< 2 Wafalme 18 >

1 Ikawa katika mwaka wa tatu wa Hoshea mwana wa Ela, mfalme wa Israeli, Hezekia mwana wa Ahazi, mfalme wa Yuda akaanza kutawala.
W trzecim roku Ozeasza, syna Eli, króla Izraela, Ezechiasz, syn Achaza, króla Judy, [zaczął] królować.
2 Alikuwa na umri wa miaka ishirini na tano alipoanza kutawala; alitawala miaka ishirini na tisa katika Yerusalemu. Jina la mama yake alikuwa anaitwa Abija; alikuwa binti wa Zekaria.
Miał on dwadzieścia pięć lat, kiedy zaczął królować, i królował dwadzieścia dziewięć lat w Jerozolimie. Jego matka [miała] na imię Abi [i była] córką Zachariasza.
3 Alifanya yaliyo mema usoni pa Yahwe, kufuata mfano wa yote ambayo Daudi, babu yake, aliyoyafanya.
Czynił on to, co było słuszne w oczach PANA, wszystko tak, jak czynił Dawid, jego ojciec.
4 Alipaondoa mahali pa juu, akaiharibu nguzo ya jiwe, akaikata hiyo nguzo ya Ashera. Akavunja vipande vipande ile nyoka ambayo Musa aliyokuwa ameifanya, kwa sababu siku zile wana wa Israeli walikuwa wakichoma ubani katika hiyo; ilikuwa inaitwa “Nehushtani.”
Zniósł wyżyny, rozbił posągi, powycinał gaje i potłukł węża miedzianego, którego uczynił Mojżesz, bo aż do tego czasu synowie Izraela palili mu kadzidło, i nazwał go Nehustan.
5 Hezekia alimwamini Yahwe, Mungu wa Israeli, hivyo basi baada ya yeye hapakuwa kama yeye miongoni mwa wafalme wote wa Yuda, wala miongoni mwa wafalme ambao walikuwa kabla yake.
Zaufał PANU, Bogu Izraela. I spośród wszystkich królów Judy nie było nikogo podobnego do niego ani [z tych, którzy byli] po nim, ani [z tych], którzy byli przed nim.
6 Aliambatana na Yahwe. Hakuacha kumfuata lakini alizifuata amri zake, ambazo Yahwe alimwamuru Musa.
Przylgnął bowiem do PANA i nie odstępował od niego, ale przestrzegał jego przykazań, które PAN nadał Mojżeszowi.
7 Hivyo Yahwe alikuwa na Hezekia, kila alipokwenda alifanikiwa. Akaasi dhidi ya mfalme wa Ashuru na hakumtumikia.
A PAN był z nim i powodziło mu się, gdziekolwiek wyruszał. Zbuntował się przeciw królowi Asyrii i nie służył mu.
8 Akawashambulia Wafilisti hadi Gaza na mipaka inayoizunguka, kutoka mnara wa walinzi hadi hadi mji wenye ngome.
To on pokonał Filistynów aż do Gazy i jej granic, od wieży strażników aż do miasta warownego.
9 Katika mwaka wa nne wa Mfalme Hezekia, ambao ulikuwa mwaka wa saba wa Hoshea mwana wa Ela mfalme wa Israeli, Shalmanesa mfalme wa Ashuru akapanda hadi Samaria na kuizunguka.
W czwartym roku króla Ezechiasza – był to siódmy rok Ozeasza, syna Eli, króla Izraela – Salmanaser, król Asyrii, wyruszył przeciwko Samarii i obległ ją.
10 Mwishoni mwa miaka mitatu wakaichukua, katika mwaka wa sita wa Hezekia, ambao ulikuwa mwaka wa tisa wa Hoshea mfalme wa Israeli; hivi ndivyo Samaria ilivyotekwa.
I zdobył ją pod koniec trzeciego roku. W szóstym roku Ezechiasza – był to dziewiąty rok Ozeasza, króla Izraela – Samaria została zdobyta.
11 Basi mfalme wa Ashuru akawachukua Israeli kwenda Ashuru na kuwaweka kwenye Hala, na katika mto Habori katika Gozani, na katika mji wa Wamedi.
