< 1 Wafalme 14 >

1 Wakati huo Abiya mwana wa Yeroboamu akawa mgonjwa sana.
At that time Abijah son of Jeroboam became very sick.
2 Yeroboamu akamwambia mke wake, “amka ujibadilishe, ili wasikutambue kuwa wewe ndiye mke wangu, na uende Shilo, kwa sababu nabii Ahiya yuko huko, yeye ndiye aliyeninea mimi kuwa nitakuwa mfalme juu ya watu hawa.
Jeroboam said to his wife, “Please arise and disguise yourself, so you will not be recognized as my wife, and go to Shiloh, because Ahijah the prophet is there; he is the one who spoke about me, saying that I would become king over these people.
3 Uchukue mikate kumi, na kaki na mtungi wa asali, na uende kwa Ahiya. Naye atakuambia kitakachotokea kwa mtoto.”
Take with you ten loaves, some cakes, and a jar of honey, and go to Ahijah. He will tell you what will happen to the child.”
4 Mke wa Yeroboamu akafanya hivyo; akaenda Shilo mpaka kwenye nyumba ya Ahiya. Wakati huo Ahiya alikuwa hawezi kuona, kwa kuwa macho yake yalikuwa yameishiwa nguvu kwa sababu ya umri wake.
Jeroboam's wife did so; she left and went to Shiloh and came to the house of Ahijah. Now Ahijah could not see; he lost his sight because of old age.
5 BWANA akamwambia Ahiya, “Tazama mke wa Ahiya anakuja kutafuta kutaka ushauri toka kwako kuhusiana na mwanae, kwa kuwa ni mgonjwa. Mwambie hivi na hivi, kwa sababu atakapofika atajifanya kuwa ni mwanamke mwingine.”
Yahweh said to Ahijah, “Look, the wife of Jeroboam is coming to seek advice from you regarding her son, for he is sick. Say such and such to her, because when she comes, she will act as if she were some other woman.”
6 Naye Ahiya aliposikia sauti za miguu yake alipokuwa akiukaribia mlango, akasema, “karibu, mke wa Yeroboamu. Kwa nini unajifanya kuwa mtu mwingine? Nimetumwa kwako nikiwa na habaari mbaya.
When Ahijah heard the sound of her feet as she came in at the door, he said, “Come in, wife of Jeroboam. Why do you pretend to be someone you are not? I have been sent to you with bad news.
7 Nenda ukamwambia Yeroboamu kwamba BWANA, Mungu wa Israeli, anasema, 'Nilikuinua kutoka kati ya watu na kukufanya uwe kiongozi wa watu wangu Israeli.
Go, tell Jeroboam that Yahweh, the God of Israel, says, 'I raised you from among the people to make you the leader over my people Israel.
8 Niliugawa ufalme kutoka kwa Daudi na kukupa wewe, lakini bado hutaki kuwa kama mtumishi wangu Daudi, ambaye alizishika amri zangu na kunifuata kwa moyo wake wote, na kufanya kilichokuwa sawa mbele ya macho yangu.
I tore the kingdom away from the family of David and gave it to you, yet you have not been like my servant David, who kept my commandments and followed me with all his heart, to do only what was right in my eyes.
9 Badala yake, umefanya maovu, zaidi ya wote waliokutangulia. Umetengeneza miungu mingine, na umetengeneza sanamu za kuyeyushwa ili kunikasirisha na kunitupa nyuma yako.
Instead, you have done evil, more than all who were before you. You have made other gods, and you have cast metal images to provoke me to anger, and have thrust me behind your back.
10 Kwa hiyo, tazama, Nitaleta majanga kwenye familia yako; Nitawatupilia mbali watoto wako wote wa kiume katika Israeli, kama ni mtumwa au ni huru, na nitaiondoa familia yako, kama mtu anayechoma mavi mpaka yaishe.
Therefore, look, I will bring disaster on your family; I will cut off from you every male child in Israel, whether slave or free, and will completely remove your family, like someone who burns up dung until it is gone.
11 Yeyote ambaye ni mwanafamilia yako atakayefia mjini ataliwa na mbwa, na yeyote atakayefia shamabani ataliwa na ndege wa angani, kwa kuwa Mimi BWANA, nimesema;
Anyone who belongs to your family who dies in the city will be eaten by dogs, and anyone who dies in the field will be eaten by the birds of the heavens, for I, Yahweh, have said it.'
12 Kwa hiyo inuka wewe mke wa Yeroboamu, na uende nyumbani kwako; na mguu wako utakapokanyaga mjini, yule mtoto wa Abiya atakufa.
So arise, wife of Jeroboam, and go back to your home; when your feet enter the city, the child Abijah will die.
13 Na Israeli yote itamwombolezea na kumzika. Ni yeye pekee katika familia ya Abiya atakayepelekwa makaburini, kwa sababu ni yeye pekee yake kutoka kwenye nyumba ya Abiya, ambaye BWANA, Mungu wa Israeli alimwona kuwa ni mwema.
All Israel will mourn for him and bury him. He is the only one from Jeroboam's family who will go into a grave, because only in him, out of Jeroboam's house, was anything good found in the sight of Yahweh, the God of Israel.
14 Pia BWANA atainua mfalme katika Israeli ambaye ataifutilia mbali familia ya Yeroboamu katika siku hiyo. Leo ndiyo siku hiyo, sasa hivi.
Also, Yahweh will raise up a king of Israel who will cut off the family of Jeroboam on that day. Today is that day, right now.
15 Kwa kuwa BWANA ataishambulia Israeli kama vile majani yanavyotikiswa majini, na ataing'oa Israeli katika nchi hii njema ambayo aliwpa mababu. Atawatawanya hata ng'ambo ya Mto Frati, kwa sababu wamefanya nguzo za Ashera kumkasirisha BWANA.
