< 2 Yohana 1 >

1 Kutoka kwa mzee kwenda kwa mwanamke mteule na watoto wake, ambao niwapendao katika kweli na si mimi tu, bali na wote wale wanao ifahamu kweli,
L'aîné, à l'élue et à ses enfants, que j'aime en vérité, et non pas moi seulement, mais aussi tous ceux qui connaissent la vérité,
2 kwa sababu ya kweli iliyomo ndani yetu na itakayodumu pamoja nasi milele. (aiōn g165)
à cause de la vérité, qui demeure en nous, et qui sera avec nous pour toujours: (aiōn g165)
3 Neema, rehema, amani zitakuwa nasi kutoka kwa Mungu Baba na kutoka kwa Yesu Kristo, Mwana wa Baba, katika kweli na pendo.
Que la grâce, la miséricorde et la paix soient avec nous, de la part de Dieu le Père et du Seigneur Jésus-Christ, le Fils du Père, dans la vérité et l'amour.
4 Ninafurahi sana kwamba nimegundua baadhi ya watoto wanaenenda katika kweli, kama vile tu tulivyoipokea amri hii kutoka kwa Baba.
Je me réjouis beaucoup d'avoir trouvé quelques-uns de vos enfants marchant dans la vérité, comme le Père nous l'a commandé.
5 Na sasa nakusihi wewe, mwanamke, siyo kwamba nakuandikia amri mpya, bali ile tuliyokuwa nayo tokea mwanzo, kwamba tunapaswa kupendana sisi kwa sisi. Na huu ndiyo upendo, tunaopaswa kuenenda, kulingana na amri yake.
Or, je vous prie, chère madame, non pas comme si je vous écrivais un commandement nouveau, mais celui que nous avions dès le commencement, de nous aimer les uns les autres.
6 Hii ndiyo ile amri, kama mlivyoisikia tokea mwanzo, kwamba mnapaswa kuenenda katika hiyo.
C'est cela, l'amour, que de marcher selon ses commandements. Tel est le commandement que vous avez entendu dès le commencement, afin que vous y marchiez.
7 Kwa kuwa wadanganyifu wengi wamesambaa katika ulimwengu, na hawakiri kwamba Yesu Kristo alikuja katika mwili. Huyu ndiye mdanganyifu na mpinga Kristo.
Car plusieurs séducteurs sont sortis dans le monde, ceux qui ne confessent pas que Jésus-Christ est venu dans la chair. C'est là le séducteur et l'Antéchrist.
8 Jiangalieni wenyewe kwamba hampotezi mambo yale tuliyokwisha fanyia kazi, lakini ili kwamba mweze kuipokea tuzo kamili.
Veillez sur vous-mêmes, afin que nous ne perdions pas ce que nous avons accompli, mais que nous recevions une pleine récompense.
9 Yeyote aendeleae mbele na hadumu katika fundisho la Kristo, hana Mungu. Yeye adumuye katika fundisho anaye Baba na Mwana pia.
Celui qui transgresse et ne demeure pas dans l'enseignement du Christ n'a pas Dieu. Celui qui demeure dans l'enseignement a le Père et le Fils.
10 Kama mtu anakuja kwenu na haleti fundisho hili, msimkaribishe katika nyumba zenu na msimsalimie.
Si quelqu'un vient chez vous et n'apporte pas cet enseignement, ne le recevez pas dans votre maison et ne l'accueillez pas,
11 Kwa kuwa amsalimuye hushiriki katika matendo yake maovu.
car celui qui l'accueille participe à ses mauvaises actions.
12 Ninayo mambo mengi ya kukuandikia, na sikutaka kuyaandika kwa karatasi na wino. Lakini natumaini kuja kwenu na kuongea uso kwa uso, kwamba furaha yetu ipate kufanywa kamili.
Ayant beaucoup de choses à t'écrire, je ne veux pas le faire avec du papier et de l'encre, mais j'espère venir chez toi et te parler face à face, afin que notre joie soit complète.
13 Watoto wa dada yenu mteule wanawasalimia.
Les enfants de ta sœur élue te saluent. Amen.

< 2 Yohana 1 >