< 1 Samweli 28 >

1 Ikawa katika siku hizo Wafilisti walikusanya majeshi yao pamoja kwa ajili ya vita, wapigane na Israeli. Akishi akamwambia Daudi, “Ujue kwa hakika kwamba utakwenda nami ndani ya jeshi, wewe na watu wako.”
and to be in/on/with day [the] they(masc.) and to gather Philistine [obj] camp their to/for army: war to/for to fight in/on/with Israel and to say Achish to(wards) David to know to know for with me to come out: come in/on/with camp you(m. s.) and human your
2 Naye Daudi akamwambia Akishi, “Sasa utajua kile ambacho mtumishi wako anaweza kufanya.” Akishi akamwambia Daudi, “Basi sasa, nitakufanya uwe mlinzi wangu binafsi daima.”
and to say David to(wards) Achish to/for so you(m. s.) to know [obj] which to make: do servant/slave your and to say Achish to(wards) David to/for so to keep: guard to/for head my to set: make you all [the] day
3 Samweli alikuwa amefariki; Waisraeli wote walimwomboleza na kumzika huko Rama, katika mji wake mwenyewe. Wakati huo Sauli alikuwa amewafukuza kutoka nchini wote walioongea na wafu au pepo.
and Samuel to die and to mourn to/for him all Israel and to bury him in/on/with Ramah and in/on/with city his and Saul to turn aside: remove [the] medium and [obj] [the] spiritist from [the] land: country/planet
4 Wafilisti walijikusanya wao wenyewe wakaja na kuweka kambi huko Shunemu; na Sauli akawakusanya Israeli wote pamoja, na wakaweka kambi yao huko Gilboa.
and to gather Philistine and to come (in): come and to camp in/on/with Shunem and to gather Saul [obj] all Israel and to camp in/on/with Gilboa
5 Sauli alipoona jeshi la Wafilisti, aliogopa na moyo wake ukatetemeka sana.
and to see: see Saul [obj] camp Philistine and to fear and to tremble heart his much
6 Sauli alipomuomba BWANA kwa ajili ya msaada, BWANA hakumjibu - si kwa ndoto wala kwa Urimu, wala kwa manabii.
and to ask Saul in/on/with LORD and not to answer him LORD also in/on/with dream also in/on/with Urim also in/on/with prophet
7 Ndipo Sauli akawaambia watumishi wake, “Mnitafutie mwanamke ambaye anaweza kuongea na wafu, ili ni mwendee na kutafuta msaada wake.” Watumishi wake wakamwambia, “Tazama, yupo mwanamke huko Endori awezaye kuongea na wafu.”
and to say Saul to/for servant/slave his to seek to/for me woman mistress medium and to go: went to(wards) her and to seek in/on/with her and to say servant/slave his to(wards) him behold woman mistress medium in/on/with En-dor En-dor
8 Basi Sauli akajigeuza, akavaa nguo nyingine tofauti, akaondoka yeye pamoja na watu wawili; wakamwendea yule mwanamke wakati wa usiku. Akasema, “Nitabirie, nakuomba, kwa kuongea na wafu, na uniinulie yule nitakayekutajia.”
and to search Saul and to clothe garment another and to go: went he/she/it and two human with him and to come (in): come to(wards) [the] woman night and to say (to divine *Qk) please to/for me in/on/with medium and to ascend: establish to/for me [obj] which to say to(wards) you
9 Yule mwanamke akamwambia, “Tazama, unajua alichofanya Sauli, jinsi alivyowafukuza kutoka katika nchi wanaoongea na wafu au mizimu. Basi kwa nini mnatega mtego kwa ajili ya uhai wangu, ili kuniua?”
and to say [the] woman to(wards) him behold you(m. s.) to know [obj] which to make: do Saul which to cut: eliminate [obj] [the] medium and [obj] [the] spiritist from [the] land: country/planet and to/for what? you(m. s.) to snare in/on/with soul: life my to/for to die me
10 Sauli akamwapia kwa BWANA na kusema, “Kama BWANA aishivyo, hakuna adhabu utakayopata kutokana na jambo hili.”
and to swear to/for her Saul in/on/with LORD to/for to say alive LORD if: surely no to meet you iniquity: punishment in/on/with word: thing [the] this
11 Kisha yule mwanamke akasema, “Je, nikuinulie nani?” Sauli akasema, “Niinulie Samweli.”
and to say [the] woman [obj] who? to ascend: establish to/for you and to say [obj] Samuel to ascend: establish to/for me
12 Yule mwanamke alipomwona Samweli, akalia kwa sauti kuu na kusema na Sauli, akisema, “Kwa nini umenidanganya? Maana wewe ni Sauli.”
and to see: see [the] woman [obj] Samuel and to cry out in/on/with voice great: large and to say [the] woman to(wards) Saul to/for to say to/for what? to deceive me and you(m. s.) Saul
13 Mfalme akamwambia, “Usiogope. Unaona kitu gani?” Yule mwanamke akamwambia Sauli, “Naona mungu akitoka katika nchi.” Akamuuliza mwanamke,
and to say to/for her [the] king not to fear for what? to see: see and to say [the] woman to(wards) Saul God to see: see to ascend: rise from [the] land: soil
14 “Je, anafanana na nani?” Mwanamke akajibu, “Mtu mzee anazuka; naye amevaa kanzu.” Sauli akafahamu kuwa huyo ni Samweli, naye Sauli akainamisha uso wake hadi chini akionesha heshima.
