< 1 Samweli 29 >

1 Basi Wafilisti walikusanya pamoja majeshi yao yote huko Afeki; Waisraeli wakapiga kambi karibu na chemchemi iliyoko Yezreeli.
Now the Philistines collected all their armies to Aphek: and the Israelites encamped by a fountain which [is] in Jezreel.
2 Nao wakuu wa Wafilisti wakapitwa na mamia kwa maelfu; Daudi na watu wake wakapita wakiwa wa mwisho pamoja na Akishi.
And the lords of the Philistines passed on by hundreds, and by thousands: but David and his men passed on in the rear with Achish.
3 Kisha wakuu wa Wafilisti wakasema, “Hawa Waebrania wanafanya nini hapa?” Akishi akawaambia wakuu wengine wa Wafilisti, “Huyu si Daudi, mtumishi wa Sauli, mfalme wa Israeli, ambaye amekaa nami kwa siku hizi, au kwa miaka hii, nami nimeona hana kosa tangu aje kwangu hadi leo?”
Then said the princes of the Philistines, What [do] these Hebrews [here]? And Achish said to the princes of the Philistines, [Is] not this David, the servant of Saul the king of Israel, who hath been with me these days, or these years, and I have found no fault in him since he fell [to me] to this day?
4 Lakini wale wakuu wa Wafilisti walimkasirikia Akishi; wakamwabia, Mfukuze mtu huyo, aende kwake kule ulikompatia; usimruhusu aende nasi vitani, ili asiwe adui yetu katika vita. Kwa jinsi gani mtu huyu angeweza kufanya amani na bwana wake? Siyo kwa gharama ya vichwa vya watu wetu?
And the princes of the Philistines were wroth with him; and the princes of the Philistines said to him, Make this man return, that he may go again to his place which thou hast appointed him, and let him not go down with us to battle, lest in the battle he should be an adversary to us: for with what would he reconcile himself to his master? [would it] not [be] with the heads of these men?
5 Je, huyu siye Daudi ambaye walimuimba kwa kupokezana na kucheza, wakisema: 'Sauli ameua maelfu yake, Na Daudi makumi elfu yake?”'
[Is] not this David, of whom they sung one to another in dances, saying, Saul slew his thousands, and David his ten thousands?
6 Ndipo Akishi alimwita Daudi na kumwambia, “Kama BWANA aishivyo, umekuwa mwema, na kutoka kwako na kuingia kwako pamoja nami katika jeshi ni kwema kama nionavyo mimi; maana sijaona kosa kwako tangu siku unakuja kwangu hadi siku hii ya leo. Hata hivyo, wakuu hawakupendi.
Then Achish called David, and said to him, Surely, [as] the LORD liveth, thou hast been upright, and thy going out and thy coming in with me in the host [is] good in my sight: for I have not found evil in thee from the day of thy coming to me to this day: nevertheless the lords favor thee not.
7 Basi sasa rudi na uende kwa amani, ili usiwakwaze wakuu wa Wafilisti.”
Therefore now return, and go in peace, that thou displease not the lords of the Philistines.
8 Daudi akamwambia Akishi, “Lakini nimefanya nini? Kitu gani umekiona kwa mtumishi wako kwa muda ambao nimekuwa mbele yako hadi leo, kiasi kwamba nisiende kupigana na adui za bwana wangu mfalme?”
And David said to Achish, But what have I done? and what hast thou found in thy servant, so long as I have been with thee to this day, that I may not go and fight against the enemies of my lord the king.
9 Akishi akajibu na kumwambia Daudi, “Najua kwamba hauna lawama mbele zangu kama alivyo malaika wa Mungu; hata hivyo, wale wakuu wa Wafilisti wamesema, Kamwe hatapanda pamoja nasi hadi vitani.'
And Achish answered and said to David, I know that thou [art] good in my sight, as an angel of God: notwithstanding, the princes of the Philistines have said, He shall not go up with us to the battle.
10 Basi sasa amka asubuhi na mapema na watumishi wa bwana wako waliokuja pamoja nawe; mara tu muamkapo asubuhi na mapema na kupata mwanga, ondokeni.”
Wherefore now rise early in the morning with thy master's servants that are come with thee: and as soon as ye shall have risen early in the morning, and have light, depart.
11 Hivyo Daudi aliamka mapema, yeye pamoja na watu wake, waondoke asubuhi, warudi kule katika nchi ya Wafilisti. Lakini Wafilisti walipanda kwenda Yezreeli.
So David and his men rose early to depart in the morning, to return into the land of the Philistines. And the Philistines went up to Jezreel.

< 1 Samweli 29 >