< 2 Nyakati 21 >

1 Yehoshafati akalala pamoja na babu zake na akizikwa pamoaja nao katika mji wa Daudi;
And he lay down Jehoshaphat with ancestors his and he was buried with ancestors his in [the] city of David and he became king Jehoram son his in place of him.
2 Yehoramu, mwanaye, akawa mfalme katika nafasi yake. Yehoramu alikuwa na ndugu, wana wa Yehoshafati: Azaria, Yerieli, Zekaria, Azaria, Mikaeli, na Shefatia. Wote hawa walikuwa wana wa Yehoshafati, mfalme wa Israeli.
And [belonged] to him brothers [the] sons of Jehoshaphat Azariah and Jehiel and Zechariah and Azariahu and Michael and Shephatiah all these [were] [the] sons of Jehoshaphat [the] king of Israel.
3 Baba yao alikuwa amewapa zawadi kubwa ya fedha, dhahabu, na vitu vingine vya thamani, na miji yenye ngome katika Yuda, lakini kiti cha enzi alimpa Yehoramu, kwa sababu alikuwa mzaliwa wake wa kwanza.
And he had given to them - father their gifts many to silver and to gold and to excellent things with cities of fortifications in Judah and the kingdom he gave to Jehoram for he [was] the firstborn.
4 Sasa Yehoramu alipokuwa ameinuka katika ufalme wa baba yake na kujiimarisha mwenyewe kama mfalme, akawaua ndugu zake wote kwa upanga, na pia viongizi wengine mbali mbali wa Israeli.
And he arose Jehoram over [the] kingdom of father his and he strengthened himself and he killed all brothers his with the sword and also some of [the] leaders of Israel.
5 Yehoramu alikuwa na umri wa mika thelathini na mbili alipoanza kutawala, na akatawala kwa miaka minane katika Yerusalemu.
[was] a son of Thirty and two year[s] Jehoram when became king he and eight years he reigned in Jerusalem.
6 Akatembea katika njia za wafalme wa Israeli, kama nyumba ya Ahabu ilivyokuwa ikifanya, kwa maana alikuwa na binti Ahabu kama mke wake, na akafanya yaliyo maovu katika macho ya Yahwe.
And he walked in [the] way of - [the] kings of Israel just as they did [the] house of Ahab for [the] daughter of Ahab she was of him wife and he did the evil in [the] eyes of Yahweh.
7 Vile vile, Yahwe hakutaka kuiangamiza nyumba ya Daudi, kwa sababu ya agano ambalo alikuwa amefanya na Daudi; alikuwa ameahidi kwamba siku zote angetoa uzima kwa ajili yake na kwa ajili ya vizazi vyake.
And not he was willing Yahweh to destroy [the] house of David on account of the covenant which he had made to David and since he had said to give to him a lamp and to descendants his all the days.
8 Katika siku za Yehoramu, Edomu wakaasi wasiwe chini ya Yuda, na wakajisimamishia mfalme juu yao.
In days his it rebelled Edom from under [the] hand of Judah and they made king over them a king.
9 Kisha Yeroboamu akavuka ng'ambo pamoja na maakida na magari yake yote. Ilikuwa usiku aliposimama na kupigana dhidi ya Waedomu ambao walikuwa wamemzunguka na maakida wa magari yake.
And he passed over Jehoram with commanders his and all the chariotry with him and it was he arose night and he struck down Edom which was surrounding him and [the] commanders of the chariotry.
10 Kwa hiyo Edomu iliasi kutoka kuwa chini ya Yuda mpaka leo. Libna pia aliasi wakati ule ule wasiwe chini yake. Kwa sababu Yehoramu alikuwa amemsahau Yahwe, Mungu wa babu zake.
And it has rebelled Edom from under [the] hand of Judah until the day this then it rebelled Libnah at the time that from under hand his for he had forsaken Yahweh [the] God of ancestors his.
