< 2 Samweli 17 >

1 Kisha Ahithofeli akamwambia Absalomu, “Niruhusu sasa nichague watu elfu kumi na mbili nami nitaondoka na kumfuatia Daudi usiku huu.
Moreover Ahithophel said unto Absalom: 'Let me now choose out twelve thousand men, and I will arise and pursue after David this night;
2 Nitampata kwa ghafla wakati amechoka na dhaifu nami nitamstukiza kwa hofu. Watu waliopamoja naye watakimbia nami nitamshambulia mfalme peke yake.
and I will come upon him while he is weary and weak-handed, and will make him afraid; and all the people that are with him shall flee; and I will smite the king only;
3 Nitawarejesha watu wote kwako kama bibi harusi ajavyo kwa bwana wake, na watu wote watakuwa katika amani chini yako.”
and I will bring back all the people unto thee; when all shall have returned, save the man whom thou seekest, all the people will be in peace.'
4 Alichokisema Ahithofeli kikampendeza mfalme na wazee wote wa Israeli.
And the saying pleased Absalom well, and all the elders of Israel.
5 Kisha Absalomu akasema, “Sasa mwiteni pia Hushai Mwarki ili tusikie yeye pia anasemavyo.”
Then said Absalom: 'Call now Hushai the Archite also, and let us hear likewise what he saith.'
6 Hushai alipofika kwa Absalomu, Absalomu akamweleza kile ambacho Ahithofeli alikuwa amesema na kisha akamwuliza Hushai, “Je tufanye alivyosema Ahithofeli? Ikiwa hapana, tueleze kile unachoshauri.”
And when Hushai was come to Absalom, Absalom spoke unto him, saying: 'Ahithophel hath spoken after this manner; shall we do after his saying? if not, speak thou.'
7 Hivyo Hushai akamwambia Absalomu, “Ushauri aliotoa Ahithofeli siyo mzuri kwa wakati huu.”
And Hushai said unto Absalom: 'The counsel that Ahithophel hath given this time is not good.'
8 Hushai akaongeza, “Unamjua baba yako na kwamba watu wake ni mashujaa na kwa sasa wanauchungu, ni kama dubu aliyenyang'anywa watoto wake mwituni. Baba yako ni mtu wa vita; hatalala na jeshi usiku huu.
Hushai said moreover: 'Thou knowest thy father and his men, that they are mighty men, and they are embittered in their minds, as a bear robbed of her whelps in the field; and thy father is a man of war, and will not lodge with the people.
9 Tazama, kwa wakati huu pengine amejificha katika shimo fulani au mahali pengine. Itakuwa kwamba baadhi ya watu wako watakapokuwa wameuawa mwanzoni mwa shambulio hata kila mtu atakayesikia atasema, mauaji yamefanyika kwa askari wanaomfuata Absalomu.'
Behold, he is hid now in some pit, or in some place; and it will come to pass, when they fall upon them at the first, and whosoever heareth it shall say: There is a slaughter among the people that follow Absalom;
10 Kisha hata askari jasiri zaidi ambao moyo wao ni kama moyo wa simba, wataogopa kwa kuwa Israeli yote inajua kwamba baba yako ni mtu mwenye nguvu na kwamba watu alionao ni wenye nguvu sana.
then even he that is valiant, whose heart is as the heart of a lion, will utterly melt; for all Israel knoweth that thy father is a mighty man, and they that are with him are valiant men.
11 Hivyo ninashauri kwamba Israeli wote wakutanike kwako pamoja kutoka Dani hadi Beersheba, wengi kama mchanga ufuoni mwa bahari na kwamba wewe mwenyewe uende vitani.
But I counsel that all Israel be gathered together unto thee, from Dan even to Beer-sheba, as the sand that is by the sea for multitude; and that thou go to battle in thine own person.
12 Kisha tutampata popote atakapokuwa nasi tutamfunika kama umande uangukavyo juu ya nchi. Hatutamwachia hata mmoja aliye hai kati ya watu wake wala yeye mwenyewe.
So shall we come upon him in some place where he shall be found, and we will light upon him as the dew falleth on the ground; and of him and of all the men that are with him we will not leave so much as one.
13 Ikiwa ataingia ndani ya mji kisha Israeli wote tutaleta kamba juu ya mji huo na kuukokotea mtoni, hata kusionekane hata jiwe moja dogo lililosalia.”
Moreover, if he withdraw himself into a city, then shall all Israel bring up ropes to that city, and we will draw it into the valley until there be not one small stone found there.'
14 Kisha Absalomu na watu wa Israeli wakasema, “Shauri la Hushai Mwarki ni jema kuliko lile la Ahithofeli. Yahwe aliwafanya wakatae shauri jema la Ahithofeli ili kumwangamiza Absalomu.
And Absalom and all the men of Israel said: 'The counsel of Hushai the Archite is better than the counsel of Ahithophel.' — For the LORD had ordained to defeat the good counsel of Ahithophel, to the intent that the LORD might bring evil upon Absalom.
15 Kisha Hushai akawambia Sadoki na Abiathari makuhani, “Ahithofeli alimshauri Absalomu na wazee wa Israeli hivi na hivi, lakini mimi nimeshauri vinginevyo.
Then said Hushai unto Zadok and to Abiathar the priests: 'Thus and thus did Ahithophel counsel Absalom and the elders of Israel; and thus and thus have I counselled.
16 Sasa basi, nendeni haraka na mmtaarifu Daudi kusema, 'Usipige kambi usiku huu katika vivuko vya Araba, lakini kwa namna yoyote vukeni, tofauti na hapo mfalme atamezwa pamoja na watu wote walio pamoja naye.”
