< 2 Nyakati 3 >

1 Kisha Selemani akaanza kuijenga nyumba ya Yahwe katika Yerusalemu juu ya Mlima Moria, ambako Yahwe alimtokea Daudi baba yake. Aliandaa sehemu ambayo Daudi aliikusudia, katika sakafu ya kupuria ya Arauna Myebusi.
Then Solomon began to build the house of Jehovah at Jerusalem on Mount Moriah, where he appeared to David his father, at the place that David had designated, on the threshing floor of Ornan the Jebusite.
2 Alianza kujenga siku ya pili ya mwezi wa pili, katika mwaka wa nne wa utawala wake.
And he began to build in the second month, in the fourth year of his reign.
3 Sasa hivi ndinyo vipimo vya ule msingi ambao Selemani alijenga kwa ajili ya nyumba ya Mungu. Akitumia mtindo wa vipimo vya zamani, urefu ulikuwa mikono sitini, na upana ulikuwa mikono ishirini.
Now these are the foundations which Solomon laid for the building of God's house. The length, using the former standard measure, was one hundred three feet and four inches, and the breadth was thirty-four feet and five inches, and its height was fifty-one feet and eight inches.
4 Urefu wa ukumbi mbele ya nyumba ulikuwa mikono ishirini, ukilingana na upana wa nyumba, urefu wake kwenda juu pia ulikuwa mikono ishirini, na Selemani akaifunika sehemu ya ndani kwa dhahabu halisi.
The porch that was in front of the house was the same as the width of the house, thirty-four feet and five inches, and the depth was seventeen feet and three inches; and he overlaid it on the inside with pure gold.
5 Akailitengeneza paa la ukumbi mkuu kwa miti ya miberoshi, ambayo aliifunika kwa dhahabu halisi, na ambayo aliifunika kwa miti ya mitende na minyororo.
The greater house he made a ceiling with fir wood, which he overlaid with fine gold, and ornamented it with palm trees and chains.
6 Akaipamba nyumba kwa vito vya thamani; dhahabu ilikuwa dhahabu kutoka Parvaimu.
He garnished the house with precious stones for beauty: and the gold was gold of Parvaim.
7 Pia akazifunika boriti zake, vizingiti, kuta, na milango kwa dhahabu; akachonga makerubi juu ya kuta zake.
He overlaid also the house, the beams, the thresholds, and its walls, and its doors, with gold; and engraved cherubim on the walls.
8 Akaijenga sehemu ya patakatifu pa patakatifu. Urefu wake ulilingana na upana wa nyumba, mikono ishirini, na upana wake pia ulikuwa mikono ishirini. Aliifunika kwa dhahabu halisi, thamani yake ilikuwa talanta mia sita.
He made the most holy house: its length, according to the breadth of the house, was thirty-four feet and five inches, and its breadth thirty-four feet and five inches; and he overlaid it with fine gold, amounting to six hundred talents.
9 Uzito wa misumari ulikuwa shekeli hamsini za dhahabu. Alizifunika sehemu za juu kwa dhahabu.
The weight of the nails was fifty shekels of gold. He overlaid the upper rooms with gold.
10 Akachonga makerubi wawili kwa ajili ya sehemu za patakatifu pa patakatifu, wahunzi wakayafunika kwa dhahabu. (Maandishi ya kale yanasema: makerubi wawili waliochongwa kwenye mbao).
In the most holy house he made two cherubim of sculptured work; and he overlaid them with gold.
11 Mabawa ya makerubi yalikuwa na urefu wa mikono ishirini yote kwa pamoja; bawa la kerubi mmoja lilikuwa na urefu wa mikono mitano, lilifikia kwenye ukuta wa chumba; bawa jingine lilikuwa na urefu wa mikono mitano pia.
The wings of the cherubim were thirty-four feet and five inches: the wing of the one was eight feet and seven inches, reaching to the wall of the house; and the other wing was eight feet and seven inches, reaching to the wing of the other cherub.
12 Bawa la kerubi mwingine lilikuwa mikono mitano, likifikia kwenye ukuta wa chumba; bawa lake jingine lilikuwa mikono mitano pia, likigusana na bawa la kerubi wa kwanza.
The wing of the other cherub was eight feet and seven inches, reaching to the wall of the house; and the other wing was eight feet and seven inches, joining to the wing of the other cherub.
13 Mabawa ya makerubi hawa yalienea jumla ya mikono mitano. Makerubi yalisimama kwa miguu yake, na nyuso zake zikiuelekea ukumbi mkuu.
The wings of these cherubim were extended thirty-four feet and five inches: and they stood on their feet, and their faces were toward the house.
14 Akatengeneza pazia la samawati, dhambarau, na sufu nyekundu, na kitani safi, na akachora makerubi juu yake.
He made the veil of blue, and purple, and crimson, and fine linen, and ornamented it with cherubim.
15 Selemani pia akatengeneza nguzo mbili, kila moja ikiwa na urefu wa mikono thelathini na tano kwenda juu, kwa maana mbele ya nyumba; taji ambazo zilikuwa juu ya nguzo zilikuwa na urefu wa mikono mitano kwenda juu.
Also he made before the house two pillars sixty feet and three inches high, and the capital that was on the top of each of them was eight feet and seven inches.
16 Akatengeneza minyororo kwa ajili ya nguzo na akaiweka juu yake, pia akatengeneza maakomamanga mia moja na akayaunganisha kwenye minyororo.
He made chains in the inner sanctuary, and put them on the tops of the pillars; and he made one hundred pomegranates, and put them on the chains.
17 Akazisimamisha nguzo mbele ya hekalu, mkono wa kulia, na nyingine mkono wa kushoto; akaiita nguzo ya kulia Yakini, na nguzo ya kushoto akaiita Boazi.
He set up the pillars before the temple, one on the right hand, and the other on the left; and called the name of that on the right hand Jakin, and the name of that on the left Boaz.

< 2 Nyakati 3 >