< 2 Samweli 2 >

1 Ikawa baada ya haya Daudi akamuuliza Yahwe, “Je naweza kuupandia mmojawapo wa miji ya Yuda?” Yahweh akamjibu, “Panda.” Daudi akauliza, “Niuendee mji upi? Yahwe akajibu, “Hebroni”
And it was after thus and he enquired David by Yahweh - saying ¿ will I go up in one of [the] cities of Judah and he said Yahweh to him go up and he said David where? will I go up and he said Hebron towards.
2 Hivyo Daudi akakwea pamoja na wake zake wawili, Ahinoamu wa Yezreeli, na Abigaili wa Karmeli, mjane wa Nabali.
And he went up there David and also [the] two wives his Ahinoam the Jezreelite [woman] and Abigail [the] wife of Nabal the Carmelite.
3 Daudi akawaleta watu waliokuwa pamoja naye, na kila mmoja akaleta familia yake katika mji wa Hebroni walipoanza kuishi.
And men his who [were] with him he brought up David each man and household his and they dwelt in [the] cities of Hebron.
4 Kisha watu wa Yuda wakaja na kumtia Daudi mafuta kuwa mfalme juu ya nyumba ya Yuda. Wakamwambia Daudi, “Watu wa Yabeshi Gileadi wamemzika Sauli.”
And they came [the] people of Judah and they anointed there David to king over [the] house of Judah and people told to David saying [the] men of Jabesh Gilead who they buried Saul.
5 Hivyo Daudi akatuma wajumbe kwa watu wa Yabeshi Gileadi akawambia, “Mbarikiwe na Yahwe, kwa kuwa mmeonesha utiifu huu kwa bwana wenu Sauli mliyemzika.
And he sent David messengers to [the] people of Jabesh Gilead and he said to them [be] blessed you by Yahweh that you have done the loyalty this with lord your with Saul and you have buried him.
6 Sasa Yahwe awadhihirishie utiifu na uaminifu wa kiagano. Nami pia nitawaonesha wema kwa sababu ya yale mliyoyafanya.
And now may he do Yahweh with you covenant loyalty and faithfulness and also I I will do with you the good this that you have done the thing this.
7 Sasa basi, mikono yenu itiwe nguvu; mwe jasiri kwa maana Sauli bwana wenu amekufa, na nyumba yote ya Yuda imenitia mafuta niwe mfalime wao.
And now - let them be strong hands your and become sons of strength for he has died lord your Saul and also me they have anointed [the] house of Judah to king over them.
8 Lakini Abneri mwana wa Neri, mkuu wa jeshi la Sauli, akamchukuwa Ishboshethi mwana wa Sauli akamleta Mahanaimu.
And Abner [the] son of Ner [the] commander of [the] army which [belonged] to Saul he had taken Ish-bosheth [the] son of Saul and he had brought over him Mahanaim.
9 Akamfanya Ishboshethi mfalme juu ya Gileadi, Asheri, Yezreeli, Efraimu, Benjamini na juu ya Israeli yote.
And he made king him to Gilead and to the Ashurite[s] and to Jezreel and over Ephraim and over Benjamin and over Israel all of it.
10 Ishiboshethi mwana wa Sauli alikuwa na umri wa miaka arobaini alipoanza kutawala juu ya Israeli, akatawala miaka miwili. Lakini nyumba ya Yuda ikaambatana na Daudi.
[was] a son of Forty year[s] Ish-bosheth [the] son of Saul when became king he over Israel and two years he reigned only [the] house of Judah they were after David.
11 Muda ambao Daudi alikuwa mfalme juu ya nyumba ya Yuda huko Hebroni ni miaka saba na miezi sita.
And it was [the] number of the days which he was David king in Hebron over [the] house of Judah seven years and six months.
12 Abneri mwana wa Neri na watumishi wa Ishboshethi mwana wa Sauli walitoka Mahanaimu kwenda Gibeoni.
And he went out Abner [the] son of Ner and [the] servants of Ish-bosheth [the] son of Saul from Mahanaim Gibeon towards.
13 Yoabu mwana wa Seruya na watumishi wa Daudi wakatoka na kukutana nao katika bwawa la Gibeoni. Wakakaa pale, kundi moja upande huu wa bwawa na kundi lingine upande wa pili.
And Joab [the] son of Zeruiah and [the] servants of David they went out and they met them at [the] pool of Gibeon together and they sat down these [men] at the pool from this and these [men] at the pool from this.
14 Abneri akamwambia Yoabu, “haya, vijana na wainuke na kushindana mbele yetu.” Yoabu akajibu, “haya na wainuke.”
And he said Abner to Joab let them arise please the young men and let them play before us and he said Joab let them arise.
15 Ndipo vijana walipoinuka na kukutana, kumi na wawili kwa ajili ya Banjamini na Ishboshethi mwana wa Sauli, na kumi na wawili kutoka kwa watumishi wa Daudi.
And they arose and they passed by by number two plus ten for Benjamin and for Ish-bosheth [the] son of Saul and two plus ten from [the] servants of David.
16 Kila mtu akakamata kichwa cha adui yake na kupiga upanga wake katika ubavu wa adui yake, wakaanguka chini pamoja. Kwa hiyo mahali pale pakaitwa kwa Kiebrania, “Helkath Hazzurim,” yaani “konde la upanga,” lililopo Gibeoni.