Wtedy król Asyrii uprowadził Izraela do Asyrii i osiedlił ich w Chalach i Chaborze, przy rzece Gozanu, i w miastach Medów;
12 Alifanya hivi kwasababu hakutii sauti ya Yahwe Mungu wao, lakini walikiuka makubaliano ya agano lake, yote yale ambayo Musa yule mtumishi wa Yahwe aliwaamuru. Walikataa kuyasikiliza au kuyafanya.
Ponieważ nie posłuchali głosu PANA, swego Boga, ale przekroczyli jego przymierze [oraz] to wszystko, co nakazał Mojżesz, sługa PANA. Nie słuchali tego i nie wypełniali.
13 Kisha katika mwaka wa kumi na nne wa mfalme Hezekia, Senakerebu mfalme wa Ashuru akaishambulia miji yote yenye boma na kuwateka mateka.
W czternastym roku króla Ezechiasza Sennacheryb, król Asyrii, wyruszył przeciw wszystkim warownym miastom Judy i zdobył je.
14 Basi Hezekia mfalme wa Yuda akatuma neno kwenda kwa mfalalme wa Yuda akatuma neno kwa mfalme wa Ashuru, ambaye alikuwa Lachishi, akisema, “Nimekuudhi. Nichukue. Popote utakaponiweka nitavumulia”. Mfalme wa Ashuru akamtaka Hezekia mfalme wa Yuda kulipa talanta mia tatu za fedha na talanta thelathini za dhahabu.
Wtedy Ezechiasz, król Judy, posłał do króla Asyrii do Lakisz, mówiąc: Postąpiłem źle, odstąp ode mnie. Cokolwiek na mnie nałożysz, poniosę. Król Asyrii nałożył więc na Ezechiasza, króla Judy, trzysta talentów srebra i trzydzieści talentów złota.
15 Hivyo Hezekia akampatia fedha zote ambazo zilikuwa zimepatikana kwenye nyumba ya Yahwe na kawenye hazina nyumba ya mfalme.
I Ezechiasz dał mu całe srebro, które się znalazło w domu PANA i w skarbcach domu królewskiego.
16 Kisha Hezekia akaikata ile dhahabu kutoka kwenye milango ya hekalu la Yahwe na kutoka juu ya nguzo; akampatia dhahabu mfalme wa Ashuru.
W tym samym czasie Ezechiasz zerwał złoto z drzwi domu PANA oraz ze słupów, które obił [sam] Ezechiasz, król Judy, i dał je królowi Asyrii.
17 Lakini mfalme wa Ashuru akalihamasisha jeshi lake kubwa, akawatuma Tartani na Rabsarisi na amiri jeshi mkuu kutoka Lakishi kwenda kwa Hezekia huko Yerusalemu. Wakasafiri hadi kwenye mabarabara na kufika nje ya Yerusalemu. Wakakaribia karibu na mfereji wa birika la juu, kwenye barabara kuu ya shamba la dobi, na kusimama hapo.
Jednakże król Asyrii posłał z Lakisz Tartana, Rabsarisa i Rabszaka z wielkim wojskiem do Jerozolimy, do króla Ezechiasza. Wyruszyli i przybyli do Jerozolimy. Gdy przybyli, przyszli i zatrzymali się przy kanale górnej sadzawki, która jest przy drodze pola folusznika.
18 Wakati walipokuwa wamemwita Mfalme Hezekia, Eliakimu mwana wa Hilkia, ambaye alikuwa kiongozi wa nyumba ya mfalme na Shebna mwandishi, na Joa mwana wa Asafu, anayeandika kumbukumbu, wakatoka nje kwenda kuwalaki
A gdy wołali do króla, wyszli do nich Eliakim, syn Chilkiasza, przełożony domu, Szebna, pisarz, oraz Joach, syn Asafa, kronikarz.
19 Basi yule amiri jeshi mkuu akawaambia wamwambie Hezekia kile alichosema mfalme mkuu, mfalme wa Ashuru, amesema: “Nini chanzo cha ujasiri wako?
Wtedy Rabszak powiedział do nich: Powiedzcie Ezechiaszowi: Tak mówi wielki król, król Asyrii: Co to za ufność, na której polegasz?
