< 1 Samweli 30 >

1 Ikawa, Daudi na watu wake walipokuwa wamefika Ziklagi siku ya tatu, Waamaleki walifanya mashambulizi katika Negevu na Ziklagi. Waliupiga Ziklagi, wakauchoma moto mji,
And it was when came David and men his Ziklag on the day third and [the] Amalekite[s] they had made a raid against [the] Negev and against Ziklag and they had struck Ziklag and they had burned it with fire.
2 na kuwachukua mateka wanawake na kila mmoja aliyekuwa ndani yake, mkubwa kwa mdogo. Wao hawakuua hata mmoja, lakini waliwachukua watu na kuondoka nao.
And they had taken captive the women who [were] in it from small and unto great not they had killed anyone and they had driven them away and they had gone to way their.
3 Daudi na watu wake walipofika kwenye mji, ulikuwa umechomwa moto - na wake zao, watoto wao wakiume na wakike walichukuliwa mateka.
And he came David and men his to the city and there! [it was] burned with fire and wives their and sons their and daughters their they had been taken captive.
4 Ndipo Daudi na watu aliokuwa nao wakapaza sauti zao na kulia hadi walipokuwa hawana nguvu zaidi za kulia.
And he lifted up David and the people which [was] with him voice their and they wept until that not [was] in them strength to weep.
5 Wake wawili wa Daudi walichukuliwa mateka, yaani Ahinoamu Myezreeli, na Abigaili aliyekuwa mke wa Nabali Mkarmeli.
And [the] two [the] wives of David they had been taken captive Ahinoam the Jezreelite [woman] and Abigail [the] wife of Nabal the Carmelite.
6 Daudi aliguswa sana, maana watu walikuwa wanaongea kuhusu kumpiga mawe, kwa sababu roho za watu wote walihuzunika, kila mtu kwa ajili ya mtoto wake wakiume na wakike, lakini Daudi alijiimarisha katika BWANA, Mungu wake.
And it was distress to David exceedingly for they said the people to stone him for it was bitter [the] soul of all the people everyone on (sons his *QK) and on daughters his and he strengthened himself David in Yahweh God his.
7 Daudi akamwambia Abiathari, kuhani, mwana wa Ahimeleki, “Tafadhali, niletee hapa ile naivera.”Abiathari akaileta hiyo naivera kwa Daudi.
And he said David to Abiathar the priest [the] son of Ahimelech bring near! please to me the ephod and he brought near Abiathar the ephod to David.
8 Daudi akamwomba BWANA kwa ajili ya mwongozo, akisema, “Je, kama nikiliandama jeshi hili, nitalipata?” BWANA akamjibu, “Wafuate, maana kweli utawapata, na kwa hakika utarudisha kila kitu.”
And he enquired David by Yahweh saying will I pursue? after the marauding band this ¿ will I overtake it and he said to him pursue for certainly you will overtake [it] and certainly you will rescue [them].
9 Kwa hiyo Daudi akaenda, yeye na wale watu mia sita waliokuwa pamoja naye; nao wakafika katika kijito cha Bethori, mahali walipokaa wale walioachwa nyuma.
And he went David he and six hundred man who [were] with him and they came to [the] wadi of Besor and those [who] were left behind they remained.
10 Lakini Daudi aliendelea kuwafuata, yeye na watu mia nne; maana wale mia mbili walibaki nyuma, wakiwa wamechoka kiasi cha kutoweza kuvuka kijito cha Besori.
And he pursued David he and four hundred man and they remained two hundred man who they were [too] exhausted for passing over [the] wadi of Besor.
11 Nao walimkuta Mmisri shambani na wakamleta kwa Daudi; wakampatia mkate, na akala; wakampa maji ya kunywa;
And they found a man Egyptian in the open country and they took him to David and they gave to him bread and he ate and they gave to drink him water.
12 kisha walimpa kipande cha keki ya tini na vishada viwili vya zabibu. Alipomaliza kula, akapata nguvu tena, kwa kuwa alikuwa hajala mkate wala kunywa maji, siku tatu mchana na usiku.
And they gave to him a slice of fig cake and two bunches of raisins and he ate and it returned spirit his to him for not he had eaten food and not he had drunk water three days and three nights.
13 Ndipo Daudi akamuuliza, “Wewe ni mtu wa nani? Je, unatoka wapi?” Naye akajibu, “Mimi ni kijana wa Misri, mtumishi wa Mwamaleki mmoja; bwana wangu aliniacha, kwa sababu siku tatu zilizopita nilikuwa mgonjwa.
And he said to him David [belong] to whom? you and where? from this [are] you and he said [am] a young man Egyptian I a slave of a man Amalekite and he abandoned me master my if I was sick the day three.
14 Tulifanya mashambulizi dhidi ya Negevu ya Wakerethi, na iliyochini ya Yuda, na ile Negevu ya Kalebu, na kuichoma moto Ziklagi.”
We we had made a raid [the] Negev of the Kerethite[s] and on [that] which [belongs] to Judah and on [the] Negev of Caleb and Ziklag we had burned with fire.
15 Daudi akamwambia, “Je, utanipeleka hadi kwa jeshi lililofanya mashabulizi?” Huyo Mmisri akasema, “Uniapie kwa Mungu kwamba hautaniua au kunisaliti na kuniweka katika mikono ya bwana wangu, nami nitakupeleka liliko hilo jeshi.”
And he said to him David ¿ will you take down me to the marauding band this and he said swear! to me by God if you will kill me and if you will deliver up me in [the] hand of master my and I will take down you to the marauding band this.