11 Zaidi ya hayo, Yehoramu pia alikuwa amezijenga sehemu zake za juu katika milma ya Yuda na akawafanya wakaaji wa Yuda kuishi kama makahaba, na akawaongoza Yuda katika upotevu.
Also he he made high places in [the] mountains of Judah and he made prostitute [themselves] [the] inhabitants of Jerusalem and he thrust aside Judah.
12 Barua kutoka kwa nabii Eliya ikaja kwa Yerohamu. Ilisema, “Hivi ndivyo Yahwe, Mungu wa Daudi, babu yako, anasema: Kwa sababu hujatembea katika njia za Yehoshafafati, baba yako, wala katika njia za Asa, mfalme wa Yuda,
And it came to him a writing from Elijah the prophet saying thus - he says Yahweh [the] God of David ancestor your because that not you have walked in [the] ways of Jehoshaphat father your and in [the] ways of Asa [the] king of Judah.
13 bali umetembea katika njia za wafalme wa Israeli, na umewafanya Yuda na wakaaji wa Yerusalemu kuenenda kama kahaba, kama nyumba ya Ahabu walivyofanya—na kwa sababu pia umewaua ndugu zako katika familia ya baba yako kwa upanga, watu waliokuwa bora kuliko wewe mwenyewe—
And you have walked in [the] way of [the] kings of Israel and you have made prostitute [themselves] Judah and [the] inhabitants of Jerusalem as made [them] prostitute [themselves] [the] house of Ahab and also brothers your [the] house of father your good more than you you killed.
14 ona, Yahwe atawapiga watu wako na pigo kubwa, watoto wako, wake zako, na mali zako zote.
Here! Yahweh [is] about to strike a blow great on people your and on sons your and on wives your and on all property your.
15 Wewe mwenyewe utakuwa na ugonjwa mwingi kwa sababu ya ugonjwa kataika katika utumbo wako, mpaka utumbo wako uanguke nje kwa sababu ya ugonjwa, siku baada ya siku.
And you [will be] in sickness great in [the] sickness of bowels your until they will come out bowels your from the sickness days to days.
16 Yahwe akaichochea roho ya Wafilisiti dhidi ya Yuda na ya Waarabu waliokuwa karibu na Waethipia.
And he stirred up Yahweh on Jehoram [the] spirit of the Philistines and the Arabs who [were] on [the] hand [the] Cushites.
17 Wakaivamia Yuda, wakavamia katika nyumba ya mfalme. Pia wakawachukua wanaye na wake zake. Hakuna mwana aliyebakizwa kwa ajili yake ispokuwa, Yehoshafati, mwanaye mdogo.
And they came up on Judah and they broke into it and they took captive all the property which was found to [the] house of the king and also sons his and wives his and not he remained to him a son that except Jehoahaz [the] young [one] of sons his.
18 Baada ya haya yote, Yahwe akampiga katika utumbo wake kwa ugonjwa usiopona.
And after all this he struck him Yahweh - in bowels his to a sickness to there not [was] healing.
19 Ikawa wakati ulipofika, katika mwisho wa miaka miwili, kwamba utumbo wake ukaaanguka nje kwa sababu ya ugonjwa wake, na kwamba akafa kwa ugonjwa mkali. Watu wake hawakutengeneza moto kwa ajili ya heshima yake kama walivyokuwa wamefanyia babu zake.
And it was to days - from days and about [the] time of [the] going out of the end of days two they came out bowels his with sickness his and he died in diseases harmful and not they made for him people his a burning like [the] burning of ancestors his.
20 Alikuwa ameanza kutawala alipokuwa na umrai wa miaka thelatahini na mbaili; akatawala katika Israeli kwa miaka minane, na alikufa bila kuaombolezwa. Wakamzika katika mji wa Daudi, lakini siyo katika makaburi ya kifalme.
A son of thirty and two [years] he was when became king he and eight years he reigned in Jerusalem and he went with not desire and people buried him in [the] city of David and not in [the] graves of the kings.

< 2 Nyakati 21 >