< 1 Samweli 15 >

1 Samweli akamwambia Sauli, “BWANA alinituma nikutie mafuta uwe mfalme wa watu wake Israeli. Basi sikiliza maneno ya BWANA.
And he said Samuel to Saul me he sent Yahweh to anoint you to king over people his over Israel and therefore listen to [the] voice of [the] words of Yahweh.
2 Hivi ndivyo BWANA wa majeshi asemavyo, 'Nilichunguza jinsi Amaleki alivyomfanyia Israeli kwa kuwapinga njiani, walipopanda kutoka Misri.
Thus he says Yahweh of hosts I have paid attention to [that] which it did Amalek to Israel [that] which it set to it on the way when came up it from Egypt.
3 Sasa nenda umshambulie Amaleki na ukaangamize kabisa vitu vyote walivyo navyo. Usiwaache, ua wote mwanamme na mwanamke, mtoto na mtoto mchanga, ng'ombe na kondoo, ngamia na punda.”'
Now go and you will attack Amalek and you will totally destroy all that [belongs] to it and not you must have compassion on it and you will put to death from a man unto a woman from a child and unto a sucking child from an ox and unto a sheep from a camel and unto a donkey.
4 Sauli akwaita watu na kuwahesabu katika mji wa Talemu: watu mia mbili elfu waendao kwa miguu, na watu elfu kumi kutoka Yuda.
And he summoned Saul the people and he mustered them at Telaim two hundred thousand foot soldier[s] and ten thousand with man of Judah.
5 Kisha Sauli akaja hadi mji wa Amaleki akangoja huko bondeni.
And he came Saul to [the] city of Amalek and he lay in wait in the wadi.
6 Ndipo Sauli akawaambia Wakeni, “Nendeni, muondoke, mkajitenge na Waamaleki, nisije kuwaangamiza pamoja nao. Kwa maana ulionesha wema kwa watu wote wa Israeli, walipotoka Misri.” Kwa hiyo Wakeni wakajitenga na Waamaleki.
And he said Saul to the Kenite[s] go depart go down from among [the] Amalekite[s] lest I should destroy you with it and you you did loyalty with all [the] people of Israel when came up they from Egypt and it departed [the] Kenite[s] from among Amalek.
7 Kisha sauli akawashambulia Waamaleki, kutoka Havila hadi kufika Shuri, ulio mashariki mwa Misri.
And he attacked Saul Amalek from Havilah coming you Shur which [is] on [the] face of Egypt.
8 Basi akamchukua Agagi mfalme wa Waamaleki akiwa hai; aliwaangamiza kabisa watu wote kwa ncha ya upanga.
And he seized Agag [the] king of Amalek alive and all the people he totally destroyed to [the] mouth of [the] sword.
9 Lakini Sauli na watu wake wakamwacha Agagi akiwa hai, pamoja na kondoo wazuri, ng'ombe, ndama wanono, na wanakondoo. Kila kitu kilichokuwa kizuri, hawakukiangamiza. Bali waliangamiza kabisa chochote kilichodharaulika na kisicho na thamani.
And he had compassion Saul and the people on Agag and on [the] best of the sheep and the cattle and the second and on the lambs and on all the good and not they were willing to totally destroy them and all the property despised and worthless it they totally destroyed.
10 Baadaye neno la BWANA likamjia Samweli, kusema,
And it came [the] word of Yahweh to Samuel saying.
11 “Inanihuzunisha kwamba nimemchagua Samweli awe mfalme, kwa maana aligeuka nyuma asinifuate na hakutekeleza maagizo yangu.” Samweli alikasirika; akamlilia BWANA usiku kucha.
I regret that I have made king Saul to king for he has turned back from after me and words my not he has carried out and it burned to Samuel and he cried out to Yahweh all the night.
