< 2 Nyakati 32 >

1 Baada ya mambo haya na matendo haya ya uaminifu, Senakeribu, mfalme wa Ashuru, akaja na kuingia Yuda. Alipiga kambi kwa ajili ya kuivamia miji yenye ngome, ambayo alikusudia kuiteka kwa ajili yake.
After these things and these acts of faithfulness, Sennacherib, king of Assyria, came and entered Judah. He camped to attack the fortified cities, which he intended to capture for himself.
2 Sedekia alipoona kwamba Senakeribu amekuja na kwamba amedhamiria kupigana zidi ya Yerusalemu,
When Hezekiah saw that Sennacherib had come and that he intended to fight against Jerusalem,
3 aliwashirikisha viongozi wake na watu wake wenye nguvu kuyazuia maji ya chemichemi yaliyokuwa nje ya mji; waalimsaidia kufanya hivyo.
he consulted with his leaders and his powerful men to stop up the waters of the springs that were outside the city; they helped him do so.
4 Kwa hiyo watu wengi wakakusanyika na kuyazuia maji ya chemichemi zote na mikondo yote amabayo ilikuwa inatiririka katikati ya nchi. wakasema, “Kwa nini mfalme wa Ashuru aje na kupata maji mengi?”
So many people gathered together and stopped up all the springs and the stream that was flowing through the middle of the land. They said, “Why should the kings of Assyria come and find a lot of water?”
5 Hezekia akijipa ujasiri na kuujeenga ukuta wote uliokuwa umeangushwa chini. Akaijenga minara mirefu, na pia ukuta mwingine nje. Pia akaiimarisha Milo katika mji wa Dudi, na akafanya kiasi kikubwa cha silaha na ngao. (Maanshi ya kale yanasema hivi: “Badala ya, “akajenga minara amirefu”, baadhi ya matoleo ya zamani na kisasa yanasema, “akajenga minara mirefu juu yake”, Hii ni juu ya ukuta).
Hezekiah took courage and built up all the wall that was broken down. He built the towers higher, and also the other wall outside. He also strengthened the Millo in the city of David, and he made large amounts of weapons and shields.
6 Akaweka maamri jeshi juu wa watu. Akawakusanya pamoja kwake katika sehemu pana kwenye lango la mji na akasema kwao kwa ujasiri. Akasema,
He placed military commanders over the people. He gathered them together to him in the broad place at the city gate and spoke encouragingly to them. He said,
7 “Muwe imara na wenye ujasiri mzuri. Msiogope wala kukata tamaa kwa sababu ya mfalme wa Ashuru na jeshi lote ambalo liko naye, kwa maana kuna mtu yuko pamoja nasi ambaye ni mkuu kuliko
“Be strong and of good courage. Do not be afraid or discouraged because of the king of Assyria and all the army that is with him, for someone is with us who is greater than those with him.
8 walio naye mfalme wa Ashuru. walionaye ni jeshi la mwili tu, lakini aliye nasi ni Yahwe, Mungu wetu, kwa ajili ya kutusaidia, na kupiagana vita vyetu.” Kisha watu wakajifariji wenyewe kwa maneno ya Hezekia, mfalme wa Yuda.
With him is only an arm of flesh, but with us is Yahweh, our God, to help us, and to fight our battles.” Then the people comforted themselves with the words of Hezekiah, king of Judah.
9 Baada ya hayo, Senakeribu, mfalme wa Ashuru, aliwatuma watumishi wake kwenda Yetusalemu (sasa alikuwa mbe ya Lakishi, na jeshi lake lote lilikuwa pamoja naye), kwa Hezekia, mfaalme wa Yuda, na watu wote wa Yuda walikuwa Yerusalemu. Akasema,
After this, Sennacherib, king of Assyria, sent his servants to Jerusalem (now he was in front of Lachish, and all his army was with him), to Hezekiah, king of Judah, and to all of Judah who were in Jerusalem. He said,
10 “Hivi ndivyo Senakeribu, mfalme wa Ashuru, anasema: Ni kitu gani mnategemea kwa ajili ya kuhimili uvamizi katika Yerusalemu?
“This is what Sennacherib, king of Assyria, says: What are you relying on in order to endure a siege in Jerusalem?
11 Je, Hezekia hawapotoshi ninyi, ili kwamba awatoe kufa kwa njaa na kiu, anapowaambia, “Yahwe Mungu wetu atatuokoa na mkono wa mfalme wa Ashuru?
Is not Hezekiah misleading you, that he may give you over to die by famine and by thirst, when he tells you, 'Yahweh our God will rescue us from the hand of the king of Assyria'?
12 Je, siyo Hezekia yule yule ambaye amezipeleka juu sehemu zake na madhabahu zake na kuwaamuru Yuda na Yerusalemu, juu ya madhabahu moja lazima muabudu, na juu yake lazima mchome sadaka zenu?
