< 2 Samweli 18 >

1 Daudi akawahesabu askari waliokuwa pamoja naye na akaweka akida wa elfu na akida wa mia juu yao.
And David mustered the people who were with him, and appointed commanders of thousands and commanders of hundreds over them.
2 Kisha Daudi akalipeleka jeshi, thelusi moja chini ya Yoabu, thelusi nyingine chini ya Abishai mwana wa Seruya, ndugu wa Yoabu, na thelusi nyingine tena chini ya Itai Mgiti. Mfalme akaliambia jeshi, “kwa hakika mimi mwenyewe pia nitakwenda pamoja nanyi.
David divided the army into three, a third part under the hand of Joab, and a third part under the hand of Abishai the son of Zeruiah, Joab's brother, and a third part under the hand of Ittai the Gittite. The king said to the people, "I will surely go forth with you myself also."
3 Lakini watu wakasema, “Wewe usiende vitani, kwani ikiwa tutakimbia hawatatujari sisi, ama nusu yetu wakifa hawatajari. Lakini wewe ni zaidi ya elfu kumi yetu sisi! Kwa hiyo ni afadhari zaidi ukitusaidia ukiwa mjini.”
But they said, "You must not go out, for if we retreat, no one will care about us. If half of us die, no one will care about us. But you are worth ten thousand of us. So it is better for you to be in the city to help."
4 Hivyo mfalme akawajibu, “Nitafanya lolote lionekanalo jema machoni penu.” Mfalme akasimama kati ya lango la mji wakati jeshi lilipoondoka katika mamia na katika maelfu.
The king said to them, "I will do what seems best to you." The king stood beside the gate, and all the people went out by hundreds and by thousands.
5 Mfalme akawaagiza Yoabu, Abishai, na Itai kusema, “Mmtendee huyo kijana, Absalomu, kwa upole kwa ajili yangu.” Watu wote wakasikia jinsi mfalme alivyowaagiza maakida kuhusu Absalomu.
The king gave this order to Joab and Abishai and Ittai, saying, "Be gentle for my sake with the young man Absalom." And all the people were listening when the king gave orders to all the commanders concerning Absalom.
6 Hivyo jeshi likaenda nyikani dhidi ya Israeli; vita ikaenea katika msitu wa Efraimu.
So the people went out into the field against Israel, and the battle took place in the forest of Ephraim.
7 Jeshi la Israeli likashindwa mbele ya askari wa Daudi; kulikuwa na machinjo makuu kwa watu elfu ishirini siku hiyo.
And the people of Israel were struck there before the servants of David, and a great slaughter took place that day of twenty thousand men.
8 Vita ikaenea katika eneo lote na watu wengi wakaangamizwa na msitu kuliko upanga.
For the battle spread over the entire region, and the forest devoured more people that day than the sword devoured.
9 Ikatukia kwamba Absalomu akakutana na askari wa Daudi. Absalomu alikuwa amepanda juu ya nyumbu wake na nyumbu akapita chini ya matawi manene ya mti wa mwaloni, na kichwa chake kikanaswa katika matawi ya mti. Akaachwa akining'inia kati ya nchi na anga wakati nyumbu alipoendelea mbele.
And Absalom happened to meet the servants of David. And he was riding on his mule, and the mule went under the thick branches of a great oak, and his head got caught in the oak, and he was left suspended in midair, while the mule that was under him kept going.
10 Mtu mmoja akaona lililotukia na akamwambia Yoabu, “Tazama, nilimwona Absalomu akining'inia katika mwaloni!”
And someone saw it and told Joab, and said, "Look, I saw Absalom hanging in an oak."
11 Yoabu akamwambia aliyemwambia kuhusu Absalomu, “Tazama! Ulimwona! Kwa nini haukumpiga hata chini. Ningekupa shekeli kumi za fedha na mkanda.”
Then Joab said to the man who reported it, "Look, you saw this. So why didn't you strike him there to the ground? I would have given you ten pieces of silver, and a belt."
12 Yule mtu akamjibu Yoabu, “Hata kama ningepewa shekeli elfu za fedha hata hivyo nisingeinua mkono wangu juu ya mwana wa mfalme, kwa maana sisi sote tulimsikia mfalme akiwaagiza wewe, Abishai na Itai kusema, mtu asimguse huyo kijana Absalomu.'
