< 1 Wafalme 13 >

1 Mtu wa Mungu alikuja tokea Yuda kwa neno la BWANA kule Betheli. Naye Yeroboamu alikuwa amesimama karibu na madhabahu ili kufukiza uvumba.
Look, there came a man of God out of Judah by the word of Jehovah to Beth El: and Jeroboam was standing by the altar to burn incense.
2 Akalia kinyume na zile madhabahu kwa neno la BWANA: “Ee madhabahu, madhabahu” hivi ndivyo asemavyo BWANA, 'Tazama, mwana aitwaye Yosia atazaliwa katika familia ya Daudi, na juu yenu atawachinja makuhani ambao sasa wanafukiza uvumba mahali hapa pa juu kwa ajili yako. Juu yako watachoma mifupa ya watu.'”
He cried against the altar by the word of Jehovah, and said, "Altar, altar, thus says Jehovah: 'Look, a son shall be born to the house of David, Josiah by name. On you he shall sacrifice the priests of the high places who burn incense on you, and they will burn men's bones on you.'"
3 Kisha mtu wa Mungu akatoa ishara siku hiyohiyo, akisema, “Hii ndiyo isharaya kwamba BWANA amesema: 'Tazama, madhabahu zitavuunjika, na majivu yaliyo juu yatamwagika.”
He gave a sign the same day, saying, "This is the sign which Jehovah has spoken: Look, the altar will be split apart, and the ashes that are on it will be poured out."
4 Naye mfalme aliposikia kile mtu wa Mungu alichosema, kwamba amelia kinyume cha zile madhabahu kule Betheli, Yeroboamu akanyosha mkono wake kutoka madhabahuni, akisema, “mkamateni.” Ndipo ule mkono aliokuwa ameunyosha dhidi ya mtu wa Mungu ukakauka, kiasi kwamba hakuweza kuurudisha mwenyewe.
It happened, when the king heard the saying of the man of God, which he cried against the altar in Bethel, that Jeroboam put out his hand from the altar, saying, "Seize him." His hand, which he put out against him, dried up, so that he could not draw it back again to himself.
5 Na ile madhabahu ikavunjika vipande vipande, na yale majivu yakamwagika kutoka madhabahuni, kama ilivyokuwa imefafanuliwa kuwa ndiyo ishara ya kwamba mtu wa Mungu alikuwa amepewa kwa neno la BWANA.
The altar also was split apart, and the ashes poured out from the altar, according to the sign which the man of God had given by the word of Jehovah.
6 Mfalme Yeroboamu akajibu akimwambia mtu wa Mungu, “Msihi BWANA, Mungu wako akupe neema ili uniombee, ili kwamba mkono wangu urejee kwangu tena.” Kwa hiyo mtu wa Mungu akamwomba BWANA, na mkono wa mfalme ukarejea katika hali yake tena, na ukawa kama ulivyokuwa mwanzoni.
The king answered the man of God, "Now plead for the favor of Jehovah your God, and pray for me, that my hand may be restored me again." The man of God entreated Jehovah, and the king's hand was restored him again, and became as it was before.
7 Yule mfalme akamwambia mtu wa Mungu, “twende nyumbani kwangu upate chakula, nami nitakupa zawadi.”
The king said to the man of God, "Come home with me, and refresh yourself, and I will give you a reward."
8 Yule mtu wa Mungu akamwambia mfalme, “Hata kama utanipa nusu ya miliki yako. staende na wewe, wala sitakula au kunywa maji mahali hapa,
The man of God said to the king, "Even if you gave me half of your house, I would not go in with you, neither would I eat bread nor drink water in this place;
9 kwa sababu BWANA ameniamuru kwa neno lake, 'hutakula mkate wala kunywa maji, wala kurudi kwa njia ulioijia.'”
for so was it commanded me by the word of Jehovah, saying, 'You shall eat no bread, nor drink water, neither return by the way that you came.'"
10 Kwa hiyo mtu wa Mungu akaondoka na hakurudi nyumbani kwa njia aliyokuja nayo huko Betheli.
So he went another way, and did not return by the way that he came to Bethel.
