< 1 Wafalme 16 >

1 Neno la BWANA lilimjia Yehu mwana wa Hanani kinyume cha Baasha, likisema,
Wtedy słowo PANA doszło do Jehu, syna Chananiego, przeciw Baszy:
2 Ingawa Nilikuinua kutoka kwenye mavumbi na kukufanya kuwa kiongozi wa watu wangu Israeli, Lakini umetembea katika njia za Yeroboamu na umewafanya watu wangu Israeli kufanya dhambi, ili kunikasirisha dhidi ya dhambi zao.
Ponieważ wywyższyłem cię z prochu i ustanowiłem cię wodzem nad swoim ludem Izraelem, a ty poszedłeś drogą Jeroboama i skłoniłeś do grzechu mój lud, Izraela, aby mnie pobudzić do gniewu jego grzechami;
3 Tazama, Nitamfagia kabisa Baasha na familia yake na nitaifanya familia yako kama familia ya Yeroboamu mwana wa Nebati.
Oto zgładzę potomstwo Baszy i potomstwo jego domu i postąpię z twoim domem jak z domem Jeroboama, syna Nebata.
4 Mbwa watamla yeyote ambaye anatoka kwa Baasha wanaofia mjini, na ndege wa angani watamla yeyote anayaefia shambani.”
Tego, kto [z rodu] Baszy umrze w mieście, zjedzą psy, a tego, kto umrze na polu, zjedzą powietrzne ptaki.
5 Lakini kwa mambo mengine yanayohusiana na Baasha, aliyofanya, na uwezo wake, je, hayakuandikwa katika kitabu cha matukio ya wafalme wa Israeli?
A pozostałe dzieje Baszy i to, co czynił, i jego potęga, czyż nie są zapisane w kronikach królów Izraela?
6 Baasha akalala na mababu zake na akazikwa Tirza, na Ela mwanae akawa mfalme mahali pake.
Potem Basza zasnął ze swoimi ojcami i został pogrzebany w Tirsie, a jego syn Ela królował w jego miejsce.
7 Kwa kupitia nabii Yehu mwana wa Hanani neno la BWANA likaja kinyume na Baasha na familia yake, wote kwa sababu ya maovu yote aliyofanya machoni pa BWANA, akamghadhabisha kwa kazi ya mikono yake, kama familia ya Yeroboamu, na kwa sababu alikuwa ameiua familia yote ya Yeroboamu.
Ponownie przez proroka Jehu, syna Chananiego, doszło słowo PANA przeciw Baszy i przeciw jego domowi za całe zło, które czynił w oczach PANA, pobudzając go do gniewu czynami swoich rąk, stając się podobnym do domu Jeroboama, i za to, że go zabił.
8 Katika mwaka wa kumi na sita wa Asa mfalme wa Yuda, Ela mwana wa Baasha akaanza kutawala juu ya Israeli kule Tirza; akatawala kwa miaka miwili.
W dwudziestym szóstym roku Asy, króla Judy, nad Izraelem w Tirsie zaczął królować Ela, syn Baszy, i [królował] dwa lata.
9 Mtumishi wake Zimri, mkuu wa nusu ya magari yake akatengeneza hila dhidi yake. Wakati huo Ela alikuwa Tirza, akinywa na kulewa kwenye nyumba ya Arza, ambaye alikuwa mkuu wa watumishi wa nyumbani huko Tirza.
A jego sługa Zimri, dowódca połowy rydwanów, uknuł spisek przeciw niemu, gdy w Tirsie Ela oddawał się pijaństwu w domu Arsy, szafarza domu [królewskiego] w Tirsie.
10 Zimri akaiingia ndani, akamshambulia na kumwua, katika mwaka wa ishirini na saba wa Asa mfalme wa Yuda, naye akawa mfalme mahali pake.
Zimri wszedł tam, uderzył go i zabił – w dwudziestym siódmym roku Asy, króla Judy, i królował w jego miejsce.
11 Zimri alipoaanza kutawala, mara tu baada ya kukaa kwenye kiti cha enzi, akawaua wanafamilia wote wa Baasha. Hakumwacha mtoto hata mmoja wa kiume, hakuna hata wa ndugu yake wala wa rafiki zake.
A gdy tylko zaczął królować i zasiadł na swoim tronie, wymordował cały dom Baszy. Nie pozostawił z niego nikogo – ani z jego krewnych, ani przyjaciół – aż do najmniejszego szczenięcia.
