< 1 Samweli 10 >

1 Ndipo Samweli akachukua chupa ya mafuta, akayamimina juu ya kichwa cha Sauli, na akambusu. Akasema, “Je, Mungu hajakutia mafuta uwe mtawala juu ya urithi wake?
And Samuel took a vial of oil, and poured [it] on his head, and kissed him, and said to him, Has not the Lord anointed you for a ruler over his people, over Israel? and you shall rule amongst the people of the Lord, and you shall save them out of the hand of their enemies; and this [shall be] the sign to you that the Lord has anointed you for a ruler over his inheritance.
2 Utakapoondoka kwangu leo, utawaona wanaume wawili na kaburi la Raheli, katika nchi ya Benyamini hapo Selsa. Watu hao watakuambia, 'Wale punda mliokuwa mkiwatafuta wamepatikana. Sasa, Baba yako ameacha kuwatunza punda, na ana hofu juu yenu, anasema, “Nitafanya nini kuhusu mwanangu?”
[As soon] as you shall have departed this day from me, you shall find two men by the burial-place of Rachel on the mount of Benjamin, exulting greatly; and they shall say to you, The asses are found which you went to seek; and, behold, your father has given up the matter of the asses, and he is anxious for you, saying, What shall I do for my son?
3 Kisha utakwenda mbele kutoka hapo, na utafika katika mwaloni wa Tabori. Utakutana na watu watatu hapo wakienda kwa Mungu huko Betheli, mmoja akibeba wana-mbuzi watatu, mwingine akibeba mikate mitatu, na mwingine akibeba kiriba cha divai.
And you shall depart thence, and shall go beyond that as far as the oak of Thabor, and you shall find there three men going up to God to Baethel, one bearing three kids, and another bearing three vessels of bread, and another bearing a bottle of wine.
4 Watawasalimu na watawapatia mikate miwili, kutoka mikononi mwao.
And they shall ask you how you do, and shall give you two presents of bread, and you shall receive them of their hand.
5 Baada ya hayo, utafika katika mlima wa Mungu, mahali ilipo ngome ya Wafilisti. Utakapofika mjini, utakutana na kundi la manabii wakiteremka chini kutoka mahali pa juu wakiwa na kinanda, tari, kinubi na filimbi mbele yao; na watakuwa wakitabiri.
And afterward you shall go to the hill of God, where is the encampment of the Philistines; there [is] Nasib the Philistine: an it shall come to pass when you shall have entered into the city, that you shall meet a band of prophets coming down from the Bama; and before them will be lutes, and a drum, and a pipe, and a harp, and they shall prophesy.
6 Roho ya BWANA itakujaza, nawe utatabiri pamoja nao, na utabadilishwa na kuwa mtu tofauti.
And the Spirit of the Lord shall come upon you, and you shall prophesy with them, and shall be turned into another man.
7 Basi, ishara hizi zikikufikia, fanya lolote ambalo mikono yako itaona ifanye, kwa sababu Mungu yu pamoja nawe.
And it shall come to pass when these signs shall come upon you, —[then] do you whatever your hand shall find, because God [is] with you.
8 Nenda ushuke mbele yangu hadi Gilgali. Kisha nitakufuata huko nitoe dhabihu za kuteketezwa na kutoa dhabihu za amani. Nisubiri kwa muda wa siku saba hadi nije kwako na nikuoneshe unachopaswa kufanya.”
And you shall go down in front of Galgal, and behold, I come down to you to offer a whole burnt offering and peace-offerings: seven days shall you wait until I shall come to you, and I will make known to you what you shall do.
9 Sauli alipotega mgongo amuache Samweli, Mungu akampa moyo mwingine. Ndipo ishara zote hizi zikatimia siku hiyo.
And it came to pass when he turned his back to depart from Samuel, God gave him another heart; and all these signs came to pass in that day.
10 Walipofika mlimani, kundi la manabii lilikutana naye, na Roho ya Mungu ikamjilia kwa nguvu ili atabiri pamoja nao.
And he comes thence to the hill, and behold a band of prophets opposite to him; and the Spirit of God came upon him, and he prophesied in the midst of them.
11 Kila mtu aliyemfahamu kabla hajamwona akitabiri pamoja na manabii, watu waliambizana wao kwa wao:”Kitu gani kimempata mtoto wa Kishi? Hivi Sauli ni mmoja wa manabii siku hizi?”
And all that had known him before came, and saw, and behold, he [was] in the midst of the prophets: and the people said every one to his neighbour, What [is] this that has happened to the son of Kis? [is] Saul also amongst the prophets?
12 Mtu mmoja kutoka eneo hilo akajibu, “Na ni nani baba yao?” Kwa sababu ya jambo hili, ukawapo msemo, “Hivi Sauli naye ni mmoja wa manabii?”
