< 2 Wafalme 2 >

1 Hivyo ilipokuja kuhusu, wakati Yahwe alipokuwa akienda kumchukua Eliya kwenda mbinguni kwa uvumi, ambapo Eliya aliondoka pamoja na Elisha kutoka Gigali.
And it came to pass, when the LORD would take up Elijah by a whirlwind into heaven, that Elijah went with Elisha from Gilgal.
2 Eliya akamwambia Elisha, '“kaa hapa, tafadhali, kwa sababu Yahwe alinituma kwa Betheli.'” Elisha akajibu, “Kama Yahwe aishivyo, na kama uishivyo, sintokuacha.'” Hivyo wakashuka chini kulekea Betheli.
And Elijah said unto Elisha: 'Tarry here, I pray thee; for the LORD hath sent me as far as Beth-el.' And Elisha said: 'As the LORD liveth, and as thy soul liveth, I will not leave thee.' So they went down to Beth-el. —
3 Wana wa manabii ambao walikuwa Betheli walikuja kwa Elisha na kumwambia, je unajua kwamba Yahwe atamwondoa bwana wako kuanzia leo?”' Elisha akajibu, “Ndiyo, nalijua hilo, ila msizungumze kuhusu hilo.”'
And the sons of the prophets that were at Beth-el came forth to Elisha, and said unto him: 'Knowest thou that the LORD will take away thy master from thy head to-day?' And he said: 'Yea, I know it; hold ye your peace.' —
4 Eliya akamwambia, “Elisha, subiri hapa, tafadhali, kwa kuwa Yahwe amenituma niende Yeriko.” Kisha Elisha akajibu, '“Kama Yahwe aishivyo, na kama uishivyo, sintokuacha.” Hivyo wakaenda Yeriko.
And Elijah said unto him: 'Elisha, tarry here, I pray thee; for the LORD hath sent me to Jericho.' And he said: 'As the LORD liveth, and as thy soul liveth, I will not leave thee.' So they came to Jericho. —
5 Kisha wana wa manabii ambao walikuwa Yeriko wakaja kwa Elisha na kumwambia, “'Je unajua kwamba Yahwe atamwondoa bwana wako kutoka kwako leo?” Elisha akajibu, “Ndiyo, nalijua hilo, lakini msilizungumzie hilo.”
And the sons of the prophets that were at Jericho came near to Elisha, and said unto him: 'Knowest thou that the LORD will take away thy master from thy head to-day?' And he answered: 'Yea, I know it; hold ye your peace.' —
6 Kisha Eliya akamwambia, '“kaa hapa, tafadhali, kwa kuwa Yahwe amenituma kwenda Yeriko.” Elisha akajibu, “Kama Yahwe ishivyo, na kama uishivyo, sintokuacha.” Hivyo wawili wakaenda mbele.
And Elijah said unto him: 'Tarry here, I pray thee; for the LORD hath sent me to the Jordan.' And he said: 'As the LORD liveth, and as thy soul liveth, I will not leave thee.' And they two went on.
7 Baadaye watu hamsini wa watoto wa wale manabii wakasimama kuwakabili kwa mbali kidogo wale wawili wakasimama karibu na Yordani.
And fifty men of the sons of the prophets went, and stood over against them afar off; and they two stood by the Jordan.
8 Eliya akachukua vazi lake, akaliviringisha, na kuyapiga maji kwa kutumia lile vazi. Ule mto ukagawanyika katika sehemu mbili hivyo basi wawili hao wakatembea hadi nchi kavu.
And Elijah took his mantle, and wrapped it together, and smote the waters, and they were divided hither and thither, so that they two went over on dry ground.
9 Ilitokea, walipokwisha kuvuka, kwamba Eliya akamwambia Elisha, “Niambie unachotaka nifanye kwako kabla sijaondolewa kutoka kwako.” Elisha akajibu, “Naomba sehemu kubwa ya roho yako ije kwangu.
And it came to pass, when they were gone over, that Elijah said unto Elisha: 'Ask what I shall do for thee, before I am taken from thee.' And Elisha said: 'I pray thee, let a double portion of thy spirit be upon me.'
10 Eliya akajibu, “Umeomba jambo gumu. Hata hivyo, kama ukiniona wakati nitakapoondolewa kutoka kwako, hii itatokea kwako, lakini kama sivyo, haitatokea.”
And he said: 'Thou hast asked a hard thing; nevertheless, if thou see me when I am taken from thee, it shall be so unto thee; but if not, it shall not be so.'
11 Ikawa walipokuwa bado wakienda mbele na kuzungumza, gari la kukokotwa na farasi lenye moto na farasi wa moto ikatokea, ambapo iliwatenga wale watu wawili kutoka kila mmoja, na Eliya akaenda juu kwa uvumi wa upepo kwenda mbinguni.
And it came to pass, as they still went on, and talked, that, behold, there appeared a chariot of fire, and horses of fire, which parted them both assunder; and Elijah went up by a whirlwind into heaven.