11 Sasa kulikuwa na nabii mwingine mzee aliyekuwa akiishi Betheli, na mmoja wa wana wake akaja kumwambia mambo yote ambayo mtu wa Mungu amefanya siku hiyo kule Betheli. Wana wake wakamwambia pia maneno ambayo Yule mtu wa Mungu alimwambia mfalme.
Now there lived an old prophet in Bethel; and one of his sons came and told him all the works that the man of God had done that day in Bethel. And they also told their father the words which he had spoken to the king.
12 Baba yao akawaambia, “Alienda kwa njia gani?” Wale wanawe walikuwa wamemwona yule mtu wa Mungu kutoka Yuda njia aliyotumia kurudi.
Their father said to them, "Which way did he go?" Now his sons showed him the way the man of God went, who came from Judah.
13 Kwa hiyo akawaambia wanawe, “Nitandikeni punda.” Kwa hiyo wakamtandikia punda naye akampanda.
He said to his sons, "Saddle the donkey for me." So they saddled the donkey for him; and he rode on it.
14 Yule nabii mzee akamfuata yule mtu wa Mungu na akamkuta amekaa chini ya mti wa mwaloni; akamwambia, “Je, wewe ndiye mtu wa Mungu aliyetoka Yuda?” Naye akamjibu, “Mimi ndiye.”
He went after the man of God, and found him sitting under an oak. He said to him, "Are you the man of God who came from Judah?" He said, "I am."
15 Kisha yule nabii mzee akamwambia, “twende nyumbani kwangu ukale chakula.”
Then he said to him, "Come home with me, and eat bread."
16 Yule mtu wa Mungu akamjibu, “Siwezi kurudi na wewe wala kuingia ndani na wewe, tena sitakula chakula wala kunywa maji pamoja na wewe mahali hapa,
He said, "I may not return with you, nor go in with you; neither will I eat bread nor drink water with you in this place.
17 kwa sababu niliamuriwa hivyo kwa neno la BWANA, 'Hautakula chakula wala kunywa maji kule, wala kurudi kwa njia utakayokuja nayo.'”
For it was said to me by the word of Jehovah, 'You shall eat no bread nor drink water there, nor turn again to go by the way that you came.'"
18 Kwa hiyo yule nabii mzee akamwambia, “Mimi pia ni nabii kama ulivyo, na malaika amesema na mimi neno la BWANA, akisema, 'Mrudishe aje na wewe katika nyumba yako, ili aweze kula chakula na kunywa maji.'” Lakini alikuwa anamdanganya mtu wa Mungu.
He said to him, "I also am a prophet as you are; and an angel spoke to me by the word of Jehovah, saying, 'Bring him back with you into your house, that he may eat bread and drink water.'" He lied to him.
19 Kwa hiyo yule mtu wa Mungu akarudi pamoja na yule nabii mzee na akala chakula nyumbani kwake na akanywa maji.
So he went back with him, and ate bread in his house, and drank water.
20 Walipokuwa wamekaa mezani, neno la BWANA likamjia yule nabii aliyemrudisha,
It happened, as they sat at the table, that the word of Jehovah came to the prophet who brought him back;
21 naye akalia kwa mtu wa Mungu aliyetoka Yuda, akisema “BWANA anasema, 'Kwa kuwa umeshindwa kutii nenola BWANA na umeshindwa kuishika amri ya BWANA ambayo Mungu wako alikupa,
and he cried to the man of God who came from Judah, saying, "Thus says Jehovah, 'Because you have been disobedient to the mouth of Jehovah, and have not kept the commandment which Jehovah your God commanded you,
22 bali umerudi na umekula chakula na kunywa maji mahali ambapo BWANA alikwambia usile chakula wala kunywa maji, basi mwili wako hautazikwa kwenye makaburi ya baba zako.'”
but came back, and have eaten bread and drunk water in the place of which he said to you, "Eat no bread, and drink no water"; your body shall not come to the tomb of your fathers.'"
