< 2 Wafalme 8 >

1 Basi, Elisha alikuwa amemwambia yule mwanamke ambaye alimfufulia mtoto wake. Akamwambia, “Inuka na uenede pamoja na nyumba yako, na uishi popote uwezapo katika nchi nyingine, kwa sababu Yahwe ameiita njaa ambayo itakuja katika hii nchi kwa miaka saba.”
And Elisha he spoke to the woman whom he had restored to life son her saying arise and go (you *QK) and household your and sojourn in where you will sojourn for he has called Yahweh for famine and also it will come to the land seven years.
2 Basi yule mwanamke akainuka na akatii lile neno la mtumishi wa Mungu. Akaenda na nyumba yake na kuishi kwenye nchi ya Wafilisti miaka saba.
And she arose the woman and she did according to [the] word of [the] man of God and she went she and household her and she sojourned in [the] land of [the] Philistines seven years.
3 Ikafika kama mwishoni mwa miaka saba yule mwanamke akarudi kutoka kwenye ile nchi ya Wafilisti, na kwenda kwa mfalme kumuomba nyumba yake na kwa ajili ya nchi yake.
And it was from [the] end of seven years and she returned the woman from [the] land of [the] Philistines and she went out to cry out to the king concerning house her and concerning field her.
4 Basi mfalme alikuwa anaongea na Gehazi yule mtumishi wa Mungu, akisema, “Tafadhali niambie yale mambo makubwa ambayo Elisha ameyafanya.”
And the king [was] speaking to Gehazi [the] servant of [the] man of God saying recount! please to me all the great [things] which he has done Elisha.
5 Basi alipokuwa akimwambia yule mfalme jinsi gani Elisha alivyomfufua yule mtoto aliyekufa, huyo mwanamke ambaye mtoto wake aliyekuwa amefufuliwa akaja kumuomba yule mfalme kwa ajili ya nyumba yake na nchi yake. Gehazi akasema, “Bwana wangu, mfalme, huyu ndiye yule mwanamke, na huyu ndiye mtoto wake, ambaye Elisha amemfufua.”
And he was he recounting to the king this: he had restored to life the dead [one] and there! the woman whom he had restored to life son her [was] crying out for help to the king on house her and on field her and he said Gehazi O lord my the king this [is] the woman and this [is] son her whom he restored to life Elisha.
6 Wakati yule mfalme alipomuuliza yule mwanamke kuhusu mtoto wake, alimwelezea yule mfalme. Ndipo mfalme akamwagizia ofisa makini, akisema, “Mrudishie vyote vilivyokuwa vyake na mavuno yake yote ya kwenye mashamba tangu siku alipoondoka hadi sasa.”
And he asked the king the woman and she recounted to him and he assigned to her the king a court-official one saying restore all that [belonged] to her and all [the] produce of the field from [the] day [when] she left the land and until now.
7 Elisha akaja Damaskasi ambako Ben Hadadi yule mfalme wa Shamu alikuwa anaumwa. Yule mfalme aliambiwa, “Yule mtu wa Mungu amekuja hapa.”
And he went Elisha Damascus and Ben Hadad [the] king of Aram [was] sick and it was told to him saying he has come [the] man of God to here.
8 Mfalme akamwambia Hazaeli, “Chukua zawadi kwenye mkono wako na uende ukakutane na mtu wa Mungu, na ukazungumze na Yahwe kupitia yeye, ukisema, “Je nitapona huu ugonjwa wangu?”
And he said the king to Hazael take in hand your a gift and go to meet [the] man of God and you will consult Yahweh from him saying ¿ will I live from sickness this.
9 Basi Hazaeli akaenda kuonana naye na kuchukua zawadi zake za kila kitu kizuri cha Damskasi, akabeba ngamia arobaini. Hivyo Hazaeli akaja na kusimama mbele ya Elisha na kusema, “Mtoto wako Ben Hadadi mfalme wa Shamu amenituma kwako, kusema, “Je nitapona huu ugonjwa?”
