< 1 Samweli 26 >

1 Wazifi wakamwendea Sauli huko Gibea na kusema, “Je, Daudi akujificha katika vilima vya Hakila, ambavyo viko mbele ya jangwa?”
The Ziphites came to Saul to Gibeah, saying, "Doesn't David hide himself on the hill of Hakilah, which is before Jeshimon?"
2 Kisha Sauli akaamka na kwenda chini ya jangwa la Zifu, akiwa na watu elfu tatu waliochaguliwa katika Israeli, wamtafute Daudi katika jangwa la Zifu.
Then Saul arose, and went down to the wilderness of Ziph, having three thousand chosen men of Israel with him, to seek David in the wilderness of Ziph.
3 Sauli akaweka kambi kwenye kilima cha Hakila, kilicho mbele ya jangwa, kando ya barabara. Lakini Daudi alikuwa akikaa nyikani, na akaona kwamba Sauli alikuwa anamfuatia huko jangwani.
Saul camped on the hill of Hakilah, which is before Jeshimon, near the road. But David stayed in the wilderness, and he saw that Saul came after him into the wilderness.
4 Hivyo Daudi akawatuma wapelelezi na akafahamu kwamba hakika Sauli alikuwa amekuja.
David therefore sent out spies, and understood that Saul had certainly come.
5 Daudi akaamka na kwenda hadi mahali ambapo Sauli alipiga kambi; akaona mahali alipolala Sauli, na Abneri mwana wa Neri, mkuu wa jeshi lake; Sauli alilala katikati ya kambi, na watu walipiga kambi kumzunguka, na wote wamesinzia.
David arose, and came to the place where Saul had camped; and David saw the place where Saul lay, and Abner the son of Ner, the captain of his army: and Saul lay within the place of the wagons, and the people were camped around him.
6 Ndipo Daudi akamwambia Ahimeleki Mhiti, na Abishai mwana wa Seruya, ndugu yake Yoabu, “Ni nani atakwenda nami kambini kwa Sauli? Abishai akasema, “Mimi nitashuka pamoja nawe.”
Then answered David and said to Ahimelech the Hethite, and to Abishai the son of Zeruiah, brother to Joab, saying, "Who will go down with me to Saul to the camp?" Abishai said, "I will go down with you."
7 Hivyo Daudi na Abishai wakaliendea jeshi usiku. Na Sauli alikuwapo akisinzia ndani ya kambi, mkuki wake umechomekwa chini pembeni mwa kichwa chake. Abneri na Askari wake wamelala kwa kumzunguka.
So David and Abishai came to the people by night: and, look, Saul lay sleeping within the place of the wagons, with his spear stuck in the ground at his head; and Abner and the people lay around him.
8 Kisha Abishai akamwambia Daudi, “Leo Mungu amemweka adui yako mkononi mwako. Basi tafadhali acha nimchome mkuki nimtoboe hadi chini kwa pigo moja. Sitampiga mara mbili.”
Then Abishai said to David, "God has delivered up your enemy into your hand this day. Now therefore please let me strike him with the spear to the earth at one stroke, and I will not strike him the second time."
9 Daudi akamwambia Abishai, “Usimwangamize; kwa maana nani awezaye kunyoosha mkono wake dhidi ya mtiwa mafuta wa BWANA na asiwe na hatia?”
David said to Abishai, "Do not destroy him; for who can put forth his hand against Jehovah's anointed, and be guiltless?"
10 Daudi akasema, “Kama BWANA aishivyo, BWANA atamuua, au siku ya kufa kwake itakuja, au atakwenda katika vita na ataangamia.
David said, "As Jehovah lives, Jehovah will strike him; or his day shall come to die; or he shall go down into battle and perish.
11 BWANA apishe mbali nisinyooshe mkono wangu dhidi ya mtiwa mafuta wake; lakini sasa, nakusihi chukua mkuki uliokichwani pake na jagi la maji, tuondoke.”
Jehovah forbid that I should put forth my hand against Jehovah's anointed; but now please take the spear that is at his head, and the jar of water, and let us go."
12 Hivyo Daudi akachukua mkuki na jagi la maji kutoka kichwani pa Daudi, wakatoweka. Hakuna mtu aliyewaona au kufahamu habari hii, wala hakuna aliyetoka usingizini, maana wote walisinzia, kwa sababu usingizi mzito kutoka kwa BWANA uliwaangukia.
So David took the spear and the jar of water from Saul's head; and they went away: and no man saw it, nor knew it, neither did any awake; for they were all asleep, because a deep sleep from Jehovah was fallen on them.
13 Kisha Daudi akaenda upande mwingine na akasimama juu ya mlima mbali sana; ukiwepo umbali mkubwa katikati yao.
Then David went over to the other side, and stood on the top of the mountain afar off; a great space being between them.
