< 2 Nyakati 5 >

1 Wakati ilipomalizika kazi aliyofanya Selemani kwa ajili ya Yahwe, Selemani akapeleka vitu ndani, ambavyo Daudi, baba yake, aliviweka wakifu kwa kusudi hilo, pamoja na zile fedha, dhahabu, na vyombo vyote akavileta ndani ya hazina ya nyumba ya Mungu.
When all the work that Solomon did for the house of Yahweh was completed, Solomon brought in the things that David, his father, had set apart for this purpose, including the silver, the gold, and all the furnishings—he placed them into the treasuries of the house of God.
2 Kisha Selemanai akawakusanya wazee wa Israeli, wakuu wa makabila yote, na viongozi wa familia za watu wa Israeli, katika Yerusalemu, ili walilete sanduku la agano la Yahwe kutoka mji wa Daudi, ambao ni Sayuni.
Then Solomon assembled the elders of Israel, all the heads of the tribes, and the leaders of the families of the people of Israel, in Jerusalem, to bring up the ark of the covenant of Yahweh from the city of David, that is, Zion.
3 Wanaume wote wa Israeli wakakusanyika mbele za mfalme katika sikukuu, ambayo ilikuwa katika mwezi wa saba.
All the men of Israel assembled before the king at the feast, which was in the seventh month.
4 Wazee wote wa Israeli wakaja, na Walawi wakalichukua sanduku.
All the elders of Israel came, and the Levites took up the ark.
5 Wakalileta sanduku, hema ya kukutania, na vyombo vitakatifu vyote ambavyo vilikuwa ndani ya hema. Makuhani waliokuwa wa kabila la Lawi wakavileta vtu hivyo.
They brought up the ark, the tent of meeting, and all the holy furnishings that were in the tent. The priests who were of the tribe of Levi brought these things up.
6 Mfalme Selemanai na kusanyiko lote la Israeli wakaja pamoja, mbele ya sanduku, wakitoa sadaka za kondoo na maksai ambao hawakuweza kuhesabika.
King Solomon and all the assembly of Israel came together before the ark, sacrificing sheep and oxen that could not be counted.
7 Makuhani wakalileta sanduku la anago la Yahwe ndani mahali pake, katika chumba cha ndani cha nyumba, kwenye patakatifu pa patakatifu, chini ya mabawa ya makerubi.
The priests brought in the ark of the covenant of Yahweh to its place, into the inner room of the house, to the most holy place, under the wings of the cherubim.
8 Kwa kuwa makerubi walitandaza mabawa yao juu ya mahali pa sanduku, na walilifunika sanduku na na miti yake ya kulibebea.
For the cherubim spread out their wings over the place of the ark, and they covered the ark and the poles by which it was carried.
9 Miti ilikuwa mirefu sana kwamba ncha zake zlionekana kutoka ile sehemu takatifu mbele ya chumba cha andani, lakini hazikuweza kuonekana kutoka nje. Zipo hapo hadi leo.
The poles were so long that their ends were seen from the holy place in front of the inner room, but they could not be seen from outside. They are there to this day.
10 Hapakuwa na kitu katika sanaduku isipokuwa zile meza mbili ambazo Musa aliziweka humo huko Horebu, wakati Mungu alipofanya agano na watu wa Israeli, walipotoka nje ya Misri.
There was nothing in the ark except the two tablets that Moses had put there at Horeb, when Yahweh made a covenant with the people of Israel, when they came out of Egypt.
11 Ilikuwa makuhani walipotoka nje ya sehemu takatifu. Makuhanai wote wliokuwepo wakajiweka wakifu wenyewe kwa Yahwe, bila kujiamuru wenyewe kulingana na sehemu zao.
It came about that the priests came out of the holy place. All the priests who were present had consecrated themselves to Yahweh, not ordering themselves according to their divisions.
12 Pia makuhani waliokuwa waimbaji, wote kwa ujumla wao, pamoja na Asafu, Hemani, Yeduthuni, na wana wao na ndugu zao, wakiwa wamevalia kitani safi na wakipiga matoazi, vinanda, na vinubi, wakaasimama upande wa mashariki wa mwisho wa madhabahu. Pamoja nao palikuwa na makuhuni 120 wakipuliza tarumbeta.
Also the Levites who were the singers, all of them, including Asaph, Heman, Jeduthun, and their sons and brothers, clothed in fine linen and playing cymbals, harps, and lyres, stood at the east end of the altar. With them were 120 priests blowing trumpets.
13 Ikawa kwamba wapuruza tarumbeta na waimbaji wakafanya mziki pamoja, wakifanya sauti moja isikike kwa ajili ya kumsifu na kumshukuru Yahwe. Walipaza sauti zao kwa tarumbeta, toazi na vyombo vingine, na wakamsifu Yahwe. Wakaimba, “Kwa maana Yeye ni mwema, kwa kuwa uaminifu wa agano lake wadumu milele.” Kisha nyumba, ile nyumba ya Yahwe, ikajawa na wingu.
It came about that the trumpeters and singers made music together, making one sound to be heard for praising and thanking Yahweh. They raised their voices with the trumpets and cymbals and other instruments, and they praised Yahweh. They sang, “For he is good, for his covenant loyalty endures forever.” Then the house, the house of Yahweh, was filled with a cloud.
14 Makuhani hawakuweza kusimama ili wahudumu kwa sababu ya lile wingu, kwa maana utukufu wa Yahwe uliijaza nyumba yake.
The priests could not stand in order to serve because of the cloud, for the glory of Yahweh filled his house.

< 2 Nyakati 5 >