23 Baada ya kula chakula na kunywa maji, Yule nabii akatandika punda wa mtu wa Mungu, yule mtu aliyerudi naye.
It happened, after he had eaten bread, and after he had drunk, that he saddled the donkey for the prophet whom he had brought back.
24 Baada ya mtu wa Mungu kuondoka, akakutana na simba njiani na kumwua barabarani, na mwili wake uliachwa barabarani. Na yule punda akasimama pembeni yake, na yule simba naye akasimama pembeni ya ule mwili.
When he had gone, a lion met him by the way, and killed him. His body was cast in the way, and the donkey stood by it. The lion also stood by the body.
25 Watu walipopita na kuuona ule mwili umeachwa barabarani, na yule simba akisimama karibu na ule mwili, walikuja wakaeleza habari hiyo mjini kule ambako yule nabii mzee aliishi.
Look, men passed by, and saw the body cast in the way, and the lion standing by the body; and they came and told it in the city where the old prophet lived.
26 Yule nabii aliyemrudisha toka njiani aliposikia, akasema, “Yeye mtu wa Muugu ndiye aliyeshindwa kutii neno la BWANA. Kwa hiyo BWANA alimtoa kwa simba, ambaye amemrarua katika vipande vipande na kumwua, kama vile neno la BWANA lilivyokuwa limemwonya.”
When the prophet who brought him back from the way heard of it, he said, "It is the man of God who was disobedient to the mouth of Jehovah. Therefore Jehovah has delivered him to the lion, which has mauled him and slain him, according to the word of Jehovah, which he spoke to him."
27 Kwa hiyo yule nabii mzee akawaamnbia wanawe, akisema, “Tandikeni punda wangu,” nao wakamtandikia.
He spoke to his sons, saying, "Saddle the donkey for me." They saddled it.
28 Akaenda akaukuta mwili umeachwa barabarani, punda na simba wamesimama pembeni ya ule mwili. Yule simba hakuula ule mwili, wala hakumshambulia yule punda.
He went and found his body cast in the way, and the donkey and the lion standing by the body. The lion had not eaten the body, nor mauled the donkey.
29 Yule nabii akauchukua ule mwili wa mtu wa Mungu, akaulaza juu ya punda, na akaurudisha. Akaja kwenye mji wake kuomboleza na kuuzika.
The prophet took up the body of the man of God, and laid it on the donkey, and brought it back. And he came to the city of the old prophet to mourn and to bury him.
30 Akaulaza mwili kwenye kaburi lake, nao wakamwombolezea, wakisema, “Aa! ndugu yangu!”
He laid his body in his own grave; and they mourned over him, saying, "Alas, my brother."
31 Kisha baada ya kumzika, yule nabii mzee akawaambia wanawe, akasema, “Nitakapokufa, mtanizika kwenye kaburi ambalo tumemzika mtu wa Mungu. Mtalaza mifupa yangu pembeni mwa mifupa yake.
It happened, after he had buried him, that he spoke to his sons, saying, "When I am dead, then bury me in the tomb in which the man of God is buried. Lay my bones beside his bones.
32 Kwa kuwa ule ujumbe uliosemwa na BWANA, dhidi ya madhabahu kule Betheli na dhidi ya nyumba zote za mahali pa juu katika mji wa Samaria, hakika yatatokea.
For the saying which he proclaimed by the word of Jehovah against the altar in Bethel, and against all the houses of the high places which are in the cities of Samaria, will surely happen."
33 Baada ya haya Yeroboamu hakuuacha uovu wake, aliendelea kuchagua makuhani wa kawaida kwa ajili ya mahali pa juu kutoka kwa watu wa kila aina. Yeyote ambaye angeweza kutumika alimtakasa kuwa kuhani.
After this thing Jeroboam did not return from his evil way, but again made priests of the high places from among all the people. He consecrated anyone who wanted to be a priest at the high places.
34 Jambo hili likawa dhambi kwenye familia ya Yeroboamu na kusababisha familia yake kuangamizwa na kuondolewa kabisa katika uso wa dunia.
This thing became sin to the house of Jeroboam, even to cut it off, and to destroy it from off the surface of the earth.

< 1 Wafalme 13 >