12 Kwa hiyo Zimri aliingamiza familia yote ya Baasha, kama alivyokuwa ameambiwa kwa neno la BWANA, ambalo lilinenwa kinyume na Baasha na nabii Yehu,
W ten sposób Zimri wytracił cały dom Baszy zgodnie ze słowem PANA, które wypowiedział przeciw Baszy przez proroka Jehu;
13 kwa dhambi zote za Baasha na za Ela mwanae ambazo walizifanya, ambazo kwazo waliisababisha Israeli kufanya dhambi, kiasi c ha kumghadhabisha BWANA, Mungu wa Israeli, kuzikasilikia sanamu zao.
Z powodu wszystkich grzechów Baszy i grzechów jego syna Eli, które popełnili i którymi doprowadzili Izraela do grzechu, pobudzając PANA, Boga Izraela, do gniewu swymi marnościami.
14 Kwa mambo mengine yanayohusiana na Ela, yote ambayo alifanya, je hayajaandikwa kwenye kitabu cha matukio ya wafalme wa Israeli?
A pozostałe dzieje Eli i wszystko, co czynił, czyż nie są zapisane w kronikach królów Izraela?
15 Katika mwaka wa ishirini na saba wa Asa mfalme wa Yuda, Zimri alitawala kwa siku saba tu kule Tirza. Jeshi likafanya kambi kule Gibethoni, ambao ni mji wa Wafilisti.
W dwudziestym siódmym roku Asy, króla Judy, Zimri królował siedem dni w Tirsie. Lud oblegał wtedy Gibbeton, który należy do Filistynów.
16 Lile jeshi lililokuwa limeweka kambi kule lilisikika lilksema, “Zimri amepanga njama na amemwua mfalme.” Kwa hiyo siku hiyo hapo kambini, Israeli yote ikamtangaza Omri, mkuu wa jeshi, kuwa mfalme wa Israeli.
A gdy lud oblegający [miasto] usłyszał wieść: Zimri uknuł spisek i zabił króla, wtedy cały Izrael w tym samym dniu w obozie ustanowił królem Omriego, który był dowódcą wojska Izraela.
17 Omri akapanda kutoka Gibethoni na Israeli yote pamoja naye, nao wakauhusuru Tirza.
Wtedy Omri wyruszył spod Gibbeton wraz z całym Izraelem i oblegli Tirsę.
18 Kwa hiyoZimri alipoona kuwa mji umetekwa, akaingia kwenye ngome na akaivamia ikulu ya mfalme na kulichoma moto jengo lote pamoja na yeye; kwa hiyo akafa kwa moto.
A gdy Zimri zobaczył, że miasto zostało zdobyte, wszedł do pałacu domu królewskiego i podpalił nad sobą dom królewski, i umarł.
19 Hii ilikuwa ni kwa sababu ya dhambi alizofanya kwa kufanya maovu mbele ya macho ya BWANA, kwa kutembea katika njia ya Yeroboamu na katika dhambi ambazo alifanya, kiasi cha kuifanya Israeli wafanye dhambi.
[Stało się tak] z powodu jego grzechów, których się dopuścił, czyniąc to, co złe w oczach PANA, idąc drogą Jeroboama i w jego grzechu – którego się dopuszczał i do którego skłonił Izraela.
20 Pia kwa mambo mengiine yanayomhusu Zimri, na fitina yake aliyofanya, je, hayakuandikwa kwenye kitabu cha matukio ya wafalme wa Israeli?
A pozostałe dzieje Zimriego i spisek, który uknuł, czyż nie są zapisane w kronikach królów Izraela?
21 Sasa watu wa Israeli walikuwa wamegawanyika katika makundi mawili. Nusu ya watu walimfuata Tibni mwana wa Ginathi, wakamfanya kuwa mfalme, na Nusu walimfufata Omri.
Wtedy lud Izraela podzielił się na dwie części: połowa ludu szła za Tibnim, synem Ginata, aby go obwołać królem, a połowa szła za Omrim.
22 Lakini watu waliomfuata Omri walikuwa na nguvu kuliko wale waliomfuata Tibni mwana wa Ginathi. Kwa hiyo Tibni akafa, na Omri akawa mfalme.
Lecz lud, który był za Omrim, przemógł lud, który był za Tibnim, synem Ginata. I umarł Tibni, a królował Omri.
23 Omri alianza kutawala juu ya Israeli katika mwaka wa thelathini na moja wa Asa mfalme wa Yuda, naye akatawala miaka kumi na miwili. Alitawala akiwa Tirza kwa miaka sita.
W trzydziestym pierwszym roku Asy, króla Judy, nad Izraelem zaczął królować Omri [i panował] dwanaście lat. W Tirsie królował sześć lat.
