< 2 Nyakati 22 >

1 Wakaaji wa Yersusalemu wakamfanya Ahazia, mwana mdodgo wa Yehoramu, mfalme katika nafasi yake, kwa maana kundi la watu ambalo lilikuja na Waarabu katika ngome lilikuwa limewauwa wanaye wakubwa wote. Kwa hiyo Ahazia mwana wa Yehoramu, mfalme wa Yuda, akawa mfalme.
And the inhabitants of Jerusalem made Ahaziah his youngest son king in his stead; for the band of men that came with the Arabians to the camp had slain all the eldest. So Ahaziah the son of Jehoram king of Judah reigned.
2 Ahazia alikuwa na umri wa mika arobaini na mbili alipoanza kutawala; alitawala kwa mwaka mmoja katika Yerusalemu. Jina la mama yake aliitwa Athalia; alikuwa binti Omri.
Forty and two years old was Ahaziah when he began to reign; and he reigned one year in Jerusalem; and his mother's name was Athaliah the daughter of Omri.
3 Pia Ahazia alitembea katika njia za nyumba ya Ahabu kwa maana mama yake alikuwa mshauri katika kufanya mamabo maovu.
He also walked in the ways of the house of Ahab; for his mother was his counsellor to do wickedly.
4 Ahazia alifanya yaliyokuwa maovu katika macho ya Yahwe, kama nyumba ya Ahabu walivyokuwa wakifanya, kwa maana walikuwa washauri wake baada ya kifo cha baba yake, hadi kuangamia kwake.
And he did that which was evil in the sight of the LORD, as did the house of Ahab; for they were his counsellors after the death of his father, to his destruction.
5 Pia aliufuata ushauri wao; akaenda pamoja na Yoramu mwana wa Ahabu, mfalme wa Israeli, kwa ajili ya kupigana dhidi ya Hazaeli, mfalme wa Aramu, huko Ramothi-gileadi. Waaramu wakamjeruhi Yoramu.
He walked also after their counsel, and went with Jehoram the son of Ahab king of Israel to war against Hazael king of Aram at Ramoth-gilead; and the Arameans wounded Joram.
6 Yoramu akaraudi Yezreeli kwa ajili ya kuponywa majeraha ambayo walipa huko Rama, alipopigana dhidi ya Hazaeli, mfalme wa Aramu. Kwa hiyo Ahazia mwana wa Yehoramu, mfalme wa Yuda, akaenda chini Yezreeli ili kumuona Yoramu mwana wa Ahabu, kwa sababu Yoramu alikuwa amejeruhiwa.
And he returned to be healed in Jezreel of the wounds which they had given him at Ramah, when he fought against Hazael king of Aram. And Azariah the son of Jehoram king of Judah went down to see Jehoram the son of Ahab in Jezreel, because he was sick.
7 Sasa uharibifu wa Ahazia ulikuwa umeletwa na Mungu kupitia kutembelewa na Yoramu. Alipokuwa amewasiri, alienda pamoja na Yeharamu ili kumvamia Yehu mwana wa Nimshi, ambaye Yahwe alikuwa amemchagua kwa ajili ya kuingamiza nyumba ya Ahabu.
Now the downfall of Ahaziah was of God, in that he went unto Joram; for when he was come, he went out with Jehoram against Jehu the son of Nimshi, whom the LORD had anointed to cut off the house of Ahab.
8 Ikawa kwamba, Yehu alikuwa akichukua hukumu ya Mungu juu ya nyumba ya Ahabu, kwamba aliwakuta viongozi wa Yuda na wana wa ndugu zake Ahazia wakimtumikia Ahazia. Yehu akawauwa.
And it came to pass, when Jehu was executing judgment upon the house of Ahab, that he found the princes of Judah, and the sons of the brethren of Ahaziah, ministering to Ahaziah, and slew them.
9 Yehu akamtafuta Ahazia; Wakamkamata akiwa amejificha katika Samaraia, wakamleta kwa Yehu, na wakamuuwa. Kisha wakamzika, kwa maana walisema, “Ni mwana wa Yehoshafati, ambaye alimtafuta Yahwe kwa moyo wake wote.” Kwa hiyo nyumba ya Ahazia haikuwa na nguvu zaidi kwa ajili ya kuutawala ule ufalme.
And he sought Ahaziah, and they caught him — now he was hiding in Samaria — and they brought him to Jehu, and slew him; and they buried him, for they said: 'He is the son of Jehoshaphat, who sought the LORD with all his heart.' And there was none of the house of Ahaziah that had power to hold the kingdom.
10 Sasa Athalia, mama wa Ahazia, akaoana kwamba mwanaye alikuwa amekufa, akaianuka na kuwauwa watoto wote wa kifalme katika nyumba ya Yehu.
Now when Athaliah the mother of Ahaziah saw that her son was dead, she arose and destroyed all the seed royal of the house of Judah.
11 Lakini Yehoshaba, binti wa mfalme, akamchukua Yoashi, mwana wa Ahazia, na akamvutia mbali kutoka miongoni mwa wana wa mfalme ambao waliuawa. Akamuweka yeye na mlezi wake katika chumba cha kulala. Kwa hiyo Yehoshaba, binti wa mfalme Yehoramu, mke wa Yehoiada kuhani (kwa maana alikuwa dada yake Ahazia), akamficha asimuone Athalia, kwa hiyo Athalia hakumuuwa.
But Jehoshabeath, the daughter of the king, took Joash the son of Ahaziah, and stole him away from among the king's sons that were slain, and put him and his nurse in the bed-chamber. So Jehoshabeath, the daughter of king Jehoram, the wife of Jehoiada the priest — for she was the sister of Ahaziah — hid him from Athaliah, so that she slew him not.
12 Alikuwa pamoja nao, wakiwa wamejificha katika nyumba ya Mungu kwa miaka sita, Athalia alipotawala juu ya Yuda.
And he was with them hid in the house of God six years; and Athaliah reigned over the land.

< 2 Nyakati 22 >