< 2 Wafalme 9 >

1 Nabii Elisha akamwita mmoja wa watoto wa manabii na kumwambia, “Vaa kwa kwa safari, halafu chukua hii chupa ndogo ya mafuta kwenye mikono yako na uende Romoth Geliadi.
Profeten Elisa kaldte en af Profetsønnerne til sig og sagde til ham: »Omgjord dine Lænder, tag denne Flaske Olie med og drag til Ramot i Gilead.
2 Wakati utakapofika, mtafute Yehu mwana wa Yehoshafati mwana wa Nimshi, na uende ukaingie na kumfanya ainuke kutoka miongoni mwa rafiki zake, na ukampeleke katika chumba cha ndani.
Naar du kommer derhen, opsøg saa Jehu, Nimsjis Søn Josjafats Søn; gaa hen og faa ham til at staa op fra sine Fæller og før ham ind i det inderste Hammer;
3 Kisha chukua ile chupa ya mafuta na imiminie kwenye kichwa chake na kusema, 'Yahwe anasema hivi: “Nimekumiminia mafuta uwe mfalme juu ya Israeli. “Halafu fungua mlango, na kukimbia; usichelewe.”
tag saa Olieflasken og gyd Olien ud over hans Hoved med de Ord: Saa siger HERREN: Jeg salver dig til Konge over Israel! Derefter skal du lukke Døren op og flygte ufortøvet!«
4 Basi yule kijana, yule nabii kijana, akaenda Romoth Geliadi.
Den unge Mand, Profetens Tjener, drog saa til Ramot i Gilead;
5 Wakati alipofika, kumbe, wale manahodha wa lile jeshi walikuwa wamekaa. Hivyo yule nabii kijana akasema, “Nimekuja mara moja naneno kwako, nahodha.” Yehu akajibu, “kwa yupi katika sisi?” Yule nabii kijana akajibu, “Kwako nahodha.”
og da han kom derhen, traf han Hærførerne siddende sammen. Han sagde da: »Jeg har et Ærinde til dig, Hærfører!« Jehu spurgte: »Til hvem af os?« Han svarede: »Til dig, Hærfører!«
6 Basi Yehu akainuka na kwenda kwenye nyumba, na yule nabii akammiminia mafuta kwenye kichwa chake na kumwambia Yehu, “Yahwe, Mungu wa Israeli, anasema hivi: 'Nimekumiminia mafuta uwe mfalme juu ya watu wa Yahwe, juu ya Isaraeli.
Saa rejste han sig og gik ind i Huset; der gød han Olien ud over hans Hoved og sagde til ham: »Saa siger HERREN, Israels Gud: Jeg salver dig til Konge over HERRENS Folk, over Israel!
7 Wewe lazima uiue familia ya Ahabu bwana wako, ili niweze kulipiza kisasi cha damu ya watumishi wangu manabii, na damu ya watumishi wote wa Yahwe, ambao waliokuwa wameuawa kwa mkono wa Yezebeli.
Du skal hugge din Herre Akabs Hus ned, saa jeg faar Hævn over Jesabel for mine Tjenere Profeternes og alle HERRENS Tjeneres Blod.
8 Kwa kuwa nyumba yote ya Ahabu itaangamia, na nitamkatilia mbali kila mtoto wa kiume wa Ahabu, yeyote awe mtumwa au mtu huru.
Hele Akabs Hus skal omkomme, jeg vil udrydde hvert mandligt Væsen, hver og en af Akabs Slægt i Israel;
9 Nitaifanya nyumba ya Ahabu kama nyumba ya Yerobohamu mwana wa Nebati na kama nyumba ya Baasha mwana wa Ahiya.
jeg vil handle med Akabs Hus som med Jeroboams, Nebats Søns, og Ba'sjas, Ahijas Søns, Hus.
10 Mbwa watamla Yezebeli katika Yezreeli, na hakutakuwa na mtu wa kumzika.” Kisha nabii akafungua mlango na kukimbia.
Og Jesabel skal Hundene æde paa Jizre'els Mark, og ingen skal jorde hende!« Derpaa lukkede han Døren op og flygtede.