12 Elisha akaiona akalia kwa sauti, “Baba yangu, baba yangu, gari la kukokotwa na farasi la Israeli na waendesha farasi!'” Hakumwona Eliya tena, na akashikilia nguo zake mwenyewe na kugawanya kwenye vipande viwili.
And Elisha saw it, and he cried: 'My father, my father, the chariots of Israel and the horsemen thereof!' And he saw him no more; and he took hold of his own clothes, and rent them in two pieces.
13 Akachukua vazi la Eliya lililokuwa limemwangukia, na kurudi kusimama kwenye ukingo wa Yordani.
He took up also the mantle of Elijah that fell from him, and went back, and stood by the bank of the Jordan.
14 Akayapiga maji pamoja na lile vazi la Eliya alilokuwa ameliangusha na kusema, “Yahwe yuko wapi, Mungu wa Eliya?'” Wakati alipoyapiga yale maji, yaligawanyika katika pande mbili na Elisha akavuka.
And he took the mantle of Elijah that fell from him, and smote the waters, and said: 'Where is the LORD, the God of Elijah?' and when he also had smitten the waters, they were divided hither and thither; and Elisha went over.
15 Wakati hao wana wa manabii ambao walitoka Yeriko walipomuona akikatiza kwao, wakasema, “roho ya Eliya imepumzika kwa Elisha!” Hivyo wakaja kuonana naye, na wakasujudu aridhini mbele yake.
And when the sons of the prophets that were at Jericho some way off saw him, they said: 'The spirit of Elijah doth rest on Elisha.' And they came to meet him, and bowed down to the ground before him.
16 Wakamwambia, “Ona sasa, miongoni mwa watumishi wako kuna watu hamsini hodari. Tunakuomba Waache waende, na kumtafuta bwana wako, endapo huyo Roho wa Yahwe alipomchukua juu na kumtupa juu ya mlima mmoja au kwenye bonde moja.” Elisha akajibu, “Hapana, msiwatume.”
And they said unto him: 'Behold now, there are with thy servants fifty strong men; let them go, we pray thee, and seek thy master; lest peradventure the spirit of the LORD hath taken him up, and cast him upon some mountain, or into some valley.' And he said: 'Ye shall not send.'
17 Lakini walimsihi Elisha hadi akaona aibu, akasema, “Watume.”Ndipo wakawatuma watu hamsini, na wakatafuta kwa mda wa siku tatu, lakini hawakumpata.
And when they urged him till he was ashamed, he said: 'Send.' They sent therefore fifty men; and they sought three days, but found him not.
18 Wakarudi kwa Elisha, wakati alipokuwa bado yuko Yeriko, na akasema, “Je sikusema, 'msiende'?”
And they came back to him, while he tarried at Jericho; and he said unto them: 'Did I not say unto you: Go not?'
19 Watu wa mjini wakamwambia Elisha, “Ona, tunakuomba, hali ya mjini hapa ni pazuri, kama bwana wangu awezavyo kuona, lakini maji ni mabaya na hiyo nchi haiwezi kuzaa matunda.”
And the men of the city said unto Elisha: 'Behold, we pray thee, the situation of this city is pleasant, as my lord seeth; but the water is bad, and the land miscarrieth.
20 Elisha akajibu, “Nileteeni bakuli jipya na muweke chumvi ndani ya hilo bakuli,” hivyo wakamletea.
And he said: 'Bring me a new cruse, and put salt therein.' And they brought it to him.
21 Elisha akaenda hadi kwenye chemichemi za maji na kutupia chumvi ndani; halafu akasema, “Yahwe asema hivi, 'Nimeyaponya haya maji. Kuanzia mda huu, hakutakuwa na kifo au nchi isiyozaa matunda.
And he went forth unto the spring of the waters, and cast salt therein, and said: 'Thus saith the LORD: I have healed these waters; there shall not be from thence any more death or miscarrying.'
22 “Hivyo hayo maji yakaponya hata leo, kwa lile neno ambalo Elisha aliongea.
So the waters were healed unto this day, according to the word of Elisha which he spoke.
23 Ndipo Elisha akapanda kutoka pale mpaka Betheli. Naye alipokuwa akienda hadi kwenye barabara, wakatokea vijana nje ya mji na kumtania, wakamwambia, “Panda juu, wewe mwenye kipara! Panda juu, wewe mwenye kipara!”
And he went up from thence unto Beth-el; and as he was going up by the way, there came forth little children out of the city, and mocked him, and said unto him: 'Go up, thou baldhead; go up, thou baldhead.'
24 Elisha alipotazama nyuma yake na kuwaona; alimwambia Yahwe awalaani. Ndipo dubu wa kike wawili wakatokea kichakani na kuwajeruhi vijana arobaini na mbili.
And he looked behind him and saw them, and cursed them in the name of the LORD. And there came forth two she-bears out of the wood, and tore forty and two children of them.
25 Ndipo Elisha alipoondoka pale na kuelekea Mlima Karmeli, na kutoka huko alirudi samaria.
And he went from thence to mount Carmel, and from thence he returned to Samaria.

< 2 Wafalme 2 >