< 1 Samweli 9 >

1 Basi kulikuwa na mtu mmoja kutoka Benyamini, mtu mashuhuri. Jina lake aliitwa Kishi mwana wa Abieli, mwana wa Zerori, mwana wa Bekorathi, mwana wa Afia, mwana wa Mbenyamini.
And he was a man (from Benjamin *QK) and name his [was] Kish [the] son of Abiel [the] son of Zeror [the] son of Becorath [the] son of Aphiah a son of a man a Jaminite a mighty [man] of wealth.
2 Huyu alikuwa na mtoto wa kiume aliyeitwa Sauli, kijana mzuri wa uso. Hapakuwapo mwanaume mzuri wa uso kuliko huyu miongoni mwa watu wote wa Israeli. Kutoka mabegani kwenda juu alikuwa mrefu kuliko watu wengine.
And to him he belonged a son and name his [was] Saul a young man and good and not a man from [the] people of Israel [was] good more than him from shoulder his and up-wards [he was] tall more than all the people.
3 Na punda wa Kishi, baba yake na Sauli walipotea. hivyo Kishi akamwambia Sauli mwanawe, “Mchukue mmoja wa watumishi; uamke uende kuwatafuta punda,”
And they were lost the she-asses of Kish [the] father of Saul and he said Kish to Saul son his take please with you one from the young men and arise go seek the she-asses.
4 Sauli akapita katika nchi ya vilima vilima ya Efraimu na akaenda akapita katika nchi ya Shalisha, lakini hawakuwaona. Kisha walipita katika nchi ya Shaalimu, lakini hawakuwa huko. Baadaye alipita katika nchi ya Wabenyamini, lakini hawakuwaona wale punda.
And he passed in [the] hill country of Ephraim and he passed in [the] land of Shalisha and not they found [them] and they passed in [the] land of Shaalim and there not and he passed in [the] land of [the] Jaminite[s] and not they found [them].
5 Na walipofika nchi ya Sufu, Sauli alimwambia mtumishi wake aliyekuwa naye, “Njoo na turudi, pengine baba aweza kuacha kuchunga punda na kuanza kutuhofia sisi.”
They they came in [the] land of Zuph and Saul he said to servant his who [was] with him come! so let us turn back lest he should cease father my from the she-asses and he will be anxious to us.
6 Lakini mtumishi akamwmbia, “Sikiliza, Yupo mtu wa Mungu katika mji huu. Naye ni mtu wa kuheshimiwa sana; kila asemalo huwa kweli. Hebu twende huko; labda anaweza kutuambia tupitie wapi katika safari yetu.”
And he said to him here! please a man of God [is] in the city this and the man [is] honored all that he speaks actually it comes now let us go there perhaps he will tell to us journey our which we have walked on it.
7 Ndipo Sauli akamwambia mtumish iwake, “Lakini kama tukienda kwake, twaweza kumpelekea nini? Maana hata mkate katika mfuko wetu umekwisha, na hakuna zawadi ya kumpelekea mtumishi wa Mungu. Tuna kitu gani?
And he said Saul to servant his and here! we will go and what? will we bring to the man for the bread it has been used up from bags our and [is] a gift there not to bring to [the] man of God what? [is] with us.
8 Huyo mtumishi akamjibu Sauli na kusema, “Hapa, ninayo robo ya shekeli ya fedha ambayo nitampa mtumishi wa Mungu, atuambie ni njia ipi yatupasa tuiendee.”
And he repeated the servant to answer Saul and he said here! [is] found in hand my a fourth part of a shekel of silver and I will give [it] to [the] man of God and he will tell to us journey our.
9 (Zamani katika Israeli, mtu alipotaka kujua neno kuhusu mapenzi ya Mungu, alisema, “Njoo, haya twende kwa mwonaji.” Kwa maana nabii wa leo, zamani aliitwa Mwonaji).
Before - in Israel thus he said the man when went he to consult God come so let us go to the seer for to the prophet this day it was called before the seer.
10 Ndipo Sauli akamwambia mtumishi wake, “Umesema vyema. Haya, njoo twende.” Basi wakaenda katika mji ambao mtu wa Mungu alikuwamo.
And he said Saul to servant his [is] good word your come! - let us go and they went to the city where [was] there [the] man of God.
11 Walipopanda mlima kuelekea mjini, walikutana na wasichana wakienda kuteka maji; Sauli na mtumishi wake wakawauliza, “Mwonaji hupo hapa?”
They [were] going up on [the] ascent of the city and they they found young women coming out to draw water and they said to them ¿ [is] there in this [place] the seer.
12 Nao wakawajibu, na kusema, “Yupo; tazameni, yuko mbele yenu. Harakisheni, kwa maana anakuja mjini leo, sababu leo watu wanatoa dhabihu zao mahali pa juu.
And they answered them and they said there is there! before you hurry - now for this day he has come to the city for a sacrifice this day [belongs] to the people at the high place.
13 Mara tu mtakapoingia mjini mtamuona, kabla hajapanda mahali pa juu kla chakula. Watu hawatakula hata atakapokuja, kwa sababu ndiye ataibariki dhabihu; na baadaye wale ambao wamealikwa hula. Basi pandeni, mtamuona sasa hivi.”
When come you the city thus you will find! him before he will go up the high place towards to eat for not it will eat the people until comes he for he he will bless the sacrifice after thus they will eat those [who] were invited and now go up for him as the day you will find! him.
