< 1 Samweli 9 >

1 Basi kulikuwa na mtu mmoja kutoka Benyamini, mtu mashuhuri. Jina lake aliitwa Kishi mwana wa Abieli, mwana wa Zerori, mwana wa Bekorathi, mwana wa Afia, mwana wa Mbenyamini.
Now there was a man of Benjamin, whose name was Kish, the son of Abiel, the son of Zeror, the son of Becorath, the son of Aphiah, the son of a Benjamite, a mighty man of valour.
2 Huyu alikuwa na mtoto wa kiume aliyeitwa Sauli, kijana mzuri wa uso. Hapakuwapo mwanaume mzuri wa uso kuliko huyu miongoni mwa watu wote wa Israeli. Kutoka mabegani kwenda juu alikuwa mrefu kuliko watu wengine.
And he had a son, whose name was Saul, young and goodly, and there was not among the children of Israel a goodlier person than he: from his shoulders and upward he was higher than any of the people.
3 Na punda wa Kishi, baba yake na Sauli walipotea. hivyo Kishi akamwambia Sauli mwanawe, “Mchukue mmoja wa watumishi; uamke uende kuwatafuta punda,”
Now the asses of Kish Saul's father were lost. And Kish said to Saul his son: 'Take now one of the servants with thee, and arise, go seek the asses.'
4 Sauli akapita katika nchi ya vilima vilima ya Efraimu na akaenda akapita katika nchi ya Shalisha, lakini hawakuwaona. Kisha walipita katika nchi ya Shaalimu, lakini hawakuwa huko. Baadaye alipita katika nchi ya Wabenyamini, lakini hawakuwaona wale punda.
And he passed through the hill-country of Ephraim, and passed through the land of Shalishah, but they found them not; then they passed through the land of Shaalim, and there they were not; and he passed through the land of the Benjamites, but they found them not.
5 Na walipofika nchi ya Sufu, Sauli alimwambia mtumishi wake aliyekuwa naye, “Njoo na turudi, pengine baba aweza kuacha kuchunga punda na kuanza kutuhofia sisi.”
When they were come to the land of Zuph, Saul said to his servant that was with him: 'Come and let us return; lest my father leave caring for the asses, and become anxious concerning us.'
6 Lakini mtumishi akamwmbia, “Sikiliza, Yupo mtu wa Mungu katika mji huu. Naye ni mtu wa kuheshimiwa sana; kila asemalo huwa kweli. Hebu twende huko; labda anaweza kutuambia tupitie wapi katika safari yetu.”
And he said unto him: 'Behold now, there is in this city a man of God, and he is a man that is held in honour; all that he saith cometh surely to pass; now let us go thither; peradventure he can tell us concerning our journey whereon we go.'
7 Ndipo Sauli akamwambia mtumish iwake, “Lakini kama tukienda kwake, twaweza kumpelekea nini? Maana hata mkate katika mfuko wetu umekwisha, na hakuna zawadi ya kumpelekea mtumishi wa Mungu. Tuna kitu gani?
Then said Saul to his servant: 'But, behold, if we go, what shall we bring the man? for the bread is spent in our vessels, and there is not a present to bring to the man of God; what have we?'
8 Huyo mtumishi akamjibu Sauli na kusema, “Hapa, ninayo robo ya shekeli ya fedha ambayo nitampa mtumishi wa Mungu, atuambie ni njia ipi yatupasa tuiendee.”
And the servant answered Saul again, and said: 'Behold, I have in my hand the fourth part of a shekel of silver, that will I give to the man of God, to tell us our way.' —
9 (Zamani katika Israeli, mtu alipotaka kujua neno kuhusu mapenzi ya Mungu, alisema, “Njoo, haya twende kwa mwonaji.” Kwa maana nabii wa leo, zamani aliitwa Mwonaji).
Beforetime in Israel, when a man went to inquire of God, thus he said: 'Come and let us go to the seer'; for he that is now called a prophet was beforetime called a seer. —
10 Ndipo Sauli akamwambia mtumishi wake, “Umesema vyema. Haya, njoo twende.” Basi wakaenda katika mji ambao mtu wa Mungu alikuwamo.
Then said Saul to his servant: 'Well said; come, let us go.' So they went unto the city where the man of God was.
11 Walipopanda mlima kuelekea mjini, walikutana na wasichana wakienda kuteka maji; Sauli na mtumishi wake wakawauliza, “Mwonaji hupo hapa?”
As they went up the ascent to the city, they found young maidens going out to draw water, and said unto them: 'Is the seer here?'
12 Nao wakawajibu, na kusema, “Yupo; tazameni, yuko mbele yenu. Harakisheni, kwa maana anakuja mjini leo, sababu leo watu wanatoa dhabihu zao mahali pa juu.
And they answered them, and said: 'He is; behold, he is before thee; make haste now, for he is come to-day into the city; for the people have a sacrifice to-day in the high place.
13 Mara tu mtakapoingia mjini mtamuona, kabla hajapanda mahali pa juu kla chakula. Watu hawatakula hata atakapokuja, kwa sababu ndiye ataibariki dhabihu; na baadaye wale ambao wamealikwa hula. Basi pandeni, mtamuona sasa hivi.”
As soon as ye are come into the city, ye shall straightway find him, before he go up to the high place to eat; for the people will not eat until he come, because he doth bless the sacrifice; and afterwards they eat that are bidden. Now therefore get you up; for at this time ye shall find him.'