12 Samweli aliamka mapema akutane na Sauli wakati wa asubuhi. Samweli aliambiwa, “Sauli alifika Karmeli na amejijengea ukumbusho kwa ajili yake, kisha aligeuka na kuendelea chini hadi Gilgali.” Ndipo
And he rose early Samuel to meet Saul in the morning and it was told to Samuel saying he came Saul Carmel towards and there! [he was] setting up for himself a monument and he turned and he passed on and he went down Gilgal.
13 Samweli akamwendea Sauli, na Sauli akamwambia, “Umebarikiwa na BWANA! Nami nimetekeleza amri ya BWANA.”
And he came Samuel to Saul and he said to him Saul [be] blessed you by Yahweh I have carried out [the] word of Yahweh.
14 Samweli akasema, “Hicho kilio cha kondoo ni cha nini basi masikioni mwangu, na hiyo milio ya ng'ombe ninayosikia?
And he said Samuel and what? [is] [the] sound of the sheep this in ears my and [the] sound of the cattle which I [am] hearing.
15 Sauli akamjibu, “Wao wamewaleta kutoka kwa Waamaleki. Kwa sababu watu waliwaacha hai kondoo wazuri na ng'ombe, kwa ajili ya sadaka kwa BWANA Mungu wako. Zilizobaki tuliziangamiza kabisa.”
And he said Saul from [the] Amalekite[s] people brought them that it had compassion the people on [the] best of the sheep and the cattle so as to sacrifice [them] to Yahweh God your and the rest we totally destroyed.
16 Ndipo Samweli akamwambia Sauli, “Subiri nitakumbia kile ambacho BWANA amekisema kwangu usiku.” Sauli akamwambia, “Sema!”
And he said Samuel to Saul be quiet so let me tell to you [that] which he said Yahweh to me this night (and he said *QK) to him speak.
17 Samweli akasema, “Ingawa wewe ni mdogo machoni pako mwenyewe, je, hukufanywa mkuu wa kabila za Israeli? Na BWANA akakutia mafuta uwe mfalme juu ya Israeli;
And he said Samuel ¿ not though [were] small you in own eyes your [the] head of [the] tribes of Israel [are] you and he anointed you Yahweh to king over Israel.
18 BWANA alikutuma katika safari yako akisema, 'nenda na uangamize kabisa wenye dhambi, Waamaleki, na upigane dhidi yao hadi wameangamizwa.'
And he sent you Yahweh on a journey and he said go and you will totally destroy the sinners Amalek and you will wage war against it until destroy they them.
19 Kwa nini basi haukuitii sauti ya BWANA, bali badala yake ulishikilia nyara na ukafanya uovu machoni pa BWANA?”
And why? not did you listen to [the] voice of Yahweh and did you rush? to the plunder and did you do? the evil in [the] eyes of Yahweh.
20 Ndipo Sauli akamwambia Samweli, “Kweli kabisa niliitii sauti ya BWANA, Na nimeifuata njia ambayo BWANA alinituma. Nimemteka Agagi, mfalme wa Waamaleki, na kuwaangamiza kabisa Waamaleki.
And he said Saul to Samuel that I listened to [the] voice of Yahweh and I went on the journey which he sent me Yahweh and I brought Agag [the] king of Amalek and Amalek I totally destroyed.
21 Lakini watu walichukua baadhi ya nyara-kondoo na ng'ombe, na vitu vizuri vilivyokusudiwa kuangamizwa, ili wavitoe dhabihu kwa BWANA, Mungu wako, huko Gilgali.”
And it took the people from the plunder sheep and cattle [the] choicest of the object[s] for destruction to sacrifice [them] to Yahweh God your in Gilgal.
22 Samweli akajibu, “Je, BWANA hufurahia sadaka za kuteketezwa na dhabihu kama ilivyo kuitii sauti yake? Utii ni bora kuliko dhabihu, na kusikia ni bora kuliko mafuta ya beberu.
And he said Samuel ¿ [does] delight [belong] to Yahweh in burnt offerings and sacrifices like listening to [the] voice of Yahweh here! to obey more than sacrifice [is] good to pay attention more than [the] fat of rams.
