< 2 Wafalme 9 >

1 Nabii Elisha akamwita mmoja wa watoto wa manabii na kumwambia, “Vaa kwa kwa safari, halafu chukua hii chupa ndogo ya mafuta kwenye mikono yako na uende Romoth Geliadi.
Elisha the prophet called one of the sons of the prophets and said to him, “Dress for travel, then take this little bottle of oil in your hand and go to Ramoth Gilead.
2 Wakati utakapofika, mtafute Yehu mwana wa Yehoshafati mwana wa Nimshi, na uende ukaingie na kumfanya ainuke kutoka miongoni mwa rafiki zake, na ukampeleke katika chumba cha ndani.
When you arrive, look for Jehu son of Jehoshaphat son of Nimshi, and go in and make him arise up from among his companions, and conduct him to an inner chamber.
3 Kisha chukua ile chupa ya mafuta na imiminie kwenye kichwa chake na kusema, 'Yahwe anasema hivi: “Nimekumiminia mafuta uwe mfalme juu ya Israeli. “Halafu fungua mlango, na kukimbia; usichelewe.”
Then take the bottle of oil and pour it on his head and say, 'Yahweh says this: “I have anointed you king over Israel.”' Then open the door, and run off; do not delay.”
4 Basi yule kijana, yule nabii kijana, akaenda Romoth Geliadi.
So the young man, the young prophet, went to Ramoth Gilead.
5 Wakati alipofika, kumbe, wale manahodha wa lile jeshi walikuwa wamekaa. Hivyo yule nabii kijana akasema, “Nimekuja mara moja naneno kwako, nahodha.” Yehu akajibu, “kwa yupi katika sisi?” Yule nabii kijana akajibu, “Kwako nahodha.”
When he arrived, behold, the captains of the army were sitting. So the young prophet said, “I have come on an errand to you, captain.” Jehu replied, “To which of us?” The young prophet answered, “To you, captain.”
6 Basi Yehu akainuka na kwenda kwenye nyumba, na yule nabii akammiminia mafuta kwenye kichwa chake na kumwambia Yehu, “Yahwe, Mungu wa Israeli, anasema hivi: 'Nimekumiminia mafuta uwe mfalme juu ya watu wa Yahwe, juu ya Isaraeli.
So Jehu arose and went into the house, and the prophet poured the oil on his head and said to Jehu, “Yahweh, the God of Israel, says this: 'I have anointed you king over the people of Yahweh, over Israel.
7 Wewe lazima uiue familia ya Ahabu bwana wako, ili niweze kulipiza kisasi cha damu ya watumishi wangu manabii, na damu ya watumishi wote wa Yahwe, ambao waliokuwa wameuawa kwa mkono wa Yezebeli.
You must kill the family of Ahab your master, so that I may avenge the blood of my servants the prophets, and the blood of all the servants of Yahweh, who were murdered by the hand of Jezebel.
8 Kwa kuwa nyumba yote ya Ahabu itaangamia, na nitamkatilia mbali kila mtoto wa kiume wa Ahabu, yeyote awe mtumwa au mtu huru.
For the whole family of Ahab will perish, and I will cut off from Ahab every male child, whether he is a slave or a free person.
9 Nitaifanya nyumba ya Ahabu kama nyumba ya Yerobohamu mwana wa Nebati na kama nyumba ya Baasha mwana wa Ahiya.
I will make the house of Ahab like the house of Jeroboam son of Nebat and like the house of Baasha son of Ahijah.
10 Mbwa watamla Yezebeli katika Yezreeli, na hakutakuwa na mtu wa kumzika.” Kisha nabii akafungua mlango na kukimbia.
The dogs will eat Jezebel in Jezreel, and there will be no one to bury her.'” Then the prophet opened the door and ran off.
11 Kisha Yehu akatoka kwenda kwa watumishi wa bwana wake, na mmoja akamwambia, “Je kila kitu kiko sawa? Kwa nini huyu mwenda wazimu amekuja kwako?” Yehu akawajibu, “Mnamjua huyo mtu na mambo asemayo.”
Then Jehu came out to the servants of his master, and one said to him, “Is everything alright? Why did this mad fellow come to you?” Jehu answered them, “You know the man and the kinds of things he says.”
12 Wakasema, “Huo ni uongo. Tuambie.” Yehu akajibu, “Alisema hivi na vile juu yangu, na pia akasema, 'hivi ndivyo Yahwe asemavyo: Nimekumiminia mafuta kama mfalme juu ya Israeli.””
They said, “That is a lie. Tell us.” Jehu answered, “He said this and that to me, and he also said, 'This is what Yahweh says: I have anointed you as king over Israel.'”
13 Kisha kila mmoja wao akachukua vazi haraka na kuweka chini ya Yehu juu ya madaraja. Wakapiga baragumu na kusema, “Yehu ni mfalme.”
Then each of them quickly took off his outer garment and put it under Jehu at the top of the steps. They blew the trumpet and said, “Jehu is king.”