11 Kisha Yehu akatoka kwenda kwa watumishi wa bwana wake, na mmoja akamwambia, “Je kila kitu kiko sawa? Kwa nini huyu mwenda wazimu amekuja kwako?” Yehu akawajibu, “Mnamjua huyo mtu na mambo asemayo.”
Da Jehu kom ud til sin Herres Folk, spurgte de ham: »Hvorledes staar det til? Hvad vilde den gale Mand hos dig?« Han svarede: »I kender jo den Mand og hans Snak!«
12 Wakasema, “Huo ni uongo. Tuambie.” Yehu akajibu, “Alisema hivi na vile juu yangu, na pia akasema, 'hivi ndivyo Yahwe asemavyo: Nimekumiminia mafuta kama mfalme juu ya Israeli.””
Men de sagde: »Udflugter! Sig os det nu!« Da sagde han: »Saaledes sagde han til mig: Saa siger HERREN: Jeg salver dig til Konge over Israel!«
13 Kisha kila mmoja wao akachukua vazi haraka na kuweka chini ya Yehu juu ya madaraja. Wakapiga baragumu na kusema, “Yehu ni mfalme.”
Øjeblikkelig tog de da hver sin Kappe og lagde under ham paa selve Trappen, og de stødte i Hornet og udraabte Jehu til Konge.
14 Katika njia hii Yehu mwana wa Yehoshafati mwana wa Nimshi akafanya njama juu ya Yoramu. Basi Yoramu alikuwa akiilinda Ramothi Gileadi, yeye na Israeli yote, kwa sababu ya Hazaeli mfalme wa Shamu,
Saaledes stiftede Jehu, Nimsjis Søn Josjafats Søn, en Sammensværgelse mod Joram. Joram havde med hele Israel forsvaret Ramot i Gilead mod Kong Hazael af Aram;
15 lakini mfalme Yoramu alikuwa amesharudi kwa Yezreeli ili kuponywa yale majeraha aliyokuwa ameyapewa na Washami, wakati akiwa anapigana dhidi ya Hazaeli mfalme wa Shamu. Yehu akawaambia watumishi wa Yoramu, “kama hili ndilo wazo lako, kisha usimwache mtu aondoke na kwenda nje ya mji, ili aende kupeleka habari hii Yezreeli.”
men Kong Joram var vendt tilbage for i Jizre'el at søge Helbredelse for de Saar, Aramæerne havde tilføjet ham, da han kæmpede med Kong Hazael af Aram. Da sagde Jehu: »Vil I som jeg, saa lad ikke en eneste slippe ud af Byen og bringe Bud til Jizre'el.«
16 Basi Yehu akaendesha gari la farasi mpaka Yezreeli; kwa kuwa Yoramu alikuwa amelala huko. Basi Ahazi mfalme wa Yuda alikuwa ameshuka chini kuonana na Yoramu.
Derpaa steg Jehu til Vogns og kørte til Jizre'el; thi der laa Joram syg, og Kong Ahazja af Juda var rejst ned for at se til ham.
17 Mlinzi alikuwa amesimama juu ya mnara katika Yezreeli, akaliona lile kundi la Yehu alipokuwa akija kwa mbali kidogo; akasema, “Naona kundi la watu wanakuja.” Yoramu akasema, “Chukua mwendesha farasi, na umtume akakutane nao; mwambie aseme, “Je mnakuja kwa amani?””
Da Vægteren, som stod paa Taarnet i Jizre'el, saa Støvskyen efter Jehu, sagde han: »Jeg ser en Støvsky!« Da sagde Joram: »Tag en Rytter og send ham ud imod dem, for at han kan spørge, om de kommer med Fred!«
18 Hivyo mwendesha farasi akatoka kumlaki; akasema, “Mfalme asema hivi: Je mnakuja kwa amani?”' Basi Yehu akasema, “Wewe una nini na amani? Geuka na unifuate nyuma.” Kisha yule mlinzi akamwambia mfalme, Yule mjumbe ameshaonana nao, lakini anarudi.”
