< 2 Samweli 17 >

1 Kisha Ahithofeli akamwambia Absalomu, “Niruhusu sasa nichague watu elfu kumi na mbili nami nitaondoka na kumfuatia Daudi usiku huu.
Then Ahithophel said to Absalom, “Now let me choose twelve thousand men, and I will arise and pursue David tonight.
2 Nitampata kwa ghafla wakati amechoka na dhaifu nami nitamstukiza kwa hofu. Watu waliopamoja naye watakimbia nami nitamshambulia mfalme peke yake.
I will come on him while he is weary and weak and will surprise him with fear. The people who are with him will flee, and I will attack only the king.
3 Nitawarejesha watu wote kwako kama bibi harusi ajavyo kwa bwana wake, na watu wote watakuwa katika amani chini yako.”
I will bring back all the people to you, like a bride coming to her husband, and all the people will be at peace under you.”
4 Alichokisema Ahithofeli kikampendeza mfalme na wazee wote wa Israeli.
What Ahithophel said pleased Absalom and all the elders of Israel.
5 Kisha Absalomu akasema, “Sasa mwiteni pia Hushai Mwarki ili tusikie yeye pia anasemavyo.”
Then Absalom said, “Now call Hushai the Arkite, too, and let us hear what he says.”
6 Hushai alipofika kwa Absalomu, Absalomu akamweleza kile ambacho Ahithofeli alikuwa amesema na kisha akamwuliza Hushai, “Je tufanye alivyosema Ahithofeli? Ikiwa hapana, tueleze kile unachoshauri.”
When Hushai had come to Absalom, Absalom explained to him what Ahithophel had said and then asked Hushai, “Should we do what Ahithophel has said? If not, tell us what you advise.”
7 Hivyo Hushai akamwambia Absalomu, “Ushauri aliotoa Ahithofeli siyo mzuri kwa wakati huu.”
So Hushai said to Absalom, “The advice that Ahithophel has given this time is not good.”
8 Hushai akaongeza, “Unamjua baba yako na kwamba watu wake ni mashujaa na kwa sasa wanauchungu, ni kama dubu aliyenyang'anywa watoto wake mwituni. Baba yako ni mtu wa vita; hatalala na jeshi usiku huu.
Hushai added, “You know your father and his men are strong warriors, and that they are bitter, and they are like a bear robbed of her cubs in a field. Your father is a man of war; he will not sleep with the army tonight.
9 Tazama, kwa wakati huu pengine amejificha katika shimo fulani au mahali pengine. Itakuwa kwamba baadhi ya watu wako watakapokuwa wameuawa mwanzoni mwa shambulio hata kila mtu atakayesikia atasema, mauaji yamefanyika kwa askari wanaomfuata Absalomu.'
Look, right now he is probably hidden in some pit or in some other place. It will happen that when some of your men have been killed at the beginning of an attack, that whoever hears it will say, 'A slaughter has taken place among the soldiers who follow Absalom.'
10 Kisha hata askari jasiri zaidi ambao moyo wao ni kama moyo wa simba, wataogopa kwa kuwa Israeli yote inajua kwamba baba yako ni mtu mwenye nguvu na kwamba watu alionao ni wenye nguvu sana.
Then even the bravest soldiers, whose hearts are like the heart of a lion, will be afraid because all Israel knows that your father is a mighty man, and that the men who are with him are very strong.
11 Hivyo ninashauri kwamba Israeli wote wakutanike kwako pamoja kutoka Dani hadi Beersheba, wengi kama mchanga ufuoni mwa bahari na kwamba wewe mwenyewe uende vitani.
So I advise you that all Israel should be gathered together to you, from Dan to Beersheba, as numerous as the sands that are by the sea, and that you go to battle in person.
12 Kisha tutampata popote atakapokuwa nasi tutamfunika kama umande uangukavyo juu ya nchi. Hatutamwachia hata mmoja aliye hai kati ya watu wake wala yeye mwenyewe.
Then we will come on him wherever he may be found, and we will cover him as the dew falls on the ground. We will not leave even one of his men, or him himself, alive.
13 Ikiwa ataingia ndani ya mji kisha Israeli wote tutaleta kamba juu ya mji huo na kuukokotea mtoni, hata kusionekane hata jiwe moja dogo lililosalia.”
If he retreats into a city, then all Israel will bring ropes to that city and we will drag it into the river, until there is no longer even a small stone found there.”
14 Kisha Absalomu na watu wa Israeli wakasema, “Shauri la Hushai Mwarki ni jema kuliko lile la Ahithofeli. Yahwe aliwafanya wakatae shauri jema la Ahithofeli ili kumwangamiza Absalomu.
Then Absalom and the men of Israel said, “Hushai the Arkite's advice is better than Ahithophel's.” Yahweh had ordained the rejection of Ahithophel's good advice in order to bring destruction on Absalom.
15 Kisha Hushai akawambia Sadoki na Abiathari makuhani, “Ahithofeli alimshauri Absalomu na wazee wa Israeli hivi na hivi, lakini mimi nimeshauri vinginevyo.
Then Hushai said to Zadok and to Abiathar the priests, “Ahithophel advised Absalom and the elders of Israel in such and such a way, but I have advised something else.
16 Sasa basi, nendeni haraka na mmtaarifu Daudi kusema, 'Usipige kambi usiku huu katika vivuko vya Araba, lakini kwa namna yoyote vukeni, tofauti na hapo mfalme atamezwa pamoja na watu wote walio pamoja naye.”
