< 2 Wafalme 12 >

1 Katika mwaka wa saba wa Yehu, utawala wa Yoashi ulianza; alitawala kwa mda wa miaka arobaini huko Yerusalimu. Mama yake alikuwa anaitwa Sibia, wa Beersheba.
In year seven of Jehu he became king Jehoash and forty year[s] he reigned in Jerusalem and [the] name of mother his [was] Zibiah from Beer Sheba.
2 Yoashi akafanya yaliyo mema usoni mwa Yahwe siku zote, kwa sababu Yehoyada kuhani alimfundisha.
And he did Jehoash the right in [the] eyes of Yahweh all days his which he instructed him Jehoiada the priest.
3 Lakini sehemu ya juu haikuchukuliwa. Watu wakaendelea kutoa sadaka na kuchoma ubani kwenye sehemu za juu.
Only the high places not they were removed still the people [were] sacrificing and [were] making smoke at the high places.
4 Yoashi akamwambia kuhani, “Pesa zote zilizokuja kama sadaka takatifu kwenye nyumba ya Yahwe, pesa ya matumizi pesa ya watu kadiri alivyoandikiwa kila mtu, na pesa yote aonayo moyoni mwake kuileta kwenye nyumba ya Yahwe-
And he said Jehoash to the priests all [the] money of the holy gifts which it will be brought [the] house of Yahweh money passing along everyone [the] money of persons of valuation his all [the] money which it will come up on [the] heart of a person to bring [the] house of Yahweh.
5 makuhani watapokea pesa kutoka miongoni mwa mmoja wa watunza pesa na kutengeneza kila sehemu itakayoonekana imeharibika kwenye hekalu.”
Let them take themselves the priests each from with acquaintance his and they they will repair [the] damage of the house to every where it will be found there damage.
6 Lakini kama mwaka wa ishirini na tatu wa mfalme Yoashi, makuhani hawakuwa wameandaa kitu chochote kwenye hekalu.
And it was in year twenty and three year of the king Jehoash not they had repaired the priests [the] damage of the house.
7 Mfalme Yoashi akamwita Yehoyada kuhani na kuhani mwingine; akawaambia, “Kwa nini hamjaandaa kitu chochote kwenye hekalu? Sasa msichukue tena pesa kutoka kwa walipa kodi wenu, lakini chukueni kile kilichokuwa kikikusanywa kwa ajili ya matengenezo ya hekalu na uwapatia wale wanaoweza kufanya matengenezo.
And he summoned the king Jehoash Jehoiada the priest and the priests and he said to them why? [are] not you repairing [the] damage of the house and now may not you take money from with acquaintances your for for [the] damage of the house you will give it.
8 Hivyo makuhani wakakubaliana wasichukue pesa tena kutoka kwa watu na wasitengeneze wenyewe.
And they agreed the priests to not to take money from with the people and to not to repair [the] damage of the house.
9 Badala yake, Yehoyada yule kuhani akachukua kasha, akatoboa tundu kwenye kifuniko chake, na kuliweka karibu na madhabahu, upande wa kulia kama mtu anaingia kwenye madhabahu ya Yahwe. Makuhani ambao walikuwa wakilinda mlango wa hekalu wakatumbukiza pesa zote ambazo zilizokuwa zimeletwa kwenye nyumba ya Yahwe.
And he took Jehoiada the priest a chest one and he bored a hole in lid its and he put it beside the altar (from [the] right [side] *QK) when comes anyone [the] house of Yahweh and they put there the priests [who] kept of the threshold all the money which was brought [the] house of Yahweh.
10 Ikawa walipoona kwamba kulikuwa na pesa za kutosha kwenye kasha, mwadishi wa mfalme na kuhani mkuu wakaja na kuweka pesa kwenye mifuko na kisha kuhesabu, pesa ikaonekana kwenye nyumba ya Yahwe.
And it was when saw they that much the money [was] in the chest and he came up [the] scribe of the king and the priest great and they tied up and they counted the money which was found [the] house of Yahweh.
11 Wakawapa pesa ambayo ilikuwa imepimwa kwenye mikono ya watu ambao waliokuwa wanatunza nyumba ya Yahwe. Wakawalipa mafundi seremala na wajenzi ambao walikuwa wemefanya kazi kwenye nyumba ya Yahwe,
And they put the money weighed out on ([the] hands of *QK) [the] doers of the work (who were appointed *Qk) [the] house of Yahweh and they brought out it to [the] craftsmen of wood and to the builders who were working on [the] house of Yahweh.
