< 2 Nyakati 18 >

1 Sasa Yehoshafati alikauwa na utajiri mwingi na heshima kubwa; alifanya undugu na Ahabu mmoja wa watu wa familia yake akamuo binti yake.
Now Jehoshaphat had riches and honor in abundance; and he joined affinity with Ahab.
2 Baada ya miaka kadhaa, akashsuka chini kwa Ahabu huko Samaria. Ahabu akachinja kondoo na ngo'mbe wengi kwa ajili ya yake na watu waliokuwa pamoja naye. Ahabu pia akamshawishi kuivamia Ramothi-gileadi pamoja naye.
After certain years he went down to Ahab to Samaria. Ahab killed sheep and cattle for him in abundance, and for the people who were with him, and moved him to go up with him to Ramoth Gilead.
3 Ahabu, mfalme wa Israeli, akamwambia Yehoshafati, mfalme wa Yuda, “Utakwenda Ramothi-gileadi pamoja nami?” Yehoshafati akamjibu, “Mimi ni kama wewe, na watu wangu ni kama watu wako; tutakuwa pamoja nawe katika vita.”
Ahab king of Israel said to Jehoshaphat king of Judah, "Will you go with me to Ramoth Gilead?" He answered him, "I am as you are, and my people as your people. We will be with you in the war."
4 Yehoshafati akamwambia mfalme wa Israeli, Tafadhali litafute neno la Yahwe kwanza kwa ajili ya jibu lako”
Jehoshaphat said to the king of Israel, "Please inquire first for the word of Jehovah."
5 Kisha mfale wa Israeli akawakusanya manabii pamoja, wanauame mia nne, na akasema akwao, Tutaenda vitani Ramothi-gileadi, au nisiende?” Wakasema, “Vamia, kwa maana Mungu ataitia mkononi mwa mfalme.”
Then the king of Israel gathered the prophets together, four hundred men, and said to them, "Shall we go to Ramoth Gilead to battle, or shall I refrain?" They said, "Go up; for God will deliver it into the hand of the king."
6 Lakini Yehoshafati akasema, “Hakuna nabii mwingine hapa wa Yahwe ambaye kwake tunapaswa kutafuta ushauri?”
But Jehoshaphat said, "Isn't there here a prophet of Jehovah besides, that we may inquire of him?"
7 Mfale wa Israeli akamwambia Yehoshafati, Bado kuna mtu mmoja amabaye kwake lazima tuutafute ushauri wa Yahwe, Mikaya mwana wa Imla, lakini namchukia kwa sababu yeye huwa hatabiri mema kamwe kuhusu mimi, bali kila mara maovu,” Lakini Yehoshafati akasema, “Mfalme hapaswi kusema hivyo.”
The king of Israel said to Jehoshaphat, "There is yet one man by whom we may inquire of Jehovah; but I hate him, for he never prophesies good concerning me, but always evil. He is Micaiah the son of Imla." Jehoshaphat said, "Do not let the king say so."
8 Kisha mfalme wa Israeli akamwita akida na kusema, Haraka mlete Mikaya mwana wa Imla.”
Then the king of Israel called an officer, and said, "Get Micaiah the son of Imla quickly."
9 Sasa Ahabu mfalme wa Israeli na Yehoshafati mfalme wa Yuda walikuwa wamekaa kila mmoja katika kiti cha enzi, wamevalia kanzu zao, katika sehemu ya uwazi katika maingilia ya lango la Samaria, na manabii wote walikuwa wakitabairi mbele zao.
Now the king of Israel and Jehoshaphat the king of Judah sat each on his throne, arrayed in their robes, and they were sitting in an open place at the entrance of the gate of Samaria; and all the prophets were prophesying before them.
10 Zedekia mwana wa Kenaani akajitengenezea pembe za chuma na kusema, Yahwe anasema hivi: Kwa kutumia hizi pembe mtawasukuma Waaramu hadi waangamie.”
Zedekiah the son of Kenaanah made him horns of iron, and said, "Thus says Jehovah, 'With these you shall push the Arameans, until they are consumed.'"
11 Manabii wote wakatabiri kitu kile kile, wakisema, “Vamia Raamothi-gleadi na shinda. kwa maana Yahwe ameutia kwenye mkono wa mfalme.”
