< 1 Samweli 2 >

1 Hana aliomba akasema, “moyo wangu wamtukuza BWANA. Pembe yangu imejulikana katika BWANA. Kinywa changu kinatamba dhidi ya maadui zangu, kwa kuwa naufurahia wokovu wako.
And Hannah prayed, and said: my heart exulteth in the LORD, my horn is exalted in the LORD; my mouth is enlarged over mine enemies; because I rejoice in Thy salvation.
2 Hakuna aliye mtakatifu kama BWANA, kwa kuwa hakuna mwingine zaidi yako; hakuna mwamba kama Mungu wetu.
There is none holy as the LORD, for there is none beside Thee; neither is there any rock like our God.
3 Msijivune sana hivyo kwa kiburi; vinywa vyenu visitoke majivuno. Kwa kuwa BWANA ni Mungu wa maarifa; yeye huyapima matendo kwa mizani.
Multiply not exceeding proud talk; let not arrogancy come out of your mouth; for the LORD is a God of knowledge, and by Him actions are weighed.
4 Pinde za mashujaa zimevunjika, bali wale wanaojikwaa hujivika nguvu kama mshipi.
The bows of the mighty men are broken, and they that stumbled are girded with strength.
5 Wale walio na shibe ya kutosha wamejikodisha ili wapate chakula; wale waliokuwa na njaa hawana njaa tena. Hata yule aliye kuwa tasa amezaa watoto saba, bali mwanamke mwenye watoto wengi amenyong'onyea.
They that were full have hired out themselves for bread; and they that were hungry have ceased; while the barren hath borne seven, she that had many children hath languished.
6 BWANA huua na huuisha. Hushusha kuzimu na huleta tena juu. (Sheol h7585)
The LORD killeth, and maketh alive; He bringeth down to the grave, and bringeth up. (Sheol h7585)
7 BWANA humfanya maskini, na yeye ndiye humtajirisha mtu. Yeye hudhili, lakini pia hukweza
The LORD maketh poor, and maketh rich; He bringeth low, He also lifteth up.
8 Yeye humwinua juu maskini toka mavumbini: Huwainua wahitaji toka jalalani na kuwaketisha pamoja na wakuu na kuwarithisha kiti cha enzi cha utukufu. Kwa kuwa nguzo za dunia ni za BWANA na ameukalisha ulimwengu juu yake.
He raiseth up the poor out of the dust, He lifteth up the needy from the dung-hill, to make them sit with princes, and inherit the throne of glory; for the pillars of the earth are the LORD'S, and He hath set the world upon them.
9 Yeye atazilinda nyayo za watu wake waaminifu, bali waovu watanyamazishwa gizani, kwa maana hakuna atayeshinda kwa nguvu zake.
He will keep the feet of His holy ones, but the wicked shall be put to silence in darkness; for not by strength shall man prevail.
10 Wale wampingao BWANA watavunjwa vipande vipande; atawapiga radi kutokea mbinguni. BWANA atahukumu miisho ya dunia; atampa nguvu mfalme wake na kuinua pembe ya mtiwa mafuta wake.”
They that strive with the LORD shall be broken to pieces; against them will He thunder in heaven; the LORD will judge the ends of the earth; and He will give strength unto His king, and exalt the horn of His anointed.
11 Nndipo Elikana akenda Rama, nyumbani kwake. Na yule mtoto akamtumikia BWANA machoni pa Eli, kuhani.
And Elkanah went to Ramah to his house. And the child did minister unto the LORD before Eli the priest.
12 Basi, watoto wa Eli walikuwa wakorofi. Wao hawakumheshimu BWANA.
Now the sons of Eli were base men; they knew not the LORD.
13 Desturi ya makuhani na watu ilikuwa kwamba endapo mtu yeyote ametoa dhabihu, mtumishi wa kuhani angekuja akiwa na uma wa meno matatu mkononi mwake, nyama ilipokuwa inatokoswa.
And the custom of the priests with the people was, that, when any man offered sacrifice, the priest's servant came, while the flesh was in seething, with a flesh-hook of three teeth in his band;
14 Naye angeutia uma huo sufuriani, au birikani au chomboni au chunguni; nyama yote ambayo ingeinuliwa na uma huo ingetwaliwa na kuhani mwenyewe. Ndivyo walivyofanya huko Shilo kwa Waisraeli wote waliokwenda huko.
and he struck it into the pan, or kettle, or caldron, or pot; all that the flesh-hook brought up the priest took therewith. So they did unto all the Israelites that came thither in Shiloh.