14 Kwa hiyo walikwea kwenda mjini. Walipokuwa wakiingia mjini, walimuona Samweli akija mbele yao, akipanda kwenda mahali pa juu.
And they went up to the city; and as they came within the city, behold, Samuel came out toward them, to go up to the high place.
15 Siku moja kabla Sauli hajafika, BWANA alikuwa amemfunulia Samweli:
Now the LORD had revealed unto Samuel a day before Saul came, saying:
16 “Kesho wakati kama huu nitakutumia mtu kutoka nchi ya Benyamini, nawe utamtia mafuta awe mfalme juu ya watu wangu Israeli. Atawaokoa watu wangu kutoka mkono wa Wafilisti. Kwa kuwa nimewaonea huruma watu wangu na kilio cha kutaka msaada kimenifikia.”
'To-morrow about this time I will send thee a man out of the land of Benjamin, and thou shalt anoint him to be prince over My people Israel, and he shall save My people out of the hand of the Philistines; for I have looked upon My people, because their cry is come unto Me.'
17 Samweli alipomuona Sauli, BWANA akamwambia, “Huyu ndiye mtu niliyekwambia habari zake! Yeye ndiye atakayewatawala watu wangu.”
And when Samuel saw Saul, the LORD spoke unto him: 'Behold the man of whom I said unto thee: This same shall have authority over My people.'
18 Ndipo Sauli akaja karibu na Samweli katika lango na kusema, “Niambie nyumba ya Mwonaji iko wapi?
Then Saul drew near to Samuel in the gate, and said: 'Tell me, I pray thee, where the seer's house is.'
19 Samweli akamjibu Sauli akisema, “Mimi ndiye mwonaji. Tangulia mbele hadi mahali pa juu, nami nitakueleza kila kitu kilichomoyoni mwako.
And Samuel answered Saul, and said: 'I am the seer; go up before me unto the high place, for ye shall eat with me to-day; and in the morning I will let thee go, and will tell thee all that is in thy heart.
20 Kama punda wenu waliopotea siku tatu zilizopita, msihofu kuhusu hao punda, kwa kuwa wamekwishapatikana. Na yote yaliyotamanika kwa ajili ya Israeli yanamwangukia nani? Siyo kwako na nyumba ya baba yako yote?”
And as for thine asses that were lost three days ago, set not thy mind on them; for they are found. And on whom is all the desire of Israel? Is it not on thee, and on all thy father's house?'
21 Sauli akamjibu na kusema, Siyo mimi Mbenyamini, kutoka kabila lililo dogo sana kwa makabila ya Israeli? Siyo ukoo wangu ulio mdogo sana kwa kabila la Benyamini? Kwa nini basi unaniambia kwa namna hii?”
And Saul answered and said: 'Am not I a Benjamite, of the smallest of the tribes of Israel? and my family the least of all the families of the tribe of Benjamin? wherefore then speakest thou to me after this manner?'
22 Hivyo Samweli akamchukua Sauli na mtumishi wake, akawaingiza ukumbini, akawakalisha mahali pa heshima pa wale walioalikwa, idadi yao takribani watu thelathini.
And Samuel took Saul and his servant, and brought them into the chamber, and made them sit in the chiefest place among them that were bidden, who were about thirty persons.
23 Samweli akamwambia mpishi, “Lete sehemu niliyokupatia, sehemu ambayo nilikwambia hivi, “Itenge.”'
And Samuel said unto the cook: 'Bring the portion which I gave thee, of which I said unto thee: Set it by thee.'
24 Basi mpishi alichukua paja lililokuwa limeinuliwa katika dhabihu na kile kilichokuwa pamoja nalo, akaitenga mbele ya Sauli. Kisha Samweli akasema, “Angalia kile kilichokuwa kimetunzwa kwa ajili yako! Kula, kwa sababu kilitunzwa hadi wakati maalum ufike kwa ajili yako. Na kwa sasa waweza kusema, 'Nimewaalika watu.”' Kwa hiyo Sauli alikula pamoja na Samweli siku hiyo.
And the cook took up the thigh, and that which was upon it, and set it before Saul. And Samuel said: 'Behold that which hath been reserved! set it before thee and eat; because unto the appointed time hath it been kept for thee, for I said: I have invited the people.' So Saul did eat with Samuel that day.
25 Walipokuwa wamekwisha shuka chini kutoka sehemu ya juu na kuingia mjini, Samweli akazungumza na Sauli darini.
And when they were come down from the high place into the city, he spoke with Saul upon the housetop.
26 Na kulipopambazuka, Samweli alimwita Sauli darini na kusema, “Amka, kusudi nikusindikize uende zako,” Hivyo Sauli aliamka, na wote wawili, yeye na Samweli walitoka kwenda mtaani.
And they arose early; and it came to pass about the break of day, that Samuel called to Saul on the housetop, saying: 'Up, that I may send thee away.' And Saul arose, and they went out both of them, he and Samuel, abroad.
27 Walipokuwa wakienda nje ya viunga vya mji, Samweli akamwambia Sauli, “Mwambie mtumishi wako atanguliye mbele yetu(na alitangulia mbele), Lakini wewe sharti usubiri kidogo, nipate kukuambia ujumbe wa Mungu.”
As they were going down at the end of the city, Samuel said to Saul: 'Bid the servant pass on before us — and he passed on — but stand thou still at this time, that I may cause thee to hear the word of God.'

< 1 Samweli 9 >