23 Kwa maana uasi ni sawa na dhambi ya uchawi, na ukaidi ni sawa na uovu na udhalimu. Kwa kuwa umelikataa neno la BWANA, naye pia amekukataa usiwe mfalme.”
For [is the] sin of divination rebellion and [is] wickedness and teraphim presumption because you have rejected [the] word of Yahweh and he has rejected you from king.
24 Ndipo Sauli akamwambia Samweli, “Nimetenda dhambi; kwa maana nimevunja amri ya BWANA na maneno yako, kwa sababu niliwaogopa watu na kuitii sauti yao.
And he said Saul to Samuel I have sinned for I have transgressed [the] mouth of Yahweh and words your for I feared the people and I listened to voice their.
25 Sasa, tafadhali nisamehe dhambi yangu, na urudi nami ili nipate kumcha BWANA.”
And therefore forgive please sin my and return with me so I may bow down to Yahweh.
26 Samweli akamwambia Sauli, “Sitarudi pamoja na wewe; kwa sababu umekataa neno la BWANA, naye BWANA amekukataa usiwe mfalme juu ya Israeli.”
And he said Samuel to Saul not I will return with you for you have rejected [the] word of Yahweh and he has rejected you Yahweh from being king over Israel.
27 Samweli alipogeuka kuondoka, Sauli akashika pindo la kanzu yake, na likachanika.
And he turned round Samuel to go and he took hold on [the] skirt of robe his and it tore.
28 Samweli akamwambia, “BWANA ameuchana ufalme wa Israeli kutoka kwako leo na amempa ufalme huo jirani yako, aliye bora kuliko wewe.
And he said to him Samuel he has torn Yahweh [the] kingdom of Israel from with you this day and he will give it to neighbor your good more than you.
29 Pia, yeye ni Uwezo wa Israeli hatasema uongo wala kubadili nia yake; kwa sababu si mwanadamu, kwamba abadili nia yake.”
And also [the] eminence of Israel not he will deal falsely and not he will regret for not [is] a man he to regret.
30 Kisha Sauli akasema, “Nimetenda dhambi. Lakini tafadhali nipe heshima wakati huu mbele ya wakuu wa watu wangu na mbele ya Israeli. Urudi tena pamoja nami, kusudi niweze kumcha BWANA, Mungu wako.”
And he said I have sinned now honor me please before [the] elders of people my and before Israel and return with me and I will bow down to Yahweh God your.
31 Hivyo Samweli akamrudia tena Sauli, na Sauli akamcha BWANA.
And he turned back Samuel after Saul and he bowed down Saul to Yahweh.
32 Kisha Samweli akasema, “Mmlete hapa kwangu Agagi mfalme wa Waamaleki.” Agagi akafika kwake akiwa amefungwa minyororo na kusema, “Hakika uchungu wa kifo umepita.”
And he said Samuel bring near to me Agag [the] king of Amalek and he came to him Agag bonds and he said Agag truly it has departed [the] bitterness of death.
33 Naye Samweli akamjibu, “Jinsi upanga wako ulivyofanya wanawake wapoteze watoto, vivyo hivyo mama yako naye hatakuwa na mtoto miongoni mwa wanawake.” Kisha Samweli akamkata Agagi vipande vipande mbele za BWANA huko Gilgali.
And he said Samuel just as it has made childless women sword your so she will become childless from women mother your and he cut to pieces Samuel Agag before Yahweh in Gilgal.
34 Samweli akaenda Rama, na Sauli akapanda kwenda nyumbani kwake Gibea ya Sauli.
And he went Samuel Ramah towards and Saul he went up to house his Gibeah of Saul.
35 Samweli hakumuona tena Sauli hadi siku ya kifo chake, lakini alimwombolezea Sauli. Na BWANA alijuta kwa kumfanya Sauli awe mfalme juu ya Israeli.
And not he repeated Samuel to see Saul until [the] day of death his for he mourned Samuel concerning Saul and Yahweh he regretted that he had made king Saul over Israel.

< 1 Samweli 15 >