Now therefore send quickly, and tell David, saying: Lodge not this night in the plains of the wilderness, but in any wise pass over; lest the king be swallowed up, and all the people that are with him.'
17 Yonathani na Ahimaasi walikuwako katika chemichemi za En Rogeli. Hivyo kijakazi mmoja alikuwa akienda na kuwapasha habari waliyopaswa kuifahamu, ili kwamba wasihatarishe maisha yao kwa kuonwa wakiingia mjini. Ujumbe ulipofika ndipo huenda na kumtaarifu mfalme Daudi.
Now Jonathan and Ahimaaz stayed by En-rogel; and a maid-servant used to go and tell them; and they went and told king David; for they might not be seen to come into the city.
18 Lakini kijana mmoja akawaoni mara akamwambia Absalomu. Hivyo Yonathani na Ahimaasi wakaenda kwa haraka na wakaingia katika nyumba ya mtu mmoja huko Bahurimu, aliyekuwa na kisima katika ua wake wakaingia humo.
But a lad saw them, and told Absalom; and they went both of them away quickly, and came to the house of a man in Bahurim, who had a well in his court; and they went down thither.
19 Mke wa mtu huyo akachukua kifuniko na kukikufunika kwenye mlango wa kisima kisha akaanika nafaka juu yake, hivyo hakuna aliyejua kwamba Yonathani na Ahimaasi walikuwa kisimani.
And the woman took and spread the covering over the well's mouth, and strewed groats thereon; and nothing was known.
20 Watu wa Absalomu wakaja kwa mwanamke na kumwuliza, “Ahimaasi na Yonathani wako wapi?” Mwanamke akawaambia, “Wamevuka mto.” Hivyo baada ya kuwatafuta bila kuwaona kurejea Yerusalemu.
And Absalom's servants came to the woman to the house; and they said: 'Where are Ahimaaz and Jonathan?' And the woman said unto them: 'They are gone over the brook of water.' And when they had sought and could not find them, they returned to Jerusalem.
21 Ikawa baada yao kuondoka Yonathani na Ahimaasi wakatoka ndani ya kisima. Wakaenda kumtaarifu mfalme Daudi; wakamwambia, “Inuka na uvuke maji haraka kwa maana Ahithofeli ametoa mashauri haya na haya juu yako.”
And it came to pass, after they were departed, that they came up out of the well, and went and told king David; and they said unto David: 'Arise ye, and pass quickly over the water; for thus hath Ahithophel counselled against you.'
22 Kisha Daudi akainuka pamoja na watu wote walikuwa pamoja naye, nao wakauvuka Yordani. Hata ilipofika alfajiri hakuna hata mmoja aliyesalia kwa kutouvuka Yordani.
Then David arose, and all the people that were with him, and they passed over the Jordan; by the morning light there lacked not one of them that was not gone over the Jordan.
23 Ikawa Ahithofeli alipoona kwamba ushauri wake haukufuatwa, akapanda punda wake na kuondoka. Akaenda nyumbani katika mji wake mwenyewe, akaweka mambo yake katika utaratibu na kisha akajinyonga. Kwa hiyo akafa na kuzikwa katika kaburi la baba yake.
And when Ahithophel saw that his counsel was not followed, he saddled his ass, and arose, and got him home, unto his city, and set his house in order, and strangled himself; and he died, and was buried in the sepulchre of his father.
24 Ndipo Daudi akaja Mahanaimu. Lakini Absalomu yeye akavuka Yordani yeye pamoja na watu wote wa Israeli waliokuwa pamoja naye.
When David was come to Mahanaim, Absalom passed over the Jordan, he and all the men of Israel with him.
25 Absalomu alikuwa amemweka Amasa juu ya jeshi badala ya Yoabu. Naye huyo Amasa alikuwa mwana wa Yetheri Mwishmaeli, aliyekuwa amelala na Abigaili, aliyekuwa binti Nahashi na dada wa Seruya, mamaye Yoabu.
And Absalom had set Amasa over the host instead of Joab. Now Amasa was the son of a man, whose name was Ithra the Jesraelite, that went in to Abigal the daughter of Nahash, sister to Zeruiah Joab's mother.
26 Kisha Israeli na Absalomu wakapiga kambi katika nchi ya Gileadi.
And Israel and Absalom pitched in the land of Gilead.
27 Ikawa wakati Daudi alipokuwa amekuja Mahanaimu, huyo Shobi mwana wa Nahashi kutoka Raba ya Waamoni na Makiri mwana wa Amieli wa kutoka Lo Debari, na Berzilai Mgileadi wa Rogelimu,
And it came to pass, when David was come to Mahanaim, that Shobi the son of Nahash of Rabbah of the children of Ammon, and Machir the son of Ammiel of Lo-debar, and Barzillai the Gileadite of Rogelim,
28 wakaleta magodoro na mabulangeti, mabakuri na vyungu, na ngano, unga wa shayiri, nafaka zilizokaangwa, maharage, dengu,
brought beds, and basins, and earthen vessels, and wheat, and barley, and meal, and parched corn, and beans, and lentils, and parched pulse,
29 asali, siagi, kondoo na samli, ili kwamba Daudi na watu waliokuwa pamoja naye waweze kula. Kwani walisema, “Watu wana njaa, wamechoka na wana kiu huko nyikani.”
and honey, and curd, and sheep, and cheese of kine, for David, and for the people that were with him, to eat; for they said: 'The people is hungry, and faint, and thirsty, in the wilderness.'

< 2 Samweli 17 >