And he went Hazael to meet him and he took a gift in hand his and every good thing of Damascus [the] load of forty camel[s] and he came and he stood before him and he said son your Ben Hadad [the] king of Aram he has sent me to you saying ¿ will I live from sickness this.
10 Elisha akamwambia, “Nenda, kwa Ben Hadadi, 'Utapona hakika,' lakini Yahwe amenionyesha kwamba atakufa hahkika.”
And he said to him Elisha go say (to him *QK) certainly you will live and he has shown me Yahweh that certainly he will die.
11 Basi Elisha akamtumbulia macho Hazaeli hadi alipojisikia aibu, na yule mtu wa Mungu akalia machozi.
And he set face his and he set until was ashamed and he wept [the] man of God.
12 Hazaeli akauliza, kwa nini unalia, bwana wangu?” Akajibu, “Kwa sababu najua uovu ambao utakaoufanya kwa watu wa Israeli. Utazichoma moto ngome zao kwa moto, na utawaua vijana wao kwa upanga, kuwaseta vipande vipande watoto wao wachanga, na kuwapasua mimba zao wanawake wenye mimba.”
And he said Hazael why? [is] lord my weeping and he said for I know this: you will do to [the] people of Israel harm fortifications their you will send in fire and young men their with the sword you will kill and children their you will dash in pieces and pregnant [women] their you will rip open.
13 Hazaeli akajibu, Ni nani mtumwa wako, ambaye atafanya jambo hili kubwa? Yeye ni mbwa tu.” Elisha akajibu, “Yahwe amenionyesha kwamba utakuwa mfalme juu ya Shamu.”
And he said Hazael that what? [is] servant your the dog that he will do the thing great this and he said Elisha he has shown me Yahweh you king over Aram.
14 Ndipo Hazaeli akamwacha Elisha na kuja kwa bwana wake, ambaye alimwambia, “Je Elisha alikwambiaje?” Akajibu, “Ameniambia kwamba utapona bila shaka.”
And he went - from with Elisha and he came to master his and he said to him what? did he say to you Elisha and he said he said to me certainly you will live.
15 Basi siku ya pili yake Hazaeli akachukua blangeti na kulichovya kwenye maji, na kulitandaza kwenye uso wa Ben Hadadi hivyo akafa. Basi Hazaeli akawa mfalme katika sehemu sehemu yake.
And it was from [the] next day and he took the coverlet and he dipped [it] in water and he spread [it] out over face his and he died and he became king Hazael in place of him.
16 Katika mwaka wa kumi na tano wa Yoramu mwana wa Ahabu, mfalme wa Israeli, Yehoramu akaanza kutawala. Alikuwa mwana wa Yehoshafati mfalme wa Yuda. Alianza wakati Yehoshafati alikuwa mfalme wa Yuda.
And in year five of Joram [the] son of Ahab [the] king of Israel and Jehoshaphat [was] [the] king of Judah he became king Jehoram [the] son of Jehoshaphat [the] king of Judah.
17 Yoramu alikuwa na umri wa miaka thelathini na mbili alipoanza kutawala, na alitawala kwa mda wa miaka minane katika Yerusalemu.
A son of thirty and two year[s] he was when became king he and eight (years *QK) he reigned in Jerusalem.
18 Yoramu akatembea kwenye njia ya huyo mfalme wa Israeli, kama walivyokuwa wakifanya kwenye nyumba ya Ahabu; kwa kuwa alikuwa na binti wa Ahabu kama mke wake, na alifanya uovu usoni kwa Yahwe.
And he walked in [the] way of - [the] kings of Israel just as they did [the] house of Ahab for [the] daughter of Ahab she became of him a wife and he did the evil in [the] eyes of Yahweh.
19 Walakini, kwa sababu ya mtumishi wake Daudi, Yahwe hakutaka kuiharibu Yuda, tangu alipomwambia kwamba atampatia wazao.
And not he was willing Yahweh to destroy Judah for [the] sake of David servant his just as he had said to him to give to him a lamp to sons his all the days.
20 Katika siku za Yoramu, Edomu akaasi kutoka chini ya mkono wa Yuda, na wakamfanya mfalme juu yao wenyewe.
In days his it rebelled Edom from under [the] hand of Judah and they made king over themselves a king.