16 Yule Mmisri alipompeleka huko Daudi, hao wateka nyara walikuwa wametawanyika kila sehemu, wakila na kunywa, na wakicheza, kwa sababu ya nyara zote walizokuwa wamezitwaa kutoka nchi ya Wafilisti na kutoka nchi ya Yuda.
And he took down him and there! [they were] spread out over [the] face of all the land eating and drinking and celebrating in all the plunder great which they had taken from [the] land of [the] Philistines and from [the] land of Judah.
17 Daudi akawashambulia tangu jua lilipozama hadi jioni ya siku ya pili. Hakuna mtu aliyeponyoka isipokuwa vijana mia nne, waliopanda ngamia na kukimbia.
And he struck down them David from the twilight and until the evening of next day their and not he escaped of them anyone that except four hundred man young man who they rode on the camels and they fled.
18 Daudi akarudisha vyote ambavyo Waamaleki walikuwa wamevichukua; na Daudi akawaokoa wake zake wawili.
And he rescued David all that they had taken Amalek and [the] two wives his he rescued David.
19 Hakuna kilichopotea, si kidogo wala kikubwa, si watoto wa kiume wala wa kike, si mali iliyotekwa, wala chochote ambacho wavamizi alikichukuwa kwa ajili yao. Daudi akawa amerejesha kila kitu.
And not it was missing to them from the small and unto the great and unto sons and daughters and from [the] booty and unto all that they had taken for themselves everything he brought back David.
20 Akachukua makundi yote ya kondoo na ng'ombe, ambayo watu waliyatanguliza mbele ya ng'ombe wengine. Wakisema, “Hizi ni nyara za Daudi.”
And he took David all the sheep and the cattle they drove [them] before the livestock that and they said this [is] [the] booty of David.
21 Daudi akafika kwa wale watu mia mbili waliokuwa wamechoka kufuatana naye, wale walioachwa wakae katika kijito cha Besori. Watu hawa wakajitokeza kumlaki na watu waliokuwa naye.
And he came David to two hundred the men who they had been [too] exhausted - for going - after David and they had left behind them at [the] wadi of Besor and they went out to meet David and to meet the people which [was] with him and he approached David the people and he asked of them to welfare.
22 Ndipo watu wote waovu na wasiofaa miongoni mwa waliokwenda na Daudi wakasema, “Kwa sababu watu hawa hawakwenda nasi, hatutawapa chochote kutoka katika nyara tulizorudisha. Isipokuwa kila mtu aweza kuchukuwa mke na watoto wake, wawatoe na kwenda zao.”
And he answered every man evil and worthlessness from the men who they had gone with David and they said because that not they went with me not we will give to them any of the booty which we have recovered that except everyone wife his and children his so they may lead [them] away and they may go.
23 Ndipo Daudi akasema, “Ndugu zangu, msifanye hivyo, kwa vitu ambavyo BWANA ametupatia. Ametuhifadhi na kuwaweka mkononi mwetu wavamizi waliotuinukia.
And he said David not you must do thus O brothers my [that] which he has given Yahweh to us and he has kept us and he has given the marauding band which came on us in hand our.
24 Ni nani atawasikiliza kuhusu jambo hili? Kwa maana mgawo ni kwa yeyote aendae vitani, basi pia mgawo ni kwa yeyote aliyelinda mizigo; Nao watapata tena kilicho sawa.”
And who? will he listen to you to the matter this for like [the] share of - the [one who] went down in the battle and like [the] share of the [one who] remained with the baggage alike they will share.
25 Ilikuwa hivyo tangu siku hiyo hadi leo, maana Daudi aliamua iwe sheria na amri kwa Israeli.
And it was from the day that and on-wards and he made it into a statute and into a judgment for Israel until the day this.
26 Daudi alipofika Ziklagi, alituma sehemu ya nyara kwa wazee wa Yuda, kwa rafiki zake, akisema, “Tazama, hii ni zawadi yenu kutokana na nyara za adui wa BWANA.”
And he came David to Ziklag and he sent some of the booty to [the] elders of Judah to friend his saying here! [is] for you a blessing from [the] booty of [the] enemies of Yahweh.
27 Zawadi zilienda kwa wazee waliokuwa Bethueli, na kwa hao waliokuwa Ramothi iliyoko kusini, na kwa hao waliokuwa Yatiri,
For [those] who [were] in Beth-el and for [those] who [were] in Ramoth Negev and for [those] who [were] in Jattir.
28 na kwa hao waliokuwa Aroeri, na kwa hao waliokuwa Sifmothi, na kwa hao waliokuwa Eshtemoa
And for [those] who [were] in Aroer and for [those] who [were] in Siphmoth and for [those] who [were] in Eshtemoa.
29 Pia kwa wazee waliokuwa Rakali, na kwa hao waliokuwa katika miji ya Wayerameeli, na kwa hao waliokuwa katika miji ya Wakeni,
And for [those] who [were] in Racal and for [those] who [were] in [the] cities of the Jerahmeelite[s] and for [those] who [were] in [the] cities of the Kenite[s].
30 na kwa hao waliokuwa Horma, na kwa hao waliokuwa Borashani, na kwa hao waliokuwa Athaki,
And for [those] who [were] in Hormah and for [those] who [were] in Bor Ashan and for [those] who [were] in Athach.
31 na kwa hao waliokuwa Hebroni, na kwa sehemu zote ambazo Daudi mwenyewe na watu wake walizoea kwenda.
And for [those] who [were] in Hebron and for all the places where he had gone about there David he and men his.

< 1 Samweli 30 >