Now then, go quickly and report to David; say to him, 'Do not camp tonight at the fords of the Arabah, but by all means cross over, or the king will be swallowed up along with all the people who are with him.'”
17 Yonathani na Ahimaasi walikuwako katika chemichemi za En Rogeli. Hivyo kijakazi mmoja alikuwa akienda na kuwapasha habari waliyopaswa kuifahamu, ili kwamba wasihatarishe maisha yao kwa kuonwa wakiingia mjini. Ujumbe ulipofika ndipo huenda na kumtaarifu mfalme Daudi.
Now Jonathan and Ahimaaz were staying at the spring of Rogel. A female servant used to go and inform them what they needed to know, for they could not risk being seen going into the city. When the message came, then they were to go and tell King David.
18 Lakini kijana mmoja akawaoni mara akamwambia Absalomu. Hivyo Yonathani na Ahimaasi wakaenda kwa haraka na wakaingia katika nyumba ya mtu mmoja huko Bahurimu, aliyekuwa na kisima katika ua wake wakaingia humo.
But a young man saw them this time and told Absalom. So Jonathan and Ahimaaz went away quickly and came to the house of a man in Bahurim, who had a well in his courtyard, into which they descended.
19 Mke wa mtu huyo akachukua kifuniko na kukikufunika kwenye mlango wa kisima kisha akaanika nafaka juu yake, hivyo hakuna aliyejua kwamba Yonathani na Ahimaasi walikuwa kisimani.
The man's wife took the covering for the well and spread it over the well's opening, and tossed grain over it, so no one knew Jonathan and Ahimaaz were in the well.
20 Watu wa Absalomu wakaja kwa mwanamke na kumwuliza, “Ahimaasi na Yonathani wako wapi?” Mwanamke akawaambia, “Wamevuka mto.” Hivyo baada ya kuwatafuta bila kuwaona kurejea Yerusalemu.
Absalom's men came to the woman of the house and said, “Where are Ahimaaz and Jonathan?” The woman told them, “They have crossed over the river.” So after they had looked around and could not find them, they returned to Jerusalem.
21 Ikawa baada yao kuondoka Yonathani na Ahimaasi wakatoka ndani ya kisima. Wakaenda kumtaarifu mfalme Daudi; wakamwambia, “Inuka na uvuke maji haraka kwa maana Ahithofeli ametoa mashauri haya na haya juu yako.”
It came about after they had left that Jonathan and Ahimaaz came up out of the well. They went to report to King David; they said to him, “Get up and cross quickly over the water because Ahithophel has given such and such advice about you.”
22 Kisha Daudi akainuka pamoja na watu wote walikuwa pamoja naye, nao wakauvuka Yordani. Hata ilipofika alfajiri hakuna hata mmoja aliyesalia kwa kutouvuka Yordani.
Then David arose and all the people who were with him, and they crossed over the Jordan. By morning daylight not one of them had failed to cross over the Jordan.
23 Ikawa Ahithofeli alipoona kwamba ushauri wake haukufuatwa, akapanda punda wake na kuondoka. Akaenda nyumbani katika mji wake mwenyewe, akaweka mambo yake katika utaratibu na kisha akajinyonga. Kwa hiyo akafa na kuzikwa katika kaburi la baba yake.
When Ahithophel saw that his advice had not been followed, he saddled his donkey and left. He went home to his own city, set his affairs in order, and hanged himself. In this way he died and was buried in the tomb of his father.
24 Ndipo Daudi akaja Mahanaimu. Lakini Absalomu yeye akavuka Yordani yeye pamoja na watu wote wa Israeli waliokuwa pamoja naye.
Then David came to Mahanaim. As for Absalom, he crossed over the Jordan, he and all the men of Israel with him.
25 Absalomu alikuwa amemweka Amasa juu ya jeshi badala ya Yoabu. Naye huyo Amasa alikuwa mwana wa Yetheri Mwishmaeli, aliyekuwa amelala na Abigaili, aliyekuwa binti Nahashi na dada wa Seruya, mamaye Yoabu.
Absalom had set Amasa over the army instead of Joab. Amasa was the son of Jether the Ishmaelite, who had slept with Abigail, who was the daughter of Nahash and sister of Zeruiah, the mother of Joab.
26 Kisha Israeli na Absalomu wakapiga kambi katika nchi ya Gileadi.
Then Israel and Absalom camped in the land of Gilead.
27 Ikawa wakati Daudi alipokuwa amekuja Mahanaimu, huyo Shobi mwana wa Nahashi kutoka Raba ya Waamoni na Makiri mwana wa Amieli wa kutoka Lo Debari, na Berzilai Mgileadi wa Rogelimu,
It came about when David had come to Mahanaim, that Shobi son of Nahash from Rabbah of the Ammonites, and Machir son of Ammiel from Lo Debar, and Barzillai the Gileadite from Rogelim,
28 wakaleta magodoro na mabulangeti, mabakuri na vyungu, na ngano, unga wa shayiri, nafaka zilizokaangwa, maharage, dengu,
brought sleeping mats and blankets, bowls and pots, and wheat, barley flour, roasted grain, beans, lentils,
29 asali, siagi, kondoo na samli, ili kwamba Daudi na watu waliokuwa pamoja naye waweze kula. Kwani walisema, “Watu wana njaa, wamechoka na wana kiu huko nyikani.”
honey, butter, sheep, and milk curds, so that David and the people with him could eat. These men had said, “The people are hungry, weary, and thirsty in the wilderness.”

< 2 Samweli 17 >