< 2 Samweli 23 >

1 Haya ni maneno ya mwisho ya Daudi-Daudi mwana wa Yese, mtu aliyeheshimiwa sana, aliyetiwa mafuta na Mungu wa Yakobo, mwandishi mzuri wa zaburi wa Israeli.
Estas son las últimas palabras de David: David, el hijo de Isaí declara: Así dice el hombre que fue exaltado, El ungido del ʼElohim de Jacob, El dulce salmista de Israel:
2 “Roho ya Yahwe alisema nami, na neno lake lilikuwa ulimini mwangu.
El Espíritu de Yavé habla por medio de mí Y su Palabra está en mi boca.
3 Mungu wa Israeli alinena, Mwamba wa Israeli aliniambia, “Atawalaye kwa haki juu yangu, atawalaye katika hofu ya Mungu.
Dice el ʼElohim de Israel, Me habló la Roca de Israel, El que gobierna a los hombres con justicia, El que gobierna con el temor de ʼElohim.
4 Atakuwa kama nuru ya asubuhi jua linapochomoza, asubuhi isiyo na mawingu, wakati mche mwororo unapochipua kutoka ardhini kupitia mwangaza wa mng'ao wa jua baada ya mvua.
Es como la luz de la aurora cuando sale el sol, Como el resplandor de una mañana sin nubes, Como la lluvia que hace brotar la hierba de la tierra.
5 Hakika, je familia yangu haiko hivi mbele za Mungu? Je hajafanya nami agano la milele, taratibu la uhakika kwa kila njia? Je yeye haongezi wokovu wangu na kutimiza kila hitaji langu?
No es así mi casa hacia ʼElohim, Sin embargo, Él hizo conmigo un Pacto eterno, Ordenado en todo y será cumplido, Aunque aún no hace florecer toda mi salvación y mi deseo.
6 Lakini yasiyofaa yote yatakuwa kama miiba na kutupwa mbali, kwa maana haiwezekani kukusanywa kwa mikono.
Pero todos los perversos serán como espinos Que se tiran y nadie recoge,
7 Ayagusaye ni lazima atumie chombo cha chuma au au fumo la mkuki. Ni lazima yachomwe mahali yalipo.
Nadie los tocará, sino con un hierro o con un asta de lanza, Y con fuego que los queme por completo en su lugar.
8 Haya ni majina ya askari wa Daudi: Yashobeamu Mhakmoni alikuwa kiongozi wa mashujaa. Aliua watu mia nne wakati mmoja.
Estos son los nombres de los valientes que David tuvo: Joseb-basebet el tacmonita, principal de los tres capitanes, quien era llamado Adino el eznita, quien mató a 800 hombres en una ocasión.
9 Baada yake alikuwa Elieza mwana wa Dodo, mwana wa mwahohi, mmoja wa mashujaa watatu wa Daudi. Alikuwepo walipowashinda Wafilisti waliokuwa wamekusanyika kwa vita, na wakati watu wa Israeli walipokuwa wamekimbia.
Después de él estaba Eleazar, hijo de Dodo, hijo de Ahohi, uno de los tres capitanes que estaban con David cuando desafiaron a los filisteos que estaban reunidos para la batalla, aunque los hombres de Israel se retiraron de allí.
10 Elieza akasimama na kuwapiga Wafilisti mpaka mkono wake ukachoka, mpaka mkono wake ukang'ang'ania mpini wa upanga wake. Siku hiyo Yahwe akatoa ushindi mkuu. Jeshi likarejea kwa ajili ya kuteka tu nyara za waliouawa na Elieza.
[Eleazar] se levantó e hirió a los filisteos hasta que su mano se cansó y se quedó pegada a la espada. Aquel día Yavé dio una gran victoria, y el pueblo volvió tras él solo para tomar el botín.
11 Baada yake alikuwa Shama mwana wa Agee, Mharari. Wafilisti wakajikusanya pamoja palipokuwa na shamba la dengu, na jeshi likawakimbia.
Después de él estaba Samá, hijo de Ajá, el hararita. Los filisteos se concentraron donde había una parcela de tierra sembrada con lentejas, y el pueblo huyó de los filisteos.
12 Lakini Shama akasimama katikati ya shamba na kulitetea. Aliwauwa Wafilisti, na Yahwe akaleta ushindi mkuu.
Pero [Samá] se paró en medio de aquella parcela y la defendió. Derrotó a los filisteos, y Yavé dio una gran victoria.
13 Watatu kati ya askari thelathini walishuka kwa Daudi nyakati za mavuno, katika pango la Adulamu. Jeshi la Wafilisti lilikuwa limepiga kambi katika bonde la Mrefai.
También, en la época de la cosecha, hubo tres de los 30 principales que bajaron y fueron a David, a la cueva de Adulam, cuando una banda de filisteos acampaba en el valle de Refaim.
14 Wakati huo Daudi alikuwa katika ngome yake, pangoni, wakati Wafilisti walikuwa wanaimilk Bethlehemu.
David estaba entonces en el refugio, y la guarnición filistea estaba en Belén.
15 Daudi alitamani maji na akasema, “Kama ingekuwa mtu mmoja angenipa maji ya kunywa kutoka kisima kilichopo Bethlehemu, kisima kilichopo langoni!”
David tuvo un deseo y exclamó: ¡Quién me diera a beber agua del pozo de Belén, que está junto a la puerta!
16 Hivyo mashujaa hawa watatu wakapita kati ya jeshi la Wafilisti na kuchota maji katika kisima cha Bethlehemu, kilichopo langoni. Wakachukua maji na kuyaleta kwa Daudi, lakini yeye akakataa kuyanywa. Badala yake akayamwaga mbele za Yahwe.
