< 2 Nyakati 14 >

1 Abiya kalala pamoja na babu zake, na wakamzika kataika maji wa Daudi. Asa, mwanaye, akawa mfalme katika nafasi yake. Katika siku yake nchi ilikuwa na miaka kumi.
So Abijah slept with his fathers, and they buried him in the City of David; and Asa his son reigned in his place. In his days the land was quiet ten years.
2 Asa alifanya yaliyomema na sahihi katika macho ya Yahwe Mungu wake,
Asa did that which was good and right in the eyes of Jehovah his God:
3 kwa maana aliziondosha mbali madhabahu za kigeni na sehemu za juu. Akaziangusha chini nguzo za mawe na kuzikata nguzo za Maashera.
for he took away the foreign altars, and the high places, and broke down the pillars, and cut down the Asherim,
4 Akawaamuru Yuda kumtafuta Yahwe, Mungu wa babu zao, na kuzishika sheria na amri.
and commanded Judah to seek Jehovah, the God of their fathers, and to do the law and the commandment.
5 Pia akaziondosha mbali sehemu za juu na madhabahu za kufukiza kutoka miji yote ya Yuda. Ufalme ulikuwa na pumziko chini yake.
Also he took away out of all the cities of Judah the high places and the sun images: and the kingdom was quiet before him.
6 Akajenga miji ya ngome katika Yuda, kwa maana nchi ilikuwa tulivu, na hakuwa na vita katika miaka hiyo, kwa sababu Yahwe alikuwa amempa amani.
He built fortified cities in Judah; for the land was quiet, and he had no war in those years, because Jehovah had given him rest.
7 Kwa maana Asa aliwaambia Yuda, “Tuijenge miji hii na kuizungushia kuta, na minara, mageti, na makomeo; nchi bado yetu kwa sababu tumemtafuta Yahwe Mungu wetu. Tumemtafuta yeye, na ametupa amani katika kila upande.” Kwa hiyo walijenga na wakafanikiwa.
For he said to Judah, "Let us build these cities, and make walls around them, with towers, gates, and bars. The land is still ours. Since we have sought Jehovah our God, he has sought us and he has given us rest on every side." So they built and prospered.
8 Asa alikuwa na jeshi ambalo lilibeba ngao na mikuki; kutoka Yuda alikuwa na wanaume 300, 000, na kutoka Benyamini, wanaume 280, 000 waliobeba ngao na kuvuta pinde.
Asa had an army that bore bucklers and spears, out of Judah three hundred thousand; and out of Benjamin, that bore shields and drew bows, two hundred eighty thousand: all these were mighty men of valor.
9 Zera Mwethiopia akaja juu yao na jeshi la wanajeshi milioni moja na magari mia tatu; akaja Maresha.
There came out against them Zerah the Ethiopian with an army of a million troops, and three hundred chariots; and he came to Mareshah.
10 Kisha Asa akatoka nje kukutana naye, na wakapanga mistari ya vita ya mapigano katika bonde la Sefatha huko Maresha.
Then Asa went out to meet him, and they set the battle in array in the Valley of Zephathah at Mareshah.
11 Asa kamlilia Yahwe, Mungu wake, na akasema, “Yahwe, hakuna aliye kama wewe lakini ni wewe wa kumsaidia mtu asiye na nguvu anapokutana na mengi. Tusaidie, Yahwe, Mungu wetu, kwa maana tunakutegemea wewe, na katika jina lako tumekuja kupambana na idadi hii kubwa ya adui. Yahwe, wewe ni Mungu wetu; usimuache mtu akushinde.”
Asa cried to Jehovah his God, and said, "Jehovah, there is none besides you to help, between the mighty and those who have no strength. Help us, Jehovah our God; for we rely on you, and in your name we have come against this multitude. Jehovah, you are our God. Do not let man prevail against you."
12 Kwa hiyo Yahwe akawapiga Waethiopia mbele za ASa na Yuda; Waethiopia wakakimbia.
So Jehovah struck the Ethiopians before Asa, and before Judah; and the Ethiopians fled.
13 Asa pamoja na wanajeshi waliokuwa pamoja naye wakawafukuza hadi Gerari. Kwa hiyo Waethiopia wengi wakajeruhiwa kiasi kwamba hawakuweza kupona, kwa maana waliangamizwa kabisa mbele za Yahwe na jeshi lake. Jeshsi likachukua mateka wengi sana.
Asa and the people who were with him pursued them to Gerar: and there fell of the Ethiopians so many that they could not recover themselves; for they were destroyed before Jehovah, and before his army; and they carried away very much booty.
14 Jeshi likaviangamiza vijiji vyote jirani na Garari, kwa kuwa hofu ya Yahwe ilikuwa imekuja juu ya wakaaji. Jeshi likateka vijiji vyote, na vilikuwa na hazina nyingi sana ndani yake.
They struck all the cities around Gerar; for the fear of Jehovah came on them: and they plundered all the cities; for there was a great amount of plunder in them.
15 Jeshi pia likaipiga hema ya makazi yawachungaji; wakabeba kondoo kwa wingi, ngamia vile vile, na kisha wakarudi Yerusalemu.
They struck also the tents of livestock, and carried away sheep in abundance, and camels, and returned to Jerusalem.

< 2 Nyakati 14 >