< 2 Nyakati 5 >

1 Wakati ilipomalizika kazi aliyofanya Selemani kwa ajili ya Yahwe, Selemani akapeleka vitu ndani, ambavyo Daudi, baba yake, aliviweka wakifu kwa kusudi hilo, pamoja na zile fedha, dhahabu, na vyombo vyote akavileta ndani ya hazina ya nyumba ya Mungu.
So all the work which Solomon did for the house of the Lord was complete. And Solomon took the holy things which David his father had given, the silver and the gold and all the vessels, and put them in the store-houses of the house of God.
2 Kisha Selemanai akawakusanya wazee wa Israeli, wakuu wa makabila yote, na viongozi wa familia za watu wa Israeli, katika Yerusalemu, ili walilete sanduku la agano la Yahwe kutoka mji wa Daudi, ambao ni Sayuni.
Then Solomon sent for all the responsible men of Israel, all the chiefs of the tribes and the heads of families of the children of Israel, to come to Jerusalem and take the ark of the Lord's agreement up out of the town of David, which is Zion.
3 Wanaume wote wa Israeli wakakusanyika mbele za mfalme katika sikukuu, ambayo ilikuwa katika mwezi wa saba.
And all the men of Israel came together to the king at the feast in the seventh month.
4 Wazee wote wa Israeli wakaja, na Walawi wakalichukua sanduku.
All the responsible men of Israel came, and the Levites took up the ark.
5 Wakalileta sanduku, hema ya kukutania, na vyombo vitakatifu vyote ambavyo vilikuwa ndani ya hema. Makuhani waliokuwa wa kabila la Lawi wakavileta vtu hivyo.
They took up the ark and the Tent of meeting and all the holy vessels which were in the Tent; all these the priests, the Levites, took up.
6 Mfalme Selemanai na kusanyiko lote la Israeli wakaja pamoja, mbele ya sanduku, wakitoa sadaka za kondoo na maksai ambao hawakuweza kuhesabika.
And King Solomon and all the men of Israel who had come together there with him, were before the ark, making offerings of sheep and oxen more than might be numbered.
7 Makuhani wakalileta sanduku la anago la Yahwe ndani mahali pake, katika chumba cha ndani cha nyumba, kwenye patakatifu pa patakatifu, chini ya mabawa ya makerubi.
And the priests took the ark of the Lord's agreement and put it in its place, in the inner room of the house, in the most holy place, under the wings of the winged ones.
8 Kwa kuwa makerubi walitandaza mabawa yao juu ya mahali pa sanduku, na walilifunika sanduku na na miti yake ya kulibebea.
For their wings were outstretched over the place where the ark was, covering the ark and its rods.
9 Miti ilikuwa mirefu sana kwamba ncha zake zlionekana kutoka ile sehemu takatifu mbele ya chumba cha andani, lakini hazikuweza kuonekana kutoka nje. Zipo hapo hadi leo.
The rods were so long that their ends were seen from the holy place before the inmost room; but they were not seen from outside; and there they are to this day.
10 Hapakuwa na kitu katika sanaduku isipokuwa zile meza mbili ambazo Musa aliziweka humo huko Horebu, wakati Mungu alipofanya agano na watu wa Israeli, walipotoka nje ya Misri.
Nothing was in the ark but the two flat stones which Moses put there at Horeb, where the Lord made an agreement with the children of Israel when they came out of Egypt.
11 Ilikuwa makuhani walipotoka nje ya sehemu takatifu. Makuhanai wote wliokuwepo wakajiweka wakifu wenyewe kwa Yahwe, bila kujiamuru wenyewe kulingana na sehemu zao.
Now when the priests had come out of the holy place, (for all the priests who were present had made themselves holy, not keeping to their divisions;
12 Pia makuhani waliokuwa waimbaji, wote kwa ujumla wao, pamoja na Asafu, Hemani, Yeduthuni, na wana wao na ndugu zao, wakiwa wamevalia kitani safi na wakipiga matoazi, vinanda, na vinubi, wakaasimama upande wa mashariki wa mwisho wa madhabahu. Pamoja nao palikuwa na makuhuni 120 wakipuliza tarumbeta.
And the Levites who made the music, all of them, Asaph, Heman, Jeduthun, and their sons and brothers, robed in fair linen, were in their places with their brass and corded instruments at the east side of the altar, and with them a hundred and twenty priests blowing horns; )
13 Ikawa kwamba wapuruza tarumbeta na waimbaji wakafanya mziki pamoja, wakifanya sauti moja isikike kwa ajili ya kumsifu na kumshukuru Yahwe. Walipaza sauti zao kwa tarumbeta, toazi na vyombo vingine, na wakamsifu Yahwe. Wakaimba, “Kwa maana Yeye ni mwema, kwa kuwa uaminifu wa agano lake wadumu milele.” Kisha nyumba, ile nyumba ya Yahwe, ikajawa na wingu.
And when the players on horns, and those who made melody in song, with one voice were sounding the praise and glory of the Lord; with loud voices and with wind instruments, and brass and corded instruments of music, praising the Lord and saying, He is good; his mercy is unchanging for ever: then the house was full of the cloud of the glory of the Lord,
14 Makuhani hawakuweza kusimama ili wahudumu kwa sababu ya lile wingu, kwa maana utukufu wa Yahwe uliijaza nyumba yake.
So that the priests were not able to keep their places to do their work because of the cloud; for the house of God was full of the glory of the Lord.

< 2 Nyakati 5 >