< 2 Nyakati 19 >

1 Yehoshafati mfalme wa Yuda akarudi salama nyumbani kwake Yerusalemu.
And Jehoshaphat the king of Judah returned to his house in peace to Jerusalem.
2 Kisha Yehu mwana wa Hanani, mwonaji, akatoka kukutana naye na akasema kwa mfalme Yehoshafati, “Unapaswa kuwa unawasaidia waovu? Unapaswa kuwapenda wanaomchukia Yahwe? Kwa ajili ya tendo hili, ghadhabu toka kwa Yahwe iko juu yako.
And Jehu the son of Hanani the seer went out to meet him, and said to king Jehoshaphat, Should thou help the wicked, and love those who hate Jehovah? For this thing wrath is upon thee from before Jehovah.
3 Aidha, kuna baadhi ya mema ya kuonekana ndani yako, kwamba umeziondosha Maashera nje ya nchi, na umeukaza moyo wako kumtafuta Mungu.”
Nevertheless there are good things found in thee, in that thou have put away the Asheroth out of the land, and have set thy heart to seek God.
4 Yehoshafati akaishi katika Yerusalemu; na akaenda nje tena miongoni mwa watu wa Beer- sheba hadi nchi ya kilima ya Efraimu na akawarudisha kwa Yahwe, Mungu wa baba zao.
And Jehoshaphat dwelt at Jerusalem. And he went out again among the people from Beersheba to the hill-country of Ephraim, and brought them back to Jehovah, the God of their fathers.
5 Akaweka waamuzi katika nchi katika miji yote ya Yuda yenye angome, mji kwa mji.
And he set judges in the land throughout all the fortified cities of Judah, city by city,
6 Akawaambia waamuzi, “Zingatieni mnachopaswa kufanya, kwa sababu hamuamui kwa ajili ya mwanadamu, bali kwa ajili ya Yahwe; yuko pamoja nanyi katika kazi ya kuamua,
and said to the judges, Consider what ye do. For ye judge not for man, but for Jehovah, and he is with you in the judgment.
7 Basi sas iacheni hofu ya Mungu iwe juu yenu. Iweni waangaliafu mnapoamua, kwa maana hakuna uovu wa Yahwe Mungu wetu, wala hakuna upendeleo wala hongo.”
Now therefore let the fear of Jehovah be upon you. Take heed and do it. For there is no iniquity with Jehovah our God, nor respect of persons, nor taking of bribes.
8 Vile vile, katika Yerusalemu Yehoshafati akateua baadhi ya Walawi na makuhani, na baahdhi ya viongozi wa nyumba za mababu wa Israeli, kwa ajili ya kufanya hukumu kwa ajili ya Yahwe, na kwa ajili ya migogoro. Wakaishi katika Yerusalemu.
Moreover in Jerusalem Jehoshaphat set from the Levites and the priests, and from the heads of the fathers of Israel for the judgment of Jehovah, and for controversies. And they returned to Jerusalem.
9 Akawaelekeza, akisema, “Lazima mtumike kwa heshima kwa ajaili ya Yahwe, kwa uaminifu, na na kwa moyo wenu wote.
And he charged them, saying, Thus ye shall do in the fear of Jehovah, faithfully, and with a perfect heart.
10 Kila mgogoro wowote utakapokuja kwenu kutoka kwa ndugu zenu wanaoishi katika miji yao, iwe inahusu mauji, iwe inhusu torati na amri, lazim muwaonye, ili kwamba wasiwe na hatia mbele za Yahwe, la sivyo ghadhabu itakuja juu yenu na juu ya ndugu zenu. Mnapaswa kufanya hivyo na hamtakuwa na hatia
And whenever any controversy shall come to you from your brothers who dwell in their cities, between blood and blood, between law and commandment, statutes and ordinances, ye shall warn them, that they not be guilty towards Jehovah, and so wrath come upon you and upon your brothers. Do this, and ye shall not be guilty.
11 Ona, Amaria kuhani mkuu yuko juu yenu katika mambo yote ya Yahwe. Zebadia mwana wa Ishmaeli, kiongozi wa nyumba ya Yuda, ni kiongozi katika yote katika mambo yote ya mfalme. Pia, Walawi watakuwa wasimamizi wakiwatumikia ninyi. Muwe hodari na tiini maelekezo yenu, na Yahwe awe moja nao walio wema.”
And, behold, Amariah the chief priest is over you in all matters of Jehovah, and Zebadiah the son of Ishmael, the ruler of the house of Judah, in all the king's matters. The Levites shall also be officers before you. Deal courageously, and Jehovah be with the good.

< 2 Nyakati 19 >