< 1 Samweli 6 >

1 Basi sanduku la BWANA lilikaa katika nchi ya Wafilisti kwa miezi saba.
The ark of Jehovah was in the country of the Philistines seven months.
2 Ndipo Wafilisti wakawaita makuhani na waganga; wakawaambia, “Tulifanyie nini sanduku la BWANA? Twambieni jinsi ambavyo tunapaswa kulirudisha sanduku katika nchi yake.”
The Philistines called for the priests, and for the diviners, and for the magicians, saying, "What shall we do with the ark of Jehovah? Tell us how we should send it to its place."
3 Makuhani na waganga wakasema, “Kama mtalirudisha sanduku la Mungu wa Israeli, msilipeleke bila zawadi; kwa namna yoyote ile mpelekeeni sadakaa ya hatia. Hapo ndipo mtapona, na mtajua ni kwanini mkono wake hadi sasa haujaondoka juu yenu.”
And they said, "If you are going to send away the ark of the God of Israel, do not send it empty. But return to him a reparation, then you shall be healed and he will be reconciled to you. Will not, then, his hand be removed from you?"
4 Ndipo wakawauliza, “Sadaka ya hatia itakuwa nini kwamba tunampelekea?” Wakawajibu, “Majipu matano ya dhahabu na panya watano wa dhahabu, Idadi hiyo ya watano ni sawa na idadi ya viongozi wa Wafilisti. Kwa sababu tauni ya aina moja iliwashambulia ninyi na viongozi wenu.
Then they said, "What shall be the trespass offering which we shall return to him?" They said, "Five golden tumors, and five golden mice, for the number of the lords of the Philistines; for one plague was on you all, and on your lords.
5 Kwa hiyo, nilazima mtengeneze mifano ya majipu yenu, na mifano ya panya wenu ambayo huiharibu nchi, na mpeni utukufu Mungu wa Israeli. Labda ataondoa mkono wake kutoka juu yenu, kutoka juu ya miungu yenu, na kutoka juu ya nchi yenu.
Therefore you shall make images of your tumors, and images of your mice that ravage the land, and you shall give glory to the God of Israel; perhaps he will lighten his hand from off you, and from off your gods, and from off your land.
6 Kwanini mfanye mioyo yenu kwa migumu, kama vile Wamisri na Farao walifanya mioyo yao kuwa migumu? Hicho ni kipindi ambacho Mungu wa Israeli aliwashughilikia sana; Je, Wamisri hawakuwaachilia watu, na wakaondoka?
Why then do you harden your hearts, as the Egyptians and Pharaoh hardened their hearts? When he had worked wonderfully among them, did they not let the people go, and they departed?
7 Basi sasa, andaeni mkokoteni mpya pamoja na ng'ombe wawili wake wanaonyonyesha, ambao hawajawahi kufungwa nira. Wafungeni ng'ombe hao kwenye mkokoteni, lakini warudisheni wale ndama wao nyumbani.
"Now therefore take and prepare yourselves a new cart, and two milk cows, on which there has come no yoke; and tie the cows to the cart, and bring their calves home from them;
8 Kisha lichukueni sanduku la BWANA na kuliweka ndani ya mkokoteni. Wekeni ndani ya kasha yale maumbo ya dhahabu mnayompelekea ambyo ni sadaka ya hatia kando yake. Ndipo mlipeleke lipate kuondoka.
and take the ark of Jehovah, and lay it on the cart; and put the figures of gold, which you return him for a trespass offering, in a box by its side; and send it away, that it may go.
9 Kisha muwe makini; kama litapanda kwenda kwa njia hadi nchini mwake hadi Beth Shemeshi, basi mjue kuwa BWANA ndiye aliyetenda pigo hili kubwa. Lakini kama halitakwenda, ndipo tutajua kwamba siyo mkono wake uliotupatia mateso; badala yake tutajua kuwa yaliyotupata ilikuwa ni kwa bahati mbaya tu.
And watch; if it goes up by the way of its own territory to Beth Shemesh, then he has done us this great evil: but if not, then we shall know that it is not his hand that struck us; it was a chance that happened to us."
10 Watu hao wakafanya kama walivyoambiwa, walichukuwa ng'ombe wawili wanaonyonyesha, wakawafunga kwenye mkokoteni, na kuwabakiza ndama wao nyumbani.
The men did so, and took two milk cows, and tied them to the cart, and shut up their calves at home;
11 Wakaliweka sanduku la BWANA juu ya mkokoteni, pamoja na lile kasha lililobeba panya wa dhahabu na yale maumbo ya majipu yao.
and they put the ark of Jehovah on the cart, and the box with the mice of gold and the images of their tumors.