Y los tres valientes irrumpieron en el campamento filisteo y sacaron agua del pozo, junto a la puerta de Belén, y se la llevaron a David. Pero él no quiso beberla, sino que la derramó como ofrenda a Yavé, y dijo:
17 Kisha akasema, “Iwe mbali nami, Yahwe, kwamba niyanywe haya. Je ninywe damu ya watu waliohatarisha maisha yao?” Hivyo akakataa kuyanywa. Haya ni mambo yaliyofanywa na mashujaa watatu.
¡Lejos esté de mí, oh Yavé, hacer esto! ¿Beberé yo la sangre de los varones que fueron con riesgo de sus vidas? Y no quiso beberla. Tales cosas hicieron estos tres valientes.
18 Abishai, nduguye Yoabu na mwana wa Seruya, alikuwa akida wa watatu. Alipigana kwa mkuki wake na watu mia tatu na akawauwa wote mara. Mara kwa mara alitajwa kati ya mashujaa watatu.
Y Abisai, hermano de Joab, hijo de Sarvia, era el principal de los 30. Éste blandió su lanza contra 300 que fueron traspasados, y tuvo renombre entre los tres.
19 Hakuwa maarufu kuliko wale watatu? Alifanywa akida wao. Lakini, umaarufu wake haukulingana na umaarufu wa wale mashujaa watatu.
[Abisai] fue el más renombrado de los 30 y fue su jefe, pero no fue incluido entre los tres.
20 Benaya kutoka Kabseeli mwana wa Yehoyada; alikuwa mtu hodari aliyefanya matendo makuu. Aliwauwa wana wawili wa Arieli wa Moabu. Pia alishuka shimoni na kuuwa simba wakati wa theruji.
Después, Benaía, hijo de Joiada, hijo de un hombre valiente de múltiples proezas, natural de Cabseel, mató a ambos hijos de Ariel de Moab. En un día de nieve, bajó y mató a un león dentro de un foso.
21 Na alimwua Mmisri aliyekuwa mtu mnene sana. Mmisri alikuwa na mkuki mkononi, lakini Benaya alipigana naye kwa fimbo tu. Aliuchukua mkuki mkononi mwa Mmisri na kisha kumwua nao.
También mató a un egipcio de enorme estatura. El egipcio llevaba una lanza en la mano. Benaía fue contra él con un cayado, arrebató la lanza de la mano del egipcio y lo mató con su propia lanza.
22 Benaya mwana wa Yehoyada alifanya matendo haya, naye alitajwa kati ya mashujaa watatu.
Benaía, hijo de Joiada, hizo esto y tuvo renombre entre los 30 valientes.
23 Alikuwa na heshima kuliko mashujaa thelathini kwa ujumla wao, lakini hakuwa na heshima kama wale mashujaa watatu. Hata hivyo Daudi alimweka kuwa mlinzi wake.
Fue distinguido entre los 30, pero no alcanzó a los tres. David lo puso al frente de su guardia personal.
24 Wafuatao ni wale watu thelathini: Asaheli nduguye Yoabu, Elhanani mwana wa Dodo kutoka Bethlehemu,
Asael, hermano de Joab, fue de los 30, así como Elhanán, hijo de Dodo, de Belén,
25 Shama Mharodi, Elika Mharodi,
Samá harodita, Elica harodita,
26 Helesi Mpeloni, Ira mwana wa Ikeshi Mtekoi,
Heles paltita, Ira, hijo de Iques, tecoíta,
27 Abi Ezeri Mwanathothi, Mebunai Mhushathi,
Abiezer anatotita, Mebunai husatita,
28 Salmoni Mhahoi, Maharai Mnetofathi;
Salmón ahohíta, Maharai netofatita,
29 Helebu mwana wa Baana, Mnetofathi, Itai mwana wa Rabai kutoka Gibea ya Wabenjamini,
Heleb, hijo de Baana, netofatita, Itai, hijo de Ribai, de Gabaa de los hijos de Benjamín,
30 Benaya Mpirathoni, Hidai wa mabonde ya Gaashi.
Benaía piratonita, Hidai, de los arroyos de Gaas,
31 Abieliboni Mwarbathi, Azmawethi Mbarhumi,
Abi-albón arbatita, Azmavet barhumita,
32 Eliaba Mshalboni, wana wa Yasheni, Yonathani mwana wa Shama Mharari;
Eliaba saalbonita, Jonatán, de los hijos de Jasén,
33 Ahiamu mwana wa Sharari Mharari,
Samá ararita, Ahíam, hijo de Sarar, ararita,
34 Elifeleti mwana wa Ahasbai Mmaakathi, Eliamu mwana wa Ahithofeli Mgiloni,
Elifelet, hijo de Ahasbai, hijo de Maaca, Eliam, hijo de Ahitofel, gilonita,
35 Hezro Mkarmeli, Parai Mwarbi,
Hezri carmelita, Paarai arbita,
36 Igali mwana wa Nathani kutoka Soba, Bani kutoka kabila la Gadi,
Igal, hijo de Natán, de Soba, Bani gadita,
37 Zeleki Mwamoni, Naharai Mbeerothi, mbeba silaha wa Yoabu mwana wa Seruya,
Selec amonita, Naharai beerotita, escudero de Joab, hijo de Sarvia,
38 Ira Mwithri, Garebu Mwithri,
Ira itrita, Gareb itrita,
39 Uria Mhiti - jumla yao thelathini na wanane.
y Urías heteo. Total: 37.

< 2 Samweli 23 >