< 2 Nyakati 18 >

1 Sasa Yehoshafati alikauwa na utajiri mwingi na heshima kubwa; alifanya undugu na Ahabu mmoja wa watu wa familia yake akamuo binti yake.
Now Jehoshaphat had great riches and honor; he allied himself with Ahab by having one of his family marry his daughter.
2 Baada ya miaka kadhaa, akashsuka chini kwa Ahabu huko Samaria. Ahabu akachinja kondoo na ngo'mbe wengi kwa ajili ya yake na watu waliokuwa pamoja naye. Ahabu pia akamshawishi kuivamia Ramothi-gileadi pamoja naye.
After some years, he went down to Ahab in Samaria. Ahab killed many sheep and oxen for him and the people who were with him. Ahab also persuaded him to attack Ramoth Gilead with him.
3 Ahabu, mfalme wa Israeli, akamwambia Yehoshafati, mfalme wa Yuda, “Utakwenda Ramothi-gileadi pamoja nami?” Yehoshafati akamjibu, “Mimi ni kama wewe, na watu wangu ni kama watu wako; tutakuwa pamoja nawe katika vita.”
Ahab, king of Israel, said to Jehoshaphat, king of Judah, “Will you go with me to Ramoth Gilead?” Jehoshaphat answered him, “I am like you, and my people are like your people. We will be with you in the war.”
4 Yehoshafati akamwambia mfalme wa Israeli, Tafadhali litafute neno la Yahwe kwanza kwa ajili ya jibu lako”
Jehoshaphat said to the king of Israel, “Please first seek the word of Yahweh for your answer.”
5 Kisha mfale wa Israeli akawakusanya manabii pamoja, wanauame mia nne, na akasema akwao, Tutaenda vitani Ramothi-gileadi, au nisiende?” Wakasema, “Vamia, kwa maana Mungu ataitia mkononi mwa mfalme.”
Then the king of Israel gathered the prophets together, four hundred men, and said to them, “Should we go to Ramoth Gilead to battle, or should I not?” They said, “Attack, for God will give it into the hand of the king.”
6 Lakini Yehoshafati akasema, “Hakuna nabii mwingine hapa wa Yahwe ambaye kwake tunapaswa kutafuta ushauri?”
But Jehoshaphat said, “Is there not here still another prophet of Yahweh with whom we might seek advice?”
7 Mfale wa Israeli akamwambia Yehoshafati, Bado kuna mtu mmoja amabaye kwake lazima tuutafute ushauri wa Yahwe, Mikaya mwana wa Imla, lakini namchukia kwa sababu yeye huwa hatabiri mema kamwe kuhusu mimi, bali kila mara maovu,” Lakini Yehoshafati akasema, “Mfalme hapaswi kusema hivyo.”
The king of Israel said to Jehoshaphat, “There is still one man by whom we may seek the advice of Yahweh, Micaiah son of Imlah, but I hate him because he never prophesies good concerning me, but always evil.” But Jehoshaphat said, “The king should not say that.”
8 Kisha mfalme wa Israeli akamwita akida na kusema, Haraka mlete Mikaya mwana wa Imla.”
Then the king of Israel called an officer and said, “Quickly bring Micaiah son of Imlah.”
9 Sasa Ahabu mfalme wa Israeli na Yehoshafati mfalme wa Yuda walikuwa wamekaa kila mmoja katika kiti cha enzi, wamevalia kanzu zao, katika sehemu ya uwazi katika maingilia ya lango la Samaria, na manabii wote walikuwa wakitabairi mbele zao.
Now Ahab the king of Israel and Jehoshaphat the king of Judah were sitting each on a throne, clothed in their robes, in an open place at the entrance of the gate of Samaria, and all the prophets were prophesying before them.
10 Zedekia mwana wa Kenaani akajitengenezea pembe za chuma na kusema, Yahwe anasema hivi: Kwa kutumia hizi pembe mtawasukuma Waaramu hadi waangamie.”
Zedekiah son of Kenaanah made himself horns of iron and said, “Yahweh says this: With these you will push the Arameans until they are consumed.”
11 Manabii wote wakatabiri kitu kile kile, wakisema, “Vamia Raamothi-gleadi na shinda. kwa maana Yahwe ameutia kwenye mkono wa mfalme.”