Has not this same Hezekiah taken away his high places and his altars and commanded Judah and Jerusalem, 'On one altar you must worship, and on it you must burn your sacrifices'?
13 Je, hamjui mimi na babu zangu tulifanya nini kwa makundi ya wote wa inchi zingine? Je, miungu ya watu wa hizo nchi iliweza kwa njia yoyote kuziokoa nchi zao zidi ya nguvu zangu?
Do you not know what I and my ancestors have done to all the peoples of the other lands? Were the gods of the peoples of the surrounding lands able in any way to rescue their land from my power?
14 Miongoni mwa miungu yote ya mataifa hayo amabayo babu zangu waliwatekeza, je, kulikuwa na muungu yeyote aliyeweza kuwaokoa watu wake kutoka kwenye mkono wangu? Itakuwaje Mungu wenu aweze kuwakoa ninyi zidi ya nguvu zangu?
Among all the gods of those nations that my ancestors completely destroyed, was there any god who could rescue his people out of my hand? Why should your God be able to rescue you from my power?
15 Sasa msimuruhusu Hezekia awadanganye au kuwashawishi katika njia hii. Msimwamini, kwa maana hakuna muungu wa taifa lolote au ufalme amewahi kuwaokoa watu wake nje ya mkono wangu, au nje ya mkono wa babu zangu. Sembuse na Mungu wenu kwa namna gani atawaokoa na mkono wangu?
Now do not let Hezekiah deceive you or persuade you in this way. Do not believe him, for no god of any nation or kingdom has been able to rescue his people out of my hand, or out of the hand of my ancestors. How much less will your God rescue you from my hand?”
16 Watumishi wa Senakeribu hata walinena mabaya zaidi juu ya Yahwe Mungu na juu ya mtumishi wake Hezekia.
Sennacherib's servants spoke even more against Yahweh God and against his servant Hezekiah.
17 Senakeribu pia akandika barua ili kumdhihaki Yahwe, Mungu wa Israeli, na kunena kinyume naye. Alisema, “Kama ambavyo miungu ya mataifa haikuwaokoa watu wake kutoka kwenye mkono wangu, hivyo hivyo na Mungu wa Hezekia hatawaokoa watu wake kutoka kwenye mkono wangu.”
Sennacherib also wrote letters in order to mock Yahweh, the God of Israel, and to speak against him. He said, “As the gods of the nations of the lands have not rescued their people out of my hand, so the God of Hezekiah will not rescue his people out of my hand.”
18 Wakawalilia kwa lugha ya Wayahudi watu wa Yerusalemu waliokuwa juu ya ukuta, ili kuwaogopesha na kuwasumbua, ili kwamba waweze kuuteka mji.
They cried out in the language of the Jews to the people of Jerusalem who were on the wall, to frighten them and trouble them, in order that they might capture the city.
19 Wakamnenea Mungu wa Yerusalemu kama walivyowanenea miungu wa Dunia, ambao ni kazi ya mikono ya wanadamu tu.
They spoke of the God of Jerusalem as they had spoken of the gods of the other peoples of the earth, which are merely the work of men's hands.
20 Hezekia, mfalme, na Isaya mwana wa Amozi, nabii, wakaomba kwa sababu ya jambo hili na wakalia hadi mbinguni.
Hezekiah, the king, and Isaiah son of Amoz, the prophet, prayed because of this matter and he cried out to heaven.
21 Yahwe akatuma malaika, ambaye aliwaua wanaume wa kupigana vita, majemedari, na maakida wa mfalme katika kambi. Kwa hiyo Senakeribu akarudi katika nchi yake akiwa na uso wa aibu. Alipokuwa ameenda katika nyumba ya muungu wake, baadhi ya watoto wake wakamuua huko kwa upanga.
Yahweh sent an angel, who killed the fighting men, the commanders, and the officers of the king in the camp. So Sennacherib returned to his own land with shame on his face. When he had gone into the house of his god, some of his own children killed him there with the sword.
22 Katika namna hii, Yahwe akamwokoa Hezekia na wakazi wa Yerusalemu kutoka kwenye mkono wa Senakeribu, mfalme wa Ashuru, na kutoka kwenye mikono ya wengine, na akawapa pumzika juu ya kila upande. (Maandishi ya kale yanasema hivi: badala ya “akawapa pumziko juu ya kila pande”, baadhi ya matoleo ya zamani na ya kisasa yanasema, “akawaongoza juu ya kila pande”).
In this way, Yahweh saved Hezekiah and the inhabitants of Jerusalem from the hand of Sennacherib, the king of Assyria, and from the hand of all others, and gave them rest on every side.