14 Katika njia hii Yehu mwana wa Yehoshafati mwana wa Nimshi akafanya njama juu ya Yoramu. Basi Yoramu alikuwa akiilinda Ramothi Gileadi, yeye na Israeli yote, kwa sababu ya Hazaeli mfalme wa Shamu,
In this way Jehu son of Jehoshaphat son of Nimshi conspired against Joram. Now Joram had been defending Ramoth Gilead, he and all Israel, because of Hazael king of Aram,
15 lakini mfalme Yoramu alikuwa amesharudi kwa Yezreeli ili kuponywa yale majeraha aliyokuwa ameyapewa na Washami, wakati akiwa anapigana dhidi ya Hazaeli mfalme wa Shamu. Yehu akawaambia watumishi wa Yoramu, “kama hili ndilo wazo lako, kisha usimwache mtu aondoke na kwenda nje ya mji, ili aende kupeleka habari hii Yezreeli.”
but King Joram had gone back to Jezreel to be healed of the wounds that the Arameans had given him, when he had fought against Hazael king of Aram. Jehu said to the servants of Joram, “If this is your opinion, then let no one escape and go out of the city, in order to go tell this news in Jezreel.”
16 Basi Yehu akaendesha gari la farasi mpaka Yezreeli; kwa kuwa Yoramu alikuwa amelala huko. Basi Ahazi mfalme wa Yuda alikuwa ameshuka chini kuonana na Yoramu.
So Jehu rode in a chariot to Jezreel; for Joram was resting there. Now Ahaziah king of Judah had come down to see Joram.
17 Mlinzi alikuwa amesimama juu ya mnara katika Yezreeli, akaliona lile kundi la Yehu alipokuwa akija kwa mbali kidogo; akasema, “Naona kundi la watu wanakuja.” Yoramu akasema, “Chukua mwendesha farasi, na umtume akakutane nao; mwambie aseme, “Je mnakuja kwa amani?””
The watchman was standing on the tower in Jezreel, and he saw the company of Jehu as he came at a distance; he said, “I see a group of men coming.” Joram said, “Take a horseman, and send him out to meet them; tell him to say, 'Are you coming in peace?'”
18 Hivyo mwendesha farasi akatoka kumlaki; akasema, “Mfalme asema hivi: Je mnakuja kwa amani?”' Basi Yehu akasema, “Wewe una nini na amani? Geuka na unifuate nyuma.” Kisha yule mlinzi akamwambia mfalme, Yule mjumbe ameshaonana nao, lakini anarudi.”
So a man was sent on horseback to meet him; he said, “The king says this: 'Are coming in peace?'” So Jehu said, “What have you to do with peace? Turn and ride behind me.” Then the watchman told the king, “The messenger has met them, but he is not coming back.”
19 Kisha akapeleka mpanda farasi wa pili, ambaye alikuja kwao na kusema, “Mfalme asema hivi: 'Je mnakuja na amani?”' Yehu akajibu, “Wewe una nini na amani? Geuka na kunifuata nyuma.
Then he sent out a second man on horseback, who came to them and said, “The king says this: 'Are you coming in peace?'” Jehu answered, “What have you to do with peace? Turn and ride behind me.”
20 Tena yule mlinzi akatoa taarifa, “Amekwisha kuonana nao, lakini hatorudi. Kwa kuwa hilo gari la farasi limekuwa likiendeshwa ndivyo ambavyo Yehu mwana wa Nimshi aendeshavyo; anaendesha kwa kasi.”
Again the watchman reported, “He has met them, but he is not coming back. For the way that the chariot is being driven is the way that Jehu son of Nimshi drives; he is driving wildly.”
21 Hivyo Yoramu akasema, “Andaa gari langu la farasi liwe tayari.” Wakaandaa gari lake la farasi, na Yoramu mfalme wa Israeli na Ahazi mfalme wa Yuda akaendesha, kila mmoja kwenye gari lake la farasi, kumlaki Yehu. Wakamkuta kwenye mali ya Nabothi Myezreeli.
So Joram said, “Get my chariot ready.” They prepared his chariot, and Joram king of Israel and Ahaziah king of Judah rode out, each in his chariot, to meet Jehu. They found him at the property of Naboth the Jezreelite.
22 Wakati Yoramu alipomuona Yehu, alisema, “Je unakuja katika hali ya amani, Yehu?” Akajibu, “Amani gani hapo, wakati uzinzi wa ukahaba hufanywa na uchawi wa mama yako Yezebeli umejaa tele?”
When Joram saw Jehu, he said, “Are you coming in peace, Jehu?” He answered, “What peace is there, when the idolatrous acts of prostitution and witchcraft of your mother Jezebel are so many?”
23 Basi Yoramu akarudisha magari yake ya farasi na kukimbia na kumwambia Ahazia, “Kuna udanganyifu, Ahazia.
So Joram turned his chariot and fled and said to Ahaziah, “There is treachery, Ahaziah.”
24 Ndipo Yehu akauvuta upinde wake kwa nguvu zake zote na kumpiga Yoramu kati ya mabega yake; mshale ukaenda kwenye moyo wake, akaanguka chini kwenye gari lake la farasi.