All the prophets prophesied the same, saying, “Attack Ramoth Gilead and win, for Yahweh has given it into the hand of the king.”
12 Mjumbe aliyeenda kumuita Mikaya akasema kwake, akisema, “Sasa angalia, maneno ya manabii yanatangaza mambo mema kwa ajili ya mfalme kwa kinywa kimoja. Tafadhali maneno yako yawe kama maneno ya mmoja wao na sema mambo mema.”
The messenger who went to summon Micaiah said to him, “Look, the words of the prophets with one mouth are favorable to the king. Let your words agree with theirs, and speak favorably.”
13 Mikaya akajibu, “Kama Yahwe aishivyo, mimi nitasema kile mbacho Mungu anasema.”
Micaiah replied, “As Yahweh lives, it is what God says that I will say.”
14 Alipokuja kwa mfalme, mfamle akamwambaia, “Mikaya, tutaenda Ramothi -gileadi kwa ajili ya vita, au la?” Mikaya akamjibu, “Vamia na utashinda! kwa maana utakuwa ushinda mkuu.”
When he came to the king, the king said to him, “Micaiah, should we go to Ramoth Gilead for battle, or not?” Micaiah answered him, “Attack and be victorious! For it will be a great victory.”
15 Kisha mfalme akasema kwake, “Ni mara ngapi ninapaswa kukutaka kuapa kutoniambia kitu chochote sispokuwa kweli katika jina la Yahwe?
Then the king said to him, “How many times must I require you to swear to tell me nothing but the truth in the name of Yahweh?”
16 Kwa hiyo Mikaya akasema, “Niliwaoana Israeli wametawanyika ktika mlima, kama kondoo wasio na mchungaji, na Yahwe akasema, hawa hawana mchungaji. Ebu kila mtu arudi nyumbani kwake kwa amani.”
So Micaiah said, “I saw all Israel scattered on the mountains, like sheep who have no shepherd, and Yahweh said, 'These have no shepherd. Let every man return to his house in peace.'”
17 Kwa hiyo mfalme wa Israeli akamwambia Yehoshafati, “Sikukuambia kwamba asingeweza kutabiri mema juu yangu, bali majanga tu?
So the king of Israel said to Jehoshaphat, “Did I not tell you that he would not prophesy good concerning me, but only disaster?”
18 Kisha Mikaya akasema, “Kwa hiyo ninyi nyote mnapashwa kulisikia neno la Yahwe: Nilimuon Yahwe amekaa juu ya kiti chake cha enzi, na majeshi yote ya mbinguni yalikauwa yamekaa mkono wake wa kulia na mkono wake wa kushoto.
Then Micaiah said, “Therefore all of you should hear the word of Yahweh: I saw Yahweh sitting on his throne, and all the host of heaven were standing on his right hand and on his left.
19 Yahwe akasema, Ni nani atakayemrubuni Ahabu, mfalme wa Israeli, ili kwamba aende na kuanguka huko Ramothi-gileadi?' Mmoja alisema hivi na mwingine hivi.
Yahweh said, 'Who will entice Ahab, king of Israel, so that he may go up and fall at Ramoth Gilead?' One said this and another that.
20 Kisha roho ikaja moja kwa maja na kusimama mbele ya Yahwe na kusema, 'Nitamrubuni.' Yahwe akamwambia, 'Kivipi?'
Then a spirit came forward and it stood before Yahweh and said, 'I will entice him.' Yahweh said to him, 'How?'
21 Roho ikajibu, “nitatoka nje na nitakuwa roho ya uongo katika vinywa vya manabii wake wote.' Yahwe akajibu, 'utamrubuni, na pia utafanikiwa. nenda sasa na fanya hivyo.'
The spirit replied, 'I will go out and I will become a lying spirit in the mouth of all his prophets.' Yahweh replied, 'You will entice him, and you will also be successful. Go now and do so.'
22 Sasa ona, Yahwe ameweka roho ya uongo katika midomo ya manabii wako hawa, na Yahwe ametangaza majanga kwa ajili yako.”
Now see, Yahweh has put a lying spirit in the mouth of these prophets of yours, and Yahweh has decreed disaster for you.”
23 Kisha Zedekia mwana wa Kenaana, akaja, akampiga kofi mika juu ya shavu, na kusema, “Kwa njia gani Roho wa Yahwe alitoka kwangu ili aseme nawe?”
