< 2 Timotheo 4 >

1 Ninakupa agizo hili lenye uzito mbele za Mungu na Kristo Yesu, atakaye wahukumu walio hai na wafu, na kwa sababu ya kufunuliwa kwake na Ufalme wake:
Je vous prescris donc, devant Dieu et devant le Seigneur Jésus-Christ, qui jugera les vivants et les morts à son avènement et dans son royaume:
2 Hubiri Neno. Uwe tayari kwa wakati ufaao na usiofaa. Waambie watu dhambi zao, kemea, himiza, kwa uvumilivu wote na mafundisho.
prêchez la parole; soyez pressants à temps et à contretemps; reprenez, réprimandez, exhortez, avec toute la patience et l'instruction voulues.
3 Kwa maana wakati utakuja ambao watu hawatachukuliana na mafundisho ya kweli. Badala yake, watajitafutia walimu wa kufundisha kulingana na tamaa zao. kwa njia hii masikio yao yatakuwa yametekenywa.
Car le temps viendra où les hommes n'écouteront pas la saine doctrine, mais où, ayant la démangeaison d'entendre, ils s'amasseront des docteurs selon leurs propres désirs,
4 Wataacha kusikiliza mafundisho ya kweli, na kugeukia hadithi.
détourneront l'oreille de la vérité et se tourneront vers les fables.
5 Lakini wewe uwe mwaminifu katika mambo yote, vumilia magumu, fanya kazi ya mwinjilisti; timiza huduma yako.
Mais vous, soyez sobres en toutes choses, souffrez des privations, faites l'œuvre d'un évangéliste, et accomplissez votre ministère.
6 Kwa maana mimi tayari nimekwisha kumiminwa. Muda wa kuondoka kwangu umewadia.
Car je suis déjà offert, et le moment de mon départ est arrivé.
7 Nimeshindana katika haki, Mwendo nimeumaliza, Imani nimeilinda.
J'ai combattu le bon combat. J'ai achevé le parcours. J'ai gardé la foi.
8 Taji ya haki imewekwa kwa ajili yangu, ambayo Bwana, anayehukumu kwa haki, atanipa siku ile. Na siyo kwangu tu bali pia kwa wote wanaongojea kwa shauku kuonekana kwake.
Dès maintenant, je me réserve la couronne de justice que le Seigneur, le juste juge, me donnera en ce jour-là, et non seulement à moi, mais aussi à tous ceux qui ont aimé son apparition.
9 Jitahidi kuja kwagu haraka.
Soyez diligents pour venir bientôt me voir,
10 Kwa kuwa Dema ameniacha. Anaupenda ulimwengu wa sasa na amekwenda Thesalonike, Kreseni alikwenda Galatia, na Tito alikwenda Dalmatia. (aiōn g165)
car Démas m'a quitté, ayant aimé le monde présent, et il est allé à Thessalonique; Crescens, en Galatie; et Tite, en Dalmatie. (aiōn g165)
11 Luka tu ndiye yuko pamoja nami. Umchukue Marko uje naye kwani yeye ni muhimu kwangu katika huduma.
Luc seul est avec moi. Prends Marc et amène-le avec toi, car il m'est utile pour le service.
12 Nimemtuma Tikiko Efeso.
Mais j'ai envoyé Tychique à Éphèse.
13 Lile joho ambalo nililiacha Troa kwa Karpo, utakapokuja lilete, pamoja na vile vitabu hasa vile vya ngozi.
Apporte à Carpus, quand tu viendras, le manteau que j'ai laissé à Troas, et les livres, surtout les parchemins.
14 Alekizanda mfua chuma alinitendea maovu mengi. Bwana atamlipa kulingana na matendo yake.
Alexandre, le dinandier, m'a fait beaucoup de mal. Le Seigneur lui rendra selon ses actes.
15 Nawe pia jihadhari naye, kwani aliyapinga sana maneno yetu.
Méfie-toi de lui, car il s'est beaucoup opposé à nos paroles.
16 Katika utetezi wangu wa kwanza, hakuna mtu yeyote aliyesimama pamoja nami, badala yake, kila mmoja aliniacha. Mungu asiwahesabie hatia.
Lors de ma première défense, personne n'est venu me secourir, mais tous m'ont abandonné. Que cela ne leur soit pas reproché.
17 Lakini Bwana alisimama pamoja nami, akanitia nguvu ili kwamba kupitia kwangu, neno linenwe kwa ukamilifu na mataifa wapate kusikia. Niliokolewa katika kinywa cha Simba.
Mais le Seigneur s'est tenu à mes côtés et m'a fortifié, afin que, par moi, le message soit pleinement proclamé et que tous les païens l'entendent. C'est ainsi que j'ai été délivré de la gueule du lion.
18 Bwana ataniepusha na matendo yote maovu na kuniokoa kwa ajili ya ufalme wake wa mbinguni. Utukufu uwe kwake milele na milele. Amen (aiōn g165)
Et le Seigneur me délivrera de toute œuvre mauvaise et me conservera pour son Royaume céleste. A lui soit la gloire pour les siècles des siècles. Amen. (aiōn g165)
19 Msalimie Priska, Akila na nyumba ya Onesiforo.
Saluez Prisca et Aquila, et la maison d'Onésiphore.
20 Erasto alibaki huko Korintho, lakini Trifimo nilimuacha Mileto akiwa mgonjwa.
Éraste est resté à Corinthe, mais j'ai laissé Trophime malade à Milet.
21 Fanya hima uje kabla ya kipindi cha baridi. Eubulo anakusalimu, pia Pude, Lino, Claudia na ndugu wote.
Aie soin de venir avant l'hiver. Eubulus te salue, ainsi que Pudens, Linus, Claudia, et tous les frères.
22 Mungu awe pamoja na roho yako, Neema iwe nawe.
Le Seigneur Jésus-Christ soit avec votre esprit. Que la grâce soit avec vous. Amen.

< 2 Timotheo 4 >