All the prophets prophesied so, saying, "Go up to Ramoth Gilead, and prosper; for Jehovah will deliver it into the hand of the king."
12 Mjumbe aliyeenda kumuita Mikaya akasema kwake, akisema, “Sasa angalia, maneno ya manabii yanatangaza mambo mema kwa ajili ya mfalme kwa kinywa kimoja. Tafadhali maneno yako yawe kama maneno ya mmoja wao na sema mambo mema.”
The messenger who went to call Micaiah spoke to him, saying, "Look, the words of the prophets declare good to the king with one mouth. Let your word therefore, please be like one of theirs, and speak good."
13 Mikaya akajibu, “Kama Yahwe aishivyo, mimi nitasema kile mbacho Mungu anasema.”
Micaiah said, "As Jehovah lives, whatever my God says to me, that I will speak."
14 Alipokuja kwa mfalme, mfamle akamwambaia, “Mikaya, tutaenda Ramothi -gileadi kwa ajili ya vita, au la?” Mikaya akamjibu, “Vamia na utashinda! kwa maana utakuwa ushinda mkuu.”
When he had come to the king, the king said to him, "Micaiah, shall we go to Ramoth Gilead to battle, or shall I refrain?" He said, "Go up, and prosper. They shall be delivered into your hand."
15 Kisha mfalme akasema kwake, “Ni mara ngapi ninapaswa kukutaka kuapa kutoniambia kitu chochote sispokuwa kweli katika jina la Yahwe?
The king said to him, "How many times shall I adjure you that you speak to me nothing but the truth in the name of Jehovah?"
16 Kwa hiyo Mikaya akasema, “Niliwaoana Israeli wametawanyika ktika mlima, kama kondoo wasio na mchungaji, na Yahwe akasema, hawa hawana mchungaji. Ebu kila mtu arudi nyumbani kwake kwa amani.”
He said, "I saw all Israel scattered on the mountains, as sheep that have no shepherd. Jehovah said, 'These have no master. Let them return every man to his house in peace.'"
17 Kwa hiyo mfalme wa Israeli akamwambia Yehoshafati, “Sikukuambia kwamba asingeweza kutabiri mema juu yangu, bali majanga tu?
The king of Israel said to Jehoshaphat, "Did I not tell you that he would not prophesy good concerning me, but evil?"
18 Kisha Mikaya akasema, “Kwa hiyo ninyi nyote mnapashwa kulisikia neno la Yahwe: Nilimuon Yahwe amekaa juu ya kiti chake cha enzi, na majeshi yote ya mbinguni yalikauwa yamekaa mkono wake wa kulia na mkono wake wa kushoto.
Micaiah said, "Therefore hear the word of Jehovah: I saw Jehovah sitting on his throne, and all the army of heaven standing on his right hand and on his left.
19 Yahwe akasema, Ni nani atakayemrubuni Ahabu, mfalme wa Israeli, ili kwamba aende na kuanguka huko Ramothi-gileadi?' Mmoja alisema hivi na mwingine hivi.
Jehovah said, 'Who shall entice Ahab king of Israel, that he may go up and fall at Ramoth Gilead?' One spoke saying in this way, and another saying in that way.
20 Kisha roho ikaja moja kwa maja na kusimama mbele ya Yahwe na kusema, 'Nitamrubuni.' Yahwe akamwambia, 'Kivipi?'
A spirit came out, stood before Jehovah, and said, 'I will entice him.' "Jehovah said to him, 'How?'
21 Roho ikajibu, “nitatoka nje na nitakuwa roho ya uongo katika vinywa vya manabii wake wote.' Yahwe akajibu, 'utamrubuni, na pia utafanikiwa. nenda sasa na fanya hivyo.'
"He said, 'I will go forth, and will be a lying spirit in the mouth of all his prophets.' "He said, 'You will entice him, and will prevail also. Go forth, and do so.'
22 Sasa ona, Yahwe ameweka roho ya uongo katika midomo ya manabii wako hawa, na Yahwe ametangaza majanga kwa ajili yako.”
"Now therefore, look, Jehovah has put a lying spirit in the mouth of these your prophets; and Jehovah has pronounced disaster concerning you."
23 Kisha Zedekia mwana wa Kenaana, akaja, akampiga kofi mika juu ya shavu, na kusema, “Kwa njia gani Roho wa Yahwe alitoka kwangu ili aseme nawe?”