Then Zedekiah son of Kenaanah, came up, slapped Micaiah on the cheek, and said, “Which way did the Spirit of Yahweh take to go from me to speak to you?”
24 Mika akasema, Angalia, utalijua hilo katika siku hiyo, mtakapokimbia katika baadhi ya vyumba vya ndani kwa ajili ya kujificha.”
Micaiah said, “Look, you will know that on that day, when you run into some inner room to hide.”
25 Mfalme wa Israeli akasema kwa baadhi ya watumishi, “Enyi watu mkamateni Mikaya na mmpeleke hadi Amoni, mkuu wa mji na, na kwa Yoashi, mwanangu.
The king of Israel said to some servants, “You people seize Micaiah and take him to Amon, the governor of the city, and to Joash, my son.
26 Nanyi mtamwambia, 'Mfalme anasema: Mweke gerezanai huyu mtu na umlishe kwa mkate kiogo tu na maji kidogo tu, mpaka nitakaporudi salama.”
You people will say to him, 'The king says: Put this man in prison and feed him with only a little bread and only a little water, until I return safely.'”
27 Kisha Mikaya akasema, “Kama utarudi salama, Yahwe hajasema nami.”Kisha akaongeza, “Sikiliza haya, enyi watu wote.”
Then Micaiah said, “If you return safely, then Yahweh has not spoken by me.” Then he added, “Listen to this, all you people.”
28 Kwa hiyo Ahabu, mfalme wa Israeli, na Yehoshafati, mfalme wa Yuda, wakaenda juu ya Ramothi-giledi.
So Ahab, the king of Israel, and Jehoshaphat, the king of Judah, went up against Ramoth Gilead.
29 Mfalme wa Israeli akamwamabia Yehoshafati, “Nitajibadilisha mwenyewe na kwenda vitani, lakini wewe vaa mavazi yako ya kifalme.” Kwa hiyo mfalame wa Israeli akajibalisha, na wakaenda vitani.
The king of Israel said to Jehoshaphat, “I will disguise myself and go into the battle, but you put on your royal robes.” So the king of Israel disguised himself, and they went into the battle.
30 Sasa mfalme wa Aramu alikuwa amewaamuru maakida wa magari yake, akisema, Msiwavamie wanajeshsi wasio wa muhimu wala wanajeshsi muhimu. Badala yake, mvamieni mfalme wa Israeli pekee,”
Now the king of Aram had commanded the captains of his chariots, saying, “Do not attack the unimportant or the important soldiers. Instead, attack only the king of Israel.”
31 Ikawa kwamba maakida wa magari walipomuona Yehoshafati wakasema, “Yule ni mfalme wa Israeli.” Wakageka kumzunguka wamvamie, lakini Yehoshafati akalia, na Yahwe akamsaidia. Mungu akawageza nyuma kutoka kwake.
It came about that when the captains of the chariots saw Jehoshaphat they said, “That is the king of Israel.” They turned around to attack him, but Jehoshaphat cried out, and Yahweh helped him. God turned them away from him.
32 Ikawa kwamba maakida wa magari walipoona ya kuwa hakuwa mfalme wa Israeli, wakarudi nyuma wasimfukuze.
It came about that when the commanders of the chariots saw that it was not the king of Israel, they turned back from pursuing him.
33 Lakini mtu mmoja akauvuta upinde wake kwa kubahatisha na kumpiga mfalme wa Israeli kati kati ya maungio ya mavazi yake. Kisha Ahabu akamwambia dereva wa gari lake, “Geuza nyuma na nitoe nje ya mapigano, kwa maana nimejeruhiwa vibaya sana.”
But a certain man drew his bow at random and shot the king of Israel between the joints of his armor. Then Ahab said to the driver of his chariot, “Turn around and carry me out of the battle, for I am badly wounded.”
34 Mapigano yakazidi kuwa makali siku hiyo, na mfalme wa israeli akashikiliwa katika gari lake kuwaelekea Waaramu hadi jioni. Muda jua lilipokaria kwenda chini, akafa.
The battle grew worse that day, and the king of Israel was held up in his chariot facing the Arameans until the evening. About the time that the sun was going down, he died.

< 2 Nyakati 18 >