Then Jehu drew his bow with his full strength and shot Joram between his shoulders; the arrow went through his heart, and he sank down in his chariot.
25 Ndipo Yehu akamwambia Bidkari nahodha wake, “Mchukue na mtupie kwenye shamba la Nabothi Myezreeni. Fikiria kuhusu vile ambavyo wewe na mimi tulivyoendesha pamoja baada ya Ahabu baba yake, Yahwe aliuweka juu unabii dhidi yake:
Then Jehu said to Bidkar his captain, “Pick him up and throw him in the field of Naboth the Jezreelite. Think about how when you and I rode together after Ahab his father, Yahweh placed this prophecy against him:
26 Jana niliona damu ya Nabothi na damu ya watoto wake - asema Yahwe - na nitahakikisha unalipia hili shamba - asema Yahwe. Sasa basi, mchukue na mtupe kwenye hili shamba, sawa sawa na neno la Yahwe.”
'Yesterday I saw the blood of Naboth and the blood of his sons—declares Yahweh—and I will surely make you pay for it on this field—declares Yahweh. Now then, pick him up and throw him on this field, according to the word of Yahweh.”
27 Wakati Ahazi yule mfalme wa Yuda alipoliona hili, akakimbia kwa njia ya Bethi Hagani. Lakini Yehu akamfuata, na kusema, “Muulie humo kwenye gari la farasi,” na wakampiga mahali pa kupandia Guri, karibu na Ebleamu. Ahazi akakimbilia Megido na kufia pale.
When Ahaziah the king of Judah saw this, he fled up the road to Beth Haggan. But Jehu followed him, and said, “Kill him also in the chariot,” and they shot him at the ascent of Gur, which is by Ibleam. Ahaziah fled to Megiddo and died there.
28 Watumishi wake wakaubeba mwili wake kwa magari ya farasi kwenda Yerusalemu na kumzika kwenye kaburi lake pamoja na baba zake katika mji wa Daudi.
His servants carried his body in a chariot to Jerusalem and buried him in his tomb with his fathers in the city of David.
29 Basi ilikuwa mwaka wa kumi na moja wa Yoramu mwana wa Ahabu huyo Ahazia akaanza kutawala juu ya Yuda.
Now it was in the eleventh year of Joram son of Ahab that Ahaziah had begun to reign over Judah.
30 Wakati Yahu alipokuja kwa Yezebeli, Yezebeli akasikia juu ya hilo, akapaka wanja kwenye macho yake, akatengeneza nywele zake vizuri, na kuchungulia kwenye dirisha.
When Jehu came to Jezreel, Jezebel heard of it, and she painted her eyes, arranged her hair, and looked out the window.
31 Kadiri Yehu alipokuwa akiingia kwenye lango, akamwambia, “Je unakuja kwa amani, wewe Zimri, muuaji wa bwana wako?”
As Jehu was entering the gate, she said to him, “Are you coming in peace, you Zimri, your master's murderer?”
32 Yehu akatazama juu ya dirisha na kusema, “Ni nani yuko upande wangu? Nani?” Matowashi wawili au watatu wakachungulia nje.
Jehu looked up at the window and said, “Who is on my side? Who?” Then two or three eunuchs looked out.
33 Basi Yehu aksema, “Mtupeni chini.” Hivyo wakamtupa Yezebeli chini, na damu yake nyingine ikamwagika kwenye ukuta na farasi, na Yehu akamkanyaga kanyaga chini ya miguu.
So Jehu said, “Throw her down.” So they threw Jezebel down, and some of her blood spattered on the wall and the horses, and Jehu trampled her underfoot.
34 Basi Yehu akaingia hiyo sehemu, akala na kunywa. Kisha akasema, “Mtazamani sasa huyu mwanamke aliyelaaniwa na kumzika, kwa kuwa ni binti wa mfalme.”
When Jehu entered the palace, he ate and drank. Then he said, “See now to this cursed woman and bury her, for she is a king's daughter.”
35 Wakaenda kumzika, lakini hawakumkuta ila fuvu, miguu, na viganga vya mikono yake.
They went to bury her, but they found no more of her than the skull, the feet, and the palms of her hands.
36 Basi wakarudi na kumwambia Yehu. Akasema, “Hili ndilo neno la Yahwe ambalo ameliongea kupitia Eliya Mtishbi, likisema, 'Katika nchi Yezreeli mbwa ataula mwili wa Yezebeli,
So they came back and told Jehu. He said, “This is the word of Yahweh which he spoke by his servant Elijah the Tishbite, saying, 'In the land at Jezreel the dogs will eat the flesh of Jezebel,
37 na mwili wa Yezebeli utakuwa kama kinyesi juu ya uso wa mashamba katika nchi ya Yezreeli, kwa hiyo basi hakuna atakayeweza kusema, “Huyu ni Yezebeli.””
and the body of Jezebel will be like dung on the surface of the fields in the land at Jezreel, so that no one will be able to say, “This is Jezebel.”'”

< 2 Wafalme 9 >