< 1 Wathesalonike 5 >

1 Sasa, kwa habari ya muda na nyakati, ndugu, hamna haja kwamba kitu chochote kiandikwe kwenu.
Mais pour ce qui est des temps et des saisons, frères, vous n’avez pas besoin qu’on vous en écrive;
2 Kwa kuwa ninyi wenyewe mwajua kwa usahihi ya kuwa siku ya Bwana inakuja kama mwizi ajapo usiku.
car vous savez vous-mêmes parfaitement que le jour du Seigneur vient comme un voleur dans la nuit.
3 Pale wasemapo kuna “Amani na usalama”, ndipo uharibifu huwajia ghafla. Ni kama utungu umjiavyo mama mwenye mimba. Hawataepuka kwa njia yeyote.
Quand ils diront: “Paix et sûreté”, alors une subite destruction viendra sur eux, comme les douleurs sur celle qui est enceinte, et ils n’échapperont point.
4 Lakini ninyi, ndugu hampo kwenye giza hata ile siku iwajie kama mwizi.
Mais vous, frères, vous n’êtes pas dans les ténèbres, en sorte que le jour vous surprenne comme un voleur;
5 Kwa maana ninyi nyote ni wana wa nuru na wana wa mchana. Sisi siyo wana wa usiku au wa gizani.
car vous êtes tous des fils de la lumière et des fils du jour; nous ne sommes pas de la nuit ni des ténèbres.
6 Hivyo basi, tusilale kama wengine walalavyo. Bali tukeshe na kuwa makini.
Ainsi donc ne dormons pas comme les autres, mais veillons et soyons sobres;
7 Kwa kuwa wanaolala hulala usiku na wanao lewa hulewa usiku.
car ceux qui dorment, dorment la nuit, et ceux qui s’enivrent, s’enivrent la nuit;
8 Kwa kuwa sisi ni wana wa mchana, tuwe makini. Tuvae ngao ya imani na upendo, na, kofia ya chuma, ambayo ni uhakika wa wokovu wa wakati ujao.
mais nous qui sommes du jour, soyons sobres, revêtant la cuirasse de la foi et de l’amour, et, pour casque, l’espérance du salut;
9 Kwa kuwa Mungu hakutuchagua mwanzo kwa ajili ya gadhabu, bali kwa kupata wokovu kwa njia ya Bwana Yesu Kristo.
car Dieu ne nous a pas destinés à la colère, mais à l’acquisition du salut par notre seigneur Jésus Christ,
10 Yeye ndiye aliyetufia ili kwamba, tukiwa macho au tumelala, tutaishi pamoja naye.
qui est mort pour nous, afin que, soit que nous veillions, soit que nous dormions, nous vivions ensemble avec lui.
11 Kwa hiyo, farijianeni na kujengana ninyi kwa ninyi, kama ambavyo tayari mnafanya.
C’est pourquoi exhortez-vous l’un l’autre et édifiez-vous l’un l’autre, chacun en particulier, comme aussi vous le faites.
12 Ndugu, twawaomba muwatambue wale wanaotumika miongoni mwenu na wale walio juu yenu katika Bwana na wale wanao washauri.
Or nous vous prions, frères, de connaître ceux qui travaillent parmi vous, et qui sont à la tête parmi vous dans le Seigneur, et qui vous avertissent,
13 Tunawaomba pia muwatambue na kuwapa heshima katika upendo kwa sababu ya kazi yao. Muwe na amani miongoni mwenu ninyi wenyewe.
et de les estimer très haut en amour à cause de leur œuvre. Soyez en paix entre vous.
14 Twawasihi, ndugu: muwaonye wasio kwenda kwa utaratibu, watieni moyo walio kata tamaa, Wasaidieni walio wanyonge, na muwe wavumilivu kwa wote.
Or nous vous exhortons, frères: avertissez les déréglés, consolez ceux qui sont découragés, venez en aide aux faibles, usez de patience envers tous.
15 Angalieni asiwepo mtu yeyote anayelipa baya kwa baya kwa mtu yeyote. Badala yake, fanyeni yaliyo mema kwa kila mmoja wenu na kwa watu wote.
Prenez garde que nul ne rende à personne mal pour mal; mais poursuivez toujours ce qui est bon, et entre vous, et à l’égard de tous les hommes.
16 Furahini siku zote.
Réjouissez-vous toujours.
17 Ombeni bila kukoma.
Priez sans cesse.
18 Mshukuruni Mungu kwa kila jambo, kwa sababu hayo ndiyo mapenzi ya Mungu kwenu katika Yesu Kristo.
En toutes choses rendez grâces, car telle est la volonté de Dieu dans le christ Jésus à votre égard.
19 Msimzimishe Roho.
N’éteignez pas l’Esprit;
20 Msiudharau unabii.
ne méprisez pas les prophéties,
21 Yajaribuni mambo yote. Mlishike lililo jema.
mais éprouvez toutes choses; retenez ce qui est bon.
22 Epukeni kila mwonekano wa uovu.
Abstenez-vous de toute forme de mal.
23 Mungu wa amani awakamilishe katika utakatifu. Roho, nafsi na mwili vitunzwe pasipo mawaa katika kuja kwake Bwana wetu Yesu Kristo.
Or le Dieu de paix lui-même vous sanctifie entièrement; et que votre esprit, et votre âme, et votre corps tout entiers, soient conservés sans reproche en la venue de notre seigneur Jésus Christ.
24 Yeye aliyewaita ni mwaminifu, naye ndiye mwenye kutenda.
Celui qui vous appelle est fidèle, qui aussi le fera.
25 Ndugu, tuombeeni pia.
Frères, priez pour nous.
26 Wasalimuni ndugu wote kwa busu takatifu.
Saluez tous les frères par un saint baiser.
27 Nawasihi katika Bwana kwamba barua hii isomwe kwa ndugu wote.
Je vous adjure par le Seigneur que la lettre soit lue à tous les saints frères.
28 Neema ya Bwana wetu Yesu Kristo iwe pamoja nanyi.
Que la grâce de notre seigneur Jésus Christ soit avec vous!

< 1 Wathesalonike 5 >