12 na waashi na wakata mawe, kwa ajili ya kununua mbao na kukata mawe kwa ajili ya kutengenezea nyumba ya Yahwe, na yote iliyokuwa inahitajika kulipwa kwa ajili ya kuitengeneza.
And to the masons and to [the] cutters of stone and to acquire wood and stones of hewing to repair [the] damage of [the] house of Yahweh and for all that it went out on the house to repair [it].
13 Lakini ile pesa iliyokuwa imeletwa kwenye nyumba ya Yahwe haikulipwa kwa ajili ya vikombe vya fedha, mabeseni, au dhahabu au fedha yoyote ya vyombo.
Only not it was made [the] house of Yahweh basins of silver snuffers bowls trumpets any article of gold and article of silver from the money which was brought [the] house of Yahweh.
14 Waliwapa hizi fedha wale ambao waliokuwa wamefanya kazi ya kutengeneza nyumba ya Yahwe.
For to [the] doers of the work they gave it and they repaired with it [the] house of Yahweh.
15 Pia, hakukuhitajika zile pesa zilipwe kwa ajili ya matengenezo ili kuwajibika kwa kuwa watu walizipokea nakuzilipa kwa watenda kazi, kwa sababu hawa watu walikuwa waadilifu.
And not they settled accounts with the men whom they put the money on hand their to give to [the] doers of the work for in faithfulness they [were] working.
16 Lakini pesa kwa ajili ya matoleo ya hatia na pesa kwa ajili ya matoleo ya dhambi hazikuwa zimeletwa kwenye hekalu la Yahwe, kwa sababu zilikuwa mali ya makuhani.
Money of guilt offering and money of sin offerings not it was brought [the] house of Yahweh to the priests they belonged.
17 Kisha Hazaeli mfalme wa Shamu akashambuliwa na kupigana dhidi ya Gathi, na kuichukua.
Then he went up Hazael [the] king of Aram and he fought on Gath and he captured it and he set Hazael face his to go up on Jerusalem.
18 Ndipo Hazaeli akageuka kuishambulia Yerusalemu. Yoashi mfalme wa Yuda akavichukua vitu vyote ambavyo Yehoshefati na Yehoramu na Ahazia, baba zake, wafalme wa Yuda, na kuviweka wakfu, na vile alivyokuwa ameviweka wakfu, na dhahabu zote zilizokuwa zimeonekana kwenye gala la nyumba ya Yahwe na la mfalme akawatuma kwenda kwa Ahazi mfalme wa Shamu. Kisha Hazaeli akaenda zake kutoka Yerusamu.
And he took Jehoash [the] king of Judah all the holy things which they had consecrated Jehoshaphat and Jehoram and Ahaziah ancestors his [the] kings of Judah and own holy things his and all the gold which was found in [the] treasuries of [the] house of Yahweh and [the] house of the king and he sent [them] to Hazael [the] king of Aram and he went up from on Jerusalem.
19 Kama mambo mengine yanayomuhusu Yoashi, yote aliyoyafanya, je hayakuandikwa kwenye kitabu cha matukio ya wafalme wa Yuda?
And [the] rest of [the] matters of Joash and all that he did ¿ not [are] they written on [the] scroll of [the] matters of the days of [the] kings of Judah.
20 Watumishi wake wakainuka na kupanga pamoja; wakamteka Yoashi katika Bethi Milo, kwenye njia ya kushukia kwa Sila.
And they arose servants his and they conspired a conspiracy and they struck down Joash Beth-Millo which goes down Silla.
21 Yozakari mwana wa Shimeathi, na Yehozabadi mwana wa Shomeri, watumishi wake, wakamshambulia na akafa. Wakamzika Yoashi pamoja na mababu zake katika mji wa Daudi, na Amazia, mtoto wake, akawa mfalme kwenye sehemu yake.
And Jozabad [the] son of Shimeath and Jehozabad [the] son of Shomer - servants his they struck down him and he died and people buried him with ancestors his in [the] city of David and he became king Amaziah son his in place of him.

< 2 Wafalme 12 >