< 1 Wakorintho 3 >

1 Na mimi, kaka na dada zangu, sikusema nanyi kama watu kiroho, lakini kama na watu wa kimwili. Kama na watoto wadogo katika Kristo.
Frères, je n'ai pas pu vous parler comme à des spirituels, mais comme à des charnels, comme à des enfants en Christ.
2 Niliwanywesha maziwa na si nyama, kwa kuwa hamkuwa tayari kwa kula nyama. Na hata sasa hamjawa tayari.
Je vous ai nourris de lait, non de nourriture solide, car vous n'étiez pas encore prêts. Et maintenant encore, vous n'êtes pas prêts,
3 Kwa kuwa ninyi bado ni wa mwilini. Kwa kuwa wivu na majivuno yanaonekana miongoni mwenu. Je, hamuishi kulingana na mwili, na je, hamtembei kama kawaida ya kibinadamu?
car vous êtes encore charnels. En effet, s'il y a parmi vous de la jalousie, des querelles et des divisions, n'êtes-vous pas charnels, et ne marchez-vous pas selon les voies des hommes?
4 Kwa kuwa mmoja husema, “Namfuata Paulo” Mwingine husema “Namfuata Apolo,” hamuishi kama wanadamu?
Car si l'un dit: « Je suis Paul », et l'autre: « Je suis Apollos », n'êtes-vous pas charnels?
5 Apolo ni nani? na Paulo ni nani? Watumishi wa yule mliyemwamini, kwa kila ambaye Bwana alimpa jukumu.
Qui donc est Apollos, et qui est Paul, sinon des serviteurs par qui vous avez cru, et chacun selon ce que le Seigneur lui a donné?
6 Mimi nilipanda, Apolo akatia maji, lakini Mungu akakuza.
J'ai planté. Apollos a arrosé. Mais c'est Dieu qui a donné l'accroissement.
7 Kwa hiyo, si aliye panda wala aliyetia maji ana chochote. Lakini ni Mungu anayekuza.
Ainsi donc, ni celui qui plante n'est rien, ni celui qui arrose, mais Dieu qui fait croître.
8 Sasa apandaye na atiaye maji wote ni sawa, na kila mmoja atapokea ujira wake kulingana na kazi yake.
Or, celui qui plante et celui qui arrose sont pareils, mais chacun recevra sa propre récompense selon son propre travail.
9 Kwa kuwa sisi tu watendakazi wa Mungu, ninyi ni bustani ya Mungu, jengo la Mungu.
Car nous sommes les compagnons de travail de Dieu. Vous êtes l'agriculture de Dieu, la construction de Dieu.
10 Kutokana na neema ya Mungu niliyopewa kama mjenzi mkuu, niliuweka msingi, na mwingine anajenga juu yake. Lakini mtu awe makini jinsi ajengavyo juu yake.
Selon la grâce de Dieu qui m'a été donnée, j'ai posé, comme un sage maître d'œuvre, un fondement, et un autre bâtit dessus. Mais que chacun prenne garde à la manière dont il bâtit dessus.
11 Kwa kuwa hakuna mwingine awezaye kujenga msingi mwingine zaidi ya uliojengwa, ambao ni Yesu Kristo.
Car personne ne peut poser un autre fondement que celui qui a été posé, c'est-à-dire Jésus-Christ.
12 Sasa, kama mmoja wenu ajenga juu yake kwa dhahabu, fedha, mawe ya thamani, miti, nyasi, au majani,
Mais si quelqu'un bâtit sur le fondement avec de l'or, de l'argent, des pierres précieuses, du bois, du foin ou de la paille,
13 kazi yake itafunuliwa, kwa mwanga wa mchana utaidhihirisha. Kwa kuwa itadhihirishwa na moto. Moto utajaribu ubora wa kazi wa kila mmoja alichofanya.
l'œuvre de chacun sera dévoilée. Car le Jour le fera connaître, parce qu'il se révèle dans le feu; et le feu lui-même éprouvera quelle est l'œuvre de chacun.
14 Kama chochote mtu alichojenga kitabaki, yeye atapokea zawadi.
S'il reste de l'œuvre de quelqu'un ce qu'il a construit dessus, il recevra une récompense.
15 Lakini kama kazi ya mtu ikiteketea kwa moto, atapata hasara. Lakini yeye mwenyewe ataokolewa, kama vile kuepuka katika moto.
Si l'œuvre de quelqu'un est brûlée, il subira une perte, mais il sera sauvé lui-même, mais comme par le feu.
16 Hamjui kuwa ninyi ni hekalu la Mungu na kwamba Roho wa Mungu anakaa ndani yenu?
Ne savez-vous pas que vous êtes le temple de Dieu et que l'Esprit de Dieu habite en vous?
17 Kama mtu akiliharibu hekalu la Mungu, Mungu atamharibu mtu yule. Kwa kuwa hekalu la Mungu ni takatifu, na hivyo na ninyi.
Si quelqu'un détruit le temple de Dieu, Dieu le détruira, car le temple de Dieu est saint, ce que vous êtes.
18 Mtu asijidanganye mwenyewe, kama yeyote miongoni mwenu anadhani ana hekima katika nyakati hizi, awe kama “mjinga” ndipo atakuwa na hekima. (aiōn g165)
Que personne ne se trompe lui-même. Si quelqu'un pense être sage parmi vous dans ce monde, qu'il devienne fou pour devenir sage. (aiōn g165)
19 Kwa kuwa hekima ya dunia hii ni ujinga mbele za Mungu, Kwa kuwa imeandikwa, “Huwanasa wenye hekima kwa hila zao”
Car la sagesse de ce monde est folie devant Dieu. Car il est écrit: « Il a pris les sages dans leur ruse. »
20 Na tena “Bwana anajua mawazo ya wenye busara ni ubatili.”
Et encore: « Le Seigneur connaît les raisonnements des sages: ils sont sans valeur. »
21 Hivyo mtu asijivunie wanadamu! Kwa kuwa vitu vyote ni vyenu.
Que personne ne se glorifie donc dans les hommes. Car toutes choses sont à vous,
22 Kama ni Paulo, au Apolo, au Kefa, au dunia, au maisha, au kifo, au vitu vilivyopo, au vitakavyokuwepo. Vyote ni vyenu,
soit Paul, soit Apollos, soit Céphas, soit le monde, soit la vie, soit la mort, soit les choses présentes, soit les choses à venir. Tout est à vous,
23 na ninyi ni wa Kristo na Kristo ni wa Mungu.
et vous êtes à Christ, et Christ est à Dieu.

< 1 Wakorintho 3 >