20 Unaongea maneno yasiyo na maana, kusema lipo neno na nguvu ya vita. Sasa unamtumainia nani? Nani anakupa ujasiri wa kuasi dhidi yangu?
Mówisz – ale to słowa daremne – mam dość rady i siły do wojny. Teraz więc w kim pokładasz ufność, że zbuntowałeś się przeciwko mnie?
21 Tazama, unatumainia kutembelea fimbo ya mwanzi huu uliopondeka wa Misri, lakini kama mtu akiutegemea, utamchapa kwenye mkono wake na kuutoboa. Hicho ndicho Farao mfalme wa Misri kwa ymtu yeyote ambaye anayemtumainia.
Oto teraz opierasz się na tej nadłamanej lasce trzcinowej – na Egipcie – która gdy ktoś się oprze na niej, wbija mu się w dłoń i przebija ją. Taki jest faraon, król Egiptu, dla wszystkich, którzy mu ufają.
22 Lakini kama ukiniambia, 'Tunamwamini Yahwe Mungu watu; je si yeye ambaye mahali pa juu na madhabahu Hezekia amezichukua, na kumwambia Yuda na kwa Yerusalemu, 'Lazima uabudu mbele ya hii madhabahu katika Yerusalemu'?
A jeśli mi powiecie: Ufamy PANU, naszemu Bogu – czy on nie jest tym, którego wyżyny i ołtarze zniósł Ezechiasz i nakazał Judzie i Jerozolimie: Przed tym ołtarzem w Jerozolimie będziecie oddawać pokłon?
23 Basi kwa hiyo, nataka kukufanyia ahadi nzuri kutoka kwa bwana wangu mfalme wa Ashuru. Nitakupatia farasi elfu mbili, kama unaweza kuwatafuta kuwaendesha kwa ajili yao.
Dlatego teraz proszę, daj zastaw memu panu, królowi Asyrii, a dam ci dwa tysiące koni, jeśli zdołasz posadzić na nich jeźdźców.
24 Wanawezaje kumpinga hata nahodha mmoja wa watumishi walio wadogo? Mmeweka tumaini lenu katika Misri kwa magari ya farasi na waendesha farasi!
Jakże więc stawisz opór jednemu dowódcy z najmniejszych sług mego pana, a pokładasz nadzieję w Egipcie, że [otrzymasz] rydwany i jeźdźców?
25 Je nimesafiri kwenda huko juu bila Yahwe kupapigania hapa mahali na kupaharibu? Yahwe ameniambia, 'Ishambulie hii nchi na uiharibu.”'
Poza tym – czy bez [woli] PANA wyruszyłem przeciw temu miejscu, aby je zburzyć? PAN powiedział do mnie: Wyrusz przeciwko tej ziemi i spustosz ją.
26 Kisha Elikana mwana wa Hilkia, na Shebna, na Joa wakamwambia amiri jeshi mkuu, “Tafadhali ongea na watumishi wako katika lugha ya Kiaramu, kwa kuwa tunaielewa. Usiongee nasi katika lugha ya Yuda katika masikio ya watu ambao wako ukutani.”
Wtedy Eliakim, syn Chilkiasza, Szebna i Joach powiedzieli do Rabszaka: Proszę, mów do swoich sług po syryjsku, bo rozumiemy, a nie mów z nami po hebrajsku wobec ludu, który jest na murze.
27 Lakini yule amiri jeshi mkuu akawaambia, “Je bwana wangu amenituma kwa bwana wako na kuwachukua kuongea haya maneno? Je hajanituma kwa hawa watu ambao wameketi kwenye ukuta, ambao watakula kinyesi chao na kunywa mkojo wao wenyewe?”
Lecz Rabszak odpowiedział: Czy do twego pana i do ciebie posłał mnie mój pan, abym mówił te słowa? Czyż nie do tych mężczyzn siedzących na murze, aby jedli swój kał i pili swój mocz razem z wami?
28 Kisha yule amiri jeshi mkuu akasimama na akapiga kelele kubwa kwa lugha ya Kiyahudi, akisema, “Sikilizeni neno la mfalme mkuu, mfale wa Ashuru.
