< 1 Samweli 11 >

1 Ndipo Nahashi Mwamoni akaenda na kupiga kambi kuzunguka Yabeshi Gileadi. Watu wote wa Yabeshi wakamwambia Nahashi, “Fanya mkataba nasi, na tutakutumikia,”
And he went up Nahash the Ammonite and he encamped on Jabesh Gilead and they said all [the] men of Jabesh to Nahash make to us a covenant and we will serve you.
2 Nahashi Mwamoni akawajibu, “Kwa sharti hili nitafanya mkataba na ninyi, kwamba wote niwang'oe macho ya kulia, na kwa kitendo hiki kilete fedheha katika Israeli yote.”
And he said to them Nahash the Ammonite by this I will make to you by gouging out of you every eye of [the] right [side] and I will make it a reproach on all Israel.
3 Basi wazee wa Yabeshi wakamjibu, “Tuache kwa siku saba, ili tuwatume wajumbe katika nchi yote ya Israeli. Ndiposa, kama hakuna mtu wa kutuokoa, tutasalimu amri kwako.”
And they said to him [the] elders of Jabesh refrain to us seven days so let us send messengers in all [the] territory of Israel and if there not [is one who] delivers us and we will come out to you.
4 Nao wajumbe wakafika Gibea, alipoishi Sauli, na wakawaeleza watu kile kilichotokea. Watu wote wakalia kwa sauti kuu.
And they came the messengers Gibeah of Saul and they spoke the words in [the] ears of the people and they lifted up all the people voice their and they wept.
5 Na Sauli alikuwa akiwafuata nyuma maksai kutoka shambani. Sauli akauliza, “Watu wamepatwa na nini hadi wanalia?” Ndipo wakamweleza Sauli kile ambacho watu wa Yabeshi walikisema.
And there! Saul [was] coming after the cattle from the field and he said Saul what? [is] to the people that they are weeping and they recounted to him [the] words of [the] men of Jabesh.
6 Sauli aliposikia kile walichosema, Roho ya Mungu ikamjia kwa nguvu, na akakasirika.
And it rushed [the] spirit of God on Saul (just as heard he *QK) the words these and it burned anger his exceedingly.
7 Akashika nira ya maksai, akawakata hao ng'ombe vipande vipande, na akavituma hivyo vipande katika nchi yote ya Israeli kwa kuwatumia wajumbe, Akasema, “Yeyote asiyejitokeza akimfuata Sauli na Samweli, hivi ndivyo ng'ombe wake watakavyofanywa.” Na hofu ya BWANA ikawaingia watu, na wakajitokeza wote kwa pamoja.
And he took a pair of ox[en] and he cut in pieces it and he sent [them] in all [the] territory of Israel by [the] hand of the messengers - saying [the one] who not he [is] coming out after Saul and after Samuel thus it will be done to ox[en] his and it fell [the] dread of Yahweh on the people and they came out like a man one.
8 Alipowahesabu hapo Beseki, watu wa Israeli walikuwa elfu mia tatu, na watu wa Yuda elfu thelathini.
And he mustered them at Bezek and they were [the] people of Israel three hundred thousand and [the] man of Judah [was] thirty thousand.
9 Wakawaambia wale wajumbe waliotumwa, “Mtawaambia watu wa Yabeshi Gileadi, 'Kesho, wakati wa jua kali, Mtaokolewa.”' Basi wale wajumbe wakaenda na kuwaambia watu wa Yabeshi, na watu wakafurahi.
And they said to the messengers who had come thus you will say! to [the] man of Jabesh Gilead tomorrow it will belong to you deliverance (like [the] heat of *QK) the sun and they went the messengers and they told to [the] men of Jabesh and they were glad.
10 Ndipo watu wa Yabeshi wakamwambia Nahashi, “Kesho tutasalimu amri kwako, na utaweza kutufanyia chochote unachoona kinakupendeza.”
And they said [the] men of Jabesh tomorrow will we go out to you and you will do to us according to all the good in eyes your.
11 Siku iliyofuata Sauli akawapanga watu katika vikosi vitatu. Wakafika katikati ya Kambi wakati wa asubuhi, wakawashambulia na kuwashinda Waamoni ilipofika mchana. Waliosalimika nao walitawanyika, kiasi kwamba hata watu wawili hawakuachwa pamoja.
And it was from [the] next day and he made Saul the people three companies and they went in [the] midst of the camp in [the] watch of the morning and they struck down Ammon until [the] heat of the day and it was those [who] remained and they were scattered and not they remained among them two together.
12 Ndipo watu wakamwambia Samweli, “Wako wapi waliosema, 'Hivi kweli Sauli atatutawala?' Walete watu hao, ili tuwauwe.”
And it said the people to Samuel who? [is] the [one who] said Saul will he reign? over us deliver up the men so we may put to death them.
13 Lakini Sauli akasema, “Hakuna atakayeuwawa siku ya leo, kwa sababu leo BWANA amemuokoa Isreli.”
And he said Saul not he will be put to death anyone on the day this for this day he has done Yahweh deliverance in Israel.
14 Kisha Samweli akawaambia watu, “Njoni, twendeni Gilgali na tuimarishe ufalme tena huko.”
And he said Samuel to the people come so let us go Gilgal so we may renew there the kingship.
15 Hivyo watu wote wakaenda Gilgali na wakamsimika Sauli kuwa mfalme mbele za BWANA huko Gilgali. Na huko walitoa sadaka za amani mbele za BWANA, na watu wote wa Israeli wakafurahi sana.
And they went all the people Gilgal and they made king there Saul before Yahweh in Gilgal and they sacrificed there sacrifices peace offerings before Yahweh and he rejoiced there Saul and all [the] men of Israel up to muchness.

< 1 Samweli 11 >