24 Akakinunua kilima cha Samaria kutoka kwa Shemeri kwa kilo 68 za fedha. Akajenga mji juu ya mlima na ule mji akauita Samaria, kwa sababu ya jina la Shemeri, mmiliki wa awali wa kile kilima.
I kupił wzgórze Samarii od Szemera za dwa talenty srebra, i pobudował na tym wzgórzu, a miasto, które zbudował, nazwał Samarią, od imienia właściciela wzgórza, Szemera.
25 Omri akafanya maovu mbele ya BWANA na akafanya yaliyo maovu zaidi kuliko wale waliokuwa kabla yake.
Lecz Omri czynił to, co złe w oczach PANA, i dopuszczał się gorszych rzeczy niż wszyscy, którzy [byli] przed nim.
26 Kwa kuwa alitembea katika njia zote za Yeroboamu mwana wa Nebati na katika dhambi zake ambazo kwa hizo aliwaongoza Waisraeli kufanya dhambi, ili kumkasirisha BWANA, Mungu wa Israeli, ili kuwa na hasira juu ya sanamu zao za ubatili.
Chodził bowiem wszystkimi drogami Jeroboama, syna Nebata, i w jego grzechu, do którego przywiódł Izraela, pobudzając PANA, Boga Izraela, do gniewu swymi marnościami.
27 Kwa mambo mengine yanayomhusu Omri ambayo alfanya, na nguvu zake alizoonyesha, je, hayakuandikwa katika kitabu cha matukio ya wafalme wa Israeli?
A pozostałe dzieje Omriego, których dokonał, i jego potęga, którą pokazywał, czyż nie są zapisane w kronikach królów Izraela?
28 Kwa hiyo Omri akalala na mababu zake na akazikwa Samaria na Ahabu mwanae akawa mfalme mahali pake.
I Omri zasnął ze swoimi ojcami, i został pogrzebany w Samarii. A jego syn Achab królował w jego miejsce.
29 Katika mwaka wa thelathiini na nane wa Asa mfalme wa Yuda, Ahabu mwana wa Omri akaanza kutawala juu ya Israeli. Ahabu mwana wa Omri akatawala Israeli kule Samaria kwa miaka ishirini na mbili.
W trzydziestym ósmym roku Asy, króla Judy, nad Izraelem zaczął królować Achab, syn Omriego. Achab, syn Omriego, królował nad Izraelem w Samarii dwadzieścia dwa lata.
30 Ahabu mwana wa Omri akafanya yaliyo maovu mbele ya BWANA, zaidi ya wote waliokuwa kabla yake.
I Achab, syn Omriego, czynił to, co złe w oczach PANA, bardziej niż wszyscy, którzy byli przed nim.
31 Ikawa kidogo tu Ahabu ayaendee makosa ya Yeroboamu mwana wa Nebati, kwa hiyo akamwoa Yezebeli binti wa Ethibaali, mfalme wa Wasidoni; akaenda akamwabudu baali na akamsujudia.
A jakby nie wystarczyło mu popełnianie grzechów Jeroboama, syna Nebata, to jeszcze pojął za żonę Jezabel, córkę Etbaala, króla Sydończyków, i zaczął służyć Baalowi i oddawać mu pokłon.
32 Akamjengea madhabahu Baali, ambayo alikuwa ameijenga kule Samaria.
I wzniósł ołtarz dla Baala w domu Baala, który zbudował w Samarii.
33 Ahabu akatengeneza Ashera. Ahabu akafanya maovu zaidi kumghadhabisha BWANA, Mungu wa Isareli, akamkasirisha kuliko wafalme wote wa Israeli waliokuwa kabla yake.
Achab zasadził też gaj. Achab czynił więcej, by pobudzać PANA, Boga Izraela, do gniewu niż wszyscy królowie Izraela, którzy byli przed nim.
34 Katika siku zake Hieli Mbetheli aliijenga tena Yeriko. Akaijenga misingi ya mji kwa kufiwa na Abiramu mzaliwa wake wa kwanza, naye akayajenga malango ya mji kwa kufiwa na mwanae mdogo Segebu, na walifanya hivi kwa sababu walitii neno la BWANA, ambalo alikuwa amelinena kwa kinywa cha Joshua mwana wa Nuni.
Za jego czasów Chiel z Betel odbudował Jerycho. Założył fundamenty na Abiramie, swoim pierworodnym, a na Segubie, swoim najmłodszym [synu], postawił jego bramy – według słowa PANA, które wypowiedział przez Jozuego, syna Nuna.

< 1 Wafalme 16 >