Then Zedekiah the son of Kenaanah came near, and struck Micaiah on the cheek, and said, "Which way did the Spirit of Jehovah go from me to speak to you?"
24 Mika akasema, Angalia, utalijua hilo katika siku hiyo, mtakapokimbia katika baadhi ya vyumba vya ndani kwa ajili ya kujificha.”
Micaiah said, "Look, you shall see on that day, when you shall go into an inner room to hide yourself."
25 Mfalme wa Israeli akasema kwa baadhi ya watumishi, “Enyi watu mkamateni Mikaya na mmpeleke hadi Amoni, mkuu wa mji na, na kwa Yoashi, mwanangu.
The king of Israel said, "Take Micaiah, and carry him back to Amon the governor of the city, and to Joash the king's son;
26 Nanyi mtamwambia, 'Mfalme anasema: Mweke gerezanai huyu mtu na umlishe kwa mkate kiogo tu na maji kidogo tu, mpaka nitakaporudi salama.”
and say, 'Thus says the king, "Put this fellow in the prison, and feed him with bread of affliction and with water of affliction, until I return in peace."'"
27 Kisha Mikaya akasema, “Kama utarudi salama, Yahwe hajasema nami.”Kisha akaongeza, “Sikiliza haya, enyi watu wote.”
Micaiah said, "If you return at all in peace, Jehovah has not spoken by me." He said, "Listen, you peoples, all of you."
28 Kwa hiyo Ahabu, mfalme wa Israeli, na Yehoshafati, mfalme wa Yuda, wakaenda juu ya Ramothi-giledi.
So the king of Israel and Jehoshaphat the king of Judah went up to Ramoth Gilead.
29 Mfalme wa Israeli akamwamabia Yehoshafati, “Nitajibadilisha mwenyewe na kwenda vitani, lakini wewe vaa mavazi yako ya kifalme.” Kwa hiyo mfalame wa Israeli akajibalisha, na wakaenda vitani.
The king of Israel said to Jehoshaphat, "I will disguise myself, and go into the battle; but you put on your robes." So the king of Israel disguised himself; and they went into the battle.
30 Sasa mfalme wa Aramu alikuwa amewaamuru maakida wa magari yake, akisema, Msiwavamie wanajeshsi wasio wa muhimu wala wanajeshsi muhimu. Badala yake, mvamieni mfalme wa Israeli pekee,”
Now the king of Aram had commanded the captains of his chariots, saying, "Fight neither with small nor great, except only with the king of Israel."
31 Ikawa kwamba maakida wa magari walipomuona Yehoshafati wakasema, “Yule ni mfalme wa Israeli.” Wakageka kumzunguka wamvamie, lakini Yehoshafati akalia, na Yahwe akamsaidia. Mungu akawageza nyuma kutoka kwake.
It happened, when the captains of the chariots saw Jehoshaphat, that they said, "It is the king of Israel." Therefore they turned around to fight against him. But Jehoshaphat cried out, and Jehovah helped him; and God moved them to depart from him.
32 Ikawa kwamba maakida wa magari walipoona ya kuwa hakuwa mfalme wa Israeli, wakarudi nyuma wasimfukuze.
It happened, when the captains of the chariots saw that it was not the king of Israel, that they turned back from pursuing him.
33 Lakini mtu mmoja akauvuta upinde wake kwa kubahatisha na kumpiga mfalme wa Israeli kati kati ya maungio ya mavazi yake. Kisha Ahabu akamwambia dereva wa gari lake, “Geuza nyuma na nitoe nje ya mapigano, kwa maana nimejeruhiwa vibaya sana.”
A certain man drew his bow at random, and struck the king of Israel between the joints of the armor. Therefore he said to the driver of the chariot, "Turn your hand, and carry me out of the army; for I am severely wounded."
34 Mapigano yakazidi kuwa makali siku hiyo, na mfalme wa israeli akashikiliwa katika gari lake kuwaelekea Waaramu hadi jioni. Muda jua lilipokaria kwenda chini, akafa.
The battle increased that day. However the king of Israel propped himself up in his chariot against the Arameans until the evening; and about the time of the going down of the sun, he died.

< 2 Nyakati 18 >