< 2 Nyakati 11 >

1 Rehoroboamu alipofiki Yerusalemu, akawakusanya nyumba ya Yuda na Benyamini, wanaume 180, 000 walaiaochaguliwa amabao wliakuwa wanajeshi, kwa ajili ya kupigana dhiidi ya Israeli, ili kuurudisha ufalme kwa Rehoboamu. 2 Lakini neno la Yahwe likamjia Shemaya mtu wa Mungu, likisema, 3 “Sema kwa Rehoboamu mwana wa Selemani, mfalme wa Yuda, na kwa Israeli kataika Yuda na Benyamaini, 4 Yahwe anasema hivi, “Msivamie wala kufanya vita dhidi ya ndugu zako. Kila mmoja lazima arudi kwenye nyumba yake, kwa maana nimesababisha jambo hili kutokea.” Kwa hiyo wakayatii maneno ya Yahwe na kuacha kumvamia Yeroboamu. 5 Yeroboamu akaishi katika Yerusalemu na kujenga miji katika Yuda kwa ajili ya kujilinda. 6 Akaijenga Bethelehemu, EtamuTekoa, 7 Bethsusi, Soko, Adulamu, 8 Gathi, Maresha, Zifu, 9 Adoraimu, Lakishi, Azeka, 10 Sora, Aiyaloni, na Hebroni. Hii ni miji yenye ngome katika Yuda na Benyamini. 11 Akaziimarisha ngome na kuweka maamri jeshsi ndani yake, pamaoja na hazina ya chakula, mafuta, na divai. 12 Akaweka ngao na mikuki katika miji yote na kuifanya imara sana. Kwa hiyo Yuda na Benyamini zikawa zake. 13 Makuhani na Walawi waliokuwa katika Israeli yote wakaenda kwake kutoka ndani ya mipaka yao. 14 Kwa kuwa Walawi waliacha nchi za malisho yao na mali zao ili kuja Yuda na Yerusalemu, kwa maana 15 Yeroboamu na wanaaye walikuwa wamewafukuza, ili kwamba wasifanye majukumu yao ya kikuhani kwa ajili ya sehemu za juu na mbuzi na sanamu za ndama alizokuwa ametengeneza. 16 Watu kutoka kabila zote za Israeli wakaja nyuma yao, wale walio wameiilekeza mioyo yao kumtafuta Yahwe, Mungu wa Israeli; wakaja Yerusalemu kwa ajili ya kumtolea dhabihu Yahwe. Mungu wa baba zao. 17 Kwa hiyo wakauimarisha ufalame wa Yuda na kumfanya imara Rehoboamu mwana wa Selemani kwa miaka mitatu, na wakatembea kwa miaka mitatu katika njia ya Daudi na Selemani. 18 Rehoboamu akajitwalia mke: Mahalathi, binti wa Yerimothi, mwana wa Daudi na wa Abihaili, binti wa Eliabu, mwana wa Yese. 19 Akamzalia wana: Yeushi, Shemaraia, na Zahamu. 20 Baaad ya Mahalathi, Rehoboamu akamchukua Maaka, binti Absalomu; akamzalia Abiya, Atai, Ziza, na Shelomithi. 21 Rehoboamu akampenda Maaka, binti Solomoni, zaidi kuliko wake za wengine wote na masuria (alichukua wake kumi na nane na masuria sitini, na akawa baba wa wana ishirini na nane na mabinti sitini). 22 Rehoboamu akamteua Abiya mwana wa Maaka kuwa mkuu, kiongozi miongoni mwa ndugu zake alikuwa na wazo la kumfanya mfalme. 23 Rehoboamu akatawala kwa hekima; akawatawanya wanaye katika nchi yote ya Yuda na Benyamini katika kila mji imara. Pia akawapa chakula kwa wingi na akatafuta wake wengi kwa ajili yao.

< 2 Nyakati 11 >