14 Kwa hiyo walikwea kwenda mjini. Walipokuwa wakiingia mjini, walimuona Samweli akija mbele yao, akipanda kwenda mahali pa juu.
And they went up the city they [were] coming in [the] midst of the city and there! Samuel [was] coming out to meet them to go up the high place.
15 Siku moja kabla Sauli hajafika, BWANA alikuwa amemfunulia Samweli:
And Yahweh he had uncovered [the] ear of Samuel a day one before came Saul saying.
16 “Kesho wakati kama huu nitakutumia mtu kutoka nchi ya Benyamini, nawe utamtia mafuta awe mfalme juu ya watu wangu Israeli. Atawaokoa watu wangu kutoka mkono wa Wafilisti. Kwa kuwa nimewaonea huruma watu wangu na kilio cha kutaka msaada kimenifikia.”
About this time - tomorrow I will send to you a man from [the] land of Benjamin and you will anoint him to ruler over people my Israel and he will deliver people my from [the] hand of [the] Philistines for I have seen people my for it has come cry of distress its to me.
17 Samweli alipomuona Sauli, BWANA akamwambia, “Huyu ndiye mtu niliyekwambia habari zake! Yeye ndiye atakayewatawala watu wangu.”
And Samuel he saw Saul and Yahweh he answered him here! the man whom I spoke to you this [one] he will rule over people my.
18 Ndipo Sauli akaja karibu na Samweli katika lango na kusema, “Niambie nyumba ya Mwonaji iko wapi?
And he approached Saul Samuel in [the] middle of the gate and he said tell! please to me where? this [is] [the] house of the seer.
19 Samweli akamjibu Sauli akisema, “Mimi ndiye mwonaji. Tangulia mbele hadi mahali pa juu, nami nitakueleza kila kitu kilichomoyoni mwako.
And he answered Samuel Saul and he said I [am] the seer go up before me the high place and you will eat with me this day and I will send away you in the morning and all that [is] in heart your I will tell to you.
20 Kama punda wenu waliopotea siku tatu zilizopita, msihofu kuhusu hao punda, kwa kuwa wamekwishapatikana. Na yote yaliyotamanika kwa ajili ya Israeli yanamwangukia nani? Siyo kwako na nyumba ya baba yako yote?”
And to the she-asses which were lost of you this day [the] three the days may not you set heart your to them for they have been found and [belongs] to whom? every desirable thing of Israel ¿ not to you and to all [the] house of father your.
21 Sauli akamjibu na kusema, Siyo mimi Mbenyamini, kutoka kabila lililo dogo sana kwa makabila ya Israeli? Siyo ukoo wangu ulio mdogo sana kwa kabila la Benyamini? Kwa nini basi unaniambia kwa namna hii?”
And he answered Saul and he said ¿ not a Ben-jaminite [am] I from [the] small of [the] tribes of Israel and [is] clan? my the insignificant of all [the] clans of [the] tribes of Benjamin and why? have you spoken to me according to the manner this.
22 Hivyo Samweli akamchukua Sauli na mtumishi wake, akawaingiza ukumbini, akawakalisha mahali pa heshima pa wale walioalikwa, idadi yao takribani watu thelathini.
And he took Samuel Saul and servant his and he brought them [the] room towards and he gave to them a place at [the] head of those [who] were invited and they [were] about thirty man.
23 Samweli akamwambia mpishi, “Lete sehemu niliyokupatia, sehemu ambayo nilikwambia hivi, “Itenge.”'
And he said Samuel to the cook give! the portion which I gave to you which I said to you put it with you.
24 Basi mpishi alichukua paja lililokuwa limeinuliwa katika dhabihu na kile kilichokuwa pamoja nalo, akaitenga mbele ya Sauli. Kisha Samweli akasema, “Angalia kile kilichokuwa kimetunzwa kwa ajili yako! Kula, kwa sababu kilitunzwa hadi wakati maalum ufike kwa ajili yako. Na kwa sasa waweza kusema, 'Nimewaalika watu.”' Kwa hiyo Sauli alikula pamoja na Samweli siku hiyo.
And he lifted up the cook the thigh and the on it and he put [it] - before Saul and he said here! the [part which] remains set [it] before you eat [it] for to the appointed time [it was] kept for you saying the people - I have invited and he ate Saul with Samuel on the day that.
25 Walipokuwa wamekwisha shuka chini kutoka sehemu ya juu na kuingia mjini, Samweli akazungumza na Sauli darini.
And they went down from the high place the city and he spoke with Saul on the roof.
26 Na kulipopambazuka, Samweli alimwita Sauli darini na kusema, “Amka, kusudi nikusindikize uende zako,” Hivyo Sauli aliamka, na wote wawili, yeye na Samweli walitoka kwenda mtaani.
And they rose early and it was when came up the dawn and he called Samuel to Saul (the roof towards *QK) saying arise! so I may send away you and he arose Saul and they went out [the] two of them he and Samuel the outside towards.
27 Walipokuwa wakienda nje ya viunga vya mji, Samweli akamwambia Sauli, “Mwambie mtumishi wako atanguliye mbele yetu(na alitangulia mbele), Lakini wewe sharti usubiri kidogo, nipate kukuambia ujumbe wa Mungu.”
They [were] going down at [the] edge of the city and Samuel he said to Saul say to the servant so he may pass on before us and he passed on and you remain as the day so I may make hear you [the] word of God.

< 1 Samweli 9 >