15 Tena, kabla ya kuteketeza mafuta, mtumishi wa kuhani alikuja, na kumwambia aliyekuwa akitoa dhabihu, “Tenga nyama ya kuchoma kwa ajili ya kuhani; kwa sababu hataikubali ile ya kutokosa kutoka kwako, bali tu ile mbichi.”
Yea, before the fat was made to smoke, the priest's servant came, and said to the man that sacrificed: 'Give flesh to roast for the priest; for he will not have sodden flesh of thee, but raw.'
16 Ikiwa mtu atamwambia, “Wachome mafuta kwanza, na kisha uchukue kiasi utakacho.” Ndipo angesema, “Hapana, utanipatia sasa hivi; la sivyo; Nitaichukua kwa lazima.”
And if the man said unto him: 'Let the fat be made to smoke first of all, and then take as much as thy soul desireth'; then he would say: 'Nay, but thou shalt give it me now; and if not, I will take it by force.'
17 Dhambi ya vijana hawa ilikuwa mbaya sana mbele za BWANA, kwa sababu waliidharau dhabihu ya BWANA.
And the sin of the young men was very great before the LORD; for the men dealt contemptuously with the offering of the LORD.
18 Lakini Samweli alimtumikia BWANA akiwa mdogo akivaa nguo ya naivera ya kitani.
But Samuel ministered before the LORD, being a child, girded with a linen ephod.
19 Kila mwaka mama yake alimtengenezea kanzu dogo na kumletea, wakati wakija na mmewe kutoa dhabihu ya kila mwaka.
Moreover his mother made him a little robe, and brought it to him from year to year, when she came up with her husband to offer the yearly sacrifice.
20 Eli aliwabariki Elikana na mke wake na kusema, “BWANA akupatie watoto zaidi kwa mwanamke huyu kwa sababu ya ahadi yake aliyoitoa kwa BWANA.” Baadaye walirudi nyumbani kwao.
And Eli would bless Elkanah and his wife, and say: 'The LORD give thee seed of this woman for the loan which was lent to the LORD.' And they would go unto their own home.
21 BWANA alimsaidia tena Hana, akawa amebeba mimba nyingine. Akazaa watoto watatu wa kiume na wa kike wawili. Wakati huo huo mtoto Samweli akakua akiwa mbele za BWANA.
So the LORD remembered Hannah, and she conceived, and bore three sons and two daughters. And the child Samuel grew before the LORD.
22 Basi Eli alikuwa mzee sana, akayasikia yote ambayo watoto wake walikuwa wakiwafanyia Waisraeli wote, na jinsi walivyotembea na mwanamke aliyekuwa akitumika katika lango la hema ya kukutania.
Now Eli was very old; and he heard all that his sons did unto all Israel, and how that they lay with the women that did service at the door of the tent of meeting.
23 Akawaambia, “Kwa nini mnafanya mambo hayo? Kwa maana nasikia matendo yenu maovu kutoka kwa watu hawa wote.”
And he said unto them: 'Why do ye such things? for I hear evil reports concerning you from all this people.
24 Sivyo hivyo, watoto wangu, maana hii ninayoisikia siyo taarifa njema. Mnawakosesha watu wa BWANA.
Nay, my sons; for it is no good report which I hear the LORD'S people do spread abroad.
25 “Kama mtu mmoja akimkosea mwenzake, Mungu atamhukumu; Lakini mtu akimkosea BWANA, ni nani atakayemtetea mtu huyo?” Lakini hawakuitii sauti ya baba yao, sababu BWANA alinuia kuwaua.
If one man sin against another, God shall judge him; but if a man sin against the LORD, who shall entreat for him?' But they hearkened not unto the voice of their father, because the LORD would slay them.
26 Yule mtoto Samweli aliongezeka umri, na kupata kibali kwa BWANA na kwa watu pia.
And the child Samuel grew on, and increased in favour both with the LORD, and also with men.