And they took hold each - on [the] head of neighbor his and sword his [was] in [the] side of neighbor his and they fell together and someone called the place that Helkath Hazzurim which [is] in Gibeon.
17 Vita ikawa kali sana siku ile na Abneri na watu wa Israeli wakashindwa na watumishi wa Daudi.
And it was the battle severe up to muchness on the day that and he was defeated Abner and [the] men of Israel before [the] servants of David.
18 Wana watatu wa Seruya walikuwepo pale: Yoabu, Abishai na Asaheli.
And they were there three [the] sons of Zeruiah Joab and Abishai and Asahel and Asahel [was] swift on feet his like one of the gazelles which [are] in the open country.
19 Asaheli alikuwa mwepesi miguuni kama paa. Akamfuatilia Abneri kwa karibu bila kugeuka upande wowote.
And he pursued Asahel after Abner and not he turned aside to go to the right and to the left from after Abner.
20 Abneri akaangalia nyuma yake na kusema, “Ni wewe Asaheli?” Akajibu, “ni mimi.”
And he turned Abner behind him and he said ¿ you [is] this O Asahel and he said I.
21 Abneri akamwambia, “Geuka upande wako wa kuria au kushoto umshike mmojawapo wa vijana na kuchukua silaha yake.” Lakini Asaheli hakugeuka.
And he said to him Abner turn aside for yourself to right your or to left your and seize for yourself one from the young men and take for yourself spoils his and not he was willing Asahel to turn aside from after him.
22 Ndipo Abneri alipomwambia tena Asaheli, “Simama usinifuate. Kwa nini nikupige hata chini? Nitautazamaje uso wa Yoabu ndugu yako?”
And he repeated again Abner to say to Asahel turn aside for yourself from after me why? will I strike you [the] ground towards and how? will I lift up face my to Joab brother your.
23 Lakini Asaheli hakukubari kugeuka. na hivyo Abneri akamchoma kwa nchi ya mkuki wake, hata ukatokea upande wa pili. Asaheli akaanguka chini akafa. Hata ikawa kila mmoja aliyefika mahali pale Asaheli alipoanguka na kufa, alisimama hapo hapo.
And he refused to turn aside and he struck him Abner with [the] back end of the spear into the belly and it went out the spear from behind him and he fell there and he died (in place his *Qk) and it was every [one] who came to the place where he fell there Asahel and he died and they stood still.
24 Lakini Yoabu na Abishai wakamfuatilia Abneri. Wakati jua linazama walikuwa wamefika mlima wa Amma, uliopo karibu na Gia katika njia ielekeayo nyika ya Gibeoni.
And they pursued Joab and Abishai after Abner and the sun it set and they they came to [the] hill of Ammah which [is] on [the] face of Giah [the] way of [the] wilderness of Gibeon.
25 Wabenjamini wakajikusanya nyuma ya Abneri na kusimama juu ya kilima.
And they gathered together [the] descendants of Benjamin behind Abner and they became a band one and they stood on [the] top of a hill one.
26 Kisha Abneri akamwita Yoabu na kusema, “Je ni lazima upanga uendelee kurarua daima? Je haujui kwamba mwisho wake utakuwa mchungu? Hata line ndipo uwaambie watu wako waache kuwafuatia ndugu zao?”
And he called out Abner to Joab and he said ¿ to perpetuity will it devour [the] sword ¿ not do you know? that bitter it will be at the last and until when? not will you say to the people to turn back from after brothers their.
27 Yoabu akajibu, “Kama Mungu aishivyo, usingesema hivyo, askari wangu wangewafuatia ndugu zao hata asubuhi!”
And he said Joab [by] [the] life of God if if not you had spoken for then from the morning it had abandoned pursuit the people each from after brother his.
28 Ndipo Yoabu akapiga tarumbeta, na watu wake wote wakasimama na hawakuendelea kuwafuata Israeli tena wala hawakupigana tena.
And he gave a blast Joab on the trumpet and they stood all the people and not they pursued again after Israel and not they repeated again to wage war.
29 Abneri na watu wake wakasafiri usiku wote kupitia Araba. Wakavuka Yordani, wakatembea asubuhi yote iliyofuata, na hata wakafika Mahanaimu.
And Abner and men his they went in the Arabah all the night that and they passed over the Jordan and they went all Bitron and they came Mahanaim.
30 Yoabu akarudi kutoka katika kumfuatia Abneri. Akawakusanya watu wake wote, ambopo Asahali na askari wengine kumi na tisa wa Daudi walipungua.
And Joab he returned from after Abner and he gathered all the people and they were missed of [the] servants of David nine-teen man and Asah-el.
31 Lakini watu wa Daudi walikuwa wameua watu 360 wa Benjamini na Abneri.
And [the] servants of David they had struck down of Benjamin and among [the] men of Abner three hundred and sixty man they had died.
32 Kisha wakamchukua Asahali na kumzika katika kaburi la baba yake, lililokuwapo Bethlehemu. Yoabu na watu wake wakasafiri usiku wote, kukacha wakati wanafika Hebroni.
And people lifted up Asahel and they buried him in [the] tomb of father his which [was] Beth-lehem and they went all the night Joab and men his and it became light for them at Hebron.

< 2 Samweli 2 >