And one of them answered and said, And who [is] his father? and therefore it became a proverb, [Is] Saul also amongst the prophets?
13 Alipomaliza kutabiri, akafika mahali pa juu.
And he ceased prophesying, and comes to the hill.
14 Ndipo baba yake mdogo na akamuuliza Sauli na mtumishi wake, “Mlienda wapi?” Naye akamjibu, “Kuwatafuta punnda; tulipoona kwamba hatuwezi kuwapata, tukaenda kwa Samweli.”
And his kinsman said to him and to his servant, Whither went you? and they said, To seek the asses; and we saw that they were lost, and we went in to Samuel.
15 Baba yake mdogo akasema, “Tafadhali niambie kile alichosema kwako Samweli,”
And his kinsman said to Saul, Tell me, I pray you, What did Samuel say to you?
16 Sauli akamjibu baba yake mdogo, “Alituambia waziwazi kwamba punda wamepatikana.” Lakini kuhusu swala la ufalme alilosema Samweli hakumwambia.
And Saul said to his kinsman, he verily told me that the asses were found. But the matter of the kingdom he told him not.
17 Basi Samweli aliwaita watu pamoja huko Mispa.
And Samuel summoned all the people before the Lord to Massephath.
18 Akwaambia watu wa Israeli, “Hivi ndivyo BWANA, Mungu wa Israeli asemavyo: 'Niliwatoa Israeli kutoka Misri, na niliwaokoa kutoka nchi ya Wamisri, na kutoka mkono wa falme zote zilizowaonea.'
And he said to the children of Israel, Thus has the Lord God of Israel spoken, saying, I brought up the children of Israel out of Egypt, and I rescued you out of the hand of Pharao king of Egypt, and out of all the kingdoms that afflicted you.
19 Lakini leo mmemkataa Mungu wenu, awaokoaye kutoka kwenye majanga na mahangaiko; na mmemwambia, ' Tuwekee mfalme juu yetu; Sasa jihudhurisheni wenyewe mbele za BWANA kwa kabila na jamaa zenu.”
And you have this day rejected God, who is himself your Deliverer out of all your evils and afflictions; and you said, Nay, but you shall set a king over us: and now stand before the Lord according to your tribes, and according to your families.
20 Kisha Samweli akawaleta kabila zote za Isareli karibu, na kulichagua kabila la Benyamini.
And Samuel brought near all the tribes of Israel, and the tribe of Benjamin is taken by lot.
21 Akawasogeza karibu kabila la Benyamini kwa kufuata jamaa zao; na jamaa ya Wamatri ikachaguliwa; na Sauli mwana wa Kishi akachaguliwa. Lakini walipokwenda kumtafuta, hakuweza kuonekana.
And he brings near the tribe of Benjamin by families, and the family of Mattari is taken by lot: and they bring near the family of Mattari, man by man, and Saul the son of Kis is taken; and he sought him, but he was not found.
22 Kisha watu walitaka kumuuliza Mungu maswali zaidi, “Bado yupo mtu mwingine ajaye?” BWANA akajibu, “Yeye mwenyewe kajificha kwenye mizigo.”
And Samuel asked yet again of the Lord, Will the man come here? and the Lord said, Behold, he is hid amongst the stuff.
23 Wakaenda mbio na kumleta Sauli kutoka humo. Aliposimama kati yao, alikuwa mrefu kuliko watu wote kuanzia mabega yake kwenda juu.
And he ran and took him thence, and he set him in the midst of the people; and he was higher than all the people by his shoulders and upwards.
24 Kisha Samweli akawaambia watu, “Je, mnamuona mtu ambaye BWANA amemchagua? Hakuna mtu kama yeye kati ya watu wote.” Watu wote wakapiga Kelele, “Mfalme na aishi”
And Samuel said to all the people, Have you seen whom the Lord has chosen to himself, that there is none like to him amongst you all? And all the people took notice, and said, Let the king live!
25 Ndipo Samweli akawaambia watu desturi na sheria za ufalme, akaziandika katika kitabu, na kuziweke mbele za BWANA. Baadaye Samweli akawaruhusu watu waondoke kila mtu aende nyumbani kwake.
And Samuel told the people the manner of the king, and wrote it in a book, and set it before the Lord: and Samuel sent away all the people, and each went to his place.
26 Sauli pia alienda nyumbani kwake huko Gibea, akiwa na baadhi ya watu wenye nguvu, wenye mioyo iliyoguswa na Mungu.
And Saul departed to his house to Gabaa; and there went with Saul mighty men whose hearts God had touched.
27 Lakini baadhi ya watu wasiofaa walisema, “Huyu mtu atatuokoaje?” Watu hawa walimdharau Sauli na hawakumletea zawadi zozote. Lakini Sauli alinyamaza kimya.
But evil men said, Who [is] this man [that] shall save us? and they despised him, and brought him no gifts.

< 1 Samweli 10 >