27 Kisha mtu wa Mungu akamwendea Eli na kumwambia, “BWANA asema, 'Je, sikujifunua mwenyewe kwa nyumba ya baba zako, walipokuwa Misri utumwani nyumbani mwa Farao?
And there came a man of God unto Eli, and said unto him: 'Thus saith the LORD: Did I reveal Myself unto the house of thy father, when they were in Egypt in bondage to Pharaoh's house?
28 Mimi nilimchagua yeye kutoka makabila yote ya Israeli awe kuhani wangu, apande madhabahuni kwangu, na kufukiza uvumba, na kuvaa kanzu ya naivera mbele yangu. Niliwapa nyumba ya baba zako dhabihu zote za wana wa Israeli zilizotolewa kwa moto.
And did I choose him out of all the tribes of Israel to be My priest, to go up unto Mine altar, to burn incense, to wear an ephod before Me? and did I give unto the house of thy father all the offerings of the children of Israel made by fire?
29 Kwanini basi, unaidharau dhabihu yangu na sadaka ambazo ninazitaka mahali ninapoishi? Kwanini unawaheshimu watoto wako kuliko mimi, kwa kujinenepesha ninyi wenyewe kwa uzuri wa kila sadaka ya watu wangu Israeli?'
Wherefore kick ye at My sacrifice and at Mine offering, which I have commanded in My habitation; and honourest thy sons above Me, to make yourselves fat with the chiefest of all the offerings of Israel My people?
30 Maana, BWANA, Mungu wa Isareli, asema, niliahidi kwamba nyumba yako, na nyumba ya baba yako, yawapasa kwenda mbele zangu milele,' Lakini sasa BWANA asema. 'Mambo haya yapishe mbali. nami nisifanye hivi, maana nitawaheshimu wanaoniheshimu, bali wanaonidharau mimi hawatakuwa na thamani.
Therefore the LORD, the God of Israel, saith: I said indeed that thy house, and the house of thy father, should walk before Me for ever; but now the LORD saith: Be it far from Me: for them that honour Me I will honour, and they that despise Me shall be lightly esteemed.
31 Tazama, siku zinakuja nitakapoondoa nguvu zako na nguvu za nyumba za baba yako, ili kwamba pasije kuwepo mtu mzee katika nyumba yako.
Behold, the days come, that I will cut off thine arm, and the arm of thy father's house, that there shall not be an old man in thy house.
32 Nawe utalitazama hangaiko katika makao yangu. Ingawa Israeli watapewa jambo jema, hapatakuwapo tena mtu yeyote mzee katika nyumba yako.
And thou shalt behold a rival in My habitation, in all the good which shall be done to Israel; and there shall not be an old man in thy house for ever.
33 Yeyote miongoni mwenu nisiye mwondoa kutoka madhabahuni pangu, Nitasababisha macho yenu yaanguke, na ita nitasababisha huzuni maishani mwenu. Wanaume wote waliozaliwa katika familia yako watakufa.
Yet will I not cut off every man of thine from Mine altar, to make thine eyes to fail, and thy heart to languish; and all the increase of thy house shall die young men.
34 Hii ndiyo itakuwa ishara kwako ambayo itawaijia watoto wako wakiume wawili, juu ya Hofni na Finehasi: Wote wawili watakufa siku moja.
And this shall be the sign unto thee, that which shall come upon thy two sons, on Hophni and Phinehas: in one day they shall die both of them.
35 Nami nitamwinua juu kuhani wangu mwaminifu atakaye fanya kile kilichomo moyoni mwangu na nafisini mwangu. Nami nitamjengea nyumba madhubuti; naye atakwenda mbele ya mfalme wangu mbarikiwa milele.
And I will raise Me up a faithful priest, that shall do according to that which is in My heart and in My mind; and I will build him a sure house; and he shall walk before Mine anointed for ever.
36 Kila mmoja aliyebakia nyumbani mwako atakuja na kusujudu mbele ya mtu huyo, akiomba kipande cha fedha na mkate mmoja, naye atasema, “Tafadhali uniajiri katika moja ya nafasi za kuhani ili niweze kula kipande cha mkate'”'
And it shall come to pass, that every one that is left in thy house shall come and bow down to him for a piece of silver and a loaf of bread, and shall say: Put me, I pray thee, into one of the priests' offices, that I may eat a morsel of bread.'

< 1 Samweli 2 >