14 Daudi akawapigia kelele watu hao na Abneri mwana Neri; akisema, “Hujibu neno, Abneri?” Ndipo Abneri akajibu na kusema, “Wewe ni nani unayempigia mfalme kelele?”
And David called to the people, and to Abner the son of Ner, saying, "Do you not answer, Abner?" Then Abner answered, "Who are you that calls?"
15 Daudi akamwambia Abneri, “Wewe siye mtu jasiri? Ni nani yuko kama wewe katika Israeli? Kwa nini basi hukukaa macho kumlinda bwana wako mfalme? Kwa maana mtu fulani aliingia kumuua mfalme, bwana wako.
David said to Abner, "Aren't you a man? Who is like you in Israel? Why then have you not kept watch over your lord, the king? For one of the people came in to destroy the king your lord.
16 Jambo hili ulilolifanya siyo zuri. Kama BWANA aishivyo, unapaswa kufa kwa sababu hukumlinda bwana wako, mtiwa mafuta wa BWANA. Na sasa tazama ulipo mkuki wa mfalme, na jagi la maji lililokuwa kichwani pake.”
This thing isn't good that you have done. As Jehovah lives, you are worthy to die, because you have not kept watch over your lord, Jehovah's anointed. Now look, where is the king's spear, and where is the jar of water that was by his head?"
17 Sauli aliitambua sauti ya Daudi akasema, “Hiyo ni sauti yako, Daudi mwanangu?” Daudi akasema, “Ni sauti yangu, mfalme, bwana wangu.”
Saul knew David's voice, and said, "Is this your voice, my son David?" David said, "It is my voice, my lord, O king."
18 Daudi akasema, “Kwa nini bwana wangu anamwandama mtumishi wake? Nimefanya nini? Mkononi mwangu kuna uovu gani?
He said, "Why does my lord pursue after his servant? For what have I done? Or what evil is in my hand?
19 Kwa hiyo sasa, nakusihi, bwana wangu mfalme asikilize maneno ya mtumishi wake. Kama ni BWANA ndiye amekuchochea dhidi yangu, na aikubali sadaka; lakini kama ni wanadamu, na walaaniwe mbele za BWANA, maana leo wamenifukuza, nisishikamane na urithi wa BWANA; wameniambia, 'Nenda ukaabudu miungu mingine.'
Now therefore, please let my lord the king hear the words of his servant. If it is so that God has stirred you up against me, let him accept an offering. But if it is from human beings, they are cursed before Jehovah; for they have driven me out this day that I shouldn't cling to Jehovah's inheritance, saying, 'Go, serve other gods.'
20 Kwa hiyo, sasa, usiiachilie damu yangu ianguke ardhini mbali na uwepo wa BWANA; kwa kuwa mfalme wa Israeli ametoka nje kutafuta kiroboto, kama vile mtu awindavyo kware milimani.”
Now therefore, do not let my blood fall to the earth away from the presence of Jehovah; for the king of Israel has come out to seek a flea, as when one hunts a partridge in the mountains."
21 Kisha Sauli akasema, “Nimefanya dhambi. Rudi, Mwanangu, Daudi; maana sitakudhuru tena, kwa sababu leo maisha yangu yalikuwa yenye thamani machoni pako. Tazama, nimetenda upumbavu na nimekosa sana.”
Then Saul said, "I have sinned. Return, my son David; for I will no more do you harm, because my life was precious in your eyes this day. Look, I have played the fool, and have erred exceedingly."
22 Daudi akajibu na akasema, “Tazama, mkuki wako uko hapa, mfalme! Mruhusu kijana mmojawapo aje auchukue na aulete kwako.
And David answered and said, "Look, the king's spear. Now let one of the young men come over and get it.
23 Na BWANA amlipe kila mtu kwa ajili ya uadilifu wake na kwa uaminifu wake; kwa sababu leo BWANA alikuweka mkononi mwangu, lakini nisinge mpiga mtiwa mafuta wake.
Jehovah will render to every man his righteousness and his faithfulness; because Jehovah delivered you into my hand today, and I wouldn't put forth my hand against Jehovah's anointed.
24 Na tazama, kama maisha yako leo yalivyokuwa ya thamani machoni pangu, vivyo hivyo maisha yangu yathaminiwe sana machoni pa BWANA, na aweze kuniokoa katika shida zote.”
Look, as your life was respected this day in my eyes, so let my life be respected in the eyes of Jehovah, and let him deliver me out of all oppression."
25 Ndipo Sauli akamwambia Daudi, “Na ubarikiwe, mwanangu Daudi, ili uweze kutenda mambo makuu, na hakika uweze kufanikiwa.” Ndipo Daudi akaenda zake, na Sauli akarudi kwake.
Then Saul said to David, "You are blessed, my son David. You shall both do mightily, and shall surely prevail." So David went his way, and Saul returned to his place.

< 1 Samweli 26 >