< 1 Wafalme 7 >

1 Ilimchukua Sulemani miaka kumi na tatu kujenga ikulu yake.
And Solomon was building his own house thirteen years, and he finished all his house.
2 Aliijenga ikulu iliyoitwa mwitu wa Lebanoni. Urefu wake ulikuwa mita 46, na upanawake ulikuwa mita 23, na kimo chake kilikuwa mita 14. Nayo ilikuwa na safu nne ya nguzo za mierezi na mithili ya mwerezi juu ya nguzo.
For he built the house of the forest of Lebanon: the length thereof was a hundred cubits, and the breadth thereof fifty cubits, and the height thereof thirty cubits, upon four rows of cedar pillars, with cedar beams upon the pillars.
3 Paa la ikulu lilikuwa la mwerezi ambalo lilikaa juu ya mihimili. Mihili hiyo ilikuwa imeshikiliwa na nguzo. Kulikuwa na mihimili arobaini na tano, ambayo ilikuwa katika safu kumi na tano.
And it was covered with cedar above upon the side-chambers, that lay on forty and five pillars, fifteen in a row.
4 Nayo mihimili ilikuwa safu tatu, na kila dirisha lilikabili dirisha lingine katika madaraja matatu.
And there were beams in three rows; and light was over against light in three ranks.
5 Milango yote na miimo ilitengenezwa kwa mraba, na madirisha yalikuwa yakikabiliana katika madaraja matatu
And all the doors with their posts were square in the frame; and light was over against light in three ranks.
6 Akatengeneza baraza lenye uerfu wa mita 23 na upana wa mita 14. Mbele yake kulikuwa na ukumbi ulioezekwa.
And he made the porch of pillars: the length thereof was fifty cubits, and the breadth thereof thirty cubits; and a porch before them; and pillars and thick beams before them.
7 Sulemani akajenga baraza yenye kiti cha enzi ambacho alitolea hukumu ya haki. Nayo ilikuwa imeezekwa kwa mwerezi kutoka sakafu moja hadi nyingine.
And he made the porch of the throne where he might judge, even the porch of judgment; and it was covered with cedar from floor to floor.
8 Nyumba ya Sulemani ambayo alikusudia kuishi, katika behewa nyingine ndani ya sehemu ya chini ya ikulu, ilitengenezwa kwa kazi hiyo hiyo. Pia alimjengea binti wa Farao nyumba kama hii, ambaye alikuwa mke wake
And his house where he might dwell, in the other court, within the porch, was of the like work. He made also a house for Pharaoh's daughter, whom Solomon had taken to wife, like unto this porch.
9 Majengo haya yalipmbwa kwa vitu vya thamaini, mawe ya thamani, yaliyochongwa na kukatwa kwa msimeno kufuata vipimo sahihi na kulainishwa pande zote. Mawe ya namna hii ndiyo yale yaliyotumika kuanzia kwenye msingi hadi juu, pia na nje hadi kwenye baraza.
All these were of costly stones, according to the measures of hewn stones, sawed with saws, within and without, even from the foundation unto the coping, and so on the outside unto the great court.
10 Msingi ulijengwa kwa mawe makubwa sana na ya thamani yenye urefu wa mita 3. 7 na mengine mita 4. 8.
And the foundation was of costly stones, even great stones, stones of ten cubits, and stones of eight cubits.
11 Kwa juu ilipambwa kwa, mawe ya thamani yaliyochongwa sawa sawa kwa msimeno na kwa mihimili ya mierezi.
And above were costly stones, after the measure of hewn stones, and cedar-wood.
12 Na behewa kubwa iliyokuwa ikizunguka ikulu ilikuwa na safu tatu za mawe yaliyokatwa na safu moja ya mihimili ya mierezi kama ilivyo kwenye baraza la ndani la hekalu la BWANA na ule ukumbi wa hekalu.
And the great court round about had three rows of hewn stone, and a row of cedar beams, like as the inner court of the house of the LORD, and the court of the porch of the house.
13 Mfalme Sulemani alituma watu kumleta Huramu kutoka Tiro.
And king Solomon sent and fetched Hiram out of Tyre.