12 Hao ng'ombe waliondoka moja kwa moja kuelekea Beth Shemeshi. Walikwenda kwa kuifuata nija moja kuu, wakiteremka walipokuwa wakienda, na hwakugeuka upande wa kushoto au kulia. Viongozi wa Wafilisti walifuata kwa nyuma hadi mpaka wa Beth Shemeshi.
The cows took the straight way by the way to Beth Shemesh; they went along the highway, mooing as they went, and did not turn aside to the right hand or to the left. And the lords of the Philistines followed them to the territory of Beth Shemesh.
13 Nao watu wa Beth Shemeshi walikuwa wakivuna ngano yao katika bonde. Waliponyanyua macho yao juu na kuliona sanduku, wakafurahi.
And those of Beth Shemesh were reaping their wheat harvest in the valley, and they lifted up their eyes and saw the ark, and rejoiced to see it.
14 Huo mkokoteni ulifikia ndani ya shamba la Yoshua wa Beth Shemeshi na ukasimama hapo. Kulikuapo jiwe kubwa mahali hapo, wakatayarisha kuni kutokana na mkokoteni huo, na wakawatoa ng'ombe hao kama sadaka ya kuteketezwa kwa ajili ya BWANA.
The cart came into the field of Joshua of Beth Shemesh, and stood there, where there was a great stone. And they split the wood of the cart, and offered up the cows for a burnt offering to Jehovah.
15 Walawi walilitelemsha sanduku la BWANA chini pamoja na kasha lake lililoyatunza yale maumbo ya dhahabu, wakaweka vitu hivyo juu ya hilo jiwe kubwa. Watu wa Beth Shemeshi walitoa sadaka za kuteketezwa na kutoa dhabihu kwa BWANA siku iyo hiyo.
The Levites took down the ark of Jehovah, and the chest that was with it, in which the articles of gold were, and put them on the great stone. And the men of Beth Shemesh offered burnt offerings and sacrificed sacrifices the same day to Jehovah.
16 Hao viongozi watano wa Wafilisti walipoona hayo, walirejea Ekroni siku iyo hiyo.
When the five lords of the Philistines had seen it, they returned to Ekron the same day.
17 Haya ndiyo majipu ya dhahabu ambayo Wafilisti walirudisha kama sadaka ya hatia kwa BWANA: moja kwa ajili ya Ashdodi, moja kwa Gaza, moja kwa Ashkeloni, moja kwa Gathi, na moja kwa Ekroni.
These are the golden tumors which the Philistines returned for a trespass offering to Jehovah: for Ashdod one, for Gaza one, for Ashkelon one, for Gath one, for Ekron one;
18 Idadi ya wale panya wa dhahabu ilikuwa sawa na ile ya idadi ya miji yote ya Wafilisti inayomilikiwa na viongozi watano, kwa miji iliyojengewa maboma na vijiji vya mashambani. Lile jiwe kubwa, ambalo kando yake waliweka sanduku la BWANA, lipo kama ushuhuda hadi leo katika shamba la Yoshua Mbeth- Shemeshi.
and the golden mice, according to the number of all the cities of the Philistines belonging to the five lords, both of fortified cities and of country villages, even to the great stone, whereon they set down the ark of Jehovah. That stone remains to this day in the field of Joshua of Beth Shemesh.
19 BWANA akawashambulia baadhi ya watu wa Bethi Shemeshi kwa sababu walichungulia ndani ya sanduku lake. Aliwaua watu sabini. Watu wakaomboleza, kwa sababu BWANA aliwapa watu pigo kubwa mno.
But the sons of Jeconiah did not rejoice with the people of Beth Shemesh when they saw the ark of Jehovah. So he struck seventy men of them, and the people mourned, because Jehovah had struck the people with a great slaughter.
20 Watu wa Bethi Shemeshi wakasema, “Ni nani mwenye uwezo wa kushindana na BWANA, huyu Mungu mtakatifu? Na atampandia nani akitoka kwetu.”” Je, ni nani awezaye kusimama mbele ya BWANA, huyu Mungu mtakatifu? Na ni kwa nani ambako sanduku litaenda likitoka hapa.”
And the men of Beth Shemesh said, "Who is able to stand before this holy thing? And to whom should he go up from us?"
21 Wakawatuma wajumbe kwenda kwa wenyeji wa Kiriath Yearimu, wakisema, “Wafilisti wamelirudisha sanduku la BWANA; teremkeni na mkalipeleke kwenu.”
They sent messengers to the inhabitants of Kiriath Jearim, saying, "The Philistines have brought back the ark of Jehovah; come down, and bring it up to yourselves."

< 1 Samweli 6 >