hommes avec lui, et, le jour suivant, s’étant purifié, entra avec eux au temple, annonçant quand seraient accomplis les jours de leur purification, l’époque à laquelle l’offrande aurait été présentée pour chacun d’eux.
27 Siku hizo saba zilipokaribia kumalizika, baadhi ya Wayahudi kutoka Asia wakamuona Paulo Hekaluni, na makutano wakakasirika, na wakamnyoshea mikono.
Et comme les sept jours allaient s’accomplir, les Juifs d’Asie l’ayant vu dans le temple, soulevèrent toute la foule et mirent les mains sur lui,
28 Walikuwa wanapiga kelele, “Watu wa Israeli, tusaidieni. Huyu ni yule mtu anayewafundisha watu kila mahali mambo ambayo ni kinyume na watu, sheria, na mahali hapa. Pia amewaleta Wayunani katika Hekalu na kupanajisi mahali hapa patakatifu.”
s’écriant: Hommes israélites, aidez-nous! C’est ici l’homme qui partout enseigne tout le monde contre le peuple, et la loi, et ce lieu; et qui de plus a aussi amené des Grecs dans le temple et a profané ce saint lieu.
29 Kwa kuwa mwanzoni walikuwa wamemwona Trofimo Muefeso akiwa pamoja naye mjini, nao walidhani kwamba Paulo alimleta hekaluni.
Car ils avaient vu auparavant dans la ville Trophime l’Éphésien avec lui, et ils croyaient que Paul l’avait amené dans le temple.
30 Mji wote ulikuwa na taharuki, na watu wakakimbia pamoja na kumkamata Paulo. Wakamtoa nje ya Hekalu, na milango mara ikafungwa.
Et toute la ville fut en émoi, et il se fit un rassemblement du peuple; et ayant saisi Paul, ils le traînèrent hors du temple; et aussitôt les portes furent fermées.
31 Walipokuwa wakijaribu kumuua, habari zilimfikia mkuu wa jeshi la walinzi kuwa Yerusalemu yote ilikuwa imejaa ghasia.
Et comme ils cherchaient à le tuer, le bruit vint au chiliarque de la cohorte, que tout Jérusalem était en confusion;
32 Mara hiyo akawachukua askari na jemadari akaukimbilia umati. Wakati Watu walipomwona mkuu wa jeshi na askari, wakaacha kumpiga Paulo.
et aussitôt il prit des soldats et des centurions, et courut à eux; mais eux, voyant le chiliarque et les soldats, cessèrent de battre Paul.
33 Kisha mkuu wa jeshi alimkaribia na akamshika Paulo, na akaamuru afungwe minyororo miwili. Akamuuliza yeye ni nani na amefanya nini.
Alors le chiliarque s’étant approché, se saisit de lui et donna l’ordre de le lier de deux chaînes, et demanda qui il était et ce qu’il avait fait.
34 Baadhi ya watu kwenye umati walikuwa wanapayuka kitu hiki na wengine kingine. Kwa kuwa jemadari hakuweza kuwaambia chochote kwa sababu ya zile kelele, akaamuru Paulo aletwe ndani ya ngome.
Mais les uns criaient une chose, les autres une autre, dans la foule; et n’en pouvant apprendre quelque chose de certain, à cause du tumulte, il donna ordre que Paul soit mené dans la forteresse.
35 Basi alipofika kwenye ngazi, akachukuliwa na askari kwa sababu ya ghasia za umati.
Et quand il fut sur les degrés, il arriva qu’il fut porté par les soldats à cause de la violence de la foule;
36 Maana umati wa watu walimfuata na waliendelea kupiga kelele, “Mwondoeni huyu!”
car la multitude du peuple suivait, en criant: Ôte-le!
37 Paulo alipokuwa analetwa ndani ya ngome, alimwambia mkuu wa jeshi, “Naweza kukwambia kitu?” Yule mkuu wa jeshi akasema, “Je unaongea Kiyunani?
Et comme on allait faire entrer Paul dans la forteresse, il dit au chiliarque: M’est-il permis de te dire quelque chose? Et il dit: Tu sais le grec?
38 Je, wewe si yule Mmisri ambaye awali aliongoza uasi na alichukua magaidi elfu nne nyikani?”
N’es-tu donc pas l’Égyptien qui, ces jours passés, a excité une sédition et emmené au désert les 4 000 hommes des assassins?
39 Paulo akasema, “Mimi ni Myahudi, kutoka mji wa Tarso ya Kilikia. Mimi ni raia wa mji maarufu. Nawaomba, mniruhusu nizungumze na watu.”
Et Paul dit: Je suis Juif, de Tarse, citoyen d’une ville de la Cilicie qui n’est pas sans renom; je te prie, permets-moi de parler au peuple.
40 Wakati jemadari alipompa ruhusa, Paulo akasimama penye ngazi na akatoa ishara kwa watu kwa mkono wake. Wakati kulipokuwa na ukimya sana, akaongea nao kwa Kihebrania. Akasema,
Et quand il le lui eut permis, Paul, se tenant sur les degrés, fit signe de la main au peuple, et un grand silence s’étant fait, il leur parla en langue hébraïque, disant:

< Matendo 21 >