21 Basi Yehoramu akaenda na maamri jeshi na magari ya farasi yote. Ilitokea kwamba akaamka usiku na kushambulia na kuwazunguka Waedomu, waliokuwa wamemzunguka na wale maamri jeshi wa magari ya farasi. Ndipo wanajeshi wa Yehoramu wakakimbilia wajumbani kwao.
And he passed over Joram Zair towards and all the chariotry [was] with him and it was he he arose night and he struck down Edom which was surrounding him and [the] commanders of the chariotry and it fled the people to tents its.
22 Hivyo Edomu aliasi dhidi ya utawala wa Yuda katika siku hizi. Libna pia aliasi katika kipindi hicho hicho.
And it has rebelled Edom from under [the] hand of Judah until the day this then it rebelled Libnah at the time that.
23 Kwa mambo mengine yamhusuyo Yehoramu, yote aliyoyafanya, je hayakuandikwa kwenye kitabu cha matukio ya mfalme wa Yuda?
And [the] rest of [the] matters of Joram and all that he did ¿ not [are] they written on [the] scroll of [the] matters of the days of [the] kings of Judah.
24 Yehoramu akafa na kuzikwa pamoja na baba zake, na akalala pamoja na baba zake katika mji wa Daudi. Ndipo Ahazi mtoto wake akawa mfalme katika sehemu yake.
And he lay down Joram with ancestors his and he was buried with ancestors his in [the] city of David and he became king Ahaziah son his in place of him.
25 Katika mwaka wa kumi na mbili wa Yohoramu mwana wa Ahabu, mfalme wa Israeli, Ahazi mwana wa Yehoramu, mfalme wa Yuda, alianza kutawala.
In year two plus ten year of Joram [the] son of Ahab [the] king of Israel he became king Ahaziah [the] son of Jehoram [the] king of Judah.
26 Ahazi alikuwa ana umri wa miaka ishirini na mbili wakati alipoanza kutawala; alitawala kwa mda wa mwaka mmoja katika Yerusalemu. Mama yake alikuwa anaitwa Athalia; alikuwa mtoto wa Omri, mfalme wa Israeli.
[was] a son of Twenty and two year[s] Ahaziah when became king he and a year one he reigned in Jerusalem and [the] name of mother his [was] Athaliah [the] daughter of Omri [the] king of Israel.
27 Ahazia alitembelea katika nyumba ya Ahabu; alifanya yale yaliyo maovu katika uso wa Yahwe, kama nyumba ya Ahabu ilivyokuwa ikifanya, kwa kuwa Ahazia alikuwa mkwe kwenye nyumba ya Aabu.
And he walked in [the] way of [the] house of Ahab and he did the evil in [the] eyes of Yahweh like [the] house of Ahab for [was] [the] son-in-law of [the] house of Ahab he.
28 Ahazia akaenda pamoja na Yoramu mwana wa Ahabu, kupigana dhidi ya Hazaeli, mfalme wa Shamu, katika Ramath Geleadi. Washami wakamjeruhi Yoramu.
And he went with Joram [the] son of Ahab for battle with Hazael [the] king of Aram at Ramoth Gilead and they wounded [the] Arameans Joram.
29 Mfalme Yoramu akarudi ili auguzwe huko Yezreeli kwenye yale majeraha ambayo Washami walimpatia huko Rama. Wakati alipopigana dhidi ya Hazaeli mfalme wa Shamu. Hivyo Ahazi mwana wa Yehoramu, mfalme Yuda, akashuka kwa Yezreeli kumuona Yoramu mwana wa Ahabu, kwa sababu Yoramu alikuwa amejeruhiwa.
And he returned Joram the king to get himself healed in Jezreel from the wounds which they wounded him [the] Arameans at Ramah when fought he with Hazael [the] king of Aram and Ahaziah [the] son of Jehoram [the] king of Judah he went down to see Joram [the] son of Ahab in Jezreel for [was] sick he.

< 2 Wafalme 8 >