< 1 Samweli 5 >

1 Basi Wafilisti wakawa wamelitwaa sanduku la Mungu, wakalileta kutoka Ebenezeri hadi Ashdodi.
Now the Philistines had taken the ark of God, and they brought it from Eben-ezer unto Ashdod.
2 Wafilisti walilichukua sanduku la Mungu, wakalileta ndani ya nyumba ya Dagoni, na wakalikalisha pembeni mwa Dagoni.
And the Philistines took the ark of God, and brought it into the house of Dagon, and set it by Dagon.
3 Watu wa Ashdodi walipoamka mapema siku ya pili, tazama, Dagoni ilianguka chini kifudifudi mbele ya sanduku la BWANA. Hivyo waliichukua Dagoni na kuisimamisha tena katika sehemu yake.
And when they of Ashdod arose early on the morrow, behold, Dagon was fallen upon his face to the ground before the ark of the LORD. And they took Dagon, and set him in his place again.
4 Lakini walipoamka mapema kesho yake, tazama, Dagoni alikuwa ameanguka chini kifudifudi mbele ya sanduku la BWANA. Kichwa cha Dagoni na vitanga vyake miwili vilikatika na kulala mlangoni. Kiwiliwili cha Dagoni ndicho kilibaki tu.
And when they arose early on the morrow morning, behold, Dagon was fallen upon his face to the ground before the ark of the LORD; and the head of Dagon and both the palms of his hands lay cut off upon the threshold; only the trunk of Dagon was left to him.
5 Na hii ndiyo sababu, makuhani wa Dagoni na yeyote aingiae ndani ya nyumba ya Dagoni, hata leo, hawezi kukanyaga mlango wa Dagoni katika Ashdodi.
Therefore neither the priests of Dagon, nor any that come into Dagon's house, tread on the threshold of Dagon in Ashdod unto this day.
6 Mkono wa BWANA ulikuwa mzito juu ya watu wa Ashdodi. Aliwaangamiza akawatesa kwa majipu, Ashdodi na wilaya zake kwa pamoja.
But the hand of the LORD was heavy upon them of Ashdod, and He destroyed them, and smote them with emerods, even Ashdod and the borders thereof.
7 Watu wa Ashdodi walipotambua kilichokuwa kinatokea, walisema, “Sanduku la Mungu wa Israeli lisikae kwetu, kwa sababu mkono wake ni mzito juu yetu na juu ya mungu wetu Dagoni.”
And when the men of Ashdod saw that it was so, they said: 'The ark of the God of Israel shall not abide with us; for His hand is sore upon us, and upon Dagon our god.'
8 Basi wakawatuma watu wawakusanye pamoja viongozi wote wa Wafilisti; wakawambia, “Tufanye nini na sanduku la Mungu wa Israeli?” Wakawajibu, “Sanduku la Mungu wa Israeli lihamishwe na kupelekwa Gathi.” Basi wakalihamisha hilo sanduku la Mungu wa Israeli hadi huko Gathi.
They sent therefore and gathered all the lords of the Philistines unto them, and said: 'What shall we do with the ark of the God of Israel?' And they answered: 'Let the ark of the God of Israel be carried about unto Gath.' And they carried the ark of the God of Israel about thither.
9 Lakini baada ya kulipeleka huko, mkono wa BWANA ulikuwa juu ya mji huo, ukasababisha machafuko makubwa. Akawatesa watu wa mji huo, wakubwa kwa wadogo; na majipu yakaota juu ya miili yao.
And it was so, that, after they had carried it about, the hand of the LORD was against the city with a very great discomfiture; and He smote the men of the city, both small and great, and emerods broke out upon them.
10 Basi, wakalipeleka sanduku la Mungu hadi Ekroni. Lakini mara tu sanduku la Mungu lilipoingia Ekroni, watu wa Ekroni walipiga kelele wakisema, “Wametuletea sanduku la Mungu wa Israeli kutuua sisi na watu wetu.”
So they sent the ark of God to Ekron. And it came to pass, as the ark of God came to Ekron, that the Ekronites cried out, saying: 'They have brought about the ark of the God of Israel to us, to slay us and our people.'
11 Basi wakawatuma watu wawakusanye pamoja viongozi wote wa Wafilisti; wakawambia, “Lipelekeni mbali sanduku la Mungu wa Israeli, na lirudishwe katika makao yake, ili lisije kutuua sisi na watu wetu.” Kwa maana kulikuwa na hofu ya kutisha mjini mwote; Mkono wa Mungu ulikuwa mzito mno huko.
They sent therefore and gathered together all the lords of the Philistines, and they said: 'Send away the ark of the God of Israel, and let it go back to its own place, that it slay us not, and our people'; for there was a deadly discomfiture throughout all the city; the hand of God was very heavy there.
12 Watu ambao hawakufa waliteswa na majipu, na kilio cha mji kilipanda hadi mbinguni.
And the men that died not were smitten with the emerods; and the cry of the city went up to heaven.

< 1 Samweli 5 >