< 2 Nyakati 17 >

1 Yehoshafati mwana wa Asa akawa mfalme katika nafasi yake. Yehoshafati akajiimarisha dhidi ya Israeli.
And Jehoshaphat his son reigned in his stead, and strengthened himself against Israel.
2 Akaweka majeshi katika miji yote Yuda yenye ngome, na akaweka magereza katika nchi ya Yuda na katika miji ya Efraimu, ambayo Asa baba yake alikuwa ameiteka.
And he placed forces in all the fortified cities of Judah, and set garrisons in the land of Judah, and in the cities of Ephraim, which Asa his father had taken.
3 Yahwe alikuwa pamoja na Yehoshafati kwa sababu alitembea katika njia za kwanza za baba yake Daudi, na hakuwatafuta Mabaali. (Baadhi ya mandiko ya kale hayana “Daudi”, na baadhi ya matoleo ya kisasa yameacha hili jina “Daudi).
And the LORD was with Jehoshaphat, because he walked in the first ways of his father David, and sought not unto the Baalim;
4 Badala yake, alimtegemea Mungu wa baba yake, na alitembea katika amri zake, siyo katika tabia ya Israeli.
but sought to the God of his father, and walked in His commandments, and not after the doings of Israel.
5 Kwa hiyo Yahwe akaimarisha sheria katika mkono wake; Yuda wote wakaleta kodi kwa Yehoshafati. Alikuwa na utajiri na heshima kubwa.
Therefore the LORD established the kingdom in his hand; and all Judah brought to Jehoshaphat presents; and he had riches and honour in abundance.
6 Moyo wake ulikuwa umejikita katika njia za Yahwe. Pia aliziondoa sehemu za juu na Maashera mbali na Yuda.
And his heart was lifted up in the ways of the LORD; and furthermore he took away the high places and the Asherim out of Judah.
7 Katika mwaka wa tatu wa utawala wake aliwatuma wakuu wake Ben-haili, Obadia, Zekaria, Nethania, na Mikaya, ili wafundishe katika miji ya Yuda.
Also in the third year of his reign he sent his princes, even Ben-hail, and Obadiah, and Zechariah, and Nethanel, and Micaiah, to teach in the cities of Judah;
8 Pamoja nao walikuwepo Walawi: Shemaya, Nethanieli, Zebadia, Asaheli, Shemiramothi, Yehonathani, Adoniya, Tobia, na Tob-adonia, pamoja nao walikuwepo makuhani Elishama na Yehoramu.
and with them the Levites, even Shemaiah, and Nethaniah, and Zebadiah, and Asahel, and Shemiramoth, and Jehonathan, and Adonijah, and Tobijah, and Tob-adonijah, the Levites; and with them Elishama and Jehoram, the priests.
9 Walifundisha katika Yuda, wakiwa na kitabau cha sheria ya Yahwe. Wakaenda karibu miji yote ya Yuda na kufundisha miongoni mwa watu.
And they taught in Judah, having the book of the Law of the LORD with them; and they went about throughout all the cities of Judah, and taught among the people.
10 Hofu ya Yahwe ikashuka juu ya falme zote za nchi, zilizouzunguka Yuda, kwa hiyo hazikufanya vita dhidi ya Yehoshafati.
And a terror from the LORD fell upon all the kingdoms of the lands that were round about Judah, so that they made no war against Jehoshaphat.
11 Baadhi ya Wafilisti wakamletea Yehoshafati zawadi, fedha kama kodi. Waarabu pia wakamletea makundi, 7, 700 kondoo waume, na mbuzi 7, 770.
And some of the Philistines brought Jehoshaphat presents, and silver for tribute; the Arabians also brought him flocks, seven thousand and seven hundred rams, and seven thousand and seven hundred he-goats.
12 Yehoshafati akawa na nguvu sana.
And Jehoshaphat waxed great exceedingly; and he built in Judah castles and cities of store.
13 Akajenga ngome na miji ya maghala katika Yuda. Alikuwa na kazi nyingi katika miji ya Yuda, na wanajeshsi—imara, wanaume hodari—katika Yerusalemu.
And he had many works in the cities of Judah; and men of war, mighty men of valour, in Jerusalem.
14 Hapa ni rodha yao, wamepangwa kwa majina ya nyumba za baba zo: Kutoka Yuda, maakida wa maelfu; Adna yule jemedari, na pamoja naye wanaume wa kwenda vitani 300, 000;
And this was the numbering of them according to their fathers' houses: of Judah, the captains of thousands: Adnah the captain, and with him mighty men of valour three hundred thousand;
15 akifuatiwa na Yehonani jemedari, na pamoja naye wanaume 280, 00;
and next to him Jehohanan the captain, and with him two hundred and fourscore thousand;
16 akifuatiwa na Amasia mwana wa Zikri, ambaye kwa hiari alijitoa kumtumikia Yahwe; na pamoja naye wanaume wa kwenda vitani 200, 000.
and next to him Amasiah the son of Zichri, who willingly offered himself unto the LORD, and with him two hundred thousand mighty men of valour;
17 Kutoka Benyamini: Eliada mtu jasiri, na pamoja naye watu 200, 000 waliovaa upinde na ngao;
and of Benjamin: Eliada a mighty man of valour, and with him two hundred thousand armed with bow and shield;
18 akifutiwa na Yehozabadi, na pamoja naye askari 180, 000 waliotayari kwa vita.
and next to him Jehozabad, and with him a hundred and fourscore thousand ready prepared for war.
19 Hawa walikuwa ni wale ambao walimtumikia mfalme, miongoni mwao wale ambao mfalme aliwaweka katika miji ya ngome katika Yuda yote.
These were they that waited on the king beside those whom the king put in the fortified cities throughout all Judah.

< 2 Nyakati 17 >