Wstał więc Rabszak i zawołał donośnym głosem po hebrajsku tymi słowami: Słuchajcie słów wielkiego króla, króla Asyrii.
29 Mfalme asema, 'Msimwache Hezekia akawadanganya, kwa kuwa hataweza kuwaokoa kwenye nguvu yangu.
Tak mówi król: Niech was nie zwodzi Ezechiasz, bo nie będzie mógł wyrwać was z mojej ręki.
30 Msimwache Hezekia akawatumainisha katika Yahwe, akisema, “Yahwe atatuokoa hakika, na huu mji hautawekwa kwenye mkono wa mfalme wa Ashuru.'”
I nie dajcie się przekonać Ezechiaszowi, by zaufać PANU, gdy mówi: Na pewno PAN nas wybawi i to miasto nie będzie wydane w ręce króla Asyrii.
31 Msikilize Hezekia, kwa kuwa hivi ndivyo mfalme wa Ashuru asemavyo: 'Fanyeni amani pamoja nami na njooni kwangu. Kisha kila mmoja wenu atakula kutoka kwenye mzabibu wake mwenyewe na kutoka kwenye mtini wake mwenyewe, na kunywa kutoka kwenye maji kwenye maji ya birika lake mwenyewe.
Nie słuchajcie Ezechiasza. Tak bowiem mówi król Asyrii: Zawrzyjcie ze mną przymierze i wyjdźcie do mnie, a każdy będzie jeść ze swojej winorośli i ze swego drzewa figowego i każdy będzie pić wodę ze swojej studni;
32 Mtafanya hivyo hadi nitakapokuja na kuwachukua kwenda kwenye nchi kama nchi yenu, nchi ya nafaka na divai, nchi ya mkate na mashamba ya mizabibu, nchi ya miti ya mizaituni na asali, ili muweze kuishi na sio kufa.' Msimsikilize Hezekia wakati atakapojaribu kuwashawishi, akisema, 'Yahwe atatuokoa.'
Aż przyjdę i zabiorę was do ziemi podobnej do waszej, do ziemi zboża i wina, do ziemi chleba i winnic, do ziemi drzew oliwnych, oliwy i miodu. Będziecie żyć, a nie umierać. Nie słuchajcie Ezechiasza, bo was zwodzi, mówiąc: PAN nas wybawi.
33 Je miungu yeyote ya watu inayewaokoa kutoka kwenye nchi ya mfalme wa Ashuru?
Czy bogowie [innych] narodów mogli wybawić swoją ziemię z ręki króla Asyrii?
34 Iko wapi miungu ya Hamathi na Arpadi? iko wapi miungu ya Sefarvaimu, Hena, na Iva? Je imeiokoa Samaria kutoka mkono wangu?
Gdzie są bogowie Chamatu i Arpadu? Gdzie są bogowie Sefarwaim, Heny i Iwwy? Czy wyrwali Samarię z moich rąk?
35 Miongoni mwa miungu yote ya nchi, je kuna mungu ambaye ameiokoa nchi yake kutoka kwenye nguvu yangu? Inawezekanaje Yahwe akaiokoa Yerusalemu kutoka kwenye uwezo wangu?”
Którzy spośród wszystkich bogów tych ziem wybawili swoją ziemię z mojej ręki, żeby PAN miał wybawić Jerozolimę z mojej ręki?
36 Lakini watu wakabaki kimya na hawakujibu, kwa kuwa mfalme alikuwa ameamuru, “Msimjibu.”
Lecz lud milczał i nie odpowiedział mu ani słowa, bo taki był rozkaz króla: Nie odpowiadajcie mu.
37 Kisha Eliakimu mwana wa Hilkia, ambaye alikuwa juu ya nyumba ya mfalme; Shebna yule mwandishi; na Joa mwana wa Asafu, mtunza kumbukumbu, akaja kwa Hezekia pamoja na nguo zao zilizoraruliwa, na kumpatia taarifa ya maneno ya yule amiri mkuu.
Wtedy przyszli przełożony domu Eliakim, syn Chilkiasza, pisarz Szebna i kronikarz Joach, syn Asafa, do Ezechiasza, z rozdartymi szatami, i oznajmili mu słowa Rabszaka.

< 2 Wafalme 18 >