and to say to/for her what? appearance his and to say man old to ascend: rise and he/she/it to enwrap robe and to know Saul for Samuel he/she/it and to bow face land: soil [to] and to bow
15 Samweli akamwambia Sauli, “Kwa nini umenisumbua na kuniinua juu?” Sauli akajibu, “Nimetaabika sana, maana Wafilisti wamepanga vita dhidi yangu, na Mungu ameniacha na hanipi majibu tena, si kwa manabii, wala kwa ndoto. Kwa hiyo nimekuita, ili unijulishe kile nitakachofanya.”
and to say Samuel to(wards) Saul to/for what? to tremble me to/for to ascend: establish [obj] me and to say Saul to constrain to/for me much and Philistine to fight in/on/with me and God to turn aside: depart from upon me and not to answer me still also in/on/with hand: by [the] prophet also in/on/with dream and to call: call to [emph?] to/for you to/for to know me what? to make: do
16 Samweli akasema, “Kwa kuwa BWANA amekuacha, basi unaniuliza nini, naye amekuwa adui yako?
and to say Samuel and to/for what? to ask me and LORD to turn aside: turn aside from upon you and to be enemy your
17 BWANA amekutendea kile alichosema kuwa angekifanya. BWANA amerarua ufalme kutoka mkononi mwako na amempa ufalme mtu mwingine - amempa Daudi.
and to make: do LORD to/for him like/as as which to speak: speak in/on/with hand: themselves my and to tear LORD [obj] [the] kingdom from hand your and to give: give her to/for neighbor your to/for David
18 Kwa sababu hukuitii sauti ya BWANA na hukutekeleza hasira yake kali juu ya Amaleki, kwa hiyo leo naye amefanya hili kwako.
like/as as which not to hear: obey in/on/with voice LORD and not to make: do burning anger face: anger his in/on/with Amalek upon so [the] word: thing [the] this to make: do to/for you LORD [the] day: today [the] this
19 Zaidi ya hayo, BWANA atamweka Israeli pamoja na wewe katika mkono wa Wafilisti. Kesho wewe na wanao mtakuwa pamoja nami. BWANA pia ataliweka jeshi la Israeli katika mkono wa Wafilisti.”
and to give: give LORD also [obj] Israel with you in/on/with hand: power Philistine and tomorrow you(m. s.) and son: child your with me also [obj] camp Israel to give: give LORD in/on/with hand: power Philistine
20 Ndipo ghafla Sauli alianguka chini kifudifudi na aliogopa kwa sababu ya yale maneno ya Samweli. Aliishiwa nguvu mwilini mwake, kwa kuwa siku hiyo alikuwa hajala chakula, hata kwa usiku huo wote.
and to hasten Saul and to fall: fall fullness height his land: soil [to] and to fear much from word Samuel also strength not to be in/on/with him for not to eat food all [the] day and all [the] night
21 Ndipo yule mwanamke akaja kwa Sauli na akaona kwamba Sauli amepata shida, naye akamwambia, “Tazama, mjakazi wako ameisikiliza sauti yako; Nimeyaweka maisha yangu mkononi mwangu na nimeyasikiliza maneno uliyoniambia.
and to come (in): come [the] woman to(wards) Saul and to see: see for to dismay much and to say to(wards) him behold to hear: obey maidservant your in/on/with voice: message your and to set: put soul: life my in/on/with palm my and to hear: hear [obj] word: thing your which to speak: speak to(wards) me
22 Hivyo basi, nakusihi, sikiliza pia sauti ya mjakazi wako, na uniruhusu nilete chakula kidogo mbele yako. Ule ili upate nguvu za kwenda kule uendako.”
and now to hear: obey please also you(m. s.) in/on/with voice: listen maidservant your and to set: make to/for face: before your morsel food: bread and to eat and to be in/on/with you strength for to go: went in/on/with way: journey
23 Lakini Sauli alikataa na kusema, “Sitakula.” Lakini watumishi wake, pamoja na yule mwanamke, wakamlazimisha hatimaye alisikiliza sauti zao. Hivyo aliinuka kutoka chini na kukaa kitandani.
and to refuse and to say not to eat and to break through in/on/with him servant/slave his and also [the] woman and to hear: hear to/for voice their and to arise: rise from [the] land: soil and to dwell to(wards) [the] bed
24 Yule mwanamke alikuwa na ndama mnono hapo nyumbani; akafanya haraka na kumchinja; akachua unga, akaukanda, na akatengeneza mikate isiyotiwa chachu kwa unga huo.
and to/for woman calf stall in/on/with house: home and to hasten and to sacrifice him and to take: take flour and to knead and to bake him unleavened bread
25 Akaileta mbele ya Sauli na watumishi wake, nao wakala. Baaadaye waliinuka na kuondoka usiku huo.
and to approach: bring to/for face: before Saul and to/for face: before servant/slave his and to eat and to arise: rise and to go: went in/on/with night [the] he/she/it

< 1 Samweli 28 >