< 1 Samweli 31 >

1 Basi Wafilisti wakapigana dhidi ya Waisraeli. Waisraeli wakakimbia mbele ya Wafilisti na wakaanguka chini wakafa katika mlima wa Gilboa.
And [the] Philistines [were] fighting against Israel and they fled [the] men of Israel from before [the] Philistines and they fell slain on [the] mountain of Gilboa.
2 Wafilisti wakamwandama Sauli na wanawe kwa karibu. Wakawaua wanawe Yonathani, Abinadabu, and Malkishua.
And they pursued closely [the] Philistines Saul and sons his and they struck down [the] Philistines Jonathan and Abinadab and Malki-Shua [the] sons of Saul.
3 Vita vikamwelemea Sauli, na wapiga upinde wakampata. Akapata maumivu makali kwa sababu yao.
And it was heavy the battle against Saul and they found him the archers men with the bow and he was in severe pain exceedingly from the archers.
4 Kisha Sauli akamwambia mbeba silaha wake, “Chomoa upanga wako unichome nao. Vinginevyo, hawa wasiotahiriwa watakuja na kuninyanyasa.” Lakini mbeba silaha wake hakukubali, kwa kuwa aliogopa sana. Hivyo Sauli alichukua upanga wake mwenyewe na kuuangukia.
And he said Saul to [the] bearer of armor his draw out sword your - and pierce through me with it lest they should come the uncircumcised [men] these and they will pierce through me and they will deal wantonly with me and not he was willing [the] bearer of armor his for he was afraid exceedingly and he took Saul the sword and he fell on it.
5 Yule mbeba silaha akaona kwamba Sauli amekufa, yeye naye vivyo hivyo akauangukia upanga wake akafa pamoja naye.
And he saw [the] bearer of armor his that he had died Saul and he fell also he on sword his and he died with him.
6 Kwa hiyo Sauli alikufa, wanawe watatu, na mbeba silaha wake - watu hawa wote walikufa pamoja siku iyo hiyo.
And he died Saul and [the] three sons his and [the] bearer of armor his also all men his on the day that together.
7 Watu wa Israeli waliokuwa upande mwingine wa bonde, na hao waliokuwa ng'ambo ya Yordani, walipoona kwamba Waisraeli wamekimbia, na kwamba Sauli na wanawe wamekufa, waliiacha miji yao na kukimbia, nao Wafilisti wakaja na kukaa humo.
And they saw [the] men of Israel who [were] on [the] other side of the valley and who - [were] on [the] other side of the Jordan that they had fled [the] men of Israel and that they had died Saul and sons his and they abandoned the cities and they fled and they came [the] Philistines and they dwelt in them.
8 IKawa katika siku iliyofuata, Wafilisti wakafika kuchukua nyara za waliokufa, ndipo wakamuona Sauli na wanawe watatu wameanguka juu ya mlima wa Gilboa.
And it was from [the] next day and they came [the] Philistines to strip the [ones] slain and they found Saul and [the] three sons his fallen on [the] mountain of Gilboa.
9 Nao wakakata kichwa chake na kuondoa silaha zake, na wakawatuma wajumbe kwenda pande zote katika nchi ya Wafilisti kutangaza habari hizo katika mahekalu yao ya sanamu na kwa watu.
And they cut off head his and they stripped off armor his and they sent in [the] land of [the] Philistines all around to bear [the] news [the] house of idols their and the people.
10 Wakaziweka silaha zake katika hekalu la Ashtorethi, nao wakakitundika kiwiliwili chake kwenye ukuta wa mji wa Bethi Shani.
And they put armor his [the] house of Ashtaroth and corpse his they fixed on [the] wall of Beth Shan.
11 Na wenyeji wa Yabeshi Gileadi waliposikia kile Wafilisti walichomfanyia Sauli,
And they heard concerning him [the] inhabitants of Jabesh Gilead [that] which they had done [the] Philistines to Saul.
12 wapiganaji wote wakainuka na kwenda usiku wote na wakauondoa mwili wa Sauli na miili ya wanawe kutoka ukuta wa Bethi Shani. Nao wakaenda Yabeshi na wakaichoma moto hiyo miili huko.
And they arose every man of strength and they went all the night and they took [the] corpse of Saul and [the] corpses of sons his from [the] wall of Beth Shan and they went Jabesh towards and they burned them there.
13 Kisha wakachukua mifupa yao na kuizika chini ya mti wa mkwaju huko Yabeshi, na wakafunga siku saba.
And they took bones their and they buried [them] under the tamarisk tree at Jabesh and they fasted seven days.

< 1 Samweli 31 >