14 Huramu alikuwa mwana wa mjane wa kabila ya Naftali; baba yake alikuwa mtu wa Tiro, mfua shaba. Huramu alikuwa mwingi wa hekima na ufahamu na stadi za kufanya kazi kubwa za shaba. Aliletwa kwa mfalme ili kufanya kazi zilizohusiana na shaba kwa mfalme.
He was the son of a widow of the tribe of Naphtali, and his father was a man of Tyre, a worker in brass; and he was filled with wisdom and understanding and skill, to work all works in brass. And he came to king Solomon, and wrought all his work.
15 Huramu alizilemba zile nguzo mbili za shaba, kila moja ilikuwa na kimo cha mita 8. 3 na mzingo wa mita 5. 5.
Thus he fashioned the two pillars of brass, of eighteen cubits high each; and a line of twelve cubits did compass it about; and so the other pillar.
16 Akatengeneza taji mbili za shaba za kuwekwa juu ya zile nguzo. Kimo cha kila taji ilikuwa mita 2. 3.
And he made two capitals of molten brass, to set upon the tops of the pillars; the height of the one capital was five cubits, and the height of the other capital was five cubits.
17 Kulikuwa na nyavu za kuwa kama kazi ya kusuka, na masongo ya mikufu, kwa ajili ya kuvipamba vile vichwa vya nguzo, nayo yailikuwa saba kwa kila kichwa.
He also made nets of checker-work, and wreaths of chain-work, for the capitals which were upon the top of the pillars: seven for the one capital, and seven for the other capital.
18 Kwa hiyo Huramu akafanya safu mbili za komamanga kuzunguka vile vichwa vya nguzo ili kuvipamba vile vichwa.
And he made the pillars; and there were two rows round about upon the one network, to cover the capitals that were upon the top of the pomegranates; and so did he for the other capital.
19 Zile taji kwenye vile vichwa vya nguzo za ukumbi zilikuwa zimepambwa kwa maua, yenye vimo vya mita 1. 8.
And the capitals that were upon the top of the pillars in the porch were of lily-work, four cubits.
20 Hizo taji kwenye hizo nguzo mbili kwenye vichwa vyake, karibu yake kulikuwa na makomamanga mia mbili yote yakiwa kwenye safu.
And there were capitals above also upon the two pillars, close by the belly which was beside the network; and the pomegranates were two hundred, in rows round about upon each capital.
21 Alisimamisha nguzo kwenye ukumbi wa hekalu. Ile nguzo ya kuume akaipa jina la Yakini, na ile ya kushoto akaipa jina la Boazi.
And he set up the pillars at the porch of the temple; and he set up the right pillar, and called the name thereof Jachin; and he set up the left pillar, and called the name thereof Boaz.
22 Na juu ya zile nguzo kulikuwa na mapambo kama maua. Hivyo ndivyo zile nguzo zilivyotengenezwa.
And upon the top of the pillars was lily-work; so was the work of the pillars finished.
23 Tena akafanya bahari ya kusubu ya, yenye mita 2. 3 kutoka ukingo hadi ukingo, kimo chake kilikuwa mita 4. 6, mziingo wake ulikuwa mita 13. 7.
And he made the molten sea of ten cubits from brim to brim, round in compass, and the height thereof was five cubits; and a line of thirty cubits did compass it round about.
24 Na chini ya ile bahari kulikuwa na vibuyu vilivyoizunguka, vilikuwa vibuyu kumi na nane katika kila mita, vilivyowekwa katika kila hicho kipande wakati bahari inapokuwa kalibu.
And under the brim of it round about there were knops which did compass it, for ten cubits, compassing the sea round about; the knops were in two rows, cast when it was cast.
25 Bahari ikakaa juu ya makisai kumi na mbili, tatu, zilitazama kaskazini, tatu zikitazama magharibi, tatu zikitazama kusini na tatu zikitazama kaskazini. Ile bahari iliwekwa juu yao, na pande zao zote za nyuma zilikuwa ndani.
It stood upon twelve oxen, three looking toward the north, and three looking toward the west, and three looking toward the south, and three looking toward the east; and the sea was set upon them above, and all their hinder parts were inward.
26 Bahari ilikuwa nene kama upana wa mkono, na ukingo wake ulikuwakama ukingo wa kikombe, kama ua la yungi huingia bathi elfu mbili za maji.