For Yahweh will attack Israel as a reed is shaken in the water, and he will root up Israel out of this good land that he gave to their ancestors. He will scatter them beyond the Euphrates River, because they have made their Asherah poles and provoked Yahweh to anger.
16 Ataiacha Israeli kwa sababu ya dhambi ya Yeroboamu, dhambi ambazo ametenda, na kwa hizo ameifanya Israeli kufanya dhambi.
He will give Israel up because of the sins of Jeroboam, the sins that he has committed, and through which he has led Israel to sin.”
17 Kwa hiyo mke wa Yeroboamu akainuka na akaondoka na akaenda mpaka Tirza. Naye alipofika kizingitini kwa nyumba yake, yule mtoto akafa.
So Jeroboam's wife arose and left, and came to Tirzah. As she came to the threshold of her house, the child died.
18 Isareli wote wakamzika na kumwombolezea, kama vile alivyokuwa ameambiwa kwa neno la BWANA ambalo amelisema kupitia mtumishi wake nabii Ahiya.
All Israel buried him and mourned for him, just as it was told to them by the word of Yahweh which he had spoken by his servant Ahijah the prophet.
19 Na kwa mambo mengine yanayOmhusu Yeroboamu, jinsi alivyopigana vita na jinsi alivyotawala, tazama yameandikwa katika kitabu cha matukio ya wafalme wa Israeli.
As for the other matters concerning Jeroboam, how he waged war and how he reigned, see, they are written in the book of the events of the kings of Israel.
20 Yeroboamu alitawala kwa miaka ishirini na mbili naye akalala na babu zake, na Nadabu mwanawe akawa mfalme mahali pake.
Jeroboam reigned twenty-two years and then slept with his ancestors, and Nadab his son became king in his place.
21 Sasa Rehoboamu mwana wa Sulemani alikuwa mtawala wa Yuda. Rehoboamu alikuwa na umri wa miaka arobaini na moja alipokuwa mfalme, na akatawala kwa miaka kumi na saba kule Yerusalemu, mji ambao BWANA alikuwa ameuchagua kati ya makabila yote ya Israeli ili aweke jina lake kule. Jina la mama yake alikuwa Naama Mwamori.
Now Rehoboam son of Solomon was reigning in Judah. Rehoboam was forty-one years old when he became king, and he reigned seventeen years in Jerusalem, the city that Yahweh had chosen out of all the tribes of Israel in which to put his name. His mother's name was Naamah the Ammonite woman.
22 Yuda ikafanya yaliyo maovu mbele ya macho ya BWANA; wakamtia wivu kwa makosa yao, zaidi ya yote ambayo baba zao walikuwa wamefanya
Judah did what was evil in the sight of Yahweh; they provoked him to jealousy with the sins that they committed, more than everything that their fathers had done.
23 Kwa kuwa walijijengea wenyewe mahali pa juu, nguzo za mawe, na nguzo za Ashera katika kila mahali pa juu na katika kila mti wenye majani mabichi.
For they also built for themselves high places, stone pillars, and Asherah poles on every high hill and under every green tree.
24 Pia kulikuwepo na ukahaba wa kipagani katika nchi. Walifanya machukizo yaleyale kama wa mataifa yale ambayo BWANA alikuwa amewafukuza kutoka kwa watu wa Israeli.
There were also cultic prostitutes in the land. They did the same despicable practices as the nations that Yahweh had driven out before the people of Israel.
25 Ilitokea wakati wa mwaka wa tano wa mfalme Rehoboamu wakati Shishaki akiwa mfalme wa Misri, akaja kinyume na Yerusalemu.
It happened in the fifth year of King Rehoboam that Shishak king of Egypt came up against Jerusalem.
26 Akaichukua hazina iliyokuwa kwenye nyumba ya BWANA, na ile hazina iliyokuwa kwenye nyumba ya Mfalme. Akachukua kila kitu; Pia alizichukua zile ngao za dhahabu ambazo Sulemani alikuwa ametengeneza.
He took away the treasures in the house of Yahweh, and the treasures in the king's house. He took everything away; he also took all the shields of gold that Solomon had made.
27 Mfalme Rehoboamu akatengeneza ngao za shaba mahali pake na akazikabidhi kwa wakuu wa walinzi, ambao walilinda malango ya kuingia kwa mfalme.
King Rehoboam made shields of bronze in their place and entrusted them into the hands of the commanders of the guard, who guarded the doors to the king's house.
28 Na ikawa kila mfalme alipoingia kwenye nyumba ya BWANA, wale walinzi walizibeba na baadaye walizirudisha katika chumba cha walinzi.
It happened that whenever the king entered the house of Yahweh, the guards would carry them; then they would bring them back into the guardhouse.
29 Lakini katika mambo mengine kuhusiana na Rehoboamu, na yote yale aliyofanya, je, hayakuandikwa kwenye kitabu cha matukio ya wafalme wa Yuda?
As for the other matters concerning Rehoboam, and all that he did, are they not written in the book of the events of the kings of Judah?
30 Kulikuwa na mapigano yasiyokoma kati ya nyumba ya Rehoboamu na nyumba ya Yeroboamu.
There was constant warfare between Rehoboam and Jeroboam.
31 Kwa hiyo Rehoboamu akalala na mababu zake naye akazikwa pamoja nao katika mji wa Daudi Jina la mama yake alikuwa Naama Mwamori. Abiya mwanawe akawa mfalme mahali pake
So Rehoboam slept with his ancestors and was buried with them in the city of David. His mother's name was Naamah the Ammonite woman. Abijah his son became king in his place.

< 1 Wafalme 14 >