But the man said to Joab, "Even if I could feel in my hand the weight of a thousand pieces of silver in my hand, I still wouldn't lay a hand on the king's son, for in our hearing the king commanded you and Abishai and Ittai, saying, 'Be gentle for my sake with the young man Absalom.'
13 Ikiwa ningehatarisha maisha yangu kwa uongo(na hakuna jambo linalofichika kwa mfalme), ungejitenga nami.”
Otherwise, if I had dealt treacherously against his life (and there is no matter hidden from the king), then you yourself would have dissociated yourself from me."
14 Ndipo Yoabu aliposema, “sitakusubiri.” Kisha akachukua mishale mitatu mkononi mwake na akairusha katika moyo wa Absalomu wakati yu ngali hai na amening'inia katika mwaloni.
Then Joab said, "I'm not going to waste time with you." So he took three sharp sticks in his hand and thrust them into the heart of Absalom while he was still alive in the midst of the oak.
15 Kisha vijana kumi waliochukua slaha za Yoabu wakamzunguka Absalomu, wakampiga na kumwua.
Then ten young men, Joab's armor-bearers, surrounded and struck Absalom and killed him.
16 Kisha Yoabu akapiga tarumbeta na jeshi likarudi kutoka kuwafuatia Israeli, hivyo Yoabu akalirudisha jeshi.
Then Joab blew the trumpet and the people turned back from pursuing Israel, for Joab had called for the people to halt.
17 Wakamchukua Absalomu na kumtupa katika shimo kubwa msituni; wakaufukia mwili wake chini ya rundo kubwa la mawe, wakati Israeli wote walipokimbia kila mtu nyumbani kwake.
And they took Absalom and threw him into a large pit in the forest, and heaped up over him a huge pile of stones. Then all Israel fled, each one to his tent.
18 Wakati Absalomu alipokuwa yu ngali hai alijijengea nguzo kubwa ya jiwe katika Bonde la Mfalme, kwani alisema, “Sina mwana wa kuchukua kumbukumbu ya jina langu.” Akaiita nguzo kwa jina lake, hivyo inaitwa Mnara wa Absalomu hata leo.
Now Absalom in his lifetime had taken and reared up for himself the pillar, which is in the King's Valley; for he said, "I have no son to keep my name in memory." He called the pillar after his own name; and it is called Absalom's monument, to this day.
19 Kisha Ahimaasi mwana wa Sadoki akasema, “Niruhusu niende kwa mfalme na habari njema, jinsi Yahwe alivyomwokoa kutoka mkono wa adui zake.”
Then Ahimaaz the son of Zadok said, "Let me run, let me carry the king news how that Jehovah has avenged him of his enemies."
20 Yoabu akamjibu, “Wewe hautakuwa mchukua habari leo; utafanya hivyo siku nyingine. Leo hautachukua habari yoyote kwa maana mwana wa mfalme ameuawa.”
But Joab said, "You are not to bring the news today, but you may bring news another day. But today you are to bring no news." For it was because the king's son was dead.
21 Ndipo Yoabu akamwambia Mkushi, “Nenda umwambia mfalme ulichokiona.” Mkushi akamwinamia Yoabu, na kisha akakimbia.
Then Joab said to the Cushite, "Go, tell the king what you have seen." So the Cushite bowed before Joab and departed.
22 Kisha tena, Ahimaasi mwana wa Sadoki akamwambia Yoabu, “Pamoja na yote yanayoweza kutokea, tafadhari niruhusu nami pia niende nimfuate Mkushi.” Yoabu akajibu, “Mwanangu kwa nini unataka kwenda, hautapata thawabu yoyote kwa ajili ya habari hii?”
Then Ahimaaz the son of Zadok said again to Joab, "Whatever happens, please let me go after the Cushite." But Joab said, "Why do you want to run, my son, since you will have no reward for the news?"
23 “Vyovyote itakavyokuwa niache niende,” Ahimaasi alijibu. Hivyo Yoabu akamjibu, “Nenda.” Ndipo Ahimaasi akakimbia kwa njia ya tambarare na akampita Mkushi.