And it was a hand-breadth thick; and the brim thereof was wrought like the brim of a cup, like the flower of a lily; it held two thousand baths.
27 Huramu akatengeneza makalio kumi ya shaba. Kila kalio lilkuwa na urefu wa mita 1. 8, upana wa mita 1. 8, na kimo cha mita 1. 3.
And he made the ten bases of brass; four cubits was the length of one base, and four cubits the breadth thereof, and three cubits the height of it.
28 Hivi ndivyo kazi za makalio zilivyofanywa. Yalikuwa na papi ambazo zilikaa kati kati ya vipandio,
And the work of the bases was on this manner: they had borders; and there were borders between the stays;
29 na juu ya papi na vipandio kulikuwa na simba, makisai, na makerubi. Chini na juu simba kulikuwa na masongo ya kazi ya kufuliwa.
and on the borders that were between the stays were lions, oxen, and cherubim; and upon the stays it was in like manner above; and beneath the lions and oxen were wreaths of hanging work.
30 Kila kalio lilikuwa na magurudumu ya shaba na vipini, na pande zake nne na miguu yake minne ilikuwa na mataruma chini ya birika. Chini ya birika yalikuweko mataruma ya kusubu yenye masongo katika kila upande.
And every base had four brazen wheels, and axles of brass; and the four feet thereof had undersetters; beneath the laver were the undersetters molten, with wreaths at the side of each.
31 Na kinywa chake kilikuwa cha kuviringana, chenye upana wa sentimita araobaini na sita, na ile taji ilikuwa na sentimita ishirini na tatu. Na kinywa chake kilikuwa na nakshi, na papi zake zilikuwa za mraba, na wala siyo za mvringo.
And the mouth of it within the crown and above was a cubit high; and the mouth thereof was round after the work of a pedestal, a cubit and a half; and also upon the mouth of it were gravings; and their borders were foursquare, not round.
32 Yale magurudumu mawili yalikuwa chini ya papi, na mikono ya magurudumu yalikuwa ndani ya makalio. Kimo cha yale magurudumu kilikuwa sentimeta sitini na tisa.
And the four wheels were underneath the borders; and the axletrees of the wheels were in the base; and the height of a wheel was a cubit and half a cubit.
33 Yale magurudumu yalikuwa kama ya gari. Mikono yake, na maduara, matindi yake, na vipande vya ndani vyote vilikuwa vya kusubu.
And the work of the wheels was like the work of a chariot wheel; their axletrees, and their felloes, and their spokes, and their naves, were all molten.
34 Kulikuwa na mataruma manne katika pande zake nne za makalio, yaliyokuwa yameshikamanishwa na kalio lenyewe.
And there were four undersetters at the four corners of each base; the undersetters thereof were of one piece with the base itself.
35 Juu ya makalio kulikuwa na duara yenye kina cha sentimita ishirini na tatu, na juu ya makalio mashikio yake na papi zake zikiwa zimeshikamanishwa.
And in the top of the base was there a round compass of half a cubit high; and on the top of the base the stays thereof and the borders thereof were of one piece therewith.
36 Juu ya mabamba na papi zake Huramu akachora makerubi, simba, na mitende ambayo ilifunika nafasi ya juu, nayo ilikuwa imezungukwa na masongo.
And on the plates of the stays thereof, and on the borders thereof, he graved cherubim, lions, and palm-trees, according to the space of each, with wreaths round about.
37 Alitengeneza makalio kumi kwa jinsi hii. Yote yalikuwa yametengenezwa kwa kufanana, na yalikuwa ya vipimo sawa, na sura inayofanana.
After this manner he made the ten bases; all of them had one casting, one measure, and one form.
38 Huramu akatengeneza birika kumi za shaba. Birika moja liliweza kubeba bathi arobaini za maji. Kila birika lilikuwa mita 1. 8 toka birika moja hadi jingine na kulikuwa na birika moja katika kila kalio kati ya yale kumi.
And he made ten lavers of brass: one laver contained forty baths; and every laver was four cubits; and upon every one of the ten bases one laver.
39 Alitengeneza makalio tano upande wa kusini unaoelekea upande wa hekalu. Akatengeneza bahari katika upande wa mashariki, ukielekea upande wa kusini wa hekalu.