23 Wengi walikuwa wakileta sadaka kwa Yahwe katika Yarusalemu, na zawadi za thamani kwa Hezekia mfalme wa Yuda, kwa hiyo aliinuliwa mbele za macho ya mataifa yote toka wakati huo na kuendelea.
Many were bringing offerings to Yahweh in Jerusalem, and precious gifts to Hezekiah king of Judah, so that he was lifted up in the eyes of all nations from that time forward.
24 Katika siku hizo Hezekia akaugua hadi hatua ya kufa. Akaomba kwa Yahwe, ambaye alisema kwake na kumpa ishara kwamba angeponywa.
In those days Hezekiah was sick to the point of dying. He prayed to Yahweh, who spoke to him and gave him a sign that he would be healed.
25 Lakini Hezekia hakumlipa Yahwe kwa ajili ya msaada uliotolewa kwake, kwa maana moyo wake uliinuliwa juu.
But Hezekiah did not pay back Yahweh for the help given to him, for his heart was lifted up. So anger came on him, and on Judah and Jerusalem.
26 Kwa hiyo hasira ikaja juu yake, na juu ya Yuda na Yerusalemu. Hata hivyo, baadaye Hezekia alijinyenyekesha mwenyewe kwa jali ya kiburi cha moyo wake, wote Yeye na wakaaji wa Yerusalemu, hivyo hasira ya Yahwe haikuja juu yao wakati wa siku za Hezekia.
Nevertheless, Hezekiah later humbled himself for the pride of his heart, both he and the inhabitants of Jerusalem, so that Yahweh's anger did not come on them during Hezekiah's days.
27 Hezekia alikuwa na utajiri mwingi sana na heshima kubwa. Alijipatia mwenyewe vyumba vya kuhifadhia kwa ajili ya fedha, dhahabu, vito vya thamani, na kwa ajili ya manukato, na kwa ajili ya ngao na na vyombo vyote vya thamani pia.
Hezekiah had very many riches and much honor. He provided himself with storerooms for silver, gold, precious stones, and for spices, as well as for shields and for all kinds of valuable objects.
28 Pia alikuwa na nyumba za maghala kwa ajili ya mavuno ya nafaka, divai mpya, na mafuta, na malisho kwa ajili ya aina zote za wanyama.
He also had storehouses for the harvest of grain, new wine, and oil, and stalls for all kinds of animals. He also had flocks in their pens.
29 Pia alikuwa na makundi katika mazizi. Zaidi ya hayo, alijipatia mwenyewe miji na makundi ya na ng'ombe kwa wingi, kwa maana Mungu alaikuwa amempa afya tele. (Maandishi ya kale yanasema hivi: Badala ya “miji” baadji ya matoleo ya kisasa yanasema “punda”, na baadhi mengine ya kisasa yanaacaha neno nzima)
In addition, he provided himself with cities and possessions of flocks and herds in abundance, for God had given him very much wealth.
30 Alikuwa ni Hezekia huyu huyu ambaye alisimamisha chemi chemi ya juu ya maji ya Gihoni, na aliye ileta moja kwa moja chini upande wa magharibi mwa mji wa Daudi. Hezekia alifanikiwa katika miradi yake yote.
It was this same Hezekiah who also stopped up the upper spring of the waters of Gihon, and who brought them straight down on the west side of the city of David. Hezekiah succeeded in all his projects.
31 Hata hivyo, katika jambo la mabolozi wa wakuu wa Babeli, waliotumwa kwake kuwauliza waliofahamu, kuhusu ishara za miujiza iliyokuwa imefanywa katika nchi, Mungu alimwachia mwenyewe, ili kumjaribu, na kujua yote yaliyokuwa katika moyo wake.
However, in the matter of the ambassadors of the princes of Babylon, who sent to him to ask questions of those who knew, about the miraculous sign that had been done in the land, God left him to himself, in order to test him, and to know all that was in his heart.
32 Kwa mambo mengine kuhusu Hezekia, pamoja na matendo yake ya uaminifu wa agano, unaweza kuona kwamba yameandikwa katika Maono ya Nabii Isaya Mwana wa Amozi, na katika kitabu cha wafalme wa Yuda na Israeli.
As for the other matters concerning Hezekiah, including his actions of covenant loyalty, you can see that they are written in the vision of the prophet Isaiah son of Amoz, and in the book of the kings of Judah and Israel.
33 Hezekia akalala pamaoja na babu zake, na wakamzika katika mlima wa makaburi ya vizazi vya Daudi. Yuda wote na wakaaji wa Yerusalemu wakamheshimu katika kifo chake. Manase mwanaye akawa mfalme katika nafasi yake.
Hezekiah slept with his ancestors, and they buried him on the hill of the tombs of the descendants of David. All Judah and the inhabitants of Jerusalem honored him at his death. Manasseh his son became king in his place.

< 2 Nyakati 32 >