Saa red Rytteren ham i Møde og sagde: »Saaledes siger Kongen: Kommer du med Fred?« Jehu svarede: »Hvad vedkommer det dig, om det er med Fred? Omkring, følg mig!« Vægteren meldte: »Sendebudet har naaet dem, men han kommer ikke tilbage!«
19 Kisha akapeleka mpanda farasi wa pili, ambaye alikuja kwao na kusema, “Mfalme asema hivi: 'Je mnakuja na amani?”' Yehu akajibu, “Wewe una nini na amani? Geuka na kunifuata nyuma.
Saa sendte han en anden Rytter ud; og da han var kommet hen til dem, sagde han: »Saaledes siger Kongen: Kommer du med Fred?« Jehu svarede: »Hvad vedkommer det dig, om jeg kommer med Fred? Omkring, følg mig!«
20 Tena yule mlinzi akatoa taarifa, “Amekwisha kuonana nao, lakini hatorudi. Kwa kuwa hilo gari la farasi limekuwa likiendeshwa ndivyo ambavyo Yehu mwana wa Nimshi aendeshavyo; anaendesha kwa kasi.”
Vægteren meldte: »Han har naaet dem, men han kommet ikke tilbage. Og de har en Fart paa, som var det Jehu, Nimsjis Søn, thi han farer af Sted som rasende.«
21 Hivyo Yoramu akasema, “Andaa gari langu la farasi liwe tayari.” Wakaandaa gari lake la farasi, na Yoramu mfalme wa Israeli na Ahazi mfalme wa Yuda akaendesha, kila mmoja kwenye gari lake la farasi, kumlaki Yehu. Wakamkuta kwenye mali ya Nabothi Myezreeli.
Da sagde Joram: »Spænd for!« Og da der var spændt for, kørte Kong Joram af Israel og Kong Ahazja af Juda ud hver i sin Vogn. De kørte Jehu i Møde og traf ham ved Jizre'eliten Nabots Mark.
22 Wakati Yoramu alipomuona Yehu, alisema, “Je unakuja katika hali ya amani, Yehu?” Akajibu, “Amani gani hapo, wakati uzinzi wa ukahaba hufanywa na uchawi wa mama yako Yezebeli umejaa tele?”
Da Joram fik Øje paa Jehu, spurgte han: »Kommer du med Fred, Jehu?« Men han svarede: »Hvad! Skulde jeg komme med Fred, saa længe det ikke har Ende med din Moder Jesabels Bolen og hendes mange Trolddomskunster!«
23 Basi Yoramu akarudisha magari yake ya farasi na kukimbia na kumwambia Ahazia, “Kuna udanganyifu, Ahazia.
Da drejede Joram omkring og flygtede, idet han raabte til Ahazja: »Svig, Ahazja!«
24 Ndipo Yehu akauvuta upinde wake kwa nguvu zake zote na kumpiga Yoramu kati ya mabega yake; mshale ukaenda kwenye moyo wake, akaanguka chini kwenye gari lake la farasi.
Men Jehu greb sin Bue og skød Joram i Ryggen, saa at Pilen gik igennem Hjertet, og han sank sammen i Vognen;
25 Ndipo Yehu akamwambia Bidkari nahodha wake, “Mchukue na mtupie kwenye shamba la Nabothi Myezreeni. Fikiria kuhusu vile ambavyo wewe na mimi tulivyoendesha pamoja baada ya Ahabu baba yake, Yahwe aliuweka juu unabii dhidi yake:
og Jehu sagde til sin Høvedsmand Bidkar: »Tag og kast ham hen paa Jizre'eliten Nabots Mark, thi det rinder mig i Hu, hvorledes jeg og du kørte sammen bag efter hans Fader Akab, dengang HERREN fremsatte dette Udsagn imod ham:
26 Jana niliona damu ya Nabothi na damu ya watoto wake - asema Yahwe - na nitahakikisha unalipia hili shamba - asema Yahwe. Sasa basi, mchukue na mtupe kwenye hili shamba, sawa sawa na neno la Yahwe.”