And he set the bases, five on the right side of the house, and five on the left side of the house; and he set the sea on the right side of the house eastward, toward the south.
40 Huramu akatengeneza birika na koleo na besini la kunyunyizia. Kisha akamaliza kazi yote aliyofanya kwa mfalme Sulemani katika hekalu la BWANA:
And Hiram made the pots, and the shovels, and the basins. So Hiram made an end of doing all the work that he wrought for king Solomon in the house of the LORD:
41 Zile nguzo mbili, na lile besini lakawa kama taji ambalo lilikuwa juu ya zile nguzo, na nyavu mbili za mapambo za kufunika zile besini mbili za kuwa kama taji zilizokuwa juu ya nguzo.
the two pillars, and the two bowls of the capitals that were on the top of the pillars; and the two networks to cover the two bowls of the capitals that were on the top of the pillars;
42 Kisha akatengeneza makomamanga mia nne kwa ajili ya zile nyavu mbili za mapambo: safu mbili za makomamamanga kwa kila kazi ya nyavu kwa ajili ya kufunikia zile besini mbili kama taji iliyo juu ya nguzo,
and the four hundred pomegranates for the two networks, two rows of pomegranates for each network, to cover the two bowls of the capitals that were upon the top of the pillars;
43 yale makalio kumi, na birika kumi kwenye makalio.
and the ten bases, and the ten lavers on the bases;
44 Akatengeneza bahari na makisai kumi chini yake;
and the one sea, and the twelve oxen under the sea;
45 na masufuria, koleo, birika na vyombo vingine vyote. Huramu akivitengeneza kwa shaba iliyosuguliwa, kwa ajili ya mfalme Sulemani, na kawa ajili ya hekalu la BWANA.
and the pots, and the shovels, and the basins; even all these vessels, which Hiram made for king Solomon, in the house of the LORD, were of burnished brass.
46 Mfalme alivisubu katika uwanda wa Yorodani, katika udongo mfinyanzi kati ya Sukoti na Zarethani.
In the plain of the Jordan did the king cast them, in the clay ground between Succoth and Zarethan.
47 Sulemani hakuvipima vyombo vyote kwa sababu vilikuwa vingi mno kuvipima, na kwa sababu uzito wa shaba ulikuwa hauwezi kupimwa.
And Solomon left all the vessels unweighed, because they were exceeding many; the weight of the brass could not be found out.
48 Sulemani akatengeneza mapambo yote yaliyokuwa kwenye hekalu la BWANA kwa kutumia dhahabu: Ile madhabahu ya dhahabu na ile meza ambayo iliwekwa mikate ya wonyesho.
And Solomon made all the vessels that were in the house of the LORD: the golden altar, and the table whereupon the showbread was, of gold;
49 Vile vinara vya dhahabu, ambavyo vitano vilikuwa upande wa kulia na vitano mkono wa kushoto, mbele ya chumba cha ndani, vilikuwa vya dhahabu safi, na maua, na taa na koleo zilikuwa za dhahabu.
and the candlesticks, five on the right side, and five on the left, before the Sanctuary, of pure gold; and the flowers, and the lamps, and the tongs, of gold;
50 Vile vikombe, na makasi, mabakuri, na vijiko, na vyetezo vyote vilikuwa vimetengenezwa kwa dhahabu safi. na bawaba za dhahabu za milango ya ndani, ambazoo ndio mahali patakatifu sana, na milango ya ukumbi mkubwa, vyote vilitengenezwa kwa dhahabu.
and the cups, and the snuffers, and the basins, and the pans, and the fire-pans, of pure gold; and the hinges, both for the doors of the inner house, the most holy place, and for the doors of the house, that is, of the temple, of gold.
51 Kwa njia hii, kazi yote ambayo mfalme Sulemani alifanya kwa ajili ya hekalu ilimalizika. Kwa Sulemani akaviingiza ndani yake vitu vile vilivyokuwa vimewekwa wakfu na Daudi, baba yake, na fedha na dhahabu, na mapambo, na vile vya ndani ya hazina ya BWANA.
Thus all the work that king Solomon wrought in the house of the LORD was finished. And Solomon brought in the things which David his father had dedicated, the silver, and the gold, and the vessels, and put them in the treasuries of the house of the LORD.

< 1 Wafalme 7 >