But he said, "But whatever happens, I will run." So he said to him, "Run." Then Ahimaaz ran by the way of the plain, and outran the Cushite.
24 Basi Daudi alikuwa amekaa kati ya lango la ndani na lango la nje. Na mlinzi alikuwa juu ya lango ukutani naye akainua macho yake. Alipokuwa akiangalia, akamwona mtu anakaribia huku akikimbia peke yake.
Now David was sitting between the two gates, and the watchman went up to the roof of the gate by the wall and raised his eyes and looked, and there was a man running alone towards him.
25 Mlinzi akaita kwa sauti na kumwambia mfalme. Ndipo mfalme akasema, “Ikiwa yupo peke yake ana habari katika kinywa chake.” Mkimbiaji akasogea na kuukaribia mji.
Then the watchman shouted and informed the king. And the king said, "If he is alone, there is good news in his mouth." And he kept coming nearer.
26 Kisha mlinzi akaona mtu mwingine aliyekuwa anakimbia, naye akamwambia bawabu; kusema, “Tazama, kuna mtu mwingine anakimbia peke yake.” Mfalme akasema, “Yeye pia analeta habari.”
Then the watchman saw another man running. And the watchman above the gate called out, and said, "Look, another man running alone." And the king said, "He also brings good news."
27 Ndipo mlinzi akasema, Nadhani kukimbia kwake mtu aliye mbele ni kama kukimbia kwake Ahimaasi mwana wa Sadoki.” Mfalme akasema, “Yeye ni mtu mwema naye anakuja na habari njema.”
Then the watchman said, "I think the first runner is like the running of Ahimaaz the son of Zadok." And the king said, "He is a good man, and comes with good news."
28 Ndipo Ahimaasi akaita na kumwambia mfalme, “Yote ni mema.” Kisha akainama yeye mwenyewe uso wake chini mbele ya mfalme na kusema, Atukuzwe Yahwe Mungu wako, aliyewatoa watu walioinua mkono wao kinyume cha bwana wangu mfalme.”
And Ahimaaz came near and said to the king, "All is well." Then he bowed himself before the king with his face to the ground, and said, "Blessed is Jehovah your God, who has defeated the men who opposed my lord the king."
29 Hivyo mfalme akauliza, “Je huyo kijana Absalomu hajambo?” Ahimaasi akajibu, “Wakati Yoabu ananituma kwako mfalme, mimi mtumishi wa mfalme, niliona fujo kubwa sana lakini sikutambua ilihusu nini.”
And the king asked, "Is it well with the young man Absalom?" And Ahimaaz answered, "When Joab, the king's servant, sent your servant off, I saw a great commotion, but I do not know what it was."
30 Mfalme akamwambia, “Geuka usimame kando.” Hivyo Ahimaasi akageuka na kusimama.
Then the king said, "Step aside and stand here." So he stepped aside and waited.
31 Mara Mkushi akafika na kusema, “Kuna habari njema kwa bwana wangu mfalme kwa kuwa leo Yahwe amekulipia kisasi kwa wale wote walioinuka kinyume chako.”
Then look, the Cushite arrived, and he said, "Good news for my lord the king, for Jehovah has delivered you today from all those who rose up against you."
32 Ndipo mfalme akamwuliza, “Je huyo kijana Absalomu ni mzima?” Mkushi akajibu, “Adui wa bwana wangu mfalme na wote wainukao kukudhuru na wawe kama huyo kijana.”
Then the king asked the Cushite, "Is it well with the young man Absalom?" And the Cushite replied, "May the enemies of my lord the king and all who rise up against you with evil intent be like that young man."
33 Ndipo mfalme alipohuzunishwa sana naye akaenda chumbani juu ya lango na kulia. Kadili alivyokwenda aliomboleza, mwanangu Absalomu, mwanangu, mwanangu Absalomu! afadhari ningekufa badala yako, Absalomu, mwanangu, mwanangu!”
And the king was shaken, and went up to the room over the gate and wept. And as he wept he said, "My son Absalom. My son, my son Absalom. If only I had died in your place, Absalom, my son, my son."

< 2 Samweli 18 >