Sandelig, Nabots og hans Sønners Blod saa jeg i Gaar, lyder det fra HERREN, og jeg bringer Gengældelse over dig her paa denne Mark, lyder det fra HERREN! Tag derfor og kast ham hen paa Marken efter HERRENS Ord!«
27 Wakati Ahazi yule mfalme wa Yuda alipoliona hili, akakimbia kwa njia ya Bethi Hagani. Lakini Yehu akamfuata, na kusema, “Muulie humo kwenye gari la farasi,” na wakampiga mahali pa kupandia Guri, karibu na Ebleamu. Ahazi akakimbilia Megido na kufia pale.
Da Kong Ahazja at Juda saa det, flygtede han ad Vejen til Bet-Hagan; men Jehu satte efter ham og raabte: »Ogsaa ham!« Og i Gurpasset, i Nærheden af Jibleam, skød de ham ned i Vognen. Han undslap til Megiddo, men der døde han.
28 Watumishi wake wakaubeba mwili wake kwa magari ya farasi kwenda Yerusalemu na kumzika kwenye kaburi lake pamoja na baba zake katika mji wa Daudi.
Hans Folk førte ham til Jerusalem og jordede ham i hans Grav hos hans Fædre i Davidsbyen.
29 Basi ilikuwa mwaka wa kumi na moja wa Yoramu mwana wa Ahabu huyo Ahazia akaanza kutawala juu ya Yuda.
I Akabs Søn Jorams ellevte Regeringsaar blev Ahazja Konge over Juda.
30 Wakati Yahu alipokuja kwa Yezebeli, Yezebeli akasikia juu ya hilo, akapaka wanja kwenye macho yake, akatengeneza nywele zake vizuri, na kuchungulia kwenye dirisha.
Jehu kom nu til Jizre'el. Saa snart Jesabel hørte det, sminkede hun sine Øjne og smykkede sit Hoved og bøjede sig ud af Vinduet;
31 Kadiri Yehu alipokuwa akiingia kwenye lango, akamwambia, “Je unakuja kwa amani, wewe Zimri, muuaji wa bwana wako?”
og da Jehu kørte ind igennem Porten, raabte hun: »Kommer du med Fred, Zimri Kongemorder?«
32 Yehu akatazama juu ya dirisha na kusema, “Ni nani yuko upande wangu? Nani?” Matowashi wawili au watatu wakachungulia nje.
Men han saa op til Vinduet og sagde: »Hvem holder med mig? Hvem?« Saa var der et Par Hofmænd, som saa ud efter ham,
33 Basi Yehu aksema, “Mtupeni chini.” Hivyo wakamtupa Yezebeli chini, na damu yake nyingine ikamwagika kwenye ukuta na farasi, na Yehu akamkanyaga kanyaga chini ya miguu.
og han raabte: »Styrt hende ned!« Saa styrtede de hende ned, og Blodet sprøjtede op paa Muren og paa Hestene, og de traadte hende ned.
34 Basi Yehu akaingia hiyo sehemu, akala na kunywa. Kisha akasema, “Mtazamani sasa huyu mwanamke aliyelaaniwa na kumzika, kwa kuwa ni binti wa mfalme.”
Derpaa gik han ind og spiste og drak. Saa sagde han: »Tag jer af hende, den forbandede, og jord hende, hun var jo dog en Kongedatter!«
35 Wakaenda kumzika, lakini hawakumkuta ila fuvu, miguu, na viganga vya mikono yake.
Men da de gik ud for at jorde hende, fandt de ikke andet af hende end Hjerneskallen, Fødderne og Hænderne.
36 Basi wakarudi na kumwambia Yehu. Akasema, “Hili ndilo neno la Yahwe ambalo ameliongea kupitia Eliya Mtishbi, likisema, 'Katika nchi Yezreeli mbwa ataula mwili wa Yezebeli,
Og de kom tilbage og meldte ham det; da sagde han: »Det er det Ord, HERREN talede ved sin Tjener Tisjbiten Elias: Paa Jizre'els Mark skal Hundene æde Jesabels Legeme!
37 na mwili wa Yezebeli utakuwa kama kinyesi juu ya uso wa mashamba katika nchi ya Yezreeli, kwa hiyo basi hakuna atakayeweza kusema, “Huyu ni Yezebeli.””
og Jesabels Lig skal blive som Gødning paa Ageren paa Jizre'els Mark, saa ingen kan sige: